Serikali kuwapa mtaji wanaohitimu mafunzo JKT

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,001
9,866

SERIKALI imesema itaangalia namna ya kuwapa mtaji vijana wanaohitimu mafunzo katika makambi ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) ili ujuzi wanaoupata usipotee badala yake wakautumie uraiani.



WhatsApp%20Image%202021-07-03%20at%2016.32.54.jpeg

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Brigedia Jenerali Rajab Mabele,akimuonyesha ghala la kuhifadhia chakula waziri wa Ulinzi Elius Kwandika mwenye kofia la pama.


Hayo yamesemwa na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Elias Kwandika wakati akikagua mradi wa Skimu ya Umwagiliaji iliopo kikosi cha 837 Chita JKT,kinachoendesha kilimo cha Mpunga na Ufugaji wa Samaki katika mabwawa.

Kwandika, amesema wanaangalia namna ya kuwapa mitaji kwenye vikundi ili kile walichojifunza wakakitumie katika kujiajiri badala ya kutegemea ajira za serikali.

Amesema vijana hao wanapata mafunzo ya kutosha na yenye kuwajenga ambayo wanaamini wakihitimu mafunzo wanakuwa vijana bora wa mfano wa kuigwa katika kila nyanja.

“Tunaangalia namna ya kuwawezesha vijana lengo letu ni kuona vijana ujuzi wao haupotei,” amesema Kwandika.
Mbali na hilo Kwandika amewaagiza wananchi kutumia mashamba ya kilimo mkakati ya (JKT) kama shamba darasa kwa ajili ya kukuza sekta ya kilimo hapa nchini.

NIPASHE
 
Yan watu mmewafunza mbinu mbali mbsli.za kivita wanajua kutumia silaha vizuri.afu muwambie kajiajilini.kila mwaka wanahitimu wengi tu pengine.mpaka sasa wanafikia laki moja walio hitimu hiv hawa wakiungana wakaunda jeshi.la kigaid chanzo atakua nan? Kwann msiwajili.tukiwa na wanajesho wengi ni sifa nzur kwa taiga
 
Hii ni njia mojawapo ya kuandaa majambazi wa badae acha tu serikali iendelee kuwamwaga wahitimu mtaani.
 

SERIKALI imesema itaangalia namna ya kuwapa mtaji vijana wanaohitimu mafunzo katika makambi ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) ili ujuzi wanaoupata usipotee badala yake wakautumie uraiani.



WhatsApp%20Image%202021-07-03%20at%2016.32.54.jpeg




Hayo yamesemwa na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Elias Kwandika wakati akikagua mradi wa Skimu ya Umwagiliaji iliopo kikosi cha 837 Chita JKT,kinachoendesha kilimo cha Mpunga na Ufugaji wa Samaki katika mabwawa.

Kwandika, amesema wanaangalia namna ya kuwapa mitaji kwenye vikundi ili kile walichojifunza wakakitumie katika kujiajiri badala ya kutegemea ajira za serikali.

Amesema vijana hao wanapata mafunzo ya kutosha na yenye kuwajenga ambayo wanaamini wakihitimu mafunzo wanakuwa vijana bora wa mfano wa kuigwa katika kila nyanja.

“Tunaangalia namna ya kuwawezesha vijana lengo letu ni kuona vijana ujuzi wao haupotei,” amesema Kwandika.
Mbali na hilo Kwandika amewaagiza wananchi kutumia mashamba ya kilimo mkakati ya (JKT) kama shamba darasa kwa ajili ya kukuza sekta ya kilimo hapa nchini.

NIPASHE
Wataangalia kwa bajeti ipi? Ndo kwanza bajeti mpya ipo na siku 4 tu.
Namkumbusha askari na Siasa ni maji na mafuta
 
Back
Top Bottom