Serikali izibane hotel zote za kulala Tanzania zinaibia wateja

Wanasheria wetu wasomi kazi hii hapa,wananchi tumeibiwa mno,utakuta kwenye kitabu cha wageni imeandikwa KUFIKA unajaza talehe uliyofka,KUONDOKA pia unajaza talehe utakayoondoka, sasa ngoja ifike saa 4 we bwana weee!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
They are thieves.So you want American thieves to be exempted?
Marekani pia kuna Motels za kulipia kwa masaa.

Sasa kama uko level ya motel, halafu unaenda hotel, hapo kosa ni lako.

Again, hutakiwi kulalamikia Range Rover linatumia mafuta sana, kwa sababu tu umeingia cha kike na kuchukua Range Rover badala ya Vitara.

Ulitakiwa kusima fuel consumption rates kabla ya kununua gari.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naongelea hoteli kibwa zenye mamia na maelfu ya vyumba zinazohitaji a systemic way of doing things.

Si vi guest house vyenye vyumba kumi mnavyoviita hoteli.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Wenye kufanyia kazi malalamiko yako ndiyo wenye mahoteli makubwa kila kona ya nchi, unategemea watakuelewa!?
 
Hzo hotel unazozungumzia wanyonge wanaweza kwenda?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wenye kufanyia kazi malalamiko yako ndiyo wenye mahoteli makubwa kila kona ya nchi, unategemea watakuelewa!?
Wanielewe wasinielewe to hell with them bila pesa zetu wateja hawana Chao Cha hoteli Wala Nini ? Kama hawataki tutaenda lala guest house za short time wabaki na mihoteli yao ya kijizi ya kuibiwa wateja

Guest house jiiongezeni endeleeni kuchaji kwa masaa Hawa wenye mihoteli mikubwa wapigeni bao.Cha msingi Wekeni huduma nzuri vyumba viwe visafi na usalama na ulinzi uwe mzuri.Vyakula sio lazima viwepo Mtu Aweza kula popote sehemu zenye vyakula ,supu na chai jirani au popote .

Ni wakati wenu guest house kuwabwaga Hawa wapuuzi wezi Wenye mihoteli.Wabaki na mihoteli yao wale na kulala na wake zao au hawala zao .
 
Naongelea hoteli kibwa zenye mamia na maelfu ya vyumba zinazohitaji a systemic way of doing things.

Si vi guest house vyenye vyumba kumi mnavyoviita hoteli.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mwizi Ni mwizi hata awe na system za umoja wa mataifa.Huwezi lipa mfano chumba dola elfu mbili kwa siku ume check in SAA kumi usiku halafu saa sita mchana anakwambia toka Ngedere wewe au ongeza hela
 
Kiongozi, checkout time sio suala la Tanzania, ni Dunia nzima. Wanaweza kukuruhusu hadi saa sita lakini kawaida ni saa nne au saa tano.

Just imagine ratiba ya checkout iwe shagalabagala, huo usafi utafanyika muda gani?

Kama Nigeria wana utaratibu huo, labda kwenye vi Hotel vya uswahilini. International Hotel brands hawawezi kukubali upuuzi huo.
Mgeni akiona utaratibu wa short time kwenye vi lodge mchafukoge hapa Tanzania, anaweza kudhani ni utaratibu wa Bongo.
 
Hivi sisi tuliobarikiwa kuwa matajiri na kumiliki Mahotel tunawakera na nini ?
 
Hivi sisi tuliobarikiwa kuwa matajiri na kumiliki Mahotel tunawakera na nini ?
Kutudhulumu muda wa kuingia na kutoka wenzenu Nchi za Afrika Magharibi muda wa kuingia ndio wa kutoka hawadhulumu wanahakikisha unapewa masaa yako 24 mwambie Sugu na Mbowe na waaomiliki hoteli wa chadema kuwa wateja wanatukera
 
Mwizi Ni mwizi hata awe na system za umoja wa mataifa.Huwezi lips mfano chumba dola elfu mbili kwa siku ume check in SAA kumi usiku halafu saa sita mchana anakwambia toka Ngedere wewe au ongeza hela

Tuseme huu ni wizi.

Sasa, mnafanya nini kuondoa "wizi" huu zaidi ya kulalamika JF?
 
My sentiments exactly.

Watu wanachanganya levels.

Suala la checkout time hoteli kubwa linaeleweka.

Tatizo linaanza mtu anapotaka kulazimisha standards za guest house za kijijini na hotel kubwa.

Hoteli ina vyumba elfu moja, halafu unataka isiwe na standardized time ya kufanya usafi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kutudhulumu muda wa kuingia na kutoka wenzenu Nchi za Afrika Magharibi muda wa kuingia ndio wa kutoka hawadhulumu wanahakikisha unapewa masaa yako 24 mwambie Sugu na Mbowe na waaomiliki hoteli wa chadema kuwa wateja wanatukera
Masikini hebu nendeni guest house za keko magurumbasi , haya mahotel waachieni wenye uwezo
 
Tuseme huu ni wizi.

Sasa, mnafanya nini kuondoa "wizi" huu zaidi ya kulalamika JF?


Kuna comment imeniacha mdomo wazi naona kama network search
Madai yake ni kulala saa 24, halafu anakuja anasema anahama toka mahoteli makubwa kwenda kulala short time
😅
 
Umewehuka?
 
Kweli hili swala waliangalie unaingia gest saa 9 usiku saa 4 unaambiwa uache chumba Kuna siku tuliingia na jamaa yangu saa 9usiku Sasa asubui tukatoka tukawai kufanya shuguli zetu badae tu narudi saa4 tunadaiwa pesa jamaa yangu aligoma kulipa mpaka akaja mkurugenzi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…