The unpaid Seller
JF-Expert Member
- Oct 27, 2019
- 1,876
- 5,443
Peace be upon you all,
Miaka kadhaa nyuma wakati nafanya kazi katika shirika fulani la serikali nilisafiri kwenda nchi jirani kikazi kwa muda wa miezi miwili kama project consultant.
Wakati niko hapo kwa jirani yetu siku moja ya weekend katika mapumziko mida ya alasiri kuelekea usiku nikashuhudia na kupatwa na jaribu kali. Kumbe pale kulikua ni chimbo la dada poa.
Nikashuhudia gari ndogo ndogo zinaingia wanashuka mabinti wa kali tupu na kwa jirani yetu wanasifika kwa mabinti warembo katika ukanda mzima wa maziwa makuu na kati. Bwana we katika kuuliza kulikoni je kuna sherehe au tafrija, (kosa kubwa la kwanza) nikajuzwa wale ni hela yako tu unatafuna.
Walikua ni mabinti warembo sijapata kuona na maumbo yao mazuri rangi yao maridadi daaah aise acha. Nikaingiwa shauku na udadisi kujua bei, (kosa la pili) Walikua wa umri tofauti na bei zao ilikua tofauti tofauti kuanzia 20$ mpaka 100$.
Katika kutazama tazama macho yakamnasa binti mmoja mrembo sana nikajikuta namuita balaa binti anazungumza Kifaransa na Kingereza kibovu kuliko cha Mwendazake mjuba natema Kiswahili na English, ila kwa kutumia mbinu za kifidinashal nikamjua jina aliitwa Filonne na bei yake ilikua 60$
Kuna hisia zilinijia kusitisha udadisi wangu kua ungepelekea pabaya ila nikaipuuzia, (kosa la tatu) nikataka nipewe utaratibu wa kusafisha gobole ikumbukwe hiyo ilikua week nzima imepita bila kuchakata, nikaomba itifaki izingatiwe haraka iwezekanavyo. (Kosa la nne) binti akapiga simu sekunde chache ikaja taxi hao tukaelekea panako.
Umbali wa mwendo wa dakika 10 hivi tulifika kwenye hotel moja matata sana mwanadada akanikaribisha na tulipokwisha kuingia aliniuliza nalipa kwa cash au wire transfer nikamwambia cash nikampa 60$ na kila kitu kikaenda sawa kwa kadri au zaidi ya matarajio.
Balaa likazuka wakati natoka reception nikakuta sura mpya za wanaume wawili na binti mmoja (nadhani walikua wameingia shift nyingine) wakazungumza wakiniuliza sikuwaelewa wakaniuliza kwa kingereza mimi ni nani nilikua chumba gani huku wakifungua kitambu cha wageni, nikawaambia mimi sio mpangishaji nilikuja kwa mwenyeji wangu, wakaniuliza chumba gani jibu langu sijui. Halahaula mmoja alikua ni security kwa haraka akanifuata na kuniamuru nitoe vitambulisho vyangu.
Kwa kujua hali ilikua inaelekea pabaya nakuwapa vitambulisho ingepelekea balaa kuzuka kazini tena ugenini nikasema sina kitambulisho.(Kosa kubwa la tano). Aise, aise wenzetu wako makini sana na mtu wanaemtilia shaka uraia wake tofauti kabisa na kwetu hapa hata mtu akionekana sio raia hakuna anaejali.
Ghafla kwa haraka wakaitwa askari pale nikawekwa chini ya ulinzi na kupekuliwa haswa, jamaa wanapekua haswa mdomoni, chini ya ulimi, masikioni, unavua shati alafu unainua mikono juu, fungua mkanda shusha suruali wakaipekua (wakakuta vitambulisho vyangu) pekua viatu. Wakachukua vitambulisho na kuniamuru nivae nguo wakibaki na card zote za bank, simu na vitambulisho na hela yote.
Balaa zito walipogundua mimi ni Mtanzania walinitia hand seal (ni kama kamba ila ukifunga na kufuta haifunguki mpaka uikate kama pingu vile ila ni ya plastik) kuanzia hapo wakabadilisha lugha wakawa wanaongea lugha yao punde ikaja gari nikatiwa garini mpaka police post nilipofungiwa ndani ya chumba cha peke yangu, mapigo ya moyo yalikua yanakwenda mbio nikajua hawa jamaa wanaweza kunipoteza.
Tofauti na kwetu ukifika kituoni unahojiwa wao hawakunihoji na nilipowaomba wanihoji kua mimi sio mhalifu hawakujali waliscan vitambulisho vyangu na kuchukua alama za vidole wakanipiga picha kisha mwanadada fulani kwenye computer akawa kama anaadika au kutuma taarifa zangu sehemu fulani huku akiongea na kufuata maelekezo kwa njia ya simu.
Yalipita masaa kama 5 usiku ule akaja project cordinator ambae ndio alikua Spr na Project consultant mwenzangu na mtu wa ubalozini na watu wengine 3 sikuwafahamu wakawa wanaongea na maafisa wa police kwa muda kama nusu saa hivi. Badae niliitwa na kukabidhiwa vitu vyangu vyote na kuruhusiwa kuondoka. (Aaah aah qmmae AIBU aibuuu ya karhne)
Tulipotoka pale PCtr na PCnt wakaniambia kila kitu (hawa majirani zetu wako mbele sana kiupelelezi hakuna kubambikiwa kesi na uswahili kosa lako linawekwa bayana) kwa mda mfupi jamaa walifanikiwa kujua kila kitu na nilifikaje pale hotelini na wakawawasiliana na ubalozini bila kuchelewa. Basi wakaniambia kua wameambiwa kua nilichukua malaya na pale hotelini nilitiliwa shaka kama gaidi au mpelelezi kutoka Tanzania.
Sitasahau aibu niliyoipata kwa wenzangu na wakubwa wangu wa kazi kuambiwa nilitembea na madada poa. Mpaka leo nikikumbuka hua najionea haya kuu, daaaah. (Japo kale kadada kalikua ni katamu sijapata kuona nikiri wazi)
Mwenzetu aibu gani ilishakukuta, ilikuaje, ukaisolve vipi? Je, bado unajihisi hatia?
Picha kwa hisani ya mtandao, na haiusiani na tukio lilisimuliwa ila kuna mlinganyo wa 98%.
Miaka kadhaa nyuma wakati nafanya kazi katika shirika fulani la serikali nilisafiri kwenda nchi jirani kikazi kwa muda wa miezi miwili kama project consultant.
Wakati niko hapo kwa jirani yetu siku moja ya weekend katika mapumziko mida ya alasiri kuelekea usiku nikashuhudia na kupatwa na jaribu kali. Kumbe pale kulikua ni chimbo la dada poa.
Nikashuhudia gari ndogo ndogo zinaingia wanashuka mabinti wa kali tupu na kwa jirani yetu wanasifika kwa mabinti warembo katika ukanda mzima wa maziwa makuu na kati. Bwana we katika kuuliza kulikoni je kuna sherehe au tafrija, (kosa kubwa la kwanza) nikajuzwa wale ni hela yako tu unatafuna.
Walikua ni mabinti warembo sijapata kuona na maumbo yao mazuri rangi yao maridadi daaah aise acha. Nikaingiwa shauku na udadisi kujua bei, (kosa la pili) Walikua wa umri tofauti na bei zao ilikua tofauti tofauti kuanzia 20$ mpaka 100$.
Katika kutazama tazama macho yakamnasa binti mmoja mrembo sana nikajikuta namuita balaa binti anazungumza Kifaransa na Kingereza kibovu kuliko cha Mwendazake mjuba natema Kiswahili na English, ila kwa kutumia mbinu za kifidinashal nikamjua jina aliitwa Filonne na bei yake ilikua 60$
Kuna hisia zilinijia kusitisha udadisi wangu kua ungepelekea pabaya ila nikaipuuzia, (kosa la tatu) nikataka nipewe utaratibu wa kusafisha gobole ikumbukwe hiyo ilikua week nzima imepita bila kuchakata, nikaomba itifaki izingatiwe haraka iwezekanavyo. (Kosa la nne) binti akapiga simu sekunde chache ikaja taxi hao tukaelekea panako.
Umbali wa mwendo wa dakika 10 hivi tulifika kwenye hotel moja matata sana mwanadada akanikaribisha na tulipokwisha kuingia aliniuliza nalipa kwa cash au wire transfer nikamwambia cash nikampa 60$ na kila kitu kikaenda sawa kwa kadri au zaidi ya matarajio.
Balaa likazuka wakati natoka reception nikakuta sura mpya za wanaume wawili na binti mmoja (nadhani walikua wameingia shift nyingine) wakazungumza wakiniuliza sikuwaelewa wakaniuliza kwa kingereza mimi ni nani nilikua chumba gani huku wakifungua kitambu cha wageni, nikawaambia mimi sio mpangishaji nilikuja kwa mwenyeji wangu, wakaniuliza chumba gani jibu langu sijui. Halahaula mmoja alikua ni security kwa haraka akanifuata na kuniamuru nitoe vitambulisho vyangu.
Kwa kujua hali ilikua inaelekea pabaya nakuwapa vitambulisho ingepelekea balaa kuzuka kazini tena ugenini nikasema sina kitambulisho.(Kosa kubwa la tano). Aise, aise wenzetu wako makini sana na mtu wanaemtilia shaka uraia wake tofauti kabisa na kwetu hapa hata mtu akionekana sio raia hakuna anaejali.
Ghafla kwa haraka wakaitwa askari pale nikawekwa chini ya ulinzi na kupekuliwa haswa, jamaa wanapekua haswa mdomoni, chini ya ulimi, masikioni, unavua shati alafu unainua mikono juu, fungua mkanda shusha suruali wakaipekua (wakakuta vitambulisho vyangu) pekua viatu. Wakachukua vitambulisho na kuniamuru nivae nguo wakibaki na card zote za bank, simu na vitambulisho na hela yote.
Balaa zito walipogundua mimi ni Mtanzania walinitia hand seal (ni kama kamba ila ukifunga na kufuta haifunguki mpaka uikate kama pingu vile ila ni ya plastik) kuanzia hapo wakabadilisha lugha wakawa wanaongea lugha yao punde ikaja gari nikatiwa garini mpaka police post nilipofungiwa ndani ya chumba cha peke yangu, mapigo ya moyo yalikua yanakwenda mbio nikajua hawa jamaa wanaweza kunipoteza.
Tofauti na kwetu ukifika kituoni unahojiwa wao hawakunihoji na nilipowaomba wanihoji kua mimi sio mhalifu hawakujali waliscan vitambulisho vyangu na kuchukua alama za vidole wakanipiga picha kisha mwanadada fulani kwenye computer akawa kama anaadika au kutuma taarifa zangu sehemu fulani huku akiongea na kufuata maelekezo kwa njia ya simu.
Yalipita masaa kama 5 usiku ule akaja project cordinator ambae ndio alikua Spr na Project consultant mwenzangu na mtu wa ubalozini na watu wengine 3 sikuwafahamu wakawa wanaongea na maafisa wa police kwa muda kama nusu saa hivi. Badae niliitwa na kukabidhiwa vitu vyangu vyote na kuruhusiwa kuondoka. (Aaah aah qmmae AIBU aibuuu ya karhne)
Tulipotoka pale PCtr na PCnt wakaniambia kila kitu (hawa majirani zetu wako mbele sana kiupelelezi hakuna kubambikiwa kesi na uswahili kosa lako linawekwa bayana) kwa mda mfupi jamaa walifanikiwa kujua kila kitu na nilifikaje pale hotelini na wakawawasiliana na ubalozini bila kuchelewa. Basi wakaniambia kua wameambiwa kua nilichukua malaya na pale hotelini nilitiliwa shaka kama gaidi au mpelelezi kutoka Tanzania.
Sitasahau aibu niliyoipata kwa wenzangu na wakubwa wangu wa kazi kuambiwa nilitembea na madada poa. Mpaka leo nikikumbuka hua najionea haya kuu, daaaah. (Japo kale kadada kalikua ni katamu sijapata kuona nikiri wazi)
Mwenzetu aibu gani ilishakukuta, ilikuaje, ukaisolve vipi? Je, bado unajihisi hatia?
Picha kwa hisani ya mtandao, na haiusiani na tukio lilisimuliwa ila kuna mlinganyo wa 98%.