Nadhani huujui vizuri mziki wa bongo flava na mashabiki wake, Nikwambie tu siyo wote tunaompenda na kumkubali Allikiba basi ndo useme wote tunamchukia Diamond, HAPANA.
Nataka tu nikwambie kitu Allikiba ni moto mbaya sana ule, ogopa mtu mkimya na mpole mpole siku zote huwa wana nguvu hatari, sote tumeona baada ya maneno mengi na majungu kutoka kwa TeamDiamond kuwa sijui kafulia mara nini, Kiba hakusikika popote akiwajibu bali jamaa aliamua tu kwenda studio na kuwajibu kwa track ya "Mwana" ambayo mpaka leo upande wa pili kama mmepanic fulani hivi tena na baada ya kumaliza kabisa na hii ngoma mpya ya "Cheketua" basi ndo kabisa povu linawatoka.
Justly imagine kiba yupo nominated katika category 7 za KTMA just kwa wimbo mmoja wa mwana, huku Diamond akiwa nominated katika Category 2 tu tena zote kabananishwa kwenye kona na KingKiba, walahi mwaka huu mtamu sana.
Pia June KingKiba atachia kitu kipya cha sebene alichofanya na Christian Bella, Eeh hapana chezea dunia itakwenda kusimama siku hiyo.