Serikali ipige marufuku watu kuchukua video na picha za uwanja mpya wa JNIA, vibali vitolewe kwa wanaotaka kupiga picha

Richard

JF-Expert Member
Oct 23, 2006
14,939
20,400
1611499040959.png

Picha na Pixabay.

Uwanja mpya wa JKNIA ni kioo cha nchi yetu yaani ni kama uso au sebule au mapokezi ya wageni wanaotembelea nchi yetu.

Uwanja wetu mpya wa JKNIA unasifiwa kuwa ni moja ya viwanja vipya vya ndege ambavyo vina hadhi ya kimataifa na sifa hizo ni kutoka kwa wageni mbalimbali wanaofika uwanjani hapo.

Lakini, kumezuka tabia ya baadhi ya watu kujichukulia picha za video na picha za kawaida za uwanja huo mpya na kuzisambaza mitandaoni na sehemu zingine.

Si jambo baya kwa watu kupiga picha zinazowahusu au (selfie) lakini picha zingine ni lazima zipatiwe kibali maalum kutoka mamlaka ya viwanja vya ndege.

Sababu kubwa ni usalama wa uwanja huo na abiria wote wanaoondoka na kuingia nchini Tanzania pamoja na wale wasindikizaji na watumishi au wafanyakazi wa kila sekta wanaofanya kazi ndani ya uwanja huo.

Katika miaka ya hivi karibuni suala la usalama limekuwa ni la lazima na linalopewa kipaumbele na nchi nyingi tu ambazo zinakuwa zimeamua kujenga au kupanua viwanja vyao au miundombinu muhimu iwe viwanja vya ndege, njia za reli, barabara na za majini.

Matishio ya usalama kwa uwanja wa ndege kama JKNIA yanaweza kuwa ni pamoja na watu wabaya kuanza kuchukua picha za uwanja huo kwa ajili ya kutengeneza mashambulizi au kwa kiingereza huitwa "reconnaissance" au "recon" ambapo mhusika anakuwa kipita sehemu lengwa kuchukua picha za video na za kawaida kwa ajili ya kwenda kutengeneza mashambulizi.

Hivyo ni jukumu la watu wa kitengo cha usalama kiwanjani hapo kuhakikisha kunakuwepo na alama au matangazo ya kutoa onyo kukataza kuchukua picha katika eneo lote la uwanja na viunga vyake.

Iwepo adhabu ya faini kwa atakaekiuka agizo hilo au kufunguliwa mashtaka kwa kukiuka onyo lililowekwa sehemu ya wazi.

Endapo mtu atahitaji kuchukua picha za video au za kawaida basi atapaswa kuwasiliana na kitengo maalum cha mahusiano na wateja au enquiries/cutomer services ambao watamuelekeza kwa afisa habari ambae mara nyingi huitwa "uncle Frank" ambapo watapata maelekezo yote na kupatiwa kibali.

Kuwepo kwa kibali kutasaidia kudhibiti uchukuaji holela wa picha hizo na pia kuwepo na utaratibu kwa wale wambao wanahitaji kutumia uwanja huo kwa shughuli kama sherehe, uchukuaji picha za filamu au matumizi mengine ya kijamii.

Huu ni ushauri kwa vyombo vya usalama na waziri wa mambo ya ndani kwani ni jukumu lenu kuhakikisha miundombinu hii ambayo ni kielelezo cha jitihada za serikali kuikwamu nchi kiuchumi yalindwa kwa gharama zozote zile.
 
Hicho kibali itabidi kiuzwe kwa pesa nyingi ili kuongeza Pato la taifa na mlipaji alipe kwa control no.

Swali kwa mleta mada, hivi ulinzi uliokuwepo una wasiwasi nao? Una mashaka na mfumo wa CCTV uliokuwepo?
Unaongelea sehemu ipi ktk uwanja wa ndege zinaporuka ndege, mapokezi au nje ktk kuegesha magari?
 
Hicho kibali itabidi kiuzwe kwa pesa nyingi ili kuongeza Pato la taifa na mlipaji alipe kwa control no....

Swali kwa mleta mada hivi ulinzi uliokuwepo una wasiwasi nao? Huna mashaka na mfumo wa CCTV ulio kuwepo?
Unaongelea sehemu hipi ktk uwanja wa ndege zinaporuka ndege, mapokezi au nje ktk kuegesha magari?
CCTV ni sehemu ya usalama.

Lakini kuzuia watu kuchukua picha kwa onyo la picha yaitwa "pre-emptive measures".
 
Una akili za kiCCM na Magufuli kwa 💯💯💯💯💯💯

Masharti masharti kibao kama tunaishi nyumbani kwa mganga wa Jadi.

Ni kujishukushuku MUDA wote.
Nikiwa ni mtu ambae nimepita viwanja vingi nimeona kuwa uwanja wetu una mapungufu hayo.
 
Mzee umeona mke wa diamond anapigwa picha kashuka ndio unafoka. Mila za kizamani eti usipige picha kuna sehemu mahsusi zile zenye kazi mahsusi ndio usipige picha . Yaani hata mgahawani kwa Open kitchen usijipige selfie au Duty free shop tutachekwa mkuu.
 
Mzee umeona mke wa diamond anapigwa picha kashuka ndio unafoka. Mila za kizamani eti usipige picha kuna sehemu mahsusi zile zenye kazi mahsusi ndio usipige picha . Yaani hata mgahawani kwa Open kitchen usijipige selfie au Duty free shop tutachekwa mkuu.
Mkuu, kuna sehemu nimeona watu wanapiga picha za video ambazo ni nyeti sana hivyo kukiwa na udhibiti fulani kutasaidia.

Picha za kuwapokea watu na shughuli zingine za kawaida si mbaya.

Wahusika wanosoma hapa wananielewa.
 
Picha kupiga ni moja ya kujitangaza na kutoa sifa ya uwanja, ndio maana unaona kuna viwanja bora duniani na hadhi zake
Viwanja vyote duniani vipo kwenye google mpaka ndani na nje ya uwanja
Sasa tutajuaje kuna uwanja mzuri umejengwa huko kama hatuoni picha
Hayo mambo ya kizamani sana
 
Angalia National discovery channel utaona video za viwanja dubai wanaonesha sehemu zote zinazowezekana kuoneshwa. Ni aina mojawapo ya kuvutia wageni.

Nilwahi kuona video ya uwanja wa Murtala Mohamed Lagos sikupapenda kabisa japo nilikuwa naenda huko. Ingekuwa bila ulazima ningechana tiketi.
 
We jamaa asee dah! Hivi unadhani kwa teknolojia ya sasa hivi mtu akitaka chochote kutoka popote atahitaji picha kutoka kwenye simu yako? Unahisi wakitaka kufanya jambo hawawezi sababu hawana picha hadi wamtume mtu akapige picha kwa kutumia simu.

Vijana sijui kuna shida gani yaani. Kwanini mnakuwa na akili/roho za chuki na sumu kiasi hiki asee, haya maisha tayari ni magumu sana lakini hamridhiki bado mnataka kuongeza ugumu wa maisha tu. Kila mahali kukiwa na masharti na ugumu ndio utapata furaha? Kupiga picha airport kuna shida gani (Tusi) wewe? Unaona huu uwanja ni wa ajabu sana eeenh? Viwanja vikubwa mara elfu zaidi ya huo duniani watu wanapiga picha tu ndio ije kuwa huu uwanja wetu asee?

We jamaa bure kabisa. Kiufupi UNA ROHO MBAYA!
 
Back
Top Bottom