Serikali ipi imehamia Dodoma?

Serikali ipi imehamia Dodoma?

Dodoma kuifikia dar itachukua muda sana
 
Wabunge karibia wote wapo Dar, majimboni wanaenda tu kusalimia.

Serikali kuhamia Dodoma ni mkakati wa kiupigaji vile kuna fungu flani hivi litafichwa kwa kivuli cha kuhama.
 
Huko dodoma upepo wa bahari unafika? achaneni na hii biashara ya kuhamia dodoma hali ya hewa siyo rafiki labda wapande miti ya kutosha.
 
Mkuu kiuhalisia jamaa amekurupuka na kama ilivyokawaida ya yeye na waumini wake hatokubali asilani kuwa walikurupuka katika hili.

Nakumbuka kuna mwanajukwaa humu alishawahi kuanisha kuwa kuhamia dodoma serikali isingefanya pupa.

Ingelifanya swala hili kuwa la kitaifa na kimkakati zaidi na kuhamia Dodoma kungefanyika kwa awamu mathali wizara mbili zinahamia huko kwa kila baada ya miaka miatano, kwa mfano ingeanza wizara ya ardhi nyumba na makazi hii ingehamia dodoma na kuanza kuandaa ramani na kupima viwanja vya jiji zima la Dodoma.
Kisha inafuatia wizara ya nishati na maji, kisha wizara ya TAMISEMI nakadhalika na kadhalika....

Tujifunze kufanya mambo kwa awamu maana hata M/mungu hakushinda kuiumba Dunia na vilivyomo kwa siku moja bali aliumba kwa siku sita na siku ya saba alipumzika hapa kuna hekima kubwa ya kujifunza kuwa tunapaswa kufanya mambo kwa hatua na sio kukurupuka
 
Kila siku mambo muhimu ya kiserikali yanafanyika Dar es Salaam, lakini tumeambiwa na kutangaziwa kuwa serikali na bwana mkubwa Rais wamehamia rasmi Dodoma.

Mawaziri wanaapishiwa Dar

Mabalozi wanaapishiwa Dar

Mabalozi wa kigeni wanawasilisha hati zao za viapo Dar

Rais muda wote yupo Dar

Mkataba wa Barrick a.k.a Acacia na Serikali/Twiga umesainiwa Ikulu Dar

Makamu wa Rais muda wote yupo Dar

Jaji Mkuu na viongozi wa vyombo vya usalama muda wote wapo Dar

Waziri Zungu karipoti Dar kwa ofisi ya Makamu wa Rais

Waziri Jafo naye yupo Dar

Mimi naomba kueleweshwa Dodoma wamehamia kina nani? Ni serikali ipi imehamia Dodoma?
Ni kweli mambo yanadaiwa kufanyika Dar kimtazamo lakini Dar inafanya hivyo kwa niaba ya Dodoma kimkakati zaidi uhalisia yanafanyika Dodoma, ni kukaimu tu.
 
Kwa mifumo ya mawasiliano E Gov , ugatuzi madaraka, mbali ya Wabunge nani Mtanzania anahitaji kufika wizarani kwa lipi!?Tumepoteza pesa bure maamuzi Dom, hapakuwa na uhitaji as planned earlier.

Sent using Jamii Forums mobile app
Pesa ipi imepotea? Pesa zote wanakula CCM sema pesa inaliwa na CCM siyo kupotea bure hata kukomaa Dsm hukaa ili walipane posho ya Safari
 
Nivigumu sana ikulu kuwa Dodoma. Magogoni ni rahc ku escape. Sasa kule kwa wagogo njia ni mbili2 anga na nchi kavu

system error occurred
Magogoni ni rahisi kuuawa kwani wazungu wakituma nyambizi submarine na drone zao ni rahisi kuleta maafa kisha wakatokomea baharini, Dodoma pako salama kuliko hapo Dsm
 
Ni kweli mambo yanadaiwa kufanyika Dar kimtazamo lakini Dar inafanya hivyo kwa niaba ya Dodoma kimkakati zaidi uhalisia yanafanyika Dodoma, ni kukaimu tu.
Kiserikali ukisafiri mkoani unalipwa posho ya Safari , sasa wanajilipa posho kwa kusafiri toka Dodoma kwenda hapo Dsm ni matumizi mabaya ya pesa za umma
 
Kuna nchi nyingi zenye pwani ya Bahari lkn Ikulu zao zipo bara. Mfano Kenya, Nigeria, Ivory Coast, South Africa etc. Bongo tu ndio kuna matishio?
Bongo pwani ndiko si salama kuliko huko mkoani
 
Hivi Dar ni mji nao wa kupiga tambo? Ukitoka kijijini lazima ushangae kila kitu ukifika Dar. Mji kama Lusaka tu upo mbali sana kuliko huo uchafu Dar es salaam! Watu wamerundikana kama mizigo kwenye hizo squatters, maisha gani hayo? Mji gani huo? MTU anayeona Dar ni jiji LA kusifiaaa hana exposure.

Sawa lakin kwa Tanzania Daslama mwisho wa matatizo yan tusidanganyane kila kitu kikubwa kiko dar ? kwan sehemu gani hakuna squatters ? ...Lusaka sasa ndio kuna nini ? Yan Lusaka nayo ni yakuisema na Dubai utasemaje ? Mkuu sasa nkwambie kitu kweli tunaweza kuwa tunatokea bush na vitu kama ivyo ila tunajua miji mikubwa duniani, narudia tena Mangufuli akihamia dodoma nami nakuja, .. Maswali ya msingi Pamoja na joto lote na uchafu wote ulosema upo dar, kwanini mji kila siku watu wanaongezeka ? wanapenda huo uchafu na skuata ? kwanini ndio sehemu yenye watu wengi kuliko sehemu nyingine yoyote Tanzania ? dont take things personal mkuu Dar es Salaam kwa Tanzania Hakuna.....


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Kila siku mambo muhimu ya kiserikali yanafanyika Dar es Salaam, lakini tumeambiwa na kutangaziwa kuwa serikali na bwana mkubwa Rais wamehamia rasmi Dodoma.

Mawaziri wanaapishiwa Dar

Mabalozi wanaapishiwa Dar

Mabalozi wa kigeni wanawasilisha hati zao za viapo Dar

Rais muda wote yupo Dar

Mkataba wa Barrick a.k.a Acacia na Serikali/Twiga umesainiwa Ikulu Dar

Makamu wa Rais muda wote yupo Dar

Jaji Mkuu na viongozi wa vyombo vya usalama muda wote wapo Dar

Waziri Zungu karipoti Dar kwa ofisi ya Makamu wa Rais

Waziri Jafo naye yupo Dar

Mimi naomba kueleweshwa Dodoma wamehamia kina nani? Ni serikali ipi imehamia Dodoma?
Kuhamia Dodoma ni "easier said than done".

Ni ujinga unaotuadhiri kwa namna mbili.

Tumetumia hela nyingi katika mpango wa kuhama, halafu hata baada ya kutumia hela nyingi, hatuhami.

Zaidi, kama nchi yenye mambo mengi ya kufanya na pesa chache kuliko mahitaji, uamuzi wa kuhama umeondoa pesa bila sababu ya lazima kwenye mipango mingine yenye umuhimu zaidi na ulazima wa wazi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
tulia kidogo. Ikulu bado haijakamilika, pia na taasisi za ulinzi na usalama hazijakamilika (miundombinu ya Jeshi, polisi, mahakama, magereza nk).


Amiri Jeshi mkuu awezi kuhama hama tu kama mtu muha anatoka ujiji ana kuja dodoma!

Rais ni nchi, ni mamlaka, ni tunu, ni ngao.


kwa wale wa dodoma.

tunajua kabisa. Serikali nzima ipo dodoma. mawaziri wote, DPP, IGP, Mkuu wa majeshi,, makatibu wakuu nk. wapo dodoma.
 
Back
Top Bottom