Serikali inamuogopa Lissu?

Kamanda

Senior Member
Dec 5, 2007
150
176
Kutokamatwa kwa Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu na kufikishwa kortini, kumemtia hofu Hakimu Mkuu wa Mahakama ya Kisutu, Thomas Simba, kwamba serikali inamuogopa.

Hakimu Simba ameielezea hofu hiyo leo mchana wakati akiendelea kusikiliza kesi inayomkabili Lissu na mmiliki na mhariri mtendaji wa gazeti la Mawio, Simon Mkina, mhariri wake Jabir Idrissa na mchapishaji wa gazeti hilo Ismail Mahbood.

"Hivi Lissu hapa ameletwa chini ya Polisi au kajileta mwenyewe? Mbona hamjamkamata au mnataka mie nitoe uamuzi wa kumfutia dhamana wakati hamjatekeleza wajibu wenu? Simfutii," alisema Hakimu Simba.

Serikali, kupitia Polisi haikumkamata Lissu kama ilivyokuwa imeamuriwa na mahakama baada ya kusindwa kufika mahakamani hapo kwa kesi inayomkabili.

Akaongeza, mahakama kamwe haimuogopi Lissu, lakini inaonekana serikali inamuogopo mbunge huyo na mwanasheria mkuu wa Chadema.

Lissu, Mkina na wenzake wanakabiliwa na kesi ya uchochezi ambayo ilifunguliwa na serikali tangu Juni, mwaka huu. Gazeti la Mawio lilifutwa na serikali kwa tamko la waziri wenye dhamana ya habari, Nape Nnauye, Januari, mwaka huu, baada ya 'kuchongewa' kwa muda mrefu na aliyekuwa mkurugenzi wa idara ya habari, Maelezo, Assah Mwambene.
 
Mada zingine muangalie mahali pa kuandika.

Serikali yoyote Duniani huwa haimuogopi yoyote yule akiwa amevunja sheria.

Avunje sheria aone Serikali mnayosema inamuogopa itakapo mshughulikia
 
hayupo aliye juu ya sheria,kutojua sheria isiwe sababu ya kuvunja sheria..T.A.Lissu anaifahamu sheria hadi sheria ikamfahamu,na anafanya hivyo kwa sababu anajua anacheza na watu wa aina ga..kwa kifupi,hao wanamuhaha mshikaji..watamwanzia wap?
 
Hivi mnazijua serikali za nchi za Africa?

Eti serikali inamuoga Lissu.

Kumbe serikali inapompuuza mnadhani inamuoga?

Lissu hajakatiza kwenye utepe unaitwa red line ndiyo maana mnadhani serikali inamuogopa. Siku akikatiza ndio mtapata jibu sahihi.

Ninachompongeza Lissu ni kufahamu vizuri wapi kuna red line na kwa kufanya hivyo anacheza pembeni pembeni bila kukatiza.
 
Hivi mnazijua serikali za nchi za Africa?

Eti serikali inamuoga Lissu.

Kumbe serikali inapompuuza mnadhani inamuoga?

Lissu hajakatiza kwenye utepe unaitwa red line ndiyo maana mnadhani serikali inamuogopa. Siku akikatiza ndio mtapata jibu sahihi.

Ninachompongeza Lissu ni kufahamu vizuri wapi kuna red line na kwa kufanya hivyo anacheza pembeni pembeni bila kukatiza.
Unaongea na sisi au unaongea na simu?
 
hayupo aliye juu ya sheria,kutojua sheria isiwe sababu ya kuvunja sheria..T.A.Lissu anaifahamu sheria hadi sheria ikamfahamu,na anafanya hivyo kwa sababu anajua anacheza na watu wa aina ga..kwa kifupi,hao wanamuhaha mshikaji..watamwanzia wap?
Rais Magufuli yuko juu ya sheria
 
Kutokamatwa kwa Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu na kufikishwa kortini, kumemtia hofu Hakimu Mkuu wa Mahakama ya Kisutu, Thomas Simba, kwamba serikali inamuogopa.

Hakimu Simba ameielezea hofu hiyo leo mchana wakati akiendelea kusikiliza kesi inayomkabili Lissu na mmiliki na mhariri mtendaji wa gazeti la Mawio, Simon Mkina, mhariri wake Jabir Idrissa na mchapishaji wa gazeti hilo Ismail Mahbood.

"Hivi Lissu hapa ameletwa chini ya Polisi au kajileta mwenyewe? Mbona hamjamkamata au mnataka mie nitoe uamuzi wa kumfutia dhamana wakati hamjatekeleza wajibu wenu? Simfutii," alisema Hakimu Simba.

Serikali, kupitia Polisi haikumkamata Lissu kama ilivyokuwa imeamuriwa na mahakama baada ya kusindwa kufika mahakamani hapo kwa kesi inayomkabili.

Akaongeza, mahakama kamwe haimuogopi Lissu, lakini inaonekana serikali inamuogopo mbunge huyo na mwanasheria mkuu wa Chadema.

Lissu, Mkina na wenzake wanakabiliwa na kesi ya uchochezi ambayo ilifunguliwa na serikali tangu Juni, mwaka huu. Gazeti la Mawio lilifutwa na serikali kwa tamko la waziri wenye dhamana ya habari, Nape Nnauye, Januari, mwaka huu, baada ya 'kuchongewa' kwa muda mrefu na aliyekuwa mkurugenzi wa idara ya habari, Maelezo, Assah Mwambene.
Hizi ni akili za kitoto sana eti serikali inamuogopa Lisu. Kweli vijana siasa zinawauwa kufikiri na sasa sio tena great thinkers maybe mmekuwa stupid thinkers. Leteni hoja za msingi hizi za kipuuzi wanazungumza watu amboa sio great thinkers.
 
..huyo hakimu inaelekea ni mkereketwa wa chama.

..suala la msingi ni kuwa Tundu Lissu amefika mahakamani.

..kwamba amefikishwa mahakamani na polisi au kwa hiari yake mwenyewe siyo hoja ya msingi.
 
Hizi ni akili za kitoto sana eti serikali inamuogopa Lisu. Kweli vijana siasa zinawauwa kufikiri na sasa sio tena great thinkers maybe mmekuwa stupid thinkers. Leteni hoja za msingi hizi za kipuuzi wanazungumza watu amboa sio great thinkers.
Serikali na watawala na wenye mamlaka wanaogopa kifo walivyo wajinga. Werevu wana Muogopa mwenye haki tu.nashangaa wajinga kusema hakuna alive juu ya sheria.Mwenye HAKI yupo juu ya sheria zaidi hata ya Rais na wafalme.
 
Back
Top Bottom