Halafu kumbe mzee wa watu huyu alikuwa amelazwa kwenye hospitali ya private iitwayo KAM huko Arusha kwa karibu wiki mbili, na leo ndio ameondoka kwenda India kwa matibabu. Amefuatana na kiongozi mmoja wa BAKWATA na daktari anayemtibu (Dr Peter Mhando wa hospitali hiyo ya KAM), na bila shaka ni kwa gharama zake au za BAKWATA. Sasa sijui huu udaku wa kuwa kuwa yuko India na anatibiwa na serikali (na watu wakazua malalamiko kibao yasiyo na msingi) umetoka wapi?
Ingawa amechagua kutibiwa kwenye hospitali binafsi huko Arusha na baadae kwenda nje ya nchi kwa gharama zake, bado ikumbukwe ni wajibu wa serikali kugharamia matibabu ya wananchi wake wanaopewa rufaa za kwenda kutibiwa nje ya nchi(ikiwa rufaa hiyo imetokana na maoni ya kitaalamu na si matashi binafsi ya mgonjwa kwenda kutibiwa nje).
Na ushauri kwa wanachama wenzangu hapa JF, habari zenye mwelekeo wa kizushi ziwe zinakemewa inapogundulika kuwa habari hiyo ni uzushi. Wahusika wa habari kama hizo pia wanaweza kuomba radhi wenyewe (ikiwa walipotoshwa/walipotoka), la sivyo moderators muwe mnawakemea maana mambo kama haya ndio yanayoathiri hadhi ya jukwaa letu hili tukufu.
Ingawa amechagua kutibiwa kwenye hospitali binafsi huko Arusha na baadae kwenda nje ya nchi kwa gharama zake, bado ikumbukwe ni wajibu wa serikali kugharamia matibabu ya wananchi wake wanaopewa rufaa za kwenda kutibiwa nje ya nchi(ikiwa rufaa hiyo imetokana na maoni ya kitaalamu na si matashi binafsi ya mgonjwa kwenda kutibiwa nje).
Na ushauri kwa wanachama wenzangu hapa JF, habari zenye mwelekeo wa kizushi ziwe zinakemewa inapogundulika kuwa habari hiyo ni uzushi. Wahusika wa habari kama hizo pia wanaweza kuomba radhi wenyewe (ikiwa walipotoshwa/walipotoka), la sivyo moderators muwe mnawakemea maana mambo kama haya ndio yanayoathiri hadhi ya jukwaa letu hili tukufu.