Nafikiri techolojia nayo itasababisha benki wahitaji wafanyakazi wachache, nilipokuwa majuu kuna branch unakuta ina mtu mmoja tu kwa ajili ya shughuli za customer service. Ukitaka kutoa, kuweka pesa, kuhamisha, kufanya malipo wanatumia ATM machine au internet banking. Sijajua kwa nini internet banking bado haijafika bongo, lakini akaunti yangu niliyokuwa natumia nje nilikuwa naweza kuingia, kutazama salio, kuhamisha pesa yaani sikuwahi kabisa kurudi ndani ya benki baada ya kufungua....kuna siku niliingia branch kuweka pesa wakanirudisha kwenye ATM wakanielekeza namna ya ku- deposit kwa kutumia ATM...