Jidu La Mabambasi
JF-Expert Member
- Oct 20, 2014
- 15,327
- 24,209
Huduma za bodaboda na bajaj nchini zimechukuliwa kuwa za kisiasa zaidi kuliko kuwa huduma inayo hitaji udhibiti kimamilifu kwama vyombo vingine vya moto.
Kinachosikitisha zaidi ni hata vyombo vya udhibiti kisheria kama Polisi, ni kama wako paralysed kutatua matatizo ya vyombo hivi.
Wanasiasa kwa kutoelewa wamechukulia huduma ya bajaj na bodaboda kuwa mtaji wa kisiasa, na hata Rais Samia amediriki kuwaita ati ni maafisa usafirishaji.
Mimi sipingi kuweo kwao usafiri huu, bali nakomalia UDHIBITI wa huduma yao.
Matatizo makubwa yako hivi
1. Hawafuati sheria za barabarani tena wote, bodaboda na bajaj
2 wanapakia abiria kupita uwezo wa chombo
3. Bodaboda hawavai safety helmets, viatu na jackets
4. Bajaj na bodaboda chafu kuruhusiwa kungia katikati ya Jiji
5.Vyomb hivyo kuendeshwa kwa spidi kubwa katikati ya Jiji
6. Polisi hawana uwezo wa kuwachukulia hatua yoyote, hata wakifanya kosa mbele ya pua zao
7. Bodaboda kupakia kama abiria hata watoto wadogo sana wasio na uwezo kujishikilia
8. Bodaboda au bajaj ku overtake kushoto mwa gari iliyoko mbele yake
9. Baja na bodaboda kuendesha kinyume ya maelekezo ya barabara, yaani nchi hii ni Left Hand Drive, utaona wao wanakuja mbele yako wakiendesha Right Hand Drive.
10 Baja na bodaboda kuendesha hata sehemu za waenda kwa miguu.
Haya ni machache tunayoyaona kwa hawa maafisa safirishaji wa kisiasa.
Matokeo yake, kukiuka sheria za barabarani kwa makusudi kabisa, nenda MOI Muhimbili na kushuhudia miguu inayokatwa kila siku.
SERIKALI amkeni, mnatuletea janga la wananchi vilema.
Polisi wanaweza kulishughulikia tatizo hilo, kama serikali ikiondoa ganzi iliyowapiga kisiasa kuwaachia hawa watu waendelee kuua/kujiua barabarani.
NB
Shiriki kura hapo juu