Meneja Wa Makampuni
JF-Expert Member
- Jul 7, 2020
- 9,281
- 12,249
Kisheria, raia wa kigeni hawaruhusiwi kufanya biashara za rejareja (kama kuwa na fremu/store Kariakoo) kwa sababu hizo ni biashara zilizotengwa kwa Watanzania chini ya Sera ya Uwekezaji na Sheria ya Ajira na Kazi Tanzania. Kwa hiyo, mgeni anapofungua store Kariakoo kuuza bidhaa moja kwa moja kwa wateja, anakiuka sheria na anashindana moja kwa moja na mfanyabiashara wa Kitanzania ambaye kisheria ndiye anayestahili nafasi hiyo.Winga anapata shida gani mchina akiwa na store kariakoo hebu tupe point moja
Huu sio ushindani wa haki. Mchina ana mtaji mkubwa, anaagiza bidhaa moja kwa moja kutoka viwandani kwao kwa bei ya chini, hana mzigo mkubwa wa tozo kama wazawa, na mara nyingi huwa anatumia mbinu zisizo rasmi kutoroka kodi. Mwisho wa siku, winga wa Kariakoo anashindwa kuuza, faida inaporomoka, na hata kulipa kodi au kodi ya fremu kwake inakuwa ngumu. Hapo ndipo shida inapoanzia si chuki, ni uhalisia wa kiuchumi na kisheria.