Serikali iangalie namna ya kuwasaidia vijana moja kwa moja. Athari za baadaye ni kubwa zaidi

Bushmamy

JF-Expert Member
Aug 18, 2019
8,848
15,253
Hali ya maisha imewachanganya vijana wengi, mazingira na hali sio rafiki kwa biashara, Ajira na zenyewe hakuna.

Vijana wamesoma na sasa wameishia mitaani, nguvu ya wazazi nayo imeishia hapo, serikali nayo imeishia hapo, kwanini kijana asichanganyikiwe.

Ongezeko la watoto wa mtaani nao ni zao la vijana ambao wapo kwenye kundi hili hapo juu kutokana na Kukosekana kwa maadili pamoja na familia bora yenye uchumi thabiti.

Ulevi wa kupindukia, wizi, utapeli, kubeti, kamari na michezo mingine michafu limekuwa kimbilio la vijana wengi wasomi kama njia mojawapo ya kujipa furaha na kuondoa msongo wa mawazo.

Pamoja na mambo mengine mengi kukosekana kwa mfumo rasmi wa maisha juu ya vijana wetu ndio chanzo kikuu cha uovu unaendelea hivi sasa, kama vile ulawiti, ubakaji, mauaji pamoja na kuongezeka kwa wagonjwa wa akili.

Ukipita mitaani unaona vijana wasomi wanavyolewa pombe, mataptap, na kufanya vituko mitaani unabaki kusikitika tu!
 
Kama biashara sio rafiki mbona maduka hayajafungwa? Mbona Vijana wanaambiw wajiung vikundi wakopeshwe mitambo bila riba hawataki, kuna 30% ya Kaz za ujenzi zinatengwa Kwa Ajili Yao hawaelewi na namna nyingine nyingi za kuwawezesha.

Hakuna serikali itagawia pesa Vijana,wasiotaka kuwajibik Dunia itawawajibisha..

Kuna mafunzo ya ufundi uanagenzi hutolewa Bure Kwa miezi 3 mtu anafundishwa Kaz haelewi
 
Kama biashara sio rafiki mbona maduka hayajafungwa? Mbona Vijana wanaambiw wajiung vikundi wakopeshwe mitambo bila riba hawataki,Kuna 30% ya Kaz za ujenzi zinatengwa Kwa Ajili Yao hawaelewi na namna nyingine nyingi za kuwawezesha..

Hakuna serikali itagawia pesa Vijana,wasiotaka kuwajibik Dunia itawawajibisha..

Kuna mafunzo ya ufundi uanagenzi hutolewa Bure Kwa miezi 3 mtu anafundishwa Kaz haelewi
Yanapatikana wapi haya, hasa hlo la mwisho.
 
Yanapatikana wapi haya, hasa hlo la mwisho.
Sas watu mnashinda Kubet unataka nani awatafutie fursa? Saiz tuu pm amezindua mfuko wa kukopesha Vijana ila mko busy TikTok, whatsup na upuuzi mwingine badala ya kutafuta fursa..

Kwenye Kaz zote za ujenzi za TanRoads na Tarura wanatengwa Asilimia 30% Kwa Ajili ya makundi maalumu ya vijana,wamama na walemavu..

Utaratibu ni ule ule lazima usajili kikundi chako au kampuni Yako na kusajili Wala hakuna gharama zozote..

Kuna Kaz za kusafisha mitaro,kufagia,kuchimba mifereji,ujenzi mdogo mdogo nk nk

Halmashauri pia zinatoka hizo pesa tena huko naona ni rahisi mnaweza buni mradi wa tofali wakawanunulia mashine na wao ndio wakawa wateja maana wanajenga Kila siku
 
Sas watu mnashinda Kubet unataka nani awatafutie fursa? Saiz tuu pm amezindua mfuko wa kukopesha Vijana ila mko busy TikTok, whatsup na upuuzi mwingine badala ya kutafuta fursa..

Kwenye Kaz zote za ujenzi za TanRoads na Tarura wanatengwa Asilimia 30% Kwa Ajili ya makundi maalumu ya vijana,wamama na walemavu..

Utaratibu ni ule ule lazima usajili kikundi chako au kampuni Yako na kusajili Wala hakuna gharama zozote..

Kuna Kaz za kusafisha mitaro,kufagia,kuchimba mifereji,ujenzi mdogo mdogo nk nk

Halmashauri pia zinatoka hizo pesa tena huko naona ni rahisi mnaweza buni mradi wa tofali wakawanunulia mashine na wao ndio wakawa wateja maana wanajenga Kila siku
Acha kelele hakuna chochote hapo kinafanyika zaidi ya mboyoyo.

Hela wanagaiana wao kwa wao na vikundi ni vyao,hakuna kitu yoyote utapata hapo zaidi ya commission za watu.

Unasema watu wanafundishwa kuchimba mtaro??,usafi?? Hebu kuwa serious
 
Kama biashara sio rafiki mbona maduka hayajafungwa? Mbona Vijana wanaambiw wajiung vikundi wakopeshwe mitambo bila riba hawataki,Kuna 30% ya Kaz za ujenzi zinatengwa Kwa Ajili Yao hawaelewi na namna nyingine nyingi za kuwawezesha..

Hakuna serikali itagawia pesa Vijana,wasiotaka kuwajibik Dunia itawawajibisha..

Kuna mafunzo ya ufundi uanagenzi hutolewa Bure Kwa miezi 3 mtu anafundishwa Kaz haelewi
We hyo mikopo watu wanaomba kila kukicha halamshauri huko wanapeana kwa connection. ..

Game sio easy hvo hakuna mtu atakaa asitale kuchakarika wakat wenzio aliosoma nao wanasukuma FORESTER
 
Acha kelele hakuna chochote hapo kinafanyika zaidi ya mboyoyo.

Hela wanagaiana wao kwa wao na vikundi ni vyao,hakuna kitu yoyote utapata hapo zaidi ya commission za watu.

Unasema watu wanafundishwa kuchimba mtaro??,usafi?? Hebu kuwa serious
Huyu jamaakatumwa huyu hayupo Ground anaropoka tu hapa hyo mikopo waty wanaomba mara kumi kumi hawapewi kwa sababu z akijinga tu
 
We hyo mikopo watu wanaomba kila kukicha halamshauri huko wanapeana kwa connection. ..

Game sio easy hvo hakuna mtu atakaa asitale kuchakarika wakat wenzio aliosoma nao wanasukuma FORESTER
Acha uongo wewe,Kuna Halykibao wanasema Vijana hawajitokezi,harafu sio pesa za kugawa ni pesa za biashara.
 
Acha kelele hakuna chochote hapo kinafanyika zaidi ya mboyoyo.

Hela wanagaiana wao kwa wao na vikundi ni vyao,hakuna kitu yoyote utapata hapo zaidi ya commission za watu.

Unasema watu wanafundishwa kuchimba mtaro??,usafi?? Hebu kuwa serious
Endelea kulalamika basi naona unajua wanavyogawiana ila huna ufumbuzi 🤪🤪🤪🤪

Narudia tena pesa hazigawiwi ni mkopo wa biashara
 
Sas watu mnashinda Kubet unataka nani awatafutie fursa? Saiz tuu pm amezindua mfuko wa kukopesha Vijana ila mko busy TikTok, whatsup na upuuzi mwingine badala ya kutafuta fursa..

Kwenye Kaz zote za ujenzi za TanRoads na Tarura wanatengwa Asilimia 30% Kwa Ajili ya makundi maalumu ya vijana,wamama na walemavu..

Utaratibu ni ule ule lazima usajili kikundi chako au kampuni Yako na kusajili Wala hakuna gharama zozote..

Kuna Kaz za kusafisha mitaro,kufagia,kuchimba mifereji,ujenzi mdogo mdogo nk nk

Halmashauri pia zinatoka hizo pesa tena huko naona ni rahisi mnaweza buni mradi wa tofali wakawanunulia mashine na wao ndio wakawa wateja maana wanajenga Kila siku
Hayo mambo ya kukopesha vijana ni utapeli mkuu hayana ukwel wowote
 
Kimsingi tatizo liko hata kwa hao vijana wenyewe wanaamka watu kuwatetea kwamba ajira uchwara kama bodaboda ni upuuzi, wanakuja juu, uliona wapi graduate anaendesha bodaboda na anaona ni haki yake kabisa na ni halali yeye kuwa hivyo? watawala wamehakikisha hao vijana hawana tena uwezo wa kufikiri, reasoning imekuwa ya chini kiasi kwamba hawajielewi tena, na hii inawafurahisha sana watawala kwakuwa wanajua kwa mavijana ya namna hii wataendelea kutawala milele.
 
Kama biashara sio rafiki mbona maduka hayajafungwa? Mbona Vijana wanaambiw wajiung vikundi wakopeshwe mitambo bila riba hawataki, kuna 30% ya Kaz za ujenzi zinatengwa Kwa Ajili Yao hawaelewi na namna nyingine nyingi za kuwawezesha.

Hakuna serikali itagawia pesa Vijana,wasiotaka kuwajibik Dunia itawawajibisha..

Kuna mafunzo ya ufundi uanagenzi hutolewa Bure Kwa miezi 3 mtu anafundishwa Kaz haelewi
kweli kabisa, Uanajenzi, hawaendi wanaenda wachache tu, mpaka wamepunguza vituo, na Sasa Kuna mikopo ya riba nafuu crdb, Kama wataenda, ajira zikitoka utasikia zinawenyewe za kujuana zile.
 
Back
Top Bottom