Muda huu nipo kituoni nikisubiri kuandikishwa kwenye BVR. Hili ni jaribio langu la nne. Uandikishaji ulianza tarehe 09/06/2015 na siku ya kwanza nilienda kituoni nikapewa na 56 mashine iliandikisha watu 42 tu, tar 10/06 /2015 mashine iliandikisha watu 79, nikiwahi kituoni watu walikataa kututambua sisi tuliobaki Jana yake.
Tar 11/06 /2015 niliamka saa 8 usiku na kuwahi kituoni nikapewa na 64. Mashine iliandikisha watu 40 hadi saa 7 ikazima sikuweza kuandikishwa.
Leo nimefika kituoni saa 9 alfajiri na nimepewa na 86. Sijui kama leo nitaandikishwa. Nipo kituo cha Nyanza kata ya Mkolani wilaya ya Nyamagana.
Mtaa wetu una watu si chini ya 1500 wenye sifa za kuandikishwa lakini tija na ufanisi wa kuandikisha ni duni. Mwamko wa watu kujiandikisha upo juu na wamejitokeza kwa wingi lakini vitendea kazi na watenda kazi hakuna. Lengo la serikali ni nini?