Serikali 3 na gharama zake

Serikali 3 na gharama zake

Sheikh Ngruvi3 naona bado "hujanfahamu": mimi siungi mkono "udhalimu" wa Zenj dhidi ya Tanganyika.
Mimi ni muumini wa Muungano. Hofu yangu ni kwamba tukiwa na 3 basi muungano utakufa.
Ninaunga mkono 2 (zisizo na unyonyaji) kama "transitory process towards 1". Naamini baada ya miaka mingi ijayo ndoto hiyo itatimia...baada ya wale wenye "uchu wa madaraka" (kama waitwavyo) na wale "wenye uchungu sana na mapinduzi daima" kuwa wamepisha kizazi kingine ambacho kitajali zaidi maendeleo kwa wananchi kuliko historia.


Ila, kama plan B, ikiwa tumeshindwa kuafikiana kwa 2 au 3, tutafute namna ya kuachana kwa amani. Tujipe kama miaka 10 kama twataka Muungano na kwa muundo upi. Tutaachana kwa kura ya maoni kwa wananchi, na tujiulize baadaye kwa kura ya maoni kama twataka kuungana tena kwa mtindo upi. Katika kipindi hicho cha miaka 10 kila upande uendeshe mambo yake na baada ya miaka 10 iitishwe kura ya maoni.
Hili la kuelekea S1 dah ni ndoto ninayoomba nisiiote maana naweza kuamka kichwa kikuma. Mwaka 1985 tulijiita Watanzania, leo kuna Watanzania na Wazanzibar.
Mwaka 1990 tulikuwa na mambo 22, leo yanaitwa unyonyaji tunataka yapungue.
Mwaka 200 tulikuwa na katiba ya JMT, leo kuna katiba ya JMT na Katiba kuu ya JMTZNZ
Ndoto hizo mungu aniepushe nazo.

Hapo mwisho umemealizia vizuri sana, hata mimi nashauri tuvunje jahazi tugawane mbao.
Hatuna sababu za kuungana twaweza ishi kama tuishivo na Msumbiji.

Mimi sioni tabu hata kidogo wznz wakiondoka zao. Na sioni kama kuna Mtanganyika anayeona tabu isipokuwa wale watu wanaoona haya dhidi ya Utaifa wao.

Yule kichwa panzi wa BB-zanzibar kasema, znz itastawi kutokana na misaada kwasababu ni kisiwa kidogo.

Hapa JF wapo wanaodhani znz ni bora ikipata misaada, na hata kudhani misaada ni jambo la fahati! phwe
Wapo wanaodhani znz inahitaji kiti IMF, WB ili itambulike
Watanganyika wanasema waacheni wapate vitu hivyo, na wala wasisumbuliwe.

Tusichotaka kusikia ni kasehemu kadogo kakichukua kodi za Watanganyika, kuchangia zero na kulalamika 100%
Itafika mahali wznz wanalala tu, kwasababu Watanganyika wanawalipia kodi. Upuuzi huo sasa mwisho.
 
Kobello
Mwisho, Mfuko wa pamoja hauhitaji idadi ya serikali kuongezeka ama kupungua. Tunaweza unda mfuko wa pamoja ktk seirklai 1 2 ama 3 isipokuwa tutazame nini haswa tulipotaka kuelekea ktk Muungano wetu ambao hauhusiani kabisa na wingi wa serikali bali UMOJA wetu na mshikamano. Sidhani kama serikali 3 ni suluhisho la kuunda mfuko wa pamoja ila ni kuleta matatizo mengine ambayo hayakuwepo.

•Mfuko wa pamoja baina ya Nani na Nani?

•Mfuko wa pamoja nia yake ni kitu gani?

• Mfuko wa pamoja unaelezwa vipi kwa Mujibu wa Sheria?

Katika mfuko wa pamoja, ebu tufanyie mchanganuo wa:
1. Mapato.
2. Matumizi.
3 Mgawanyo.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Mkuu that is a fact, ndio maana ukiangalia post zangu zote mimi naelekea zaidi kwenye serikali moja ya Tanzania. Mara kadhaa nimesikia serikali ya Zanzibar inaomba hela kwa Bakhresa kulipa mishahara wafanyakazi wa serikali, hii inaonesha kabisa kuwa bado hakuna uwezo wa kuendesha serikali makini.
Mkuu nakubaliana sana na serikali 1 lakini je hatutaimeza Zanzibar maana tayari hili neno lipo midomoni mwa watu na linaweza kuzua balaa baadaye. Inavyoonyesha kuunda serikali moja ni kama tunawalazimisha wananchi ambao kwa fikra zao ni kutogawana umaskini. nadhani umewahi kuona familia zetu zikigombania mirathi ukiwaambia mali iwe ya wote tugawane kazi kisha tugawane mapato, basi kila mmoja hata muamini mwenziwe kushika hatamu. Waafrika kiasili hatuaminiani!

Tatizo letu sisi waafrika ni kutojiamini maana kama Tanzania ingezaliwa na mkoloni kama ilivyokuwa Trinidad and Tobago basi usingeyasikia haya leo hii ya kumezana isipokuwa maadam walotuunganisha ni weusi kama sisi basi tutahoji uhalali wake kwa sababu hawa ni kama sisi walipata wapi ridhaa ya kuunganisha nchi. Mkoloni katugawa kwa sheria zake mwenyewe ndiye anaaminiwa kuliko sisi wenyewe maana tumesoma elimu yake na hivyo ndio kuelimika kwenyewe. Na ndio haya maswali yalowakuta viongozi na waasisi wetu ambao walijua wazi kwamba haya tuyaonayo leo yatakuja kutokea na yametokea kweli!
 
•Mfuko wa pamoja baina ya Nani na Nani?

•Mfuko wa pamoja nia yake ni kitu gani?

• Mfuko wa pamoja unaelezwa vipi kwa Mujibu wa Sheria?

Katika mfuko wa pamoja, ebu tufanyie mchanganuo wa:
1. Mapato.
2. Matumizi.
3 Mgawanyo.



Sent from my iPhone using JamiiForums
Mfuko wa pamoja ni Federal taxes revenue (mapato ya kodi ya Serikali kuu) wananchi watakuwa wakichangia mifuko miwili - wa nchi na ule wa Taifa, hivyo ningekuomba usome ama google neno Federal tax revenue kwa nchi nyinginezo utapata majibu yote maana mimi sii mwandishi mzuri sana.
 
Mfuko wa pamoja ni Federal taxes (kodi za Serikali kuu) hivyo ningekuomba usome ama google neno kwa nchi nyinginezo utapata majibu yote maana mimi sii mwandishi mzuri sana.

Kweli haya ni majibu serious kwa suala serious from mtu serious mkandara?


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Mchambuzi, nguruvi,

..labda mngeanza na kunyambulisha wizara za muungano, za tanganyika, na za zanzibar.

..pia mnyambulishe mamlaka na ngazi za utawala, pamoja na taasisi mbalimbali ktk serikali hizo.

..mkikuta kuna kitu/chombo chochote kipya, kwa maana hatunacho sasa hivi, basi mtaweza kusema gharama zimeongezeka.

..kwa upande wangu nadhani gharama hazitaongezeka sana, kwasababu kwa kiwango kikubwa uundwaji wa serikali ya Tanganyika, utahusisha kuondoa watendaji, majukumu, na madaraka fulani fulani toka serikali ya muungano ya sasa hivi.

NB:

..neno SERIKALI 3 linatumika kuwatisha tu wananchi. Tunatakiwa kusema tunaunda serikali ya Tanganyika.

cc Kobello, Bongolander, Mkandara, Mwanagenzi
 
Last edited by a moderator:
Kweli haya ni majibu serious kwa suala serious from mtu serious mkandara?


Sent from my iPhone using JamiiForums
Mkuu wangu sasa unataka kunambia mnataka serikali 3 pasipo kujua kwamba kuna lazima ya serikali kuu kuwa na mfuko wa pamoja kutokana na kodi zetu? Yaani serikali 3 pasipo kujua gharama zake kwa wananchi ndio maana mnabisha au?
 
Mfuko wa pamoja ni Federal taxes revenue (mapato ya kodi ya Serikali kuu) wananchi watakuwa wakichangia mifuko miwili - wa nchi na ule wa Taifa, hivyo ningekuomba usome ama google neno Federal tax revenue kwa nchi nyinginezo utapata majibu yote maana mimi sii mwandishi mzuri sana.
Hapanaa! hujajibu swali la msingi mkuu. Na hapa ndipo huwa nawa admire wewe na Kobello, ni mafundi wazuri sana wa kukwepa core issue na kuongelea future

Swali la msingi, mfuko wa pamoja kati ya nani na nani.
Halafu mfuko huo unaelezwajwe kwa mujibu wa sheria
Mtupe mchanganuo wa mapato, gharama na matumizi.

Mfuko huo ni wa S2 mnazopendekeza.

***Hapa hatuongelei future, mfuko upo ingaw haujafanya kazi. Hivyo tuelezeni katika mazingira hayo ya S2 kwa kuogopa S3 mnautendeaji haki mfuko.
Kobello karibu ili usije sahau mabandiko yakapita, ukaunga kwa mbele
 
Last edited by a moderator:
Mkuu wangu sasa unataka kunambia mnataka serikali 3 pasipo kujua kwamba kuna lazima ya serikali kuu kuwa na mfuko wa pamoja kutokana na kodi zetu? Yaani serikali 3 pasipo kujua gharama zake kwa wananchi ndio maana mnabisha au?
Swali lipo hapo juu, kwanza tujue kwa S2 mfuko huo unafanyaje kazi ili tushawishike kuwa hakuna sababu za S3? Mfuko umelalamikiwa kuwa haufanyi kazi. Upo kumbuka hivyo tunaongelea hali ya sasa na wala si S3.
 
Kweli haya ni majibu serious kwa suala serious from mtu serious mkandara?


Sent from my iPhone using JamiiForums
Mkuu ima hakuelewa swali au ameelewa lakini ni katika spinning.
Ni yale yale ya Kobello, nimemuuliza kuondoa mambo 15 katika muungano gharama gani zimeongezeka kwa TZ, nikajikuta naambiwa habari nyingine kabisa kuhusu climate change. I real admire these fox, ni wazuri sana wa spinning.
 
Mkuu ima hakuelewa swali au ameelewa lakini ni katika spinning.
Ni yale yale ya Kobello, nimemuuliza kuondoa mambo 15 katika muungano gharama gani zimeongezeka kwa TZ, nikajikuta naambiwa habari nyingine kabisa kuhusu climate change. I real admire these fox, ni wazuri sana wa spinning.
Nadhani hii issue ipo too complex kwako.Nilibishana sana na wewe kuhusu takwimu, na yanayozungumzwa na wataalam wengi, hata hao wajumbe wa tume ya katiba nadhani unayasikia ila sidhani kama itatosha. Nilibishana na wewe kwa mara ya kwanza kuhusu Dowans na yaliyotokea mlikaa kimya tu. Pia tulishaongea kidogo mambo ya gharama mkaahidi kuleta uzi special wa gharama baada ya bajeti kusomwa, sijui yameishia wapi?

Sasa ngija nikueleze kwa ufupi,

Ukiondoa mambo 15 ya muungano, haitamaanisha kuwa mambo hayo hayatashughulikiwa na muungano. Acha ubishi, hili jambo ni obvious na siyo theoretical ni mambo yanayoendelea kwenye Federations. Hata EU inashughulikia mabo mengine yasiyo kweny articles of association, sembuse Federation? Acha kudanganyika, kwenye federation huwezi kuondoa mambo yote yawe straight kutoka kwenye States.

Tanganyika haina SUMATRA,TRA,TBS,NBS ETC... kwa sasa hivi, ila ikianzishwa itabidi iwe nayo sambamba na serikali ya muungano. Halafu jaribu kuzungumzia mahakama pia, hapo tuache bunge la muungano ingawa najua gharama yake itakuwa almost nusu ya mapato ya Zanzibar kwa mwaka.

Itawachukua muda, ila mtaelewa tu na wala msijaribu kuniaminisha tofauti kwa sababu hiyo ni sawa na kumimina maji kwenye pakacha.
 
Hapanaa! hujajibu swali la msingi mkuu. Na hapa ndipo huwa nawa admire wewe na Kobello, ni mafundi wazuri sana wa kukwepa core issue na kuongelea future

Swali la msingi, mfuko wa pamoja kati ya nani na nani.
Halafu mfuko huo unaelezwajwe kwa mujibu wa sheria
Mtupe mchanganuo wa mapato, gharama na matumizi.

Mfuko huo ni wa S2 mnazopendekeza.

***Hapa hatuongelei future, mfuko upo ingaw haujafanya kazi. Hivyo tuelezeni katika mazingira hayo ya S2 kwa kuogopa S3 mnautendeaji haki mfuko.
Kobello karibu ili usije sahau mabandiko yakapita, ukaunga kwa mbele
Mfuko huo sasa hivi hautendewi haki kwa sababu haupo. Na sababu za kutokuwepo siyo utatanishi, bali ni kushindwa kwa Zanzibar kuulipia.Zanzibar hawalipi hata umeme, sembuse 5% ya 3trilion? Huo mfuko ni hekaya za Abunuasi.

Hii mada msiiharibu kwa ushabiki wenu wa kisiasa, mmekuwa challenged wewe na Mchambuzi kwa takriban miezi mitatu sasa na mnbashindwa kutimiza ahadi zenu. Leteni thread yenu ya gharama na pia mtupe data Zinazosema watu wengi wanataka S3. Hayo mambo ya siasa si muda wake.
 
Last edited by a moderator:
Mfuko huo sasa hivi hautendewi haki kwa sababu haupo. Na sababu za kutokuwepo siyo utatanishi, bali ni kushindwa kwa Zanzibar kuulipia.Zanzibar hawalipi hata umeme, sembuse 5% ya 3trilion? Huo mfuko ni hekaya za Abunuasi.

Hii mada msiiharibu kwa ushabiki wenu wa kisiasa, mmekuwa challenged wewe na Mchambuzi kwa takriban miezi mitatu sasa na mnbashindwa kutimiza ahadi zenu. Leteni thread yenu ya gharama na pia mtupe data Zinazosema watu wengi wanataka S3. Hayo mambo ya siasa si muda wake.

Sababu juu ya kwanini mfuko wa pamoja haufanyi kazi ni Kwamba ni Vigumu kutenganisha masuala ya Tanganyika na ya muungano. Kwa maana nyingine, mfuko wa pamoja ni hekaya za abunuwasi bila ya uwepo wa Tanganyika kwani ni impossible kubaini ya pamoja ni yepi na ya kila upande kivyake ni yepi chini ya serikali Mbili. Ni Vigumu kuelewa kwanini watu makini Kama wewe na Mkandara mnashindwa ona Hilo.

Na sasa, uwepo wa nchi Mbili serikali Mbili Ndio umeua Kabisa hata hiyo ndoto ya joint finance commission. Nyinyi Hali hii inazidi kuwapa matumaini Kwamba JFC can work, na pia Kwamba serikali moja inawezekana, na several other impractical and utopian views.

Uzi wa gharama tulio ahidi upo pale pale, hakuna kilichobadilika zaidi ya suala la timing kutokana na mchakato mzima wa BLK kuingia nyongo. Vinginevyo maandalizi yapo pale pale na Uzi utapanda ndani ya siku Tatu na utaweka sawa masuala mengi ambayo mmekuwa mnayakwepa Kama sio kuyapotosha.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Hapanaa! hujajibu swali la msingi mkuu. Na hapa ndipo huwa nawa admire wewe na Kobello, ni mafundi wazuri sana wa kukwepa core issue na kuongelea future

Swali la msingi, mfuko wa pamoja kati ya nani na nani.
Halafu mfuko huo unaelezwajwe kwa mujibu wa sheria
Mtupe mchanganuo wa mapato, gharama na matumizi.

Mfuko huo ni wa S2 mnazopendekeza.

***Hapa hatuongelei future, mfuko upo ingaw haujafanya kazi. Hivyo tuelezeni katika mazingira hayo ya S2 kwa kuogopa S3 mnautendeaji haki mfuko.
Kobello karibu ili usije sahau mabandiko yakapita, ukaunga kwa mbele
Mkuu nakuelewa sana mnachodai na majibu ninayo isipokuwa yanishangaza sana mtu anapouliza mfuko wa pamoja ndio nini wakati amedai serikali 3. Ni sawwa kabisa na kubishana juu ya mwezi halafu ukiambiwa mwezi unahitaji mwanga wa jua unauliza mwanga wa nini na kwa nini mwezi unahitaji mwanga! jamani hata kujua Federal government needs to collect taxes from both sides mnashindwa kujua mfuko wa nani na nani wakati Lipuymba ndiye aloshauri na mnamuunga mkono? na mnajua fika kwamba Federal Government ndiyo serikali ya Muungano?.

Kifupi labda nikubali mimi kuachia hapa maana nachokieleza hamkielewi na itakuwa kazi mpya sana ikiwa hata kujisomea wenyewe hamtaki ama mnajua lakini hamtaki kukubali kama hao UKAWA (maskini jeuri). Maana Ukawa wanajua fika kwamba changes zinazotakiwa ni S3 ambazo zinahitaji kura ya wananchi mwishoni. Hizi S2 zipo na zitaendelea kuwepo hadi zipingwe na wananchi kwa hiyo kwa kila wanavyokataa ndivyo serikali 2 zitaendelea kutumika halafu wanajisifu kwa kukataa na kukaa nje ilihali S2 zinatumika na zittaendela kutumika kama swala hili halitafika kwa wananchi. Nyie endeleeni na Kobello mwenzangu mjuzi wa kuwaeleza japo bado hayawaingii akilini.

Labda niwaulize nyie kama maridhiano yasipokuwepo mna mpango gani wa kuhakikisha serikali 2 haziendelei kutumika ikiwa katiba hii haitaandikwa?
 
Sababu juu ya kwanini mfuko wa pamoja haufanyi kazi ni Kwamba ni Vigumu kutenganisha masuala ya Tanganyika na ya muungano. Kwa maana nyingine, mfuko wa pamoja ni hekaya za abunuwasi bila ya uwepo wa Tanganyika kwani ni impossible kubaini ya pamoja ni yepi na ya kila upande kivyake ni yepi chini ya serikali Mbili. Ni Vigumu kuelewa kwanini watu makini Kama wewe na Mkandara mnashindwa ona Hilo.

Na sasa, uwepo wa nchi Mbili serikali Mbili Ndio umeua Kabisa hata hiyo ndoto ya joint finance commission. Nyinyi Hali hii inazidi kuwapa matumaini Kwamba JFC can work, na pia Kwamba serikali moja inawezekana, na several other impractical and utopian views.

Uzi wa gharama tulio ahidi upo pale pale, hakuna kilichobadilika zaidi ya suala la timing kutokana na mchakato mzima wa BLK kuingia nyongo. Vinginevyo maandalizi yapo pale pale na Uzi utapanda ndani ya siku Tatu na utaweka sawa masuala mengi ambayo mmekuwa mnayakwepa Kama sio kuyapotosha.


Sent from my iPhone using JamiiForums
Mkuu ikiwa kila nchi itachangia mfuko huo kwa tuseme asilimia 20 tu ya pato la kila upande ili kuiwezesha serikali ya Muungano kukabiri matumizi yake. Unadhani hili ni hadith kweli wakati Tanganyika yetu yenyewe inategemea misaada kukidhi matumizi yake? nasikia mwaka huu matumizi ya ndani yamefikia mikopo ya asilimia 60 kweli hiyo asilimia 40 inayokusanywa inaweza kuendesha mambo ya ndani ya serikali ya Tanganyika bila kukopa!, watu wenyewe hawa wenye ma VX na mishahara ya millioni 12 kwa mbunge na posho juu. Lets be realistic...

Je, mnaamini hiyo serikali ya Muungano unategemea kweli inaweza kujiendesha kwa kutegemea Ushuru usiokuwa wa kodi kuwa itatosha? Kama haitoshi fedha zitoke wapi.. na nai mwenye kugharamia, hata takwimu nilizobandika hapo nyuma inaonyesha ni nmchango mdogo sana kwa Tanganyika, iwe leo nguzo ya kuendesha serikali kuu!.

Ama mnachosema hakuna haja ya serikali ya Muungano na hivyo hatuhitaji federal taxes? yaani tuvunje jahazi tugawane mbao? na kama ndivyo mnataka hizo serikali 3 za nini ikiwa tutagawana mbao?
 
Mkuu ikiwa kila nchi itachangia mfuko huo kwa tuseme asilimia 20 tu ya pato la kila upande ili kuiwezesha serikali ya Muungano kukabiri matumizi yake. Unadhani hili ni hadith kweli wakati Tanganyika yetu yenyewe inategemea misaada kukidhi matumizi yake? nasikia mwaka huu matumizi ya ndani yamefikia mikopo ya asilimia 60 kweli hiyo asilimia 40 inayokusanywa inaweza kuendesha mambo ya ndani ya serikali ya Tanganyika bila kukopa!, watu wenyewe hawa wenye ma VX na mishahara ya millioni 12 kwa mbunge na posho juu. Lets be realistic...

Je, mnaamini hiyo serikali ya Muungano unategemea kweli inaweza kujiendesha kwa kutegemea Ushuru usiokuwa wa kodi kuwa itatosha? Kama haitoshi fedha zitoke wapi.. na nai mwenye kugharamia, hata takwimu nilizobandika hapo nyuma inaonyesha ni nmchango mdogo sana kwa Tanganyika, iwe leo nguzo ya kuendesha serikali kuu!.

Ama mnachosema hakuna haja ya serikali ya Muungano na hivyo hatuhitaji federal taxes? yaani tuvunje jahazi tugawane mbao? na kama ndivyo mnataka hizo serikali 3 za nini ikiwa tutagawana mbao?
Kama alivyo sema Nguruvi3, mna uhodari wa kurukia hoja kwa Mbele; nimeuliza maswali ya msingi kwenye Bandiko #145 , mmeyahepa, sasa tutarajie mjadala gani wa maana kuhusiana na joint finance account?



Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mkuu nakuelewa sana mnachodai na majibu ninayo isipokuwa yanishangaza sana mtu anapouliza mfuko wa pamoja ndio nini wakati amedai serikali 3

jamani hata kujua Federal government needs to collect taxes from both sides mnashindwa kujua mfuko wa nani na nani wakati Lipuymba ndiye aloshauri na mnamuunga mkono? na mnajua fika kwamba Federal Government ndiyo serikali ya Muungano?.
Ni hivi, unajaribu kukwepa swali kwa kuweka mambo yasiyohusika. Unaweka hoja isiyokuwepo.
Tutaweka mambo straight uje utujibu.

1. Mnataka mfumo wa S2
2. Tume ya Amina Salum ilishauri kuhusu mfuko, na sheria ikatungwa. Malalamiko ya waznz mfuko huo haujafanya kazi.

Kwa wakati huu mnataka tuendelee na S2 lakini tuwe na mfuko wa pamoja.

Hadi hapa ni maelezo ambayo hayazungumzii S3 hata kidogo.

Tunataka mtushawishi kuhusu S2 na mfuko uliopo. Ushawishi wenu ujibu maswali haya

a)Mfuko uliopo sasa kwa mujibu wa sheria ni baina ya nani na nani. **kumbuka ni sasa hivi, I mean leo hii**

b)Mfuko wa sasa unafanya kazi vipi kwa mujibu wa sheria iliyouanzisha** kumbuka hakuna S3, ni sheria ya S2**

C) i) Mapato yake yapoje (Kwa sasa tukiwa na S2 na wala si future)
ii) Matumizi yake yapoje *kwa sasa katika mfumo wa S2**
iii) Mgawanyo wa mapato upoje ** kwa sasa na si siku za baadaye**

Nadhani hapa utaelewa swali. Narudia hakuna kipengele cha S3 hata kimoja, S3 bado zipo hewani.
Tunaongelea hali ya sasa ili tuweze kufikiria siku za baadaye.

Mkandara karibu sana
 
Last edited by a moderator:
Nimeingilia Mada Lakini SERIKALI ya Tanganyika LAZIMA itaongeza Gharama Zingine tu!!!!
Hilo lipo Wazi, Kwani Lazima ianzishe TAASISI za KIUTAWALA ktk Eneo Lake na Hili Litainvolve AJIRA za Watendaji Hawa , MISHAHARA YAO , NYUMBA ZA KUISHI, OFISI, VITENDEA KAZI,MAGARI NK NI GHARAMA Kubwa.
Zanzibar Hivi Sasa Makusanyo ni BILIONI 300 na , Mahitaji ni BILIONI 700 approx.
Leo tu Haijimudu na Nakisi inajazwa kwa Ruzuku, Sasa ikabaki peke Yake, kwanza Itajitosheleza Vipi Yenyewe, Halafu IJE Changia hiyo ya MUUNGANO ??????
Tusifikiri kwa Jazba na KUTETEA KISIASA Haya ni Mambo ya KIUCHUMI na Pressure za KIUCHUMI zinaweza Kuleta Mifarakano ya KISIASA, Mfano ni EAC ya Zamani , EU Malumbano ya EURO Baadhi ya Nchi zikitushia Kujitoa.
Ukiwapata Kina " YELTSIN" wetu Ambao kwao Sifa za Kushangiliwa Majukwaani Zimewapofusha Uwezo wa Kufikiri Vizuri na WANAROPOKA KILA WAWEZALO WAKIWA JUKWAANI Na Kutoa Matumaini MFU ILI Mradi hiyo inawaongeze Makofi kwa Baadhi ya WANANCHI na KujitengenezeA image ya PAPER WARRIORS Nchi na MUUNGANO una kwenda KUZIMU
 
Mfuko huo sasa hivi hautendewi haki kwa sababu haupo. Na sababu za kutokuwepo siyo utatanishi, bali ni kushindwa kwa Zanzibar kuulipia.Zanzibar hawalipi hata umeme, sembuse 5% ya 3trilion? Huo mfuko ni hekaya za Abunuasi.
Sawa sawa kabisa Mkuu. Kumbe unakubali kabisa kuwa gharama za sasa za S2 Mtanganyika amezibeba. Sasa pale Mtanganyika anapotaka kupunguza gharama unasema zinaongezeka. Vipi hapo?

Kwa mfano, si kuwa tu Tanganyika inabeba gharama, bali pia inafidia Zanzibar katika kujiendesha.
Nakisi ya bajeti ya znz inayofikia Bilioni 350 inatoka Tanganyika.
Hakuna mahali katika bajeti yao inaonyesha wapi wanalipia deni la JMT la ndani na la nje

Kuna gharama kama za elimu ya juu, taasisi kama Urais, Bunge zinatoka Tanganyika.
Tena hata wabunge wao wanalipiwa na Tanganyika kuja kuwakilisha nchi yao.

Wazanzibar watakuwa na mamlaka yao ikiwa ni pamoja na kwenda IMF, WB na misaada(uh).
Watakuwa na uwezo wa kujiendesha wenyewe na mambo yao bila msaada wa Tanganyika.
Watavuna gesi waliyoondoa na mafuta yao , watakuwa na uwezo

Tanganyika tutawaomba watusaidie katika, kulipia gharama ndogo ndogo kwa kuchukua jukumu.
Walipie wabunge, wanafunzi, taasisi, viongozi wao n.k.

Watusaidie kidogo walicho nacho katika ulinzi na usalama, mambo ya ndani, na kule wanakotaka balozi(mambo ya nje).

Ofisi ya msajili itakuwa na makao Dar, ile ndogo ya znz itahudumiwa na SMZ
Mapato ya TRA yatabaki huko ili waweze kuchangia chochote. Sasa hivi yanabaki huko lakini hawachangii

Hoja ni kuwa tukitenga mambo, kila mmoja atajua afanye nini na kwasababu zipi.
Gharama ndogo ndogo watatusaidia.

Sasa hapo gharama za S3 zinaongezeka vipi kwa Tanganyika?

Halafu mnasema ZNZ hawawezi, sasa kwa S2 wanawezaje.
Mbona walipoewa 21% ya ajira hamkuhoji uwezo wao wa kuzalisha ajira hizo
Mbona wanapochukua 4.5% ya pato la Tanganyika hamhoji uwezo wao

Hata tume ya Warioba hawataki kulipa mbona hamhoji uwezo wake.
Mbona hamhoji iweje wapewe 50% ya tume kama hawana uwezo
Mbona hamhoji iweje wapewe 2/3 ya maamuzi ya bunge kama hawawezi
Mbona hamhoji iweje wadai mgawanyo sawa wa madaraka kama hawezi
Mbona hamhoji madai yao (ya kipuuzi) ya wakuu wa majeshi na balozi(pumba) kama hawawezi
Mbona hamhoji walipoondoa mafuta na gesi, badari na anga, leseni za viwanda na ushuru.

Mnachotuambia ni kuwa mznzibar hawezi kuchangia, anaweza kuchota na kudai.
Hilo ni sawa sawa kabisa kwasababu linapunguza gharama!!!!!!

Tanganyika ikitaka haki mnasema gharama zitaongezeka.
Hivi unaweza kupunguza kilo 10 kutoka katika gunia ukasema uzito unaongezeka.
 
Nimeingilia Mada Lakini SERIKALI ya Tanganyika LAZIMA itaongeza Gharama Zingine tu!!!!
Hilo lipo Wazi, Kwani Lazima ianzishe TAASISI za KIUTAWALA ktk Eneo Lake na Hili Litainvolve AJIRA za Watendaji Hawa , MISHAHARA YAO , NYUMBA ZA KUISHI, OFISI, VITENDEA KAZI,MAGARI NK NI GHARAMA Kubwa.
Zanzibar Hivi Sasa Makusanyo ni BILIONI 300 na , Mahitaji ni BILIONI 700 approx.
Leo tu Haijimudu na Nakisi inajazwa kwa Ruzuku, Sasa ikabaki peke Yake, kwanza Itajitosheleza Vipi Yenyewe, Halafu IJE Changia hiyo ya MUUNGANO ??????
Tusifikiri kwa Jazba na KUTETEA KISIASA Haya ni Mambo ya KIUCHUMI na Pressure za KIUCHUMI zinaweza Kuleta Mifarakano ya KISIASA, Mfano ni EAC ya Zamani , EU Malumbano ya EURO Baadhi ya Nchi zikitushia Kujitoa.
Ukiwapata Kina " YELTSIN" wetu Ambao kwao Sifa za Kushangiliwa Majukwaani Zimewapofusha Uwezo wa Kufikiri Vizuri na WANAROPOKA KILA WAWEZALO WAKIWA JUKWAANI Na Kutoa Matumaini MFU ILI Mradi hiyo inawaongeze Makofi kwa Baadhi ya WANANCHI na KujitengenezeA image ya PAPER WARRIORS Nchi na MUUNGANO una kwenda KUZIMU
Hivi ndugu yangu, kwani nani amelalamika sana kuhusu kutotendewa haki katika muungano?
Mbona mnajitia upofu! Zanzibar wanataka mamlaka kamili ili wawe kama walivyokuwa kabla ya mapinduzi.

Unalaumu vipi Tanganyika kurejea wakati wazanzibar hawataki muungano huu.
Na ni kwa vipi unadhani waznz wana uhalali wa kudai kila kitu lakini hawana uwezo?

Wao wamesema watakopa na misaada, jambo wanalolalamikia kila siku.
Wameondoa mambo mengi katika JMT na kuyafanya katika vyombo vyao.Mbona hawajalalmika kuwa hawezi?
Ninyi Watanganyika uchungu mnaupata wapi ikiwa wao wanaweza kuendesha mambo yao.

Unaposema hawawezi mbona wanaondoa mambo na wanaendele. Hawawezi vipi? Kama hawawezi, je walipaswa kuongeza mambo au kupunguza?

Kwanini kuzinduka kwa Tanganyika kuonekane kama tatizo wakati wao wanaitaka Tanganyika ili kuwe na muungano wa haki na usawa?

Wameondoa mafuta na gesi ili wapate uchumi, mbona hamkukemea hilo kama hawana uwezo.

Na mwisho, kama hawana uwezo, wapi wanapata uwezo wa kuifanya katiba yao kuwa juu ya katiba ya JMT?

Kama hawana uwezo, wapi wanapata jeuri ya kuomba ajira 21%. Ukishasema hawana uwezo una maana hawana kitu.
Sasa wanaomba vipi kila kitu tena kwa nguvu ikiwa wao unadhani hawana kitu?

Hamkukemea kuvunjwa kwa katiba, mnakemea kuzinduka ka Tanganyika halali. Kama si ajabu ni nini!
 
Back
Top Bottom