Soma vizuri 105(3) na (4) halafu uniambie kitakachoizuia serikali ya Zanzibar kufanya kila mtaa kuwa wilaya na pia uniambie hiyo 20 umeitoa wapi?? Je, kukiwa na wilaya 40 Zanzibar mtafanya nini?
Kuhusu 2/3, hivi ni wabunge wangapi wa Zanzibar wanaotakiwa kupitisha bajeti au kutoa/kubadili matumizi ya consolidated fund? Kupitisha sheria yeyote zaidi ya Kubadilisha katiba?? two thirds ya Zanzibar ni kwenye mambo ya katiba. Kwa hiyo 2/3rd is not just 2/3rd ..... kwenye bunge la muungano lililopendekezwa 2/3rd ya Wazanzibari ni kwenye kila kitu ... it's like 50/50.
Gharama hazijabadilika Zanzibar au Tanganyika wana uhuru wa kuanzisha majimbo yao kadri wanavyotaka .... who knows we may have 200 Members of The Parliament, nani atawazuia?
Kwa hiyo mkuu mimi nadhani majitaka ni majitaka tu!, Waliozoea siasa za majitaka kama
Mag3 HUWA WAKO TOO SUPERFICIAL,HAWAANGALII VITU IN DEPTH.
Well, bunge la S3 kama shirikisho lina idadi ya wajumbe kutoka znz na Tanganyika ambao ni fixed. Kutakuwa na jumla ya 55 kwa mujibu wa rasimu.
Kama sikosei znz watakuwa 20 na Tanganyika 75, sina uhakika lakini ni karibia na hapo.
Kilichotumika na tume ni kutumia wilaya zilizopo kufikia idadi. Hebu someni muelewe.
Haikusema wabunge watategemea kuongezeka kwa wilaya.Someni muelewe kwanza msikurupuke tu
Zanzibar inaweza kuwa na wilaya 600 baada ya hapo, hilo halitaongeza idadi yao katika Bunge la shirikisho kwasababu ipo stated.
Zanzibar wanaweza kuwa na wabunge 700 BLW hakuna atakayewazuia kwasababu ni gharama zao.
Tanganyika nayo itaamua kulingana na mahitaji yake. Kuna uwezekano kukawa na wabunge 150 tukizingatia kuwa Dar es salaam yenye watu milioni 5 inao 7. Hivyo ni Watangayika watakaoamua. Inawezekana wakawa 1000 ni juu yao.
Hadi hapo unaona uzuri wa kutenga mambo, yaani unatoa fiscal autonomy.
Kwasasa znz ina BLW 50, wachache kuliko 81 wanaokuja Dodoma.
Sababu kubwa ni kuwa znz ina fiscal autonomy na inaona haimudu zaidi ya 50.
Lakini wanaleta 81 kwasababu mzigo wa gharama zao anaubeba Mtanganyika. Umeona hapo?
Kuhusu 2/3 hata kama wznz ni 10 bado 2/3 ni ile ile ambayo ni 50% katika maamuzi.
Ukiwa nao 81 ni 2/3 ile ile ambayo ni 50% ya maamuzi.
Hivi hapo huoni unapunguza gharama ukiwa nao 10 kwa uzito ule ule kuliko kuwa na 81 kwa uzito wa maamuzi usioongezeka au kupungua? Mkuu hapa ni hesabu, rudi kabatini kachukue chaki mkuu. Unazo and you live in, kwa mujibu wako.
Mnachopendekeza katika S2 ni kuwa na wabunge 81 ambao wanalipiwa na Tanganyika.
Hivyo mnafanya bunge kama sehemu ya ajira ghali sana za wazanzibar tukijua hawana lolote la kuchangia in terms of cost or idea.
Hawana! si kila siku tunawasikia wakililia nafasi za ubalozi(upuuzi sana), mkuu wa jeshi na IGP(wendawazimu)?
Lini umesikia mznz akizungumzia muungano bila kulalamika wanaonewa.
Halafu wanachoongelea hakiwahusu. Wizara ya afya, Kilimo, ujenzi, mali asili, miundo mbinu n.k haziwahusu.
Ardhi wamekataa yao isiwe ya muungano, leo munawaweka Dodoma wazungumzie ardhi ya Tanganyika kama yao.
Hivi hamuoni hawa watu wamewalisha limbwata.
Halafu jiulize ni wangapi. 1.2 nusu yao wanaishi Tanganyika. Nini cha kudhani ni muhimu kwa hao laki laki 5 kiasi cha kuwavuruga akili hadi mnashindwa kuona hata mkiibiwa
Wana zao na hizi zetu wamekataa kwa mujibu wa katiba yao ya 2010. Sasa tuite watu waje Dodoma kutalii na kupiga soga tukiwalipa mishahara mikubwa for nothing! absolutely nothing. No input of any kind you can imagine. Please
Nikuulize hiyo investment tunayofanya kwa hawa wadai ubalozi na IGP inatusaidia nini down the road.