Serikali 3 na gharama zake

Ebu Nijibu hili swali:
Political federation or unity huwa Inakuja Katika hatua gani ya integration?


Sent from my iPhone using JamiiForums
Nje ya chaki,
Hiyo ni theory ambayo imetumika kuijenga EU, the caviar is, huwezi kujiunga EU bila kuwa na vigezo fulani vya kisiasa kama vile Democracy, human rights eg. free press na most importantly kuwa na Political entity ambayo ipo recognized geographically. Yaani wanaangalia kwenye atlas map inatosema Europe (Political) na siyo Europe (Weather).

Kosovo siyo nchi inayotambuliwa na UN, kitu gani kimeifanya Parliament ya EU iikubali Kosovo na kuiweka kwenye process ya Intergration? Serbia je? .... Ain't this Political mobilization as the Precedent?

Kuhusu EA, huoni kwamba ignoring the Political will of East Africans is the Key weakness of this Economic intergration?
 
Unakwepa tu Ukweli makusudi au haujui unachojadili. Kwenye EU, Bila ya kuwa na certain macroeconomic fundamentals sawa, hata hayo ya democracy and human rights hayana uZito wowote.

Hilo swali lako kuhusu EAC ni spinning politics tu, Nguruvi3 amekupa mwanga for you to further research on your own.



Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Hoja ni kukuonyesha, muungano imara ni ule wenye kujali uchumi kwa dunia ya sasa.

Huko nyuma Marekani na zingine ulizoonyesha ziliungana kwasababu za kisiasa.
Hata sisi tuliungana kwa sababu za kisiasa zaidi.

Dunia imebadilika, siku hizi usalama wa taifa lolote hauangaliwi kwa idadi ya vifaru na magrenade.

Uchumi ndio sehemu kubwa, ikimaanisha kuwa uchumi umechukua nafasi kubwa kuliko siasa.
Hiyo haimaanishi siasa haina nafasi la hasha, ina maansisha dunia imebadilika katika vipau mbele.

Ujerumani unayosema, imeungana kutokana na hali mbaya ya uchumi wa Ujerumani mashariki

Haikuwa sababu za Hitler. Huko nyuma waligawanywa kwasababu za kisiasa ambazo baadaye zimekuwa overrided na mahitaji ya kiiugumi, wakavunja Berlin si kisiasa bali kwa hoja ya uchumi.

Watu walikufa wakiruka kuingia magharibi kwasababu za kicuhumi si mabalozi au ''IGP wa Ujerumani.

Leo Ujerumani ndio ina bail out nchi za EU, si kisiasa ni kiuchumi.

Waaingereza wanaotaka referendum wanajadiliana kuhusu mafuta kama muungano utakufa.

Wanaotaka kujitenga wanajiuliza kama nguvu yao kiuchumi bado itakuwa imara, si kama watakuwa chini ya Malikia.

SADCC ilianza kama frontline states, leo hakuna kaburu ni uchumi tu unaongelewa.
Kama utafikiria kwa mtazamo wako, basi SADCC haina maana ya uwepo wake

Hao wazanzibar unaoongelea malalamiko yao yote ni ya kichumi.

Sasa unawezaje kusema uchumi hauna role katika muungano tulio nao.

Nikuulize, katika malalamiko ya wznz ukiacha yale ya kipuuzi ya balozi na IGP nitajie lingine ambalo halina uhusiano na uchumi.

Hivyo lazima uangalie mazingira ya kale na sasa.
Ukikariri utaishia kujibiwa na hoja nyepesi lakini nzito bila kutaka.
 
Swali linakuja, kwanini kama tunataka muungano imara kwa mujibu Tanganyika ambayo haipo iwe tatizo na si zanzibar inayovunja katiba ile ile mnayosema inatulta pamoja?
 
Ungenionyesha ni kivipi nakwepa hoja. Turkrey na Ukraine ipi ina uchumi bora?
Mbona Turkey inakataliwa EU kila siku? ....
1. Armenian Genocide acceptance
2. Kurdish minority suppression
3. Occupation of Cyprus
Hizo siyo sababu za kisiasa?

Kuhusu EAC ... sijaona mwanga niliopewa na Nguruvi3. Wala sikumbuki, so you might be the one spinning. ila tuyaache haya, ni nje ya mada na sioni kama kuna logic yeyote ndani yake.
 
Last edited by a moderator:
Acha hilo tu hawa hawa wanataka Shirikisho kwa madai ya EU na hata EAC kuwa ni ya ushirika wa kiuchumi hivyo ndio maana ni imara lakini wanaikataa rasimu ya Warioba inapopendekeza marais watatu? wakidai wanaweza kuwa mawaziri wakuu! Utakuwaje na rais wa Shirikisho na kulazimisha mawaziri wakuu ktk nchi zenye kuunda shirikisho kama la EU.

Halafu basi zaidi ya hapo rasimu hiyo hiyo inasema tutakuwa na rais wa jamhuri na makamu wake, sijui hayo mashirikisho mengine yana makamu wa rais? na Je Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi wakitaka kujiunga nao wataweka wao sijui tutakuwa na makamu wa rais wangapi? EU wana nchi zao huru, EAC ina nchi zake huru kisiasa na kiuchumi sasa sielewi wanachokitaka haswa.

Halafu juu ya yote hayo Canada yenye muungano wake, USA yenye muungano wake na Mexico wana ushirika wa kiuchumi nje kabisa ya kuunda Umoja wa nchi hizo lakini hawa ndugu zangu kila mara wanataka kufananisha vitu hivi.
 
Hoja: Foundation nzuri ya muungano kati ya nchi ni nini?

Answer: Political will.

Panga pangua ... ila tuyaache hayo. Siyo ya msingi.
 
Hoja: Foundation nzuri ya muungano kati ya nchi ni nini?

Answer: Political will.

Panga pangua ... ila tuyaache hayo. Siyo ya msingi.

You are dodging the fundamental issue. Union between Tanganyika and Zanzibar was and remains to be a political union. In any union between countries, political unity ni kati ya hatua za baadae Kabisa baada ya economic fundamentals kuwekwa sawa, na hii ni sababu ya msingi ya muungano wetu kukaribia kufa. unless mnajaribu to rewrite the history.

Umefanya matumizi yasiyo sahihi on the term "political will". Be what it may, was there a political will Katika suala Zima la muungano baina ya Tanganyika and Zanzibar? Please take us through your own version of history.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Onyesha sehemu Raismu imeeleza uwepo wa marais watatu. Ukishindwa kuonyesha uombe utahibitisha spinning

Pili, nimekuuliza kwanini uwepo wa Tanganyika uwe tatizo na si uwepo wa zanzibar.
 
Ndio maana unarudia na kujichanganya kwasababu hukumbuki.
 

Hivi haujui kwanini suala la turkey EU Lina utata? Suala la turkey lipo intricate, it's a combination of politics, economics, history, culture and religion. Na Katika haya, politics isn't the prime factor. Soma historia au fanya utafiti vizuri.

Mnajaribu to divert issue ya msingi. Kama Aliyosema Nguruvi3, hakuna muungano unaoweza simama au kudumu bila kuwa na right economic fundamentals. Sijui kwanini hamwoni Kwamba siasa ni mtumwa wa uchumi.

Uhusiano wa siasa na uchumi upo Katika policy sphere. And policy analysis involves a careful calculation of how means relate to desired ends. Making policy is all about key principles of:

1. Feasibility
2. Sustainability
3. Efficiency

All these go together as a package. In the end, policy analysis ni application of economic principles to the politic process. Lakini kwa Wanasiasa wetu ni wenzao Kama wewe na mkandara, policy analysis doesn't have to be based on an economic rationale. You think of policy purely on political grounds. To you guys, in the context of the union, policy objectives not only become politics objectives, but also become an end in themselves as the calculation of costs to achieve them are completely ignored and disregarded. Kwa kweli Hadi tuweke nchi yetu Katika mkondo sawa, kazi Ipo!




Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Ndio maana unarudia na kujichanganya kwasababu hukumbuki.
Soma sura ya Nane - Uhusiano na Uratibu wa serikali ibara ya 2 kifungu cha b) na c) kinasemaje?

Tanganyika kama serikali ipo kisichokuwepo ni jina tu la uitwa Tanganyika badala ya Tanzania, kama wewe unajiita nguruvi3, sio lazima nawe uitwe kama mimi Mkandara nayetumia jina langu ili sijui iwe nini. Hatulitaji jina la la uzawa ili kumwelewa mtu na wala hatuna haja la asili maadam wewe upo na unaendelea na maisha yako na mchango wako hapa ndio muhimu kwetu.
Jingine..
 
Mkuu wewe haya unayapata wapi? A political Union ni last stage kwa nchi za EU ambazo tayari zimekwisha fanya mengine yote yalopita. Na sisi tunaweza fanya kwa EAC, SADC au Unification of Africa. Lakini haimaanishi hatukutakiwa nchi kuungana kwanza. Marekani hawakuungana baada ya hizo economic fundamentals kuwekwa sawa, Sio Uingereza, Canada, India na kadhalika. Hivyo haiondoi maana ya Political Union tunayoijua sisi kuwa ni nchi ndogo (states) zinazoungana kuunda Taifa moja. yaani unachanganya sana mambo kwa sababu sijui unaambiwa ama huelewi tu.
 
I don't have my own version, nakupa facts.

Tatizo kubwa lililopo kuhusu muungano wetu ni Political will. Sidhani kama Politically tunataka kuwa nchi moja na hilo ndiyo tatizo.

Egypt na Israel wanategemeana sana kiuchumi ila hawawezi kuwa na muungano. Pia ndiyo sababu ya ASEAN countries kuchelea kuwa na currency moja kwa sababu ya conflicts za China na India/Japan/Phillipines?vietnam ...hiyo yote ni Political factors.

Kilichoharibu EAC zamani ni Politics wala siyo uchumi ... they had one currency already.

Kwanini tuende huko wakati tunazungumzia gharama??? .. Tuache hilo, sidhani kama mnalielewa vizuri.
 
Hivi haujui kwanini suala la turkey EU Lina utata? Suala la turkey lipo intricate, it's a combination of politics, economics, history, culture and religion. Na Katika haya, politics isn't the prime factor. Soma historia au fanya utafiti vizuri.
Hehehe .... Issue ni Political, hiyo wala usiigeuze.

THE MAIN REASON IS CYPRUS!!
 
Yes ! nakubaliana nawe kuhusu suala la political will. Nisichokubaliana nawe ni sentensi kuwa 'sidhani kama tunataka kuwa nchi moja'' . Hapa ningekusahihisha bila chaki, sema hivi ''hujui kama Zanzibar wanataka tuwe nchi moja''
Hili mnalificha ili kuzuia hoja ya Tanganyika. Hamsaidii kwa namna yoyote.

Nyerere alipokuwa anatukanwa kule znz hakuna aliye raise sauti na kusema lilikuwa jambo baya.
Nyerere alitaka nchi moja mbona hamkusimama kumtetea? Ni nani wasiomtaka Nyerere kama si wazanzibar?
Nani amepanda mbegu hii ya utaifa wa kila mmoja kama si wazanzibar?

Katiba ilipovunjwa mlikaa kimya mkijua fika ni katiba ya 'nchi moja'' Waliovunja ni wazanzibar kwasababu ya Uzanzibar wao. Wakajitoa katika muungano kwasababu ya uzanzibar wao. Leo Tanganyika wanaposimama na kujitetea kama taifa mnasema ''hatutaki nchi moja''

Pili, ugomvi wa China na Japan unakuzwa kisiasa kwa kutumia kisiwa.
Nyuma ya pazia kuna ukweli kuwa Marekani ndio uchumi mkubwa, the second ni China. Nafasi ya China wamepokwa Wajapan. Tension inayoendelea kwa juu juu ni ya kisiasa, kiundani ni uchumi tu. Hilo mtakataa kuficha hoja ya Tanganyika.

Egypt na Israel wanategemeana kiuchumi. Walitambua kuwa nguvu zao hazipo katika siasa bali Uchumi.
Hilo ndilo linawaweka mezani. Unawezaji kusema uchumi hauna role, huku mwenyewe ukisema wanategemeana kicuhumi

Tatu, hili la gharama za muungano tunalionyesha kwa uwazi. Tuambieni unafuu wa sasa na ule utakaotokea kwa namba.
Kwa ufupi, kwasasa mambo yote ya muungano yamefungwa katika kapu moja linaloitwa Tanzania, anayehudumia ni Tanganyika.

Kwa mtu anayeelewa, ni wazi mambo hayo yakifunguliwa kutoka katika kikapu Tanganyika atapata unafuu zaidi.
Unafuu ni pale tutakapojua mzigo ukoje na uzito au wepesi upo wapi. Kwasasa hatujui kwasababu tunaambiwa mzigo ni mzito tu.

Ni kwa msingi huo, ninyi mnaokataa Tanganyika kuzinduka, si kwamba mnakataa kwa gharama.
Mnogopa wazi kuwa Tanganyika itabeba gunia lake kama kawaida, lakini jirani hatakuwa na nafasi ya kuficha mizigo yake.

Kwasasa Tanganyika inabeba gharama 100%, kitu gani mnachoogopa itakapopata utambulisho, nani atabeba mzigo wa jirani?

Wekeni namba mtuonyeshe unafuu, tutakubaliana nanyi. Hili la kusikia akina Nape wakisema hatulikubali.
 
Nadhani usielewa ni wewe labda. Unaonhelea muungano wa Marekani miaka 200 iliyopita ukitegema situation ile ile mwaka 2014.

Mkuu SADC haikuanza kiuchumi. Ulikuwa muungano wa kisiasa kukomboa nchi za kusini mwa Afrika kwa kutumia Frontline state. Walioongoza ni akina Brigedia Hashim Mbita. Leo SADC ni uchumi kwasababu hakuna nchi ya kukomboa.

Ukiangalia mwaka 1970 na kutaka mazingira hayo yawe ya mwaka 2014, utakuwa nyuma sana kwa wakati.
Ningeshauri utafute the latest editions za mambo unayojadili. Kwasasa bado unatumia Edition 1. Wrong mkuu.
 
Samahani ninaposema chaki ninamaanisha mpaka wa uwanja wa mpira. Kuwa nipo ndani ya mada, sasa sijui wewe unamaanisha nini? But anyways,
Hapo kama lugha hiyo inakufaa, go ahead tuseme Zanzibar hawataki huu muungano (whats the difference?).


Nimtetee kivipi? Nikapigane au unataka nishike bunduki? Thats their right, ila mimi siungi mkono serikali tatu wala mbili. Especially tatu. Ni uuaji wa muungano na uongezwaji wa gharama, bora tu tuwe nchi mbili separate.

Zanzibar ipo chini ya Muungano. Haina jeshi, haina passport, haina mabalozi, haina kiti UN haina chochote cha kujiita nchi. Ni sawa na Wales kujiita nchi katika katiba yao, hiyo ipo na England wana-tolerate kuwapa tu self determination.

Ungemuuliza Mchambuzi il uone yeye anasemaje kabla ya kupost maneno haya. China lilikuwa ni koloni la Japan na kuna deep hatred between them from the Gets go . Usiwakumbushe wachina "Long Walk" au wenyewe wanaaiita October's retreat, walitembea kwa siku 370 mfululizo kuwazunguka Wajapan huku wakisapotiwa na Peasants. Wajapan wamewaua sana Wachina so lets not go there.

Egypt na Israel wanategemeana kiuchumi. Walitambua kuwa nguvu zao hazipo katika siasa bali Uchumi.
Hilo ndilo linawaweka mezani. Unawezaji kusema uchumi hauna role, huku mwenyewe ukisema wanategemeana kicuhumi
Agreed. hapa upo right. Sikutumia mfano mzuri.

Naona unaleta vikapu vya Bab Saleh...lol..Nyinyi ndio mliotaka kuja na numbers. I got the numbers for you ila tuende kwenye uzi mpyaaa!! wa numbers na common sense. Nausubiri uzi wenu ila nyie mnaonyesha kuwa ni watu waongo maana siku ya tatu hii inawadia na bado hamjautundika. Whats up with that?
 
Kobello,
Niwie radhi kwa delays. zipo sababu kadhaa kwanini sijatimiza ahadi husika. Ni hivi - uzi wa gharama ambao utakuwa based on economics and statistics upo pale pale; uzi huu hautakuwa uzi wa ubabaishaji, na kama unavyojua, numbers dont lie, kwahiyo naomba uwe na subira, nataka kuwasilisha kitu kamili, sio siasa;

Analytical framework nitakayofanya haijawahi kufanywa na mtu yoyote, methodolody nitakayotumia haijawahi kuwepo popote katika mjadala wa muungano for the past 50 years, sio na wachumi, sio na wanasiasa; uzi huu utakata mzizi wa fitina; sababu kubwa kwanini haukuja baada ya bajeti as promised ni suala la timing - sikuona maana ya kupandisha uzi halafu bunge livunjwe kutokana na ukawa kutoka bungeni; lengo langu ni tuwe na mjadala wakati mjadala wa katiba bungeni ukiwa hai, sio vinginevyo; nilipoona dalili za mjadala kuendelea bungeni zipo, nikapata msiba ndani ya familia; Baadae, wakati najiandaa kuweka sawa updates n.k, especially numbers kwa jinsi mambo yanavyobadilika kila siku, zikaja taarifa kwamba kuna uwezekano bunge la katiba kuvunjwa;

Mkuu, tofauti kubwa kati yangu na wewe ni kwamba wewe unasukumwa zaidi na 'TIME', wakati mimi nasukumwa na 'TIMING'. Sasa kwa vile kuna dalili kwamba bunge litaendelea, i think the timing is right;

Suala lingine ni kwamba - kama unafuatilia posts zangu kwa makini, natumia sana simu, hii ni kwa sababu muda mwingi huwa nipo safarini, sija settle; lakini sasa nimerudi na nimeutulia japo kwa muda; Lakini again kuna suala limejitokeza tena - kwa sasa nipo busy na maandalizi ya mdahalo on Star TV next monday ambapo nimealikwa kuwa key note speaker kwa upande wa studio DSM, huku mtu mwingine akiwa studio ya Mwanza. Ni mdahalo kuhusu uchumi wa taifa na umaskini. Naomba nikamilishe kwanza maandalizi haya ili nikipandisha uzi wa gharama niwe active katika kujibu hoja zenu kuliko kupotea;

Final confirmationi toka kwangu ni kwamba - Uzi wa gharama utapanda jumanne au jumatano ijayo tukijaliwa kwani kuanzia siku hiyo ndio ntakuwa na muda zaidi wa kupambana jino kwa jino na hoja zenu.
 
Last edited by a moderator:
Majibu haya ungempa Mchambuzi ambaye anasema lazima ianze na Uchumi, sasa wewe umedhihirisha kwamba SADC ilikuwa Political kwanza na sasa ni uchumi. Hivyo unapingana na mwenzako usielekeze swala kwangu.

Ya Amerika na miaka 200 haipotezi maana, kama neno Siasa na Uchumi lilikuwepo miaka 200 ilopita halina maana nyingine leo. Nchi za Ulaya zilipata Uhuru miaka 200 ilopita na baadhi wakaungana kisiasa miaka hiyo hiyo, lakini wamekuja ungana kiuchumi na mataifa mengine karne hii. Mnachanganyikiwa sana nyie, wala sijui mnachotaka kusema ni kipi hapa.

Labda niwaulizeni nyie, haya ya EU kuiwekea vikwazo Russia ni Siasa ama ni katika mbinu za Kiuchumi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…