I don't have my own version, nakupa facts.
Tatizo kubwa lililopo kuhusu muungano wetu ni Political will. Sidhani kama Politically tunataka kuwa nchi moja na hilo ndiyo tatizo.
Egypt na Israel wanategemeana sana kiuchumi ila hawawezi kuwa na muungano. Pia ndiyo sababu ya ASEAN countries kuchelea kuwa na currency moja kwa sababu ya conflicts za China na India/Japan/Phillipines?vietnam ...hiyo yote ni Political factors.
Kilichoharibu EAC zamani ni Politics wala siyo uchumi ... they had one currency already.
Kwanini tuende huko wakati tunazungumzia gharama??? .. Tuache hilo, sidhani kama mnalielewa vizuri.
Yes ! nakubaliana nawe kuhusu suala la political will. Nisichokubaliana nawe ni sentensi kuwa 'sidhani kama tunataka kuwa nchi moja'' . Hapa ningekusahihisha bila chaki, sema hivi ''hujui kama Zanzibar wanataka tuwe nchi moja''
Hili mnalificha ili kuzuia hoja ya Tanganyika. Hamsaidii kwa namna yoyote.
Nyerere alipokuwa anatukanwa kule znz hakuna aliye raise sauti na kusema lilikuwa jambo baya.
Nyerere alitaka nchi moja mbona hamkusimama kumtetea? Ni nani wasiomtaka Nyerere kama si wazanzibar?
Nani amepanda mbegu hii ya utaifa wa kila mmoja kama si wazanzibar?
Katiba ilipovunjwa mlikaa kimya mkijua fika ni katiba ya 'nchi moja'' Waliovunja ni wazanzibar kwasababu ya Uzanzibar wao. Wakajitoa katika muungano kwasababu ya uzanzibar wao. Leo Tanganyika wanaposimama na kujitetea kama taifa mnasema ''hatutaki nchi moja''
Pili, ugomvi wa China na Japan unakuzwa kisiasa kwa kutumia kisiwa.
Nyuma ya pazia kuna ukweli kuwa Marekani ndio uchumi mkubwa, the second ni China. Nafasi ya China wamepokwa Wajapan. Tension inayoendelea kwa juu juu ni ya kisiasa, kiundani ni uchumi tu. Hilo mtakataa kuficha hoja ya Tanganyika.
Egypt na Israel wanategemeana kiuchumi. Walitambua kuwa nguvu zao hazipo katika siasa bali Uchumi.
Hilo ndilo linawaweka mezani. Unawezaji kusema uchumi hauna role, huku mwenyewe ukisema wanategemeana kicuhumi
Tatu, hili la gharama za muungano tunalionyesha kwa uwazi. Tuambieni unafuu wa sasa na ule utakaotokea kwa namba.
Kwa ufupi, kwasasa mambo yote ya muungano yamefungwa katika kapu moja linaloitwa Tanzania, anayehudumia ni Tanganyika.
Kwa mtu anayeelewa, ni wazi mambo hayo yakifunguliwa kutoka katika kikapu Tanganyika atapata unafuu zaidi.
Unafuu ni pale tutakapojua mzigo ukoje na uzito au wepesi upo wapi. Kwasasa hatujui kwasababu tunaambiwa mzigo ni mzito tu.
Ni kwa msingi huo, ninyi mnaokataa Tanganyika kuzinduka, si kwamba mnakataa kwa gharama.
Mnogopa wazi kuwa Tanganyika itabeba gunia lake kama kawaida, lakini jirani hatakuwa na nafasi ya kuficha mizigo yake.
Kwasasa Tanganyika inabeba gharama 100%, kitu gani mnachoogopa itakapopata utambulisho, nani atabeba mzigo wa jirani?
Wekeni namba mtuonyeshe unafuu, tutakubaliana nanyi. Hili la kusikia akina Nape wakisema hatulikubali.