Sera Mpya ya ardhi, Kaburi jipya la CHADEMA

Sera Mpya ya ardhi, Kaburi jipya la CHADEMA

EFF ya Africa kusini ni Chama cha juzi, lakin nashangaa chama kikongwe kama chadema wanakopi kutoka kwa EFF, sera zote wamekopi wanadhani sisi watanzania ni wajinga, tunajua sera za vyama vyote,
 
Mbona inaeleweka..maana yake rasilimali kama madini zitamilikiwa na wachache..ingekuwa hivyo leo tanzanite isingekuwa ya tanzania..ingekuwa ya mzee Ngoma na familia yake..nilichogundua hapa ni rahisi ukiwa nje kuona makosa ndani ya uwanja..chadema hawajachukua hata nchi wameanza kuleta ubinafsi
Huo ubinafsi umeshindwa kuwatoka.
 
Pamoja na yote lakini tumeona mara nyingi ardhi akitaifishwa na serikali toka mikononi mwa hao matajiri.....lakini huko kwingine huwezi kuona kitu kama hicho.!

Hivi mkuu Idawa ardhi kitu gani bwana kwa mwanachi wa kawaida mpaka uanzishe uzi kwa kupanic? Nina hakika wazazi wako huko kijijini wanamiliki ardhi lakini wana umasikini wa kutupa. Utakuta kila mara wanakubeep uwatumie hela ya matumizi ww unayekaa nyumba ya kupanga hapa mjini. Ukiona mwanachi anamiliki ardhi ni kwakuwa haina la maana vinginevyo serekali ingeshampora. Hao cdm wameshaona hiyo tabia ya wananchi kuporwa ardhi yenye maana, wanatengeneza ushawishi wapate kura kisha wakishapata madaraka wataweka utaratibu mzuri wa hiyo ardhi iwapo ina raslimali.
 
Bila maelezo ya kutosheleza, huo ujumbe wako ni uchochezi
 
Mkuu @idawa,kwa heshima yako humu hustahili kuandika hivi. Umeandika kitoto sana. Ulipaswa kueleza jambo la maana
Tatizo lako wewe kila anayepost huwa unajiona unaweza kumkosoa, na nashangaa unasema ni mwanasheria, sio Mara ya kwanza pengine ntakuonesha kila mtu eti kaandika kitoto kwanini uchangie mada za kitoto? Usipite kushoto tu?? Au unajiona Iq yako iko juu sana haha hatari sana, kwa hali ya kawaida hupaswi kujifanya we ndo unajua sana kujaji mada za kikubwa na kitoto
 
Hivi mkuu Idawa ardhi kitu gani bwana kwa mwanachi wa kawaida mpaka uanzishe uzi kwa kupanic? Nina hakika wazazi wako huko kijijini wanamiliki ardhi lakini wana umasikini wa kutupa. Utakuta kila mara wanakubeep uwatumie hela ya matumizi ww unayekaa nyumba ya kupanga hapa mjini. Ukiona mwanachi anamiliki ardhi ni kwakuwa haina la maana vinginevyo serekali ingeshampora. Hao cdm wameshaona hiyo tabia ya wananchi kuporwa ardhi yenye maana, wanatengeneza ushawishi wapate kura kisha wakishapata madaraka wataweka utaratibu mzuri wa hiyo ardhi iwapo ina raslimali.
Mkuu unaamini hiyo sera ya Chadema ndio matakwa ya watanzania walio wengi hadi usemame ni sera ya kuombea kura.?

Ikitokea Chadema wakashika madaraka na hiyo sera ikawafanyiwa kazi unaamini itamuondoa mtanzania kwenye lindi la umaskini.?
 
Hiyo ni nukuu toka kwenye sera mpya ya Chadema kuhusu ardhi.

Sasa maelezo gani unataka mengine zaidi ya kutumia ubongo wako kuchambua hiyo sera.
Bila maelezo ya kutosheleza, huo ujumbe wako ni uchochezi
 
Bonta kwenye wimbo wake mmoja aliwahi kuuliza "mbezi kuna nini lami hadi ndani, shinyanga kuna dhahabu vumbi hadi ndani"... Huu ndo ukweli kwamba viongozi wamekua wanahamisha utajiri wa maeneo yenye madini nakuwaachia wazawa mashimo na vyumbi, kibaya zaidi utajiri unaelekea ulaya kama gesi yetu ilivyonyang'anywa na mabepari(JPM)...ndg yng ukweli ni kwamba Tanzania hajavamiwa tena na wazungu baada ya uhuru,iko wazi viongozi kupitia ccm waliwapa mabepari rasilimali zetu kwa mgongo wa " wawekezaji". CDM imepigana kadiri walivyoweza kutuamsha ili kuona kuanzia operesheni sangara hadi kudai sera ya gesi kabla yakugawa vitalu, yaani ni ww mleta mada na viongozi wachache mlingia mtaani na vifaru kule Mtwara kuwatawanya wananchi wanaotaka gesi yao isitoroshwe, Miaka michache imepita tokea muwakebehi wanamtwara leo mnaungana tena na JPM kulalamika gesi yetu inaibiwa...kwa kifupi idara yetu nyetu T..I..S ukiongezea na Jioni Wali(JW) mnatumika km kondomu mmewasaliti umma na mmegeuzwa kondoo wa wanasiasa mnageuzwa geuzwa kama samaki anayeliwa
 
Hiyo ni kwa sababu ya ulafi wa Baba yake ambaye alichukua sehemu kubwa ya ardhi na kuwaacha Wakenya wengi wakiwa na sehemu vipande vidogo vidogo. Mbona hakuna wanachi wengine waliambiwa kurudisha ardhi.
Sio ulafi wa Baba yake ndio sera yao ya Taifa,kwamba mwenye uwezo wa kumiliki ardhi miliki kadri uwezavyo.....na kwa kuwa yeye alikuwa kiongozi aliitumia ipasavyo ile fursa.
 
Kweli mkuu, kuna watu wanaleta mada humu bila kuzidadisi nakuzielewa, wanatupa kazi nyingine yakutafuta uhalisia
Sio lazima utafuniwe kila kitu, umiza ubongo kutafsiri ujumbe.
 
Sio ulafi wa Baba yake ndio sera yao ya Taifa,kwamba mwenye uwezo wa kumiliki ardhi miliki kadri uwezavyo.....na kwa kuwa yeye alikuwa kiongozi aliitumia ipasavyo ile fursa.
Kama ni Sera yao, ina maana sasa hivi kuna Mkenya anaweza kupata ardhi ya kumiliki ilhali kila mmoja ana ardhi yake ?
 
Wale wanaotaifishwa mara nyingi ni wake walioshindwa kuziendeleza.....kulipwa fidia ama kutolipwa fidia wakati mwingine ni ubabe wa serikali...... sababu sheria za fidia zipo kwa mali zilizo juu ya ardhi sio zilizochini ya ardhi.
Kwa nini Serikali itaifishe ardhi, badala ya kuwafidia ?
 
Hii sera itatzua vita vya wenyewe kW wenyewe maana matajiri wamiliki ardhi kubwa huku wanyinge wakibakia bila ardhi.Matokeo yake itakua ni machafuko ndani ya nchi vita vya kugombea ardhi .Chadema itasababisha umwagaji wa damu Sera hii ni mbaya kwa Amani ya Tanzania.

Kwa maana hiyo wewe unaona hali ya sasa ndiyo bora? Pakigundulika mafuta au madini ardhini mwananchi automatically akose kila kitu wapewe wazungu na wachina?
WAKE UP FROM YOUR MENTAL LAZINESS.
 
Mkuu @idawa,kwa heshima yako humu hustahili kuandika hivi. Umeandika kitoto sana. Ulipaswa kueleza jambo la maana
Mkuu binafsi nimeipongeza Chadema kwa kuja na kitu ambacho kitatusaidia kujua wao wanasimamia nini. Sasa inabidi wote waelewe sera yao ili wajue wapi waunge mkono serikali na wapi wapinge badala ya hii pingapinga isiyo na macho.

idawa amegusa sehemu tu ya sera ambayo naamini imeamua tu kuwa kinzani na sera ya CCM lakini haina mantiki. Labda tulete sera ya sasa ya ardhi vs hii ya chadema ili tuelewe nini anachogusia idawa.
 
"2. USIMAMIZI WA ARDHI: Chadema itaanzisha mfumo wa umiliki wa ARDHI ambapo kila MWANANCHI atamiliki ardhi na rasilimali zake JUU na CHINI ya ARDHI hiyo. TOFAUTI na CCM, Chadema HAKIAMINI katika KUFUKUZA watanzania kwenye ARDHI YAO kufuatia UGUNDUZI wa MADINI."
===========================

Chadema hili swala la ardhi litawamaliza, Kama Baba wa Taifa angefuata hii sera yenu leo kungekuwa na mtu mmoja mwenye uwezo wa kumiliki mkoa mzima na kila kitu kilichomo ndani yake.
View attachment 880155
Hujamuelewa! Shambani kwako, anga na ardhi chini na vilivyomo ni vyako. serikali ikivitaka inakulia fidia, siyo kukuhamisha say wakipata madini hufidiwi!
 
Huo ubinafsi umeshindwa kuwatoka.

Mtu akikaa hapa akisikia mnaongelea ardhi anaweza akaona mnaongelea kitu cha maana. Mbona watanzania walio wengi wanaishi mashambani na kumiliki ardhi lakini ndio masikini wa kutupa? Kuliko kumiliki heka kumi ya ardhi huko kijijini ni bora ukae double room za kupanga hapa mjini. Kwani ww Phillipo utashindwa kumiliki heka 10 ya ardhi hapa nje ya Dar? Mbona huendi bali unabanana kwenye maVX ya serekali hapa mjini? Mtu anamiliki zaidi ya heka 30 huko kijijini na hati ya kimila juu lakini akienda bank kukopa hata 20m hapewi, lakini mtu hapa mjini akionyesha ana ofisi ya kupanga hapa mjini kwenye plaza yotote hata akitaka 50m anaipata siku hiyohiyo.

Ni rahisi sana kwenye hii sera ya ardhi kumuambia mtu amiliki ardhi, na kikugunduliwa chochote, serekali itakupa labda 0000.1% ya kilichokutwa kwenye ardhi yake mpaka hapo kilichogunduliwa kitakapoisha. Ukweli ni kuwa masikini wengi nchi hii wanamiliki ardhi na kitendo cha kuwapa waimiliki hiyo ardhi ni kuwakabidhi umasikini kihalali. Hawa wahindi wenye maisha mazuri hapa nchini umeona wanamiliki ardhi?

Cc:idawa, misuli
 
idawa nadhani utakua haujamuelewa vizuri Halima Mdee, sheria ya Ardhi nchini inampa mamlaka Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kumpa/kumnyang'anya/kumuongezea hati ya umiliki/kubatili haki ya umiliki kwa mtu yoyote anaemiliki ardhi kwa ridhaa/bila ridhaa yake, na kwa kumlipa fidia au bila kumlipa fidia.

Mara nyingi Ardhi inapogundulika kua ina madini au rasilimali nyingine chini, wananchi hua wanahamishwa kwa kulipwa fidia ya ARDHI tu (na si fidia za rasilimali iliopo katika ardhi yake au thamani ya kiwanja baada ya kugundulika kwa hizo rasilimali).

Mfano,

Una kiwanja, umekinunua Sh Milioni 1, kikagundulika kina madini ya dhahabu chini, utapewa hela ulionunulia hicho kiwanja na maendeleo uliofanya katika hicho kiwanja tu (kama vile kujenga nyumba, kupanda miti n.k) ila hautapewa fidia ya thamani ya hicho kiwanja baada ya ugunduzi wa hayo madini. Kawaida kiwanja hupanda thamani baada ya kugundulika kua kina rasilimali.
Hapo issue ingekuwa mtu kulipwa fair price na vingewekwa vigezo vinavyoweza kutoa tathimini halisi. Umiliki wa ardhi ubaki kwa jamhuri . Yanahitajika marekebisho tu
 
Hii sera itatzua vita vya wenyewe kW wenyewe maana matajiri wamiliki ardhi kubwa huku wanyinge wakibakia bila ardhi.Matokeo yake itakua ni machafuko ndani ya nchi vita vya kugombea ardhi .Chadema itasababisha umwagaji wa damu Sera hii ni mbaya kwa Amani ya Tanzania.
IT WILL NEVER HAPPEN WALAHI
Why worry kwa kitu cha ovyo ovyo?
 
Back
Top Bottom