Katika hali ya utulivu kabisa majira ya saa 2:36 leo [26/08/2012] asubuhi amekuja karani wa sensa na kujitambulisha kwangu na kueleza kilichomleta.
Bila kusita nimempa ushirikiano mzuri sana na kumwandalia chai ingawa aliktaa ila nimemwambia mchana aje kula chakula cha mchana, yaani yale maswali waliokuwa wanasema mengi kumbe ukianza kuhojiwa hata dakika 7 hazifiki, miongoni mwa maswali hayo ni Unaitwa nani, Nani aliyelala kuamkia usiku wa leo, umri wako na wengine, kuna ulemavu wowote kati yenu, kuna vifo vilivyotokea, kati yenu kuna waliojiunga na mfuko wa jamii ie nssf, pspf, unashinda maeneo gani, na wenzako wanashinda maeneo gani, unajishughusha na ufugaji, elimu yako na wenzako, lugha unazozifahamu, uraia wako, kuna mwanakaya ambaye anaishi nje, n.k
Yule karani ameniambia atarudi tena kwa ajiri vitambulisho, alikuwa hana sare ameniambia sare zimechelewa ila alikuwa na kitambulisho.
Vile vile nimemshuhudia jirani yangu wa imani ya pili naye akitoa ushirikiano huku akiangalia kama kuna watu wa imani yake kama wametumwa kumwangalia anatoa ushirikiano, nikamwambia asiwe na wasi wasi mimi naaangalia kama kuna mtu yeyote atakuja ambaye simfahamu nitamstua.