Sensa 2012: Yanayojiri

Sensa 2012: Yanayojiri





bora sisi tunaongozwa na kipofu kuliko nyinyi mnaongozwa na watu wa aina hiii


542490_357234314353514_1378533576_n.jpg

njiwa pamoja kwamba wewe ni sehemu ya Members wajinga wajinga hapa JF lakini unakwenda too low like this!! kutuletea magazeti ya Shigongo Jukwaa la siasa? kwahiyo na wewe unaamini JK alimuita Diamond Ikulu kumtuma kwenda kutumbuiza jana kwenye uzinduzi wa tawi la CCM DMV?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu usife moyo ilimradi hukuwa na nia mbaya utahesabiwa tu, hata mimi kwangu hawajafika mpaka mida hii na nasubiri kama wewe

Wasiwasi wangu ni kwamba kuanzia kesho kuna special task ntakua nafanya kutoka job samoja hadi mbili sasa itakuaje??!
 
Sishangai Wamarekani wanachofanya Uarabuni hawa watu si wa kuvumilia jamani what they believe is diferrent from what they do
 
Toa japo aya moja ya Quran Tukufu ama Hadith Sahihi za Mtume (S.A.W) ya ku-support kwamba ulichofanya ni sahihi na kinyume chake ni batili kwa mujibu wa Uislamu(Kwamba, kuhesabiwa ni kwenda kinyume na maarisho ya Allah (S.W.T).
 
[h=3][/h]

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Moahmed Shein,akijiandikisha na familia yake kwa Karani Asia Hassan Mussa,(kushoto) katika zoezi la Sensa ya Watu na Makaazi, lililoanza leo nchini kote,Rais akiwa katika Shehia ya Migombani Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja,(kulia ) Mke wa Rais Mama Mwanamwema Shein, [Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]

Rais wa Zanzibar



Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mh Seif Shariff



Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mh Seif Iddi

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Moahmed Shein,na Mkewe Mama Mwanamwema Shein,pamoja na familia yao walipojiandikisha kwa katika zoezi la Sensa ya Watu na Makaazi, lililoanza leo nchini kote, wakiwa katika Shehia ya Migombani Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, [Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]

Na Rajab Mkasaba

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein pamoja na familia yake leo asubuhi wamekamilisha zoezi la sensa ya watu na makaazi linaloendelea nchi nzima hapo nyumbani kwake Migombani Mjini Unguja, na kuwataka wananchi kushiriki kikamilifu katika zoezi hilo.

Dk. Shein aliyasema hayo mara baada ya kukamilisha zoezi la sensa lililoanza katika Kaya yake hiyo, majira ya saa tatu na nusu asubuhi na kuweza kujibu masuala yote yaliokuwemo kwenye dodoso maalum lililotayarishwa kwa ajili ya zoezi hilo.

Dk. Shein akiwa pamoja na mama Mwanamwema Shein, alitoa pongezi na shukurani kwa uongozi, Maafisa na washiriki wote wa zoezi hilo muhimu linaloendelea nchini kote na kueleza jinsi lilivyoanza vizuri.

Katika maelezo yake, Dk. Shein alisema kuwa ana matumaini makubwa kuwa wananchi watatoa majibu na mashirikiano mazuri kwa maafisa wa sensa ili kufanikisha zoezi hilo muhimu kwa maendeleo ya nchi na wananchi wake kwa jumla.

Aidha, Dk. Shein aliwataka Maafisa wa sensa na wote watakaoshiriki katika zoezi hilo kuwa na subira kutokana na kazi ya zoezi hilo kuwa ngumu.

Akitoa neno la shukurani Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Bwana Mohammed Hafidh, alimshukuru Dk. Shein kwa kushiriki kwake kikamilifu katika zoezi hilo hali ambayo itakuwa ni darasa kwa wananchi wote kutokana na umuhimu wa zoezi hilo.

Mtwakimu huyo, alieleza kuwa zoezi hilo lilianza rasmi saa sita ya usiku wa kuamkia leo, zoezi ambalo lina madodoso ya aina tano kutokana na umuhimu wake mkubwa ambapo miongoni mwa madodoso hayo ni pamoja na lile lililoanza siku tatu kabla ya sensa.

Alieleza kuwa miongoni mwa madodoso hayo ni pamoja na dodoso la jamii, dodoso linalowahusu watu wasio makaazi maalum, dodoso linalohusu Kaya za Jumuiya pamoja na lile la Wasafiri.

Kwa mujibu wa maelezo yake Mtwakwimu Mkuu huyo alieleza kuwa matokeo ya awali ya zoezi hilo yanatarajiwa kutolewa Disemba 31 mwaka huu na taarifa zote za zoezi hilo linatarajiwa kukamilika baada ya miaka mitatu.

Pamoja na hayo, alizieleza aina mbili za dodoso zinazotumika ambazo ni dodoso fupi ambazo zitatumika kwa asilimia 30 na dodoso refu ambazo zitatumika kwa asilimia 70.

Katika taarifa yake aliyoitoa hapo juzi kwa wananchi, Dk. Shein alisema kuwa lengo la kukusanya taarifa za zoezi hilo ni kuiwezesha serikali kupanga mipango ya maendeleo, kutekeleza na kutathmini mipango iliyopangwa ili kubaini hatua iliyofikiwa pamoja na mafanikio yaliyopatikana.

Sambamba na hayo, Dk. Shein alimuomba Mwnyezi Mungu kujaalia amani, utulivu katika kulifanikisha zoezi hilo bila ya dosari ili sifa ya Wazanzibari ipande na kuwataka wananchi kudhihirisha uzalendo na ustaarabu wao kwa kushiriki kikamilifu katika sensa.

Pia, Dk. Shein aliitumia fursa hiyo kwa mara nyengine tena kuwasihi wananchi wote kushiriki kikamilifu katika zoezi hilo muhimu hapa nchini ambapo litaiwezesha serikali kupanga mipango ya maendeleo, kutekeleza na kutathmini mipango iliyopangwa ili kubaini hatua iliyofikiwa pamoja na mafanikio yaliopatikana.

Sensa ya mwaka huu itakuwa ni ya tano baada ya Muungano wa iliyokuwa Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar hapo mwaka 1964 ambapo sensa nyengine zilizotangulia zilifanyika mwaka 1967, 1978,1988 na mwaka 2002.

Miongoni mwa taarifa zinazokusanywa katika zoezi hilo ni pamoja na umri, jinsia, hali ya uzazi na vifo, ulemavu, hali ya makaazi na taarifa zinazohusu maisha ya kila siku ya wananchi pamoja na hali ya makaazi wanamoishi.



Imewekwa na MAPARA at 3:15 PM
 
Kwi Kwi Kwi! We mkali aya Ngoja na Mimi niape. Mimi naapa kutoa ushirikiano wangu katika kuhesabiwa na Nina suburi kwa hamu kuhesabiwa inshallah.


ALHAMDULILAHI. NIMEFAULU MTIHANI WA IMANI YANGU. NASHUHUDIA KUA HAPANA MOLA APASAE KUABUDIWA KWA HAKI ISPOKUA ALLAH(S.W) NA MTUME MUHAMAD (S.A.W) NI MJUMBE WAKE. LEO TAREHE 26 August,2012, mida ya 11:57 jioni, nimekataa kuandikishwa katika SENSA. NA AHIDI KUA NITABAKIA MUISLAMU MTIIFU KWA MOLA WANGU, NA VIONGOZI WENYE MAMALAKA MIONGONI MWETU SISI WAISLAMU. NIKOTAYARI KUITUMIKIA DINI YANGU YA KIISLAMU WAKATI WOWOTE NA MAHALA POPOTE NITAPO HITAJIKA. SIO GOPI MANENO WALA RISASI ZA MOTO. KILA NAFSI ITAONJA MAUTI. RABI TAKABALI.
 
Mbwembwe zote za nini hizi? ni nani alyekwambia anafuata chai kwako? sensa si lazima uwepo nyumbani mimi nilikuwa peke yangu nyumbani lakini kaya yangu wote wamehesabiwa ni mimi ndio nilikuwa natowa maelezo yao. au wewe ni muhaya?

Si mbwembwe ni ukarimu tu mama alinifundisha..mi mchaga mkuu.
Kwaiyo wapangaj wenzangu wanaeza kunijibia? Au kaya maana yake ni nini? Wao hawajui kama nna ng'ombe au la..kama nna watoto au la..sasa itakuwaje??!
 
Sasa mkubwa cha msingi jitoe muhanga ile wakija hata kesho wakute majivu kabisa kwa sabb sensa mpaka sku 7
 
ALHAMDULILAHI. NIMEFAULU MTIHANI WA IMANI YANGU. NASHUHUDIA KUA HAPANA MOLA APASAE KUABUDIWA KWA HAKI ISPOKUA ALLAH(S.W) NA MTUME MUHAMAD (S.A.W) NI MJUMBE WAKE. LEO TAREHE 26 August,2012, mida ya 11:57 jioni, nimekataa kuandikishwa katika SENSA. NA AHIDI KUA NITABAKIA MUISLAMU MTIIFU KWA MOLA WANGU, NA VIONGOZI WENYE MAMALAKA MIONGONI MWETU SISI WAISLAMU. NIKOTAYARI KUITUMIKIA DINI YANGU YA KIISLAMU WAKATI WOWOTE NA MAHALA POPOTE NITAPO HITAJIKA. SIO GOPI MANENO WALA RISASI ZA MOTO. KILA NAFSI ITAONJA MAUTI. RABI TAKABALI.
Unajisifia kujamba sokoni jitambue
 
Re: SENSA IMENIINGIZIA HASARA
Nimeamka mapema leo nikasema hata kanisani siendi. Nikajiandaa kufanyafanya usafi geto nkaandaa chai na mikate nkapaka mingine jam, peanut butter na mingine blubendi ile ya prestige. Chai niliandaa thermos moja ya rangi ingine maziwa.
Nikaenda kuoga kabisa nikaa kwenye kochi nasoma zangu kitabu cha "Tough times never last, but tough people do" by Robert H. Schuller.
Nimengoja weeeee mpaka saa nne nikampigia rafiki yangu anakaa pale karibu na ferry kabisa kumuuliza vipi labda wameanzia uko kwao so wamechelewa. Akanijibu bado. Basi nikasema watafika mchana.
Nikaenda sokoni fasta wasije wakanikosa wakija...nkanunua maini nusu kilo jamaniiii...nusu kilo maini unajua ni buku nne??! Dah ngoja nifute machozi...
Nkaja home fasta nkamuliza shem wamepita? Akanambia bado nkafurai mm basi fasta nkaingia jikoni kuandaa msosi..ugali maini na mboga ya mchicha pembeni food for four pipoz...
Nkafunika kwa hotpot kabisa. Sa sita..saba..nane..tisa..kumi...kumi namoja na sasa ni 17:43.
Muda wangu wa kwenda mazoezi umepita sijaenda nkidhan watakuja wasinikute. Mechi ya watani zangu Arsenali sijaenda kuangalia kisa wao...
Kwanini lakini wananifanyia ivi? Huku kigamboni vipi hampiti? Mmegoma? Mnawaogopa wapemba ama? Kwann lakini mmeniingiza hasara ivi..kama hamji si mngesema..
Mwenyekiti wa mtaa asubuhi alikua amefunga ofisi..nimepita apo mida hii kuna prado ipo nje wako ndan na nani sijui au mnataka kupika matokeo ya kigamboni?? Wallahi kama sihesabiwi haponi mtu...
Nmemwaga chai ile..naosha vyombo sasa. Najishauri mechi ya liverpool nikaichek ama nisiende? Je bado watakuja? Wanafunga kazi saa nhapi?
Kuanzia jumatatu ntakua natoka kazini jioni mno sasa itakuaje??
Dah...na hii lunch nan atansaidia kula? Heri ningepika wali ningeweka kwa fridge..sasa ugali naufanyiaje mm??!
Wai...jamanieee waambieni wavuke basi.
Au watanikuta kibanda cha kuoneshea mpira. Siezag kuqngalia mpira kwangu mm...inaboa.
Nalog off...mia. Heheh


una akili fupi..na ni bora usihesabiwe.
 
Karan wa sensa ameniuliza na namba yangu ya simu je na wenzangu mliohesabiwa mmeulizwa namba ya simu?????
 
Mtaendelea kubaki maamuma hivyo hivyo, kama mnadhani mnawakomoa wakristo mnajidanganya, bakini mnakunywa kahawa na kucheza bao, wenzenu wanapaa.
 
ALHAMDULILAHI. NIMEFAULU MTIHANI WA IMANI YANGU. NASHUHUDIA KUA HAPANA MOLA APASAE KUABUDIWA KWA HAKI ISPOKUA ALLAH(S.W) NA MTUME MUHAMAD (S.A.W) NI MJUMBE WAKE. LEO TAREHE 26 August,2012, mida ya 11:57 jioni, nimekataa kuandikishwa katika SENSA. NA AHIDI KUA NITABAKIA MUISLAMU MTIIFU KWA MOLA WANGU, NA VIONGOZI WENYE MAMALAKA MIONGONI MWETU SISI WAISLAMU. NIKOTAYARI KUITUMIKIA DINI YANGU YA KIISLAMU WAKATI WOWOTE NA MAHALA POPOTE NITAPO HITAJIKA. SIO GOPI MANENO WALA RISASI ZA MOTO. KILA NAFSI ITAONJA MAUTI. RABI TAKABALI.

Wewe ni taahila. Huu upuuzi wako wapelekee wakeo
 
maisha yenyewe yanawapiga wengi wenu badala ya kuhesabiwa ili ijulikane jinsi mtavyosaidiwa eti mnagoma hammkomoi mtu mnawaharibia watoto wenu maisha kwani mtawajengea hiyo imani ambayo hakika hawata fika popote pale
 
Back
Top Bottom