Selfika na JF: Snap it. Show it

Kwa kweli tunaangamizwa kwa kukosa maarifa. Kuokoka au kuabudu kanisa fulani sio immune ya kutokutenda dhambi; ni vile tayari nafsi yako tayari umeshaitengeneza inakuwa "conscience" kuomba rehema na toba pale unapotenda dhambi. Ndiyo maana sio tu waumini; hata Watumishi wengi wa Mungu wanatenda dhambi; hadi mimi najiona malaika kwa muda. " for all have sinned and fall short of the glory of God". Fact kwamba umeokoka, haimaamishi kwamba ndiyo umeshafika mbinguni sasa; wapo wengi walioacha wokovu njiani.

Fact kwamba mtu hajaokoka leo, haimaanishi kwamba hawezi akaokoka kesho. Tena kuna watu wanaweza wakaokoka nyuma yako, na wakasimama na Mungu imara kuliko hata wewe. "Anayesamehewa sana, hupenda sana". So kuna watu ambao leo unaweza ukawaona ni watenda dhambi wakubwa; lakini siku wakitubu na kusamehewa; humpenda Mungu sana na kumshika sana.

Ukimuona mtu hayupo kwenye njia salama; unamuonya na kumuelekeza kwa hekima. Sio unafika kwa mtu afu unaanza kumwambia "huko unaposali umepotea ndugu yangu, hakuna Mungu". Au ndiyo wale wanakutenga kabisa kwa sababu huamini pamoja nao. Humsaidii mtu unayemuona anapotea kwa kumtenga Wakati mwingine matendo yako mema, yanaweza yakawavuta watu wakaja kwa Mungu wako. Tusipende kujiona watakatifu sana, ilhali kila mmoja wetu anajua matendo yake anayoyafanya huko sirini. "Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke". (1 Korintho 10:12)

Na hii ni kwetu generally; tuna katabia ka kuona wale wanaofanya dhambi tofauti na za kwetu ndiyo watenda dhambi sana kutuzidi. Yaani unajiona wewe ni bora kwa sababu unasengenya na mwenzako ni mzinzi; but mwisho wa siku ninyi wote wawili mnastahili mauti kama mshahara wa dhambi zenu. So kila mmoja ajichunguze, apigane vita yake taratibu. Dhambi za mtu mwingine hazikufanyi wewe kuwa mtakatifu.

"Amin nawaambia, watoza ushuru na makahaba wanatangulia mbele yenu kuingia katika ufalme wa Mungu". (Mathayo 21:31)


 
Dini ni upotoshaji wa watu weupe tu, kuna kitu walitaka kutufanya ili tukae sawa wakaona tu waseme, "mpende Bwana Mungu wako, kwa moyo wako wote, kwa akili zako zote na kwa nguvu zako zote...na jirani yako kama NAFSI yako." Just imagine unaambiwa umpende jirani yako kama NAFSI yako...never on earth, haipo hiyo!

Lakini hawa mabwana wakaleta hizo mambo wakapata nafasi ya kututawala mwanzo mwisho.

The question is, binadamu akifa anaenda wapi....ng'ombe akifa anaenda wapi"?
 
Mungu ameweka tofauti kati ya binadamu na viumbe wengine kama ng'ombe.
Wewe amekupa maisha mengine baada ya kifo.
 
☺️☺️.. . Kuna maisha ya mtu binafsi na Mungu wake - tukizungumzia MKRISTO hatuzungumzii dini, bali tunazungumzia uhusiano wa mtu binafsi na Mungu. Tunapo zungumzia Dini ni mfumo ambao mwadamu kauweka ili kutengeza chanel ya mtu au kikundi katika kufikisha elimu ya kiungu.. Dini - Earthly system katika elimu ya Mungu.. Mungu hana dini, Mungu ana uhusiano na watu wake na katika mahusiano ya mtu na Mungu, Mungu ana principal zake za uhusiano wake na watu wake
 
Ntakuwa sisimami Stop over oooh
Unanipiga kamba


Usidanganyike, kifo kwa mwanadamu hakina tofauti na mnyama mwingine yoyote, coz hata sisi ni wanyama tu..tumeongezewa utashi kidogo tu lakini bado elements za unyama tunazo.
kwahiyo unaamini ukifa ndio basi hautafufuliwa tena na Kristo??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…