Sasa kama ulijua kwenye ujambazi kuna kutenguka viuno kwanini ulimpa uhuru wa kuchagua halafu uje umuadhibu kwa uchaguzi aliofanya! Hapa siyo suala la mtoto kumlaumu baba bali ni baba kumuadhibu mtoto kwa uhuru aliompa mwenyewe!
Ukishasema wewe siyo dikteta na ukampa mtu uhuru wa kuchagua hiki au kile basi haupaswi kumuadhibu kwa uchaguzi atakaoufanya! Ukimuadhibu unarudi pale pale kwenye udikteta maana yake kumbe ulitaka achague hiki tu na siyo kile!