Hii verse ya kwanza naielekeza kwa Sarah wangu, mwanamke aliyetekaga moyo wangu kisawasawa..
Last year was remarkable, Kipenzi changu Sarah alifanya maamuzi ya kibingwa kuamua kuolewa na kidume kingine
I wish her all the best, huku akishushia na hii ngoma...
Sarah bhana!
Hello, Hello baby
Mmmh mmmh
Natamani niandike barua na niitume kwako
Ila nahisi hutaisomaa, utaikataa
Hata simu nitajisumbua, kupiga namba yako
Maana hata ukiiona utaikata
I wish yawe ndoto, haya ninayo yapitia
Ama nirudi utoto imenisonga dunia
Eti kurwa bila ndoto, hivi ni wapi ntaanzia?
Kulia bila kushoto, sijawai kusikia
Eeh, imagine siwezi kukuota (Aaah aah aah)
Maana ata usingizi sina (Sinaa)
Mwenzako wataniokota (Aaah aah aah)
Maji yamenizidi kina (Mwenzenu mimi)
Mpaka kesho, eeh eeh
Mpaka kesho, umeniganda mawazoni
Mpaka kesho, bado nakuwazaa
Mmh mmh eeh