Selfika na JF: Snap it. Show it

Selfika na JF: Snap it. Show it

Mimi hizo ndizi nakula Mara chache Sana usiku..Mara nyingi Ni wali.
Pilau Mara nyingi weekend j2.
Chipsi Ni kama breakfast yangu.
Kuna watu huwa wanasema chipsi za kujipikia hazinogi.. Mimi huwa zinanoga vizuri tu na huwa hazinikinai..Tena nikikata na kachumbari Basi jiko Zima linanukia.
Mchana wangu haujakamilika Bila ugali,ugali wa kwetu mlaini wa unga wa mahindi ya kulowekwa

Sent using Jamii Forums mobile app
IMG_20200125_131603.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kijijini mahindi mnalima wenyewe. Hili Dona letu mahindi hujui yamekaa muda gani kwenye ghala au yamewekwa dawa gani
Mimi Kijiji nilichozaliwa ilikuwa hakuna Dona Wala sembe.
Iliaminika kwamba mtu anayesaga Dona Ni yule ambaye Ana njaa na ameishiwa mahindi,katika kubana matumizi anajitahidi anasaga Dona..
Ugali wa Dona haumalizi Sana unga.
Na ndivyo ilivyokuwa.

Mahindi yakikobolewa na kupelekwa nyumbani,yanalowekwa Kwenye maji hata siku 2 Hadi 3,yanaoshwa yanaanikwa halafu yanasagwa.
Unga ukitoka mashineni unaanikwa Tena ,unachekechwa tayari kwa matumizi.
Huu unga Ni mweupe Sana na ugali wake mlaini ila unga unaisha haraka Sana.
Safari za mashineni haziishi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom