CHino umenikumbusha hapo, nilikuwaga na kampani ya kutoka, ya kaka mmoja wa kichaga bwana. Rafiki sana, sasa siku hiyo sikuwa nataka kutoka kabisa.
Akasema twende hapo, nikaenda nilikunywa kupita my limit. Yaani yule rafiki aliniambia kama hukufa ile siku, bado una maisha marefu!!!
Nilitoka pale London, kasi huwa anatabia ya kunisindikiza nyuma mpaka getini, mlinzi afungue geti naye anaondoka.
Ila hiyo siku nilimuachia vumbi π€£π€£π€£π€£π€£ fikiria pale External palivyo chinja chinja usiku. Sikusimama nilikunja kama niko highway tu.
Magari mengine yote ilibidi yasimame, bila hivyo ningefia pale, asubuhi nauliza nimefikaje home? Sijui nimejikuta nimelala na ndiyo siku nilikunywa kupitiliaza. Umenikumbusha hii siku Chino!!!