Selfika na JF: Snap it. Show it

Lol hizi Kamera tyuu mkuu!
Niko flat kabisa mimi!!
Kazini navaa mibwanga sitaki makwazo na watuuu!!
 
Hahha ndugu mwenyew nipo kama wew nimekiweka ndani kwanza hata sielew 😂😂😂😂
 
Duuh mimi sitasahau mwaka fulani kuna siku nilikuwa gerezani pale usiku, ilikuwa msimu wa mvua na kama unavyojua huu mkoa mvua zikinyesha, mafuriko na foleni kila kona plus shida ya usafiri mwee

Mimi nilikuwa natoka gerezani naenda morocco, sasa siku hiyo sijui waliamua kutukomoa abiria wa morocco, mwendokasi zote za morocco wakazipeleka kimara na mbezi yani tulipangishwa foleni tu

Nahisi waliona abiria wa morocco ni wachache hivyo wakatuweka pending kwanza, basi abiria wa kimara na mbezi nao hawapoi ilikuwa ni bumper to bumper, ikijaza moja iking'oa inayofuata nayo haikai dakika mbili inajaza inang'oa

Hapo unasikia wanatangaza abiria kituo cha kwanza ubungo terminal na bado imejaa dadeki, maana yake hiyo ni express ninyi mnaoshuka katikati hapo sijui fire hadi shekilango msipande, maana haishushi kiumbe

Daah yani katika siku nilizowahi kupanda mwendokasi nikakutana na kadhia ile siku sitakaa niisahau asee
 
Pale gerezani jioni Kuna kugombania magari utadhani watu wanapambania ufalme wa mbinguni 🤣

Morocco huwa ni wachache sana..ile route huwa naitamani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…