Selfika na JF: Snap it. Show it

Nimeipenda hii:

Huko nyuma katika siku ambazo Ujerumani iligawanywa, ukuta mkubwa ulitenganisha Berlin ya Mashariki na Magharibi.

Siku moja, baadhi ya watu katika Berlin Mashariki walichukua shehena ya lori la taka na kuzitupa upande wa Berlin Magharibi.

Watu wa Berlin Magharibi wangeweza kufanya jambo lile lile, lakini hawakufanya. Badala yake walichukua shehena ya lori la bidhaa za makopo, mkate, maziwa na vyakula vingine, na kuvipanga vizuri upande wa Berlin Mashariki. Na juu ya safu hii waliweka bango hili

β€œKILA MMOJA HUTOA ALICHO NACHO”

Huh ni ukweli mtupu! Unaweza tu kutoa kile ulichonacho.Una nini ndani yako?

Ni chuki au upendo?
Jeuri au amani?
Kifo au uzima?
uwezo wa kujenga au uwezo wa kuharibu?
Umepata nini kwa miaka mingi?

"KILA MMOJA HUTOA ALICHONACHO"

Fikiria juu yako!

Kuwa na siku njema![emoji173]
 
Kaka nitumie linki nisome uzi zako zile za elimu ya asili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…