Selelii awazima Lowassa na Rostam

Mkandara,

Unaweza kuwa sahihi kwamba RA hata angepelekewa polisi bado angekataa kuhojiwa lakini pia huwezi kujua ukweli bila kujaribu.

Kwa mhusika mkuu kama inavyoonyesha sasa kwenye baadhi ya taarifa, mimi naamini ingekuwa busara kuomba amri ya bunge kumhoji RA baada ya kukataa kuitikia ombi la kwanza.

Sio kwasababu akina RA hawafuati sheria basi na sisi tunaojifanya ni waumini sheria tuamue kupambana nao kwa kukiuka sheria hizo hizo.

Ushahidi wa kiapo wa RA ungelikuwa muhimu mno.

Lakini kikubwa zaidi ifike mahali tuachane na mambo ya Richmond na kusonga mbele. Kama tumeshindwa kuwafunga wahalifu ni bora tukakubali ukweli huo. Lakini kama kuna njia zingine za kuwawajibisha basi zifanyike haraka. Tumepoteza muda mrefu mno kujadili jambo moja huku wananchi wanaendelea kuteseka kwa matatizo mbalimbali. Maamuzi ya wanasiasa wanawajibika wakati wa kura. Kama JK ameshindwa kumshughulikia RA basi kilichobaki ni kumshitaki kwa wapiga kura mwaka 2010. Huu mduara imefika mahali imekuwa sanaa, inafurahisha macho na masikio yetu lakini haumwongezei tija Mtanzania wa kawaida.

Mtanzania, yote hayo nakubaliana nawe. Hata hivyo kuna jambo moja ambalo naona umeliruka... nalo ni nia ya hawa wahujumu uchumi. Lengo lao kubwa hivi sasa ni kujisafisha kwa hayo maovu kwa uwezo na mbinu zozote wanazoweza. Na kibaya zaidi ni nia yao ya kujisafisha kwa lengo la kuwaharibia wote waliowafichua na kuwaanika hadharani. Maelezo ya Mh. Selleli yanaonesha nia yao hii. Tumeshindwa kuwafikisha lupango, sawa, lakini kamwe tusiwaruhusu waonekane ni kondoo weupe machoni pa jamii.
 
SteveD,
Mkuu wangu mimi huwa siachi vitu vikielea hadi ijulikane. Wayahudi walikuwa watumwa miaka zaidi ya 1000 huko Soiuth Kutawaliwa zaidi ya miaka 500 lakini wazo la kujikomboa lilikuwepo kila siku yan maisha yao pamoja na kwamba mambo mengine yaliendelea. Kusema tusahau ni kukubali kushindwa na hatuwezi kusogea mbele hata kidogo...Mawazo ya Mtanzania ni mawazo ya mkata tamaa ambaye anaona botra liende ndio kilichobakia.
 
Watetezi wa mafisadi wamekuja kwa nguvu kubwa sana leo ili kuwapamba na kuwatetea mafisadi hapa jukwaani, lakini nimefarijika sana na mchango mkubwa toka kwa wale ambao wameweka mbele maslahi ya nchi yetu na kutokubali utetezi finyu toka wapambe wa mafisadi. Hii inatia moyo sana na kuonyesha kwamba Tanzania bila mafisadi inawezekana kabisa kama tukiamua kupambana nao na kutowapa nafasi ya kubadilisha ukweli wa mambo kama ambavyo unajulikana.

Alutta Continua!
 
hivi hii nchi ina vyama vya upinzani kweli? au wapo tu wanatolea macho hela za ruzuku ndio maana kila mtu anakuja na chama chake kila siku? kuwa na chama cha siasa umekua mtaji sasa badala kuja kupigania mabadiriko ndani ya nchi.kila kitu kipo wazi no actions.vyama vya upinzani vina uwezo wa kumpa changa moto raisi mpaka hatua zichukuliwe na hapo sisi wananchi tutapata nguvu ya kuwaunga mkono.lakini huu mchezo wa kila siku mambo yanafanyika na tunapiga gumzo tu na siku zinakwenda ndio maana tunafuga viongozi wa ajabu mpaka leo.majina yale yale serikalini yanazunguka tu.

kama raisi anaogopa kuchukua hatua baada kupewa ushaidi kwanini aliangaika kuomba tume iundwe ya kufanya uchunguzi?

Ndugu AS naomba nikuulize swali rahisi. Ulijiandikisha kupiga kura kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa? Na ulimpigia kura nani? Wengi wetu tunaolalamika kwamba vyama vya upinzani vimelala huwa hata hatushiriki kwenye chaguzi. Tunakubali kuchaguliwa viongozi wetu halafu tuko wepesi sana kutupa lawama mambo yanapoenda mrama.

Ndugu yangu kuanzisha chama haina maana kupata ruzuku. Unapata ruzuku baada ya kushinda kwenye uchaguzi. Ni vyama vinne tu kati ya 17 vinavyopata ruzuku. Na huo uwezo wa kumpa changa moto raisi mpaka hatua zichukuliwe ni upi? Kwa maandamano? au kwa kulalamika kwenye majukwaa na magazetini? Unaniogopesha sana unaposema unasubiri vyama vya upinzani vifanye kazi halafu uje kuwaunga mkono baadaye. Baadaye??? Kazi ya kuikomboa hii nchi ni yako wewe mweyewe na sio ya vyama vya upinzani. Vyama vya siasa vinakupa wewe fursa. Usipoitumia usimlalamikie mtu yeyote isipokuwa wewe mweyewe.

.
 
Nemesis,

Hapana, mimi niliridhishwa sana na report ya Mwakyembe na hata ukiangalia mijadala yote ya huko nyuma utaona hilo. Tatizo langu kwasasa ni hizi taarifa mpya zinazotoka na ambazo mimi naziita ni missed opportunity kwasababu laiti zingefuatiliwa zaidi huenda tungekuwa tumeukata mzizi wa fitina wa akina RA kimoja.

Kama RA ndiye kweli pesa zililipwa kwake na mpaka hata kufuatilia hizo pesa hazina, mbona ingekuwa busara kumhoji na kupata ushahidi wake kisha kupendekeza apelekwe mahakamani? Matatizo mengi tunayokumbana nayo sasa ni kwasababu ya hiyo missed opportunity.

Kuna jamaa aliwahi kusema wakati mzuri wa kulinda sheria ni pale zinapomuokoa mbaya wako. Unapo deal na watu ambao kwa njia moja ama nyingine kunaweza kuwa na tofauti zenu, inabidi kuwa makini kuhakikisha wanapewa kila opportunity ya kujitetea. Hata mimi naamini wakati mzuri wa kuitetea sheria ni pale inapomuokoa mbaya wako.
hii kazi inatakiwa ifanywe na serikali baada ya kupewa report na maamuzi ya bunge sasa lawama zozote ni vizuri ukazipeleka kunako husika, serikali kwa kushindwa kutumia madaraka, nguvu na haki za kufanya hivyo. serikali ina takukuru, usalama wa taifa, polisi na mahakama. ukiwa kiongozi mzuri sema ukaletewa report na takukuru iliyo na ulakini utamrudishia aliye kuletea pamoja na point unazo taka zifuatiliwe. hivyo mapungufu yote yapo juu ya serikali.
 
Mtanzania, yote hayo nakubaliana nawe. Hata hivyo kuna jambo moja ambalo naona umeliruka... nalo ni nia ya hawa wahujumu uchumi. Lengo lao kubwa hivi sasa ni kujisafisha kwa hayo maovu kwa uwezo na mbinu zozote wanazoweza. Na kibaya zaidi ni nia yao ya kujisafisha kwa lengo la kuwaharibia wote waliowafichua na kuwaanika hadharani. Maelezo ya Mh. Selleli yanaonesha nia yao hii. Tumeshindwa kuwafikisha lupango, sawa, lakini kamwe tusiwaruhusu waonekane ni kondoo weupe machoni pa jamii.

SteveD,

Aliyehukumiwa atajisafisha vipi kama hakuna kukata rufaa? Lowassa na RA wamehukumiwa, hata mijadala ya Richmond ikiisha sidhani kama wana nafasi ya kujisafisha. Labda sisi wananchi wenyewe tuamue tu kwamba tumewasamehe.

Mimi kusema wacha twende mbele ni kwa pande zote mbili wakiwemo hao watuhumiwa. Walikuwa na miaka mitatu ya kujitetea na kama hawajasafishika sidhani kama itasaidia kitu hata kama huu mjadala ukijadiliwa miaka 10.

Hili suala lote linaangukia kwa rais maana bunge hata lifanye nini, haliwezi kuilazimisha serikali kufuata mapendekezo yao yote. Labda waamue kupiga kura ya kutoikuwa na imani na serikali na kuitisha uchaguzi mwingine kitu ambacho nina wasiwasi kama wabunge wana guts hizo.
 
SteveD,

Aliyehukumiwa atajisafisha vipi kama hakuna kukata rufaa? Lowassa na RA wamehukumiwa, hata mijadala ya Richmond ikiisha sidhani kama wana nafasi ya kujisafisha. Labda sisi wananchi wenyewe tuamue tu kwamba tumewasamehe.

Mimi kusema wacha twende mbele ni kwa pande zote mbili wakiwemo hao watuhumiwa. Walikuwa na miaka mitatu ya kujitetea na kama hawajasafishika sidhani kama itasaidia kitu hata kama huu mjadala ukijadiliwa miaka 10.

Hili suala lote linaangukia kwa rais maana bunge hata lifanye nini, haliwezi kuilazimisha serikali kufuata mapendekezo yao yote. Labda waamue kupiga kura ya kutoikuwa na imani na serikali na kuitisha uchaguzi mwingine kitu ambacho nina wasiwasi kama wabunge wana guts hizo.

Salute!
 
Mtanzania,
nakubali maneno yako isipokuwa hapa tu..
Mimi kusema wacha twende mbele ni kwa pande zote mbili wakiwemo hao watuhumiwa. Walikuwa na miaka mitatu ya kujitetea na kama hawajasafishika sidhani kama itasaidia kitu hata kama huu mjadala ukijadiliwa miaka 10.
Mkuu wangu historia ya maovu haina muda, tutavieleza hata vijukuu vyetu na itaendelea hivyo hivyo kujadili mabaya ya Ufisadi kuliko kuyakubali yaishe..kwa kila hatua na kila atakayekumbuka jambo.. Hata wale walioficha mwanzoni kwa hofu ya Utawala, tutayapokea mawazo yao.

akuna hata siku moja Fisadi alisafishika, ni jukumu letu kuonyesha na kuendela kukemea maoivu..
Mkaburu walivyoweka Apartheid hawakuamini wala kukubali kwamba ni makosa na isingewezekama kusafishwa nchi hiyo kama wananchi wake wangekubali yaishe..Hayatakwisha na wala hatuta shake mikono na shetani kwani ni dalili yetu kukubaliana na Ushetani.
 
SteveD,
Mkuu wangu mimi huwa siachi vitu vikielea hadi ijulikane. Wayahudi walikuwa watumwa miaka zaidi ya 1000 huko Soiuth Kutawaliwa zaidi ya miaka 500 lakini wazo la kujikomboa lilikuwepo kila siku yan maisha yao pamoja na kwamba mambo mengine yaliendelea. Kusema tusahau ni kukubali kushindwa na hatuwezi kusogea mbele hata kidogo...Mawazo ya Mtanzania ni mawazo ya mkata tamaa ambaye anaona botra liende ndio kilichobakia.

Mkandara,

Kwenye management kuna kitu kinaitwa SATISFICING, ni uamuzi wako kufukuzia optimum ambayo haikamatiki au kukubali adequacy ambayo ni achievable. Ukiniuliza mimi nitachagua the later, hata kama utaniita ni mkata tamaa.

Tumeona ya akina Chiluba dola $13m kutumika kufukuzia case ya laki tano. Nikipewa chaguo, nitazitumia hizo $13m kujenga shule au hospitali kuliko kumfukuzia mtu mmoja ambaye hata sina uhakika wa kumfunga.
 
Mkandara,

Kwenye management kuna kitu kinaitwa SATISFICING, ni uamuzi wako kufukuzia optimum ambayo haikamatiki au kukubali adequacy ambayo ni achievable. Ukiniuliza mimi nitachagua the later, hata kama utaniita ni mkata tamaa.

Tumeona ya akina Chiluba dola $13m kutumika kufukuzia case ya laki tano. Nikipewa chaguo, nitazitumia hizo $13m kujenga shule au hospitali kuliko kumfukuzia mtu mmoja ambaye hata sina uhakika wa kumfunga.
tatizo lako ni gharama gani badala ya kuangalia maradha gani yanatokea... Ndio hayo ya samaki Sangara..Mkuu Ya Chiluba yaligharimu UsD 13m lakini wameponyesha billioni nyingine...unatazama karibu sana mkuu wangu.

Well thats You kwa sababu nijuavyo mimi upo upande wa makaburu (CCM)hivyo ni vigumu sana kwako kuelewa harakati na machungu ya wananchi wakati wa Apartheid..
 
Nadhani itafikia wakati inabidi tuchague watu wa kuwajibu au kuwaelimisha.

Bob, angalia wewe na Bubu ataka kusema msije mkawa mnapoteza muda wenu bure. Angalia unajadiliana na nani.

Mkuu FairPlayer,

Nashukuru umeliona hilo. Wanajibizana na "Ufisadi motion neutralizers" wa JF.

Tiba
 
Mkuu FMES,


Nikija kwenye point yako, nitashukuru ukinitafutia paragraph inayoongelea masuala ya pesa za Richmond kuingia kwenye account za kampuni za RA na yeye mwenyewe kufuatilia hizo pesa hazina. Mimi sijaiona na nitakuwa happy kusahihishwa kwa facts.

- Mkuu samahani kwamba muda wa kwenda kukutafutia ripoti nzima ambayo kuna wakati niliichambua sana hapa mpaka kuthshiwa na Lowassa na Rostam wenyewe sina, isipokuwa ninajua kwamba ukiwaomba Mods wanawezaa kukuchambulia ilipo yaani ripoti na ule uchambuzi nilioutoa baada ya ile ripoti.

- Lakini nijuavyo ni kwamba tatizo sio ushahidi wa kumkamata Rostam, wala kwangu tatizo sio Mwakyembe, tatizo ni serikali yaani Rais na Waziri Mkuu wake, kamati ilifanya kazi nzuri sana na bunge kwa kauli moja likaidhinisha ile ripoti na kutoa mapendekezo ya kufanyiwa kazi ikiwa ni pamoja na kuwwajibisha wale wote waliohusika, sasa iweje tena hili liwe tatizo la bunge tena au kamati ya Mwakyembe?

- Hili sasa ni tatizo letu wananchi wote wa Tanzania, ingakuwa nhci zingine ambazo wananchi hawana mchezo hwa viongozi wetu wasingerudi tena kwenye siasa, ila kwa kuwa ni Tanzania tutaendelea kulamiana na kushia kuwachagua wale wale hasa Kikwete, tena atarudi kwa tsunami!

Respect.


FMEs!
 
Mkandara,

Kwenye management kuna kitu kinaitwa SATISFICING, ni uamuzi wako kufukuzia optimum ambayo haikamatiki au kukubali adequacy ambayo ni achievable. Ukiniuliza mimi nitachagua the later, hata kama utaniita ni mkata tamaa.

Tumeona ya akina Chiluba dola $13m kutumika kufukuzia case ya laki tano. Nikipewa chaguo, nitazitumia hizo $13m kujenga shule au hospitali kuliko kumfukuzia mtu mmoja ambaye hata sina uhakika wa kumfunga.

Mtanzania, hapa ndipo hapo academic management ya kikampuni au kibiashara inatofautiana na management katika mambo ya siasa. Kwenye siasa na uongozi kitaifa kuna sovereignty, usawa, haki, freedom na uzalendo. Mambo haya hayanunuliki au kuwa mambo ya pick and mix kwa ajili ya kumaximize profit. Hapana mkuu. Naikubali kabisa technique hii as applied in management books lakini si katika kutunza hadhi ya Taifa. Ukifata hiyo kwenye siasa, utauzwa na kuishia kuwa mtumwa.

Kwa mfano wako wa Chilluba, je ungelipenda tuwafungulie wahalifu kutoka jela kwa vile tunaweza kusave pesa nyingi? Katika hili mimi nachoose kuwa masikini jeuri lakini haki inakuwa imetendeka.
 
tatizo lako ni gharama gani badala ya kuangalia maradha gani yanatokea... Ndio hayo ya samaki Sangara..Mkuu Ya Chiluba yaligharimu UsD 13m lakini wameponyesha billioni nyingine...unatazama karibu sana mkuu wangu.

Well thats You kwa sababu nijuavyo mimi upo upande wa makaburu (CCM)hivyo ni vigumu sana kwako kuelewa harakati na machungu ya wananchi..
Mkandara,

Nilifikiri tunajadili hili kwa maslahi ya taifa kumbe ni kwa maslahi ya CCM au CHADEMA?

Kwa wengine vyama vya siasa havina maana kabisa, what matters ni delivery on the ground. Binafsi niko tayari kufanya kazi na mtu yeyote anayethamini kazi kwa faida ya wananchi wote.

Kuna watu hapa JF ambao hata siku moja sita question motives zao maana wanachoandika leo hakina tofauti na walichoandika 2005 kule business Times.

Ifike mahali tuachane na haya ya finger-pointing na kuweka concentration kwenye hoja iliyoko mbele yetu.

Wacha nimalizane na huu mjadala na kurudi msituni kupigana kule Kyela.
 
Nemesis,



Kama RA ndiye kweli pesa zililipwa kwake na mpaka hata kufuatilia hizo pesa hazina, mbona ingekuwa busara kumhoji na kupata ushahidi wake kisha kupendekeza apelekwe mahakamani? Matatizo mengi tunayokumbana nayo sasa ni kwasababu ya hiyo missed opportunity.

inabidi kuwa makini kuhakikisha wanapewa kila opportunity ya kujitetea. Hata mimi naamini wakati mzuri wa kuitetea sheria ni pale inapomuokoa mbaya wako.

- Mkuu matatizo tuliyonayo sasa ni kwamba Rostam ni rafiki wa Rais, wala sio sheria au anything na wala hakuna missed opportunity hapo, Mahalu hakuwa rafiki wa Rais na sheria yote imefuatwa mbona hajafungwa mpaka leo?

- Balozi Mwanjabala hakuwa Rafiki wa Rais, serikali ilimthibiti mara moja kutokana na ripoti ya mkaguzi wa mahesabu, ambayo ni ripoti hiyo hiyo imekwama kumthibiti Mahalu kwa sababu alikuwa ni Rafiki wa Rais wa zamani Mkapa, ingawa Rais wa sasa alimfukuza kazi na kutishia kumfunga lakini sio siri kwamba Rais wa zamani aliingilia kati na mpaka leo haieleweki kina nini huko na kesi yake!

- Tusijaribu kutafuta visingizio vya sheria kwa vitu ambavyo viko wazi kabisa kwamba ni urafikiwa watuhumiwa na Rais ndio unatuletea taabu na sisi wananchi we are helpless na kulilia wapiganaji!

Respect.


FMEs!
 
Mtanzania,
Kwanza samahani maanake niseme ukweli kwamba maandiko yako mengi sana yamekaa ki CCM sana na mara nyingi umekuwa against hizi kuhudi za kuendelea kuwaumbua hawa mafisadi. I can only ask - What's UP!

Mkuu hoja ni UFISADI, na haiwezi hoja hii kutupwa kapuni pasipo kuwashughulikia mafisadi. Nitazidi kusema Mapinduzi yoyote huanza na wananchi ambao wako tayari kuzungumzia uovu huo mbele ya sheria inayokataza ama kupuuza juhudi hizo. Lowassa na Rostam ni baadhi ya wahusika na kwa sababu wao ni wana CCM, chama kinachoongoza ni lazima mkazo wetu ubakie ktk target hiyo. Wengine wote ni wafuasi tu ambao wamekubali hali halisi kama vile kule South kuna weusi waliojiunga na jeshi la Kaburu na kufanya hata mauaji. Mkazo wa ANC ulikuwa kukiondoa chama tawala madarakani na hapo ndipo wewe unapoingiza upinzani ktk fikra zangu..

Inanisha mshangao sana unapokazania YAISHE! hii lugha ni ya kukata tamaa ambao haitakiwa kwa mpiganaji na nikutokana na hofu hiyo ndio maana mnawapa chat wapiganaji 11. Binafsi sioni sababu kwa nini isiwe wapiganaji millioni ukiwa nawe upande wao.
 
SteveD,

Aliyehukumiwa atajisafisha vipi kama hakuna kukata rufaa? Lowassa na RA wamehukumiwa, hata mijadala ya Richmond ikiisha sidhani kama wana nafasi ya kujisafisha. Labda sisi wananchi wenyewe tuamue tu kwamba tumewasamehe.

Mimi kusema wacha twende mbele ni kwa pande zote mbili wakiwemo hao watuhumiwa. Walikuwa na miaka mitatu ya kujitetea na kama hawajasafishika sidhani kama itasaidia kitu hata kama huu mjadala ukijadiliwa miaka 10.

Hili suala lote linaangukia kwa rais maana bunge hata lifanye nini, haliwezi kuilazimisha serikali kufuata mapendekezo yao yote. Labda waamue kupiga kura ya kutoikuwa na imani na serikali na kuitisha uchaguzi mwingine kitu ambacho nina wasiwasi kama wabunge wana guts hizo.
lowasa haku-hukumiwa report ilisema ajipime mwenyewe kama mtu mwenye busara na kiongozi wa serikali.
 
Mtanzania, hapa ndipo hapo academic management ya kikampuni au kibiashara inatofautiana na management katika mambo ya siasa. Kwenye siasa na uongozi kitaifa kuna sovereignty, usawa, haki, freedom na uzalendo. Mambo haya hayanunuliki au kuwa mambo ya pick and mix kwa ajili ya kumaximize profit. Hapana mkuu. Naikubali kabisa technique hii as applied in management books lakini si katika kutunza hadhi ya Taifa. Ukifata hiyo kwenye siasa, utauzwa na kuishia kuwa mtumwa.

Kwa mfano wako wa Chilluba, je ungelipenda tuwafungulie wahalifu kutoka jela kwa vile tunaweza kusave pesa nyingi? Katika hili mimi nachoose kuwa masikini jeuri lakini haki inakuwa imetendeka.

SteveD,

Hapana, sio kwenye makampuni tu bali hata serikali. Mfano ni hapa UK kwenye money for peerages na Blair. Kulikuwa na ushahidi lakini prosecutor akaona uwezo wa kushinda ni mdogo, akaamua kuiachia case.

Hicho ndio ninachoongelea mimi, ni tofauti na kuwaachia wahalifu ambao wamehukumiwa au kutumia pesa nyingi kumhukumu na kumfunga mhalifu. Kama unaona uwezo wa kumfunga ni mdogo, ni bora kutumia hizo pesa kwenye mambo ya maana.

Kama tumekubali suala la akina RA mwamuzi ni JK, ifike mahali tumwachie yeye na sisi wananchi tutoe hukumu yetu 2010.
 
SteveD,

Hapana, sio kwenye makampuni tu bali hata serikali. Mfano ni hapa UK kwenye money for peerages na Blair. Kulikuwa na ushahidi lakini prosecutor akaona uwezo wa kushinda ni mdogo, akaamua kuiachia case.

Hicho ndio ninachoongelea mimi, ni tofauti na kuwaachia wahalifu ambao wamehukumiwa au kutumia pesa nyingi kumhukumu na kumfunga mhalifu. Kama unaona uwezo wa kumfunga ni mdogo, ni bora kutumia hizo pesa kwenye mambo ya maana.

Kama tumekubali suala la akina RA mwamuzi ni JK, ifike mahali tumwachie yeye na sisi wananchi tutoe hukumu yetu 2010.
Mkuu haya unazungumza kwenye nchi yenye SHERIA. Hatufanani katu ni mbingu na ardhi.
Sisi vita yetu ni kusimamisha sheria na hapa (kwa mafisadi) ndipo tunapoanzia.
 
Sera ya CCM kwa muda mrefu sasa imekuwa ni kulindana. Kama sio kulindana tusingekuwa na ubabaisha kwenye hili suala la Richmond mpaka leo. Rostam, Lowassa na Kikwete walikuwa kitu kimoja kwenye uchaguzi wa 2005. Urafiki wao haukuanzia barabarani kama Lowassa alivyosema. Wana siri zao. Wanalindana. Ukimwangusha mmoja naye anaweza kuwaangusha wenzake. Hivyo wataendelea kulindana. Kamati ya Mwakyembe ililmpibu JK, JK amekula pozi. Anavuta subira mpaka 2010 ipite, hapo ndipo JK atakapoweza kuamua urafiki wao ufe. Until then itakuwa ni ngonjera tuu.

Bunge ndicho chombo cha kutunga sheria. Kama wanaona rais anazembea katika kuchukua hatua wangeenda a step further. Lakini bunge letu linajali zaidi maslahi ya chama kuliko maslahi ya taifa. Wanaendeleza sera za kulindana. Mduara unaendelea. Wapiganaji nao wanawaandama mafisadi lakini kwa sababu za kulinda maslahi yao wanamsifu fisadi mkuu, JK. Unafiki. Kamwe hatutaweza kushinda vita dhidi ya mafisadi kama hii vita haitapata support kutoka juu, kwa rais mwenyewe. Na rais huyo anatakiwa awe msafi, asiwe na mikono yenye damu ya ufisadi. Kwa sasa mikono ya JK imechafuka. Hivyo kuanzia sasa hadi uchaguzi wa 2010 kutakuwa hamna progress yoyote ya maana katika vita hii ya ufisadi. Sanasana kutakuwa na majeruhi katika vita vya kujipanga kugombania ubunge, ufisadi ukitumiwa kama silaha mojawapo.

.
 
Back
Top Bottom