Nawashukuru wote mliotoa michango kunihusu na hasa mliolenga maisha binafsi, pili nikupongeze sana Dr kigwangala kwa kujibu post hii nikiomba ukaze buti maana safari bado ni ndefu na wale wenye mawazo kuwa kila anayegombea Nzega katumwa basi pole zao na hasa nikiwajulisha kuwa selelii kurudi nzega kama Mbunge ni miujiuza! maana kabanwa kila kona ndo kwanza kaondoka jana kwenda Dom nadhani kuna mpambe ake humu Jf kampigia simu kibaya zaidi ana ahadi nyingi zisizotekelezeka kwenye maeneo mengi lakini cha kusikitisha zaidi kwa muda wa miaka mitano kuna maeneo hajakanyaga kabisa what do you expect kwa wapiga kura? ametumia miaka mitano kuzungumzia ,asuala ya Rich mond ambayo wana kijiji wa Mwamesu wala hawajui what is Rich mond; kama kuna wanao kereka sana na hili karibu Nzega mumuokoe Ndugu yenu hali yake ni mbaya kupita maelezo. keep it up Dr kigwangala!
Ahsante sana Zyansiku kwa kunifagilia na kunipa pongezi.
Wengine wanadhani mimi na wewe tuna ubia, naomba tu kusema hapa kwamba sikufahamu wala sijawahi kuwasiliana na wewe wala kujadili lolote lile kuhusu azma yangu ya kuwania Ubunge Nzega! Naomba tu pia niwataarifu ndugu zangu wanaJF kwamba mimi sina ubia na mtu yeyote yule katika harakati zangu za kuwania Ubunge, sijaombwa na wazee, sijatumwa na mtu yeyote yule - ila ni nafsi na dhamira yangu pekee iliyonituma kuutafuta Ubunge wa Nzega!
Jimbo la Nzega lina mtego tu kwamba yeyote atakayejitokeza kugombea basi atadhaniwa kuwa ametumwa na mtu, hususan akiwa na ushawishi na anakubalika zaidi ya Selelii! Hili lilijitokeza hata pale nilipoamua kutangaza nia yangu kwa umma kupitia vyombo vya habari, pale Habari maelezo! Hili linakuja kutokana na Selelii kujipambanua kama ni mbunge shupavu anayepambana na ufisadi! Wengi wanakuja kufikiri kwamba jimbo la Nzega lina maslahi ya watu fulani wanaoitwa mafisadi...na kwamba yeyote anayempinga Selelii basi anaungwa mkono na au ametumwa na hawa watu.....and this is a big misnomer! Kugombea Uongozi ni haki ya kikatiba ya kila Mtanzania, na hatuwezi kuliacha jimbo chini ya Selelii kwa kuhofia kusemwa tumetumwa! Tayari kuna watu zaidi ya watano wamekwishatangaza nia ya kuwania Jimbo la Nzega. Hivi wote hawa ni vibaraka wa mafisadi?
Regards,
Dr. Hamisi Kigwangalla.
Mwenye macho haiambiwi ona, mkuu una post 41 zote zinamponda au mkejeli Samwel Sitta na Lucas Seleli. Mwenye macho anaona na kuujua ukweli, fisadis at work!.
Umekusudia au imekutoka kwa kuwa wewe ni wa kiraracha.Umeiweka nji hii njia panda
Safi kabisa!!! Kata mzizi wa fitina
Najaribu kuingia serikalini.
Siku nikifika nafasi ambayo ninaweza kumshughulikia RA atapata cha moto tu. Sijali itachukua miaka mingapi lakini nitafikia lengo langu tu. Na mtu wa kwanza kushughulika naye atakuwa RA. Lazima arudishe na kulipa kila senti hadi ya mwisho.
Sorry RA nitakuwinda popote utakapokuwa duniani hata huko kwenu Iran nitakufuata. Umeiweka nji hii njia panda na kuifanya kama ni property yako ya mfukoni.
Ahsante sana Zyansiku kwa kunifagilia na kunipa pongezi.
Wengine wanadhani mimi na wewe tuna ubia, naomba tu kusema hapa kwamba sikufahamu wala sijawahi kuwasiliana na wewe wala kujadili lolote lile kuhusu azma yangu ya kuwania Ubunge Nzega! Naomba tu pia niwataarifu ndugu zangu wanaJF kwamba mimi sina ubia na mtu yeyote yule katika harakati zangu za kuwania Ubunge, sijaombwa na wazee, sijatumwa na mtu yeyote yule - ila ni nafsi na dhamira yangu pekee iliyonituma kuutafuta Ubunge wa Nzega!
Jimbo la Nzega lina mtego tu kwamba yeyote atakayejitokeza kugombea basi atadhaniwa kuwa ametumwa na mtu, hususan akiwa na ushawishi na anakubalika zaidi ya Selelii! Hili lilijitokeza hata pale nilipoamua kutangaza nia yangu kwa umma kupitia vyombo vya habari, pale Habari maelezo! Hili linakuja kutokana na Selelii kujipambanua kama ni mbunge shupavu anayepambana na ufisadi! Wengi wanakuja kufikiri kwamba jimbo la Nzega lina maslahi ya watu fulani wanaoitwa mafisadi...na kwamba yeyote anayempinga Selelii basi anaungwa mkono na au ametumwa na hawa watu.....and this is a big misnomer! Kugombea Uongozi ni haki ya kikatiba ya kila Mtanzania, na hatuwezi kuliacha jimbo chini ya Selelii kwa kuhofia kusemwa tumetumwa! Tayari kuna watu zaidi ya watano wamekwishatangaza nia ya kuwania Jimbo la Nzega. Hivi wote hawa ni vibaraka wa mafisadi?
Regards,
Dr. Hamisi Kigwangalla.
Ahsante sana Zyansiku kwa kunifagilia na kunipa pongezi...
Dr. Hamisi Kigwangalla.
Wakuu,
Acheni kuwa negative sana, mtaishia kukatisha tamaa watu wengi sana.
Hata hao mnaowaona mashujaa leo waliwapinga/waliwaondoa madarakani watu wengine.
Kugombea ni haki ya raia yeyote anayetaka, na kwa mbunge mchapa kazi hata siku moja hatakiwi kuwaogopa watu wapya wanaotaka kugombea kwenye majimbo yao. Wananchi sio wajinga, kama katimiza wajibu wake basi watampa kura. Waswahili wanasema kitanda usichokilalia, huwezi kujua Kunguni wake. Mtu anaweza kuwa hero kitaifa lakini kumbe kule kwao akawa na matatizo mengi sana. Akina Malecela waliangushwa kule kwao shauri ya mambo hayo hayo.
Kama ilivyo JF siku zote, mchambueni huyu mgombea na kama ana madudu huko nyuma basi yaanikeni hapa. Hii ya kuanza kuita watu mafisadi au wametumwa na mtu bila hata kuwa na chembe ya ushahidi kwa kweli inashusha hadhi nzima ya JF where we dare to speak openly with facts.
Dr Nakutakia mafanikio mema na nguvu na afya njema maana mpambano wa ubunge kwa Tanzania ni hekaheka kubwa. Muhimu ni dhamira yako mwenyewe na ndio itakusuta au kukushangilia maana wewe mwenyewe ndio unajua ukweli wote kwanini unaenda huko jimboni. Jitahidi sana kutokutumia njia chafu maana hazitakusaidia.
Mimi sijazielewa hizi degree za huyu daktari (MD, MPH, MBA), labda kama hiyo MD ni 'Managing Director', ndipo zitaendana na hizo nyingine, vinginevyo kama anamaanisha 'Medical Doctor' kama wale washkaji zangu wanaopiga lile buku zito la Muhimbili, nina wasiwasi huyu ni msanii flani, hana hizo degree. Hilo degree la MD balaa lake usiombe, washkaji niliomaliza nao skonga wakajiunga na chama hilo bado hawajamaliza masomo, wakati mimi tayari nilishaingia mzigoni kitambo na degree ninayo tayari. Huyu anadanganya. Huwezi kupiga MD halafu ati ukasome hizo degree za Mzumbe, wapi na wapi? Mwongo huyu, na wala simshangai, wanasiasa ndio tabia zao kudanganya elimu, sasa hivi watu wameshaona kujiita 'Dr' ni dili la kupatia kura, ila huyu kachemsha kiukweli, anadanganyia na lidigrii la kiukweli kama MD? Noma mwanangu, yaani nimechoka. Bora hata angedanganyia na PhD feki kama wenzie kibao hukohuko kwenye siasa. E bana ningekuwa na simu ya msela wangu Kainerugaba Msemakweli ningemtonya amfuatilie huyu mbwiga, si ajabu ni fisadi wa elimu.
Go deeper man go......ningeshangaa kama ningesoma negative response dhidi ya zyasiku au huyu Dr toka kwa mtanzania. Hakika ningeshangaa sana.same, urambo, kyela, nzega, simanjiro, nk. tatizo si mabadiliko ndugu, tatizo ni dhamira iliyo nyuma yenu.... namjua hamisi vizuri sana na dhamira zake pia.... NEED WE GO DEEPER?