Sehemu 1: Uumbaji Mpaka Gharika

Sehemu 1: Uumbaji Mpaka Gharika

Hadithi ya 47: Mwivi Katika Israeli

attachment.php



TAZAMA anachozika mwanamume huyu katika hema yake! Ni vazi zuri, dhahabu na vipande vya fedha. Amevichukua katika mji wa Yeriko. Lakini vitu hivyo Yeriko vilitakiwa vifanyiwe nini? Unakumbuka?
Viharibiwe, dhahabu na fedha zipelekwe kwenye hazina ya hema ya Yehova. Basi watu hawa hawakumtii Mungu. Wameiba mali

ya Mungu. Jina la mwanamume huyo ni Akani, na walio pamoja naye ni wa jamaa yake. Ebu tuone yanayotokea.
Akani akiisha kuiba vitu hivyo, Yoshua anatuma watu wakaupige mji wa Ai. Lakini wanapigwa vitani. Wengine wanauawa, na wanaobaki wanakimbia. Yoshua anasikitika sana. Analala kifulifuli na kumwomba Yehova hivi: ‘Kwa nini umeacha haya yatupate?’

Yehova anajibu: ‘Amka! Israeli ametenda dhambi. Wamechukua vitu vilivyotakiwa kuharibiwa au vitolewe kwenye hema ya Yehova. Waliiba vazi zuri na kulificha. Sitawabariki ninyi mpaka mtakapoliharibu pamoja na mtu aliyechukua vitu hivyo.’ Yehova anasema atamwonyesha Yoshua mtu huyo mbaya.
Basi Yoshua anakusanya watu wote, naye Yehova anamtenga Akani mbaya kati yao. Akani anasema: ‘Nimefanya dhambi. Niliona vazi zuri, dhahabu na vipande vya fedha. Nilivitaka sana nikavichukua. Mtaviona vimezikwa ndani ya hema yangu.’
Vitu hivyo vinapopatikana na kupelekwa kwa Yoshua, anamwambia Akani hivi: ‘Kwa nini umetuletea taabu? Yehova atakuletea taabu wewe!’ Kisha watu wote wanapiga kwa mawe Akani na jamaa yake mpaka wanakufa. Ni onyo kwamba tusichukue vitu vya wengine, sivyo?
Baada ya hapo Israeli wanaenda tena kuupiga Ai. Wakati huu Yehova anasaidia watu wake, nao wanashinda vita.
Yoshua 7:1-26; 8:1-29.

 

Attachments

  • Mwivi Katika Israeli.jpg
    Mwivi Katika Israeli.jpg
    32.5 KB · Views: 196
Hadithi ya 48: Wagibeoni Wenye Akili

SASA miji mingi katika Kanaani inajitayarisha kupigana na Israeli. Wanadhani wanaweza kushinda. Lakini watu wa mji jirani wa Gibeoni hawadhani hivyo. Wanaamini Mungu anawasaidia Waisraeli, nao hawataki kupigana na Mungu. Basi unajua Wagibeoni hao wanafanya nini?
Wanajifanya kama wanakaa mbali sana. Basi wengine kati yao wanavaa nguo zilizopasuka-pasuka na viatu vilivyokwisha. Wanapakia punda zao mifuko ya zamani, na kuchukua mikate iliyokauka. Kisha wanamwendea Yoshua wakimwambia: ‘Tumetoka mbali sana, kwa kuwa tulisikia habari za Mungu wenu mkuu, Yehova. Tulisikia yote aliyowafanyia huko Misri. Basi viongozi wetu walituambia tutayarishe chakula cha safari tuje tukuambie: “Sisi ni watumishi wako. Utupe ahadi ya kwamba hutapigana na sisi.” Tazama nguo zetu zimekwisha kwa sababu ya safari ndefu na mkate nao umekauka.’
Yoshua na viongozi wengine wanawaamini Wagibeoni hao. Basi wanaahidi wasipigane nao. Lakini baada ya siku tatu wanajua kwamba kumbe Wagibeoni hao wanakaa karibu sana.
‘Mbona mlituambia mmetoka mbali sana?’ Yoshua anawauliza.
Wagibeoni wanajibu hivi: ‘Tulisema hivyo kwa sababu tuliambiwa kwamba Mungu wenu Yehova alikuwa ameahidi kuwapa ninyi nchi yote hii ya Kanaani. Tuliogopa kwamba labda mtatuua.’ Lakini Waisraeli wanafuata ahadi yao, wasiwaue Wagibeoni. Wanawafanya kuwa watumishi wao.
Mfalme wa Yerusalemu anakasirika kwa sababu Wagibeoni wamefanya amani na Israeli. Basi anawaambia wafalme wengine wanne hivi: ‘Njoni mnisaidie kupiga Gibeoni.’ Wafalme hao watano wanafanya hivyo. Je! Wagibeoni walionyesha akili kwa kufanya amani na Israeli? Tutaona.
Yoshua 9:1-27; 10:1-5.
attachment.php



 

Attachments

  • Wagibeoni Wenye Akili.jpg
    Wagibeoni Wenye Akili.jpg
    22.8 KB · Views: 190
Hadithi ya 49: Jua Linasimama Tu

MTAZAME Yoshua. Anasema: ‘Jua, simama!’ Jua linasimama. Linakaa siku nzima katikati ya anga. Yehova anafanya hivyo! Lakini ebu tuone kwa nini Yoshua anataka jua liendelee kung’aa.
attachment.php



Wale wafalme wabaya watano katika nchi ya Kanaani wanapoanza kupigana na Wagibeoni, hao Wagibeoni wanamtuma mtu aende kumwomba Yoshua msaada. ‘Njoo kwetu upesi!’ asema. ‘Utuokoe! Wafalme wote wa vilimani wamekuja kupigana na watumishi wako.’
Mara hiyo Yoshua na wanajeshi wake wote wanakwenda. Wanasafiri usiku kucha. Wanapofika Gideoni, wale askari wa wafalme watano wanaogopa na kuanza kukimbia. Ndipo Yehova anaangusha mawe makubwa ya mvua kutoka angani. Askari wengi wanakufa kwa mvua ya mawe kuliko wanaouawa na wanajeshi wa Yoshua.
attachment.php


Yoshua anaona kwamba karibu jua litatua. Kutakuwa usiku, na askari wengi wa wafalme watano wabaya watakimbia. Ndiyo sababu Yoshua anamwomba Yehova na kusema: ‘Jua, simama!’ Jua linapoendelea kung’aa, Waisraeli wanashinda vita.
Kuna wafalme wabaya wengi zaidi katika Kanaani wanaochukia watu wa Mungu. Inamchukua Yoshua na jeshi lake karibu miaka sita kushinda wafalme 31 katika nchi hiyo. Kisha, Yoshua anahakikisha kwamba nchi ya Kanaani imegawanywa ili makabila yanayohitaji eneo, yapewe.
Kunapita miaka mingi, mwishowe Yoshua anakufa akiwa mwenye miaka 110. Wakati yeye na rafiki zake bado hai, watu wanamtii Yehova. Lakini watu hao wema wanapokufa, watu wanaanza kutenda mabaya na kutaabika. Huu ndio wakati wanapohitaji msaada wa Mungu.
Yoshua 10:6-15; 12:7-24; 14:1-5; Waamuzi 2:8-13.


 

Attachments

  • Jua Linasimama Tu.jpg
    Jua Linasimama Tu.jpg
    5.2 KB · Views: 185
  • Jua Linasimama Tu 1.jpg
    Jua Linasimama Tu 1.jpg
    16.3 KB · Views: 189
Hadithi ya 50: Wanawake Hodari Wawili

WAISRAELI wanapopata taabu, wanamlilia Yehova. Yehova anawajibu kwa kuwapa viongozi hodari wawasaidie. Biblia inawataja viongozi hao, waamuzi. Yoshua alikuwa mwamuzi wa kwanza, na waamuzi wachache waliomfuata ni Oth′nieli, Ehudi na Shamgara. Lakini wanawake wawili wanaosaidia Israeli ni Debora na Yaeli.
attachment.php



Debora ni nabii-mke. Yehova anampasha habari wakati ujao, kisha anawaambia watu maneno ya Yehova. Debora ni mwamuzi pia. Anakaa chini ya mtende katika nchi ya vilima, na watu wanamwendea awasaidie magumu yao.
Wakati huu Yabini ndiye mfalme wa Kanaani. Ana magari ya vita 900. Jeshi lake lina nguvu sana hata Waisraeli wengi wamelazimika kuwa watumishi wa Yabini. Mkuu wa jeshi la Mfalme Yabini ni Sisera.
Siku moja Debora anampelekea Mwamuzi Baraki habari hii: ‘Yehova amesema hivi: “Chukua watu 10,000 kwenye Mlima Tabori. Nitamleta Sisera kwako huko. Nitakupa ushindi juu yake na jeshi lake.”’
Baraki anamwambia Debora hivi: ‘Nitakwenda ikiwa wewe pia utakwenda nami.’ Debora anaenda naye, lakini anamwambia Baraki hivi: ‘Wewe hutasifiwa kwa kushinda, kwa kuwa Yehova ataweka Sisera katika mkono wa mwanamke.’ Inakuwa hivyo.
Baraki anatelemka Mlima Tabori akutane na askari wa Sisera. Mara moja Yehova anafanyiza maji mengi, na askari adui wengi wanazama. Lakini Sisera anashuka katika gari lake huyo, anakimbia.
attachment.php



Baada ya muda kidogo Sisera anafika kwenye hema ya Yaeli. Anamkaribisha ndani, na kumpa maziwa. Yanamtia usingizi, upesi analala usingizi mwingi. Ndipo Yaeli anachukua msumari wa hema na kuupigilia katika kichwa cha mtu huyo mbaya. Baraki anapokuja, Yaeli anamwonyesha Sisera amekufa! Basi, unaona yanatimia maneno ya Debora.
Halafu Mfalme Yabini pia anauawa, Waisraeli wanakuwa na amani tena kwa muda.
Waamuzi 2:14-22; 4:1-24; 5:1-31.


 

Attachments

  • Wanawake Hodari Wawili 1.jpg
    Wanawake Hodari Wawili 1.jpg
    10.5 KB · Views: 181
  • Wanawake Hodari Wawili.jpg
    Wanawake Hodari Wawili.jpg
    24.5 KB · Views: 184
Hadithi ya 51: Ruthu na Naomi

UTAONA kitabu kinachoitwa Ruthu (Ruta) katika Biblia. Ni hadithi juu ya jamaa iliyokaa wakati Waisraeli walipokuwa na waamuzi. Ruthu ni mwanamke kijana kutoka nchi ya Moabu; si wa taifa la Mungu la Israeli. Lakini Ruthu anapopata habari za Mungu wa kweli Yehova, anampenda sana sana. Naomi ni mwanamke mzee aliyemsaidia Ruthu amjue Yehova.

Naomi ni Mwisraeli. Yeye na mumewe na wana wawili walihama kwenda Moabu ilipotokea njaa katika Israeli. Ndipo siku moja mume wa Naomi akafa. Baadaye wana wa Naomi wakaoa wasichana wawili Wamoabi, Ruthu na Or′pa. Lakini baada ya miaka kama 10 hivi, wana wawili wa Naomi wakafa. Lo! Naomi alihuzunika sana, na wasichana wawili pia! Sasa Naomi atafanya nini?

Siku moja Naomi anaamua kurudi kwa watu wake. Ruthu na Or′pa wanataka kukaa naye, wanafuata. Lakini wakiisha kusafiri kidogo, Naomi anageuka na kuwaambia wasichana hao wawili hivi: ‘Rudini kwenu mkakae na mama zenu.’

Naomi anawabusu wasichana hao, akiwaambia kwa heri. Kwa hiyo wanaanza kulia, kwa sababu wanampenda Naomi sana sana. Wanasema: ‘Sivyo! Sisi tutakwenda nawe kwa watu wako.’ Lakini Naomi anajibu hivi: ‘Ni lazima mrudi, binti zangu. Itakuwa bora ninyi kukaa kwenu.’ Or′pa anaanza kurudi kwao. Lakini Ruthu akataa kurudi.


Naomi anageuka na kumwambia: ‘Or′pa amekwenda. Wewe pia nenda kwenu.’ Lakini Ruthu ajibu: ‘Usiniambie nikuache! Acha niende nawe. Mahali uendapo nitakwenda, mahali unapokaa nitakaa. Watu wako watakuwa watu wangu, na Mungu wako, Mungu wangu. Mahali ambapo utakufa nitakufa, na kuzikwa hapo.’ Ruthu anaposema hivyo, Naomi anaacha.


Mwishowe wanawake hao wawili wanafika Israeli. Wanakaa huko. Mara hiyo Ruthu anaanza kufanya kazi mashambani, maana ni wakati wa kuvuna shayiri. Mwanamume mmoja jina lake Boazi anamruhusu akusanye shayiri katika mashamba yake. Unamjua mama ya Boazi? Ni Rahabu wa Yeriko.

Siku moja Boazi anamwambia Ruthu hivi: ‘Nimesikia habari zako zote, jinsi umehurumia Naomi. Najua ulivyoacha baba na mama yako na nchi yako ukaja kukaa na watu ambao hukujua zamani. Yehova akubariki!’

Ruthu anajibu hivi: ‘Unanionyesha fadhili nyingi, bwana. Umenifariji kwa maneno yako mazuri.’ Boazi anampenda Ruthu sana sana, na muda si muda wanaoana. Jambo hili lamfurahisha Naomi kama nini! Lakini Naomi anafurahi hata zaidi wakati Ruthu na Boazi wanapopata mwana wao wa kwanza, jina lake Obedi. Baadaye Obedi anakuwa babu ya Daudi, ambaye tutajua habari zake nyingi baadaye.

attachment.php


Kitabu cha Biblia cha Ruthu (Ruta).



 

Attachments

  • Ruthu na Naomi.jpg
    Ruthu na Naomi.jpg
    35.3 KB · Views: 185
Hadithi ya 52: Gideoni na Wanaume Wake 300

UNAONA yanayofanyika hapa? Wote hao ni wanajeshi wa Israeli. Wanaume hao wanaoinama wanakunywa maji. Mwamuzi Gideoni ndiye anayesimama karibu yao. Anatazama wanavyokunywa maji.
Ebu watazame sana wanaume hao wanavyokunywa kwa namna tofauti. Wengine wanatia uso wao karibu na maji. Lakini mmoja anachota maji kwa mkono wake, ili aone yanayotendeka karibu yake. Hilo ni la maana, kwa kuwa Yehova alimwambia Gideoni achague wanaume wale tu walio macho wanapokunywa. Wengine, Mungu akasema, warudishwe nyumbani. Ebu tuone sababu.
Tena Waisraeli wanapata taabu nyingi. Wamekataa kumtii Yehova. Wamidiani wamewazidi nguvu na wanawaumiza. Basi Waisraeli hao wanamlilia Yehova awasaidie. Yehova asikia vilio vyao.
Yehova anamwambia Gideoni atayarishe jeshi. Basi Gideoni akusanya wanajeshi 32,000. Lakini wanajeshi wanaopigana na Israeli ni 135,000. Hata hivyo Yehova anamwambia Gideoni hivi: ‘Una wanajeshi wengi mno.’ Kwa nini Yehova alisema hivyo?
Kwa sababu Waisraeli wakishinda, labda watadhani wameshinda kwa uwezo wao. Labda watadhani hawakutaka Yehova awasaidie washinde. Basi Yehova anamwambia Gideoni hivi: ‘Waambie wanaume wote ambao ni waoga warudi nyumbani.’ Gideoni anapofanya hivyo, wanajeshi 22,000 wanarudi nyumbani. Wanabaki wanajeshi 10,000 wa kupigana na askari wote 135,000.
attachment.php



Lakini, sikiliza! Yehova anasema: ‘Bado una wanajeshi wengi mno.’ Basi anamwambia Gideoni awanyweshe maji penye mto huu na kuwarudisha wote wale wanaoinamisha uso wao karibu na maji wanywe. ‘Nitakupa ushindi kwa wanaume hawa 300 ambao wamekuwa macho walipokunywa maji,’ asema Yehova.

Wakati wa vita wafika. Gideoni anagawa wanaume wake 300 kuwa vikundi vitatu. Anampa kila mwanamume tarumbeta, na mtungi ulio na mwenge ndani. Kama usiku wa manane hivi, wote wanaizunguka kambi ya askari maadui. Kisha, wakati ule ule, wote wazipiga tarumbeta zao na kuivunga mitungi yao, wakipiga kelele hivi: ‘Upanga wa Yehova na wa Gideoni!’ Askari maadui wanapoamka, wanatatizwa na kuogopa. Wote wanaanza kukimbia, na Waisraeli wanashinda.
Waamuzi sura ya 6 mpaka 8.


 

Attachments

  • Gideoni na Wanaume Wake 300.jpg
    Gideoni na Wanaume Wake 300.jpg
    62.4 KB · Views: 180
Hadithi ya 53: Ahadi ya Yeftha

attachment.php

UMEPATA kutoa zawadi ukaona vigumu kuitimiza? Mwanamume katika picha hii, alitoa ahadi, ndiyo sababu ana huzuni sana. Huyo ni Yeftha, mwamuzi hodari wa Israeli.
Yeftha anakaa wakati Waisraeli hawamwabudu Yehova tena. Wanafanya mabaya tena. Yehova anaruhusu Waamoni wawaumize. Hilo lawafanya Waisraeli wamlilie Yehova hivi: ‘Tumekukosea. Tafadhali, utuokoe!’
attachment.php



Watu wanatubu mabaya waliyofanya. Wanaonyesha kutubu kwao kwa kumwabudu Yehova tena. Yehova anawasaidia tena.
Yeftha anachaguliwa na watu akapigane na Waamoni wabaya. Yeftha anataka sana Yehova amsaidie vitani. Basi anamwahidi Yehova hivi: ‘Ikiwa utanisaidia nishinde Waamoni, mtu wa kwanza kutoka nyumbani mwangu kuja kunilaki nirudipo nitakupa huyo.’
Yehova anasikiliza ahadi ya Yeftha, naye anamsaidia kushinda. Yeftha anaporudi nyumbani, unajua nani wa kwanza kutoka amlaki? Ni binti yake, mtoto wake mmoja tu. ‘O-o, binti yangu!’ Yeftha analia. ‘Unanihuzunisha sana. Lakini nimemwahidi Yehova, siwezi kuvunja ahadi hiyo.’
Binti Yeftha anapojua ahadi ya baba yake, kwanza anahuzunika. Maana ataacha baba na rafiki zake. Lakini atatumia maisha yake akimtumikia Yehova katika hema yake huko Shilo. Basi anamwambia baba yake hivi: ‘Ikiwa umemwahidi Yehova, timiza.’
Basi binti Yeftha aenda Shilo, na anamtumikia Yehova maisha yake yote katika hekalu lake. Kila mwaka wanawake wa Israeli wanamtembelea huko siku nne, na kufurahi pamoja. Watu wanampenda binti Yeftha kwa sababu ni mtumishi mzuri wa Yehova.
Waamuzi 10:6-18; 11:1-40.

 

Attachments

  • Ahadi ya Yeftha.jpg
    Ahadi ya Yeftha.jpg
    7.4 KB · Views: 171
  • Ahadi ya Yeftha 1.jpg
    Ahadi ya Yeftha 1.jpg
    15.4 KB · Views: 176
Hadithi ya 54: Mwanamume Mwenye Nguvu Kuliko Wote

UNAJUA jina la mwanamume mwenye nguvu kuliko wote? Ni mwamuzi Samsoni. Yehova anampa Samsoni nguvu hizo. Hata kabla ya Samsoni kuzaliwa, Yehova anamwambia mama yake hivi: ‘Upesi utazaa mwana. Ataongoza kuokoa Israeli kutokana na Wafilisti.’
attachment.php


Wafilisti ni watu wabaya wanaoishi Kanaani. Wana wanajeshi wengi, na wanawaumiza Waisraeli sana. Wakati mmoja, Samsoni anapokwenda kwa Wafilisti, simba mkubwa anatokea akinguruma kukutana naye. Lakini Samsoni anamwua simba huyo kwa mikono yake tu. Pia anaua mamia ya Wafilisti wabaya.

Baadaye Samsoni anapendana na mwanamke, Delila. Viongozi Wafilisti wanaahidi kwamba kila mmoja wao atampa Delila vipande 1,100 vya fedha akiwaambia kinachompa Samsoni nguvu nyingi hivyo. Delila anataka fedha zote hizo. Yeye si rafiki wa kweli wa Samsoni, wala wa watu wa Mungu. Anazidi kumwuliza Samsoni kinachompa nguvu nyingi hivyo.
attachment.php



Mwishowe, Delila amshawishi Samsoni. Naye Samsoni anamwambia siri ya nguvu zake, akisema: ‘Mimi sijanyolewa nywele. Tangu kuzaliwa kwangu, Mungu alinichagua niwe mtumishi wake wa pekee, yaani, Mnadhiri. Nikinyolewa nywele, nitapoteza nguvu.’

Delila anapojua hayo, anamlaza Samsoni katika paja lake. Kisha amwita mtu aje amnyoe nywele. Samsoni anapoamka, anakuta amepoteza nguvu. Ndipo Wafilisti wanakuja kumkamata. Wanamwondoa macho yake mawili, na kumfanya mtumwa wao.
attachment.php


Siku moja Wafilisti wanafanya karamu kubwa ili waabudu Dagoni mungu wao. Wanamtoa Samsoni gerezani ili wamcheke. Wakati huo, nywele za Samsoni zimekua tena. Samsoni anamwambia kijana anayemwongoza kwa mkono: ‘Acha nishike nguzo za jengo hili.’ Kisha Samsoni anamwomba Yehova ampe nguvu, naye anashika nguzo hizo. Anapaza sauti hivi: ‘Acha nife pamoja na Wafilisti.’ Wafilisti wanaokula karamu ni 3,000. Samsoni anapoegemea nguzo hizo, jengo laanguka na kuua watu wote hao wabaya.

Waamuzi sura ya 13 mpaka 16.


 

Attachments

  • Mwanamume Mwenye Nguvu Kuliko Wote 1.jpg
    Mwanamume Mwenye Nguvu Kuliko Wote 1.jpg
    32.6 KB · Views: 181
  • Mwanamume Mwenye Nguvu Kuliko Wote 2.jpg
    Mwanamume Mwenye Nguvu Kuliko Wote 2.jpg
    21.5 KB · Views: 182
  • Mwanamume Mwenye Nguvu Kuliko Wote.jpg
    Mwanamume Mwenye Nguvu Kuliko Wote.jpg
    12.6 KB · Views: 179
Hadithi ya 55: Mvulana Mdogo Anamtumikia Mungu

JE! HUYU si kivulana mzuri? Jina lake ni Samweli. Na mwanamume anayeweka mkono wake juu ya kichwa cha Samweli ni Eli, kuhani mkuu wa Israeli. Yule ni Elkana, baba ya Samweli, Hana mama yake wanaompeleka Samweli kwa Eli.
attachment.php



Samweli ana miaka minne au mitano tu. Lakini atakaa katika hema ya Yehova pamoja na Eli na makuhani wengine. Kwa nini Elkana na Hana wanamtoa Samweli mtoto amtumikie Yehova hemani? Ebu tuone.
Miaka michache kabla ya hayo, Hana huyo alihuzunika sana. Hakuweza kuzaa mtoto, naye alitaka mtoto sana sana. Basi siku moja Hana alipotembelea hema ya Yehova, alisali hivi: ‘Ee Yehova, usinisahau mimi! Ukinipa mwana, nakuahidi kukupa huyo akutumikie maisha yake yote.’
Yehova akajibu sala ya Hana, na baada ya miezi fulani akamzaa Samweli. Hana akampenda kivulana wake, akaanza kumfundisha habari za Yehova akiwa bado mdogo sana. Akamwambia mumewe hivi: ‘Upesi Samweli akiisha kuacha kunyonya, nitampeleka hemani akamtumikie Yehova huko.’
Ndivyo tunavyoona Hana na Elkana wakifanya katika picha hii. Na kwa vile Samweli amefundishwa vizuri na wazazi wake, anafurahia kumtumikia Yehova katika hema ya Yehova. Kila mwaka Hana na Elkana wanakuja kuabudu katika hema hii ya pekee, na kumtembelea kivulana wao mdogo. Na kila mwaka Hana anamletea Samweli vazi jipya ambalo amemshonea.
Miaka inapita, na Samweli anazidi kutumikia katika hema ya Yehova. Yehova na watu wanampenda. Lakini Hofni na Finehasi, wana wa Eli kuhani mkuu si wazuri. Wanafanya mabaya mengi, wanazuia wengine pia kumtii Yehova. Ingempasa Eli awaondoe katika ukuhani, lakini hawaondoi.
Kijana Samweli hakubali kuacha kumtumikia Yehova kwa sababu ya mabaya yanayoendelea hemani. Lakini kwa vile watu wachache sana ndio wanaompenda Yehova, Yehova ameacha kusema na mwanadamu ye yote. Inakuwa hivi wakati Samweli anapokuwa mkubwa kidogo:
Samweli amelala hemani anapoamshwa na sauti. Anajibu hivi: ‘Mimi hapa.’ Anaamka na kumkimbilia Eli, akisema: ‘Uliniita, nimekuja.’
Lakini Eli anajibu: ‘Sikukuita; nenda kalale.’ Samweli anarudi kulala.
Tena anaitwa mara ya pili: ‘Samweli!’ Samweli anaamka na kumkimbilia Eli tena. ‘Uliniita, nimekuja,’ asema. Lakini Eli anamjibu: ‘Sikukuita, mwanangu. Kalale tena.’ Samueli arudi kulala.
‘Samweli!’ sauti yaita mara ya tatu. Samweli amkimbilia Eli. ‘Nimekuja, maana umeniita sasa,’ anasema. Sasa Eli anajua kwamba ni Yehova anayeita. Amwambia Samweli hivi: ‘Nenda kalale tena, na akiita tena, useme: “Sema, Yehova, maana mtumishi wako anasikiliza.”’
Ndivyo Samweli anasema Yehova anapoita tena. Kisha Yehova amwambia Samweli kwamba ataadhibu Eli na wanawe. Baadaye Hofni na Finehasi wanakufa katika kupigana na Wafilisti, Eli anaposikia yaliyotokea anaanguka, anavunja shingo yake na kufa pia. Neno la Yehova latimia.
Samweli anakuwa mkubwa, na kuwa mwamuzi wa mwisho wa Israeli. Anapozeeka, watu wanamwomba hivi: ‘Chagua mfalme wa kututawala sisi.’ Samweli hataki kufanya hivyo, kwa kuwa Yehova ndiye mfalme wao. Lakini Yehova anamwambia asikilize watu hao.
1 Samweli 1:1-28; 2:11-36; 4:16-18; 8:4-9.

 

Attachments

  • Mvulana Mdogo Anamtumikia Mungu.jpg
    Mvulana Mdogo Anamtumikia Mungu.jpg
    19.8 KB · Views: 226
Sehemu 4: Mfalme wa Kwanza wa Israeli Mpaka Utumwa Babeli

Sauli (Saulo) akawa mfalme wa kwanza wa Israeli. Lakini Yehova alimkataa, Daudi akachaguliwa awe mfalme badala yake. Tunajifunza mambo mengi juu ya Daudi. Akiwa kijana, alipigana na jitu Goliathi. Baadaye alimkimbia Mfalme Sauli mwenye wivu. Kisha Abigaili mwenye sura nzuri akamzuia asitende upumbavu.
Halafu, tunajifunza mengi juu ya Sulemani (Solomono), mwana wa Daudi, aliyechukua mahali pa Daudi awe mfalme wa Israeli. Kila mmoja wa wafalme watatu wa kwanza wa Israeli alitawala kwa miaka 40. Baada ya Sulemani kufa, Israeli waligawanyika kuwa falme mbili, ufalme wa kaskazini na wa kusini.
Ufalme wa kaskazini wa makabila 10 uliendelea muda wa miaka 257 kabla ya kuharibiwa na Waashuru. Halafu miaka 133 baadaye, ufalme wa kusini wa makabila mbili ukaharibiwa pia. Wakati huu Waisraeli walihamishwa kupelekwa Babeli. Hivyo Sehemu ya 4 inazungumza historia ya miaka 510, muda ambao mambo mengi ya kusisimua yanatukia mbele yetu.

attachment.php
 

Attachments

  • Mfalme wa Kwanza wa Israeli Mpaka Utumwa Babeli.jpg
    Mfalme wa Kwanza wa Israeli Mpaka Utumwa Babeli.jpg
    36.3 KB · Views: 206
Hadithi ya 56: Sauli—Mfalme Wa Kwanza Wa Israeli

attachment.php


MTAZAME Samweli anamwaga mafuta kichwani pa mtu. Ndivyo walivyokuwa wakimfanyia mtu waonyeshe amechaguliwa kuwa mfalme. Yehova anamwambia Samweli amwage mafuta kichwani pa Sauli (Saulo). Ni mafuta ya pekee yenye harufu nzuri.
Sauli hakudhani alifaa kuwa mfalme. ‘Mimi ni wa kabila la Benyamini, dogo zaidi katika Israeli,’ anamwambia Samweli. ‘Kwa nini wasema nitakuwa mfalme?’ Yehova anampenda Sauli kwa sababu hana kiburi. Ndiyo maana anamchagua kuwa mfalme.

Lakini Sauli si maskini wala mtu mdogo. Anatokana na jamaa tajiri, naye ana sura nzuri sana, mwanamume mrefu. Ni mrefu kuliko mtu ye yote katika Israeli! Sauli ni mwenye mbio sana kuliko watu wote, na mwenye nguvu sana. Watu wanafurahi kwa vile Yehova amemchagua Sauli awe mfalme. Wote wanaanza kupiga kelele hivi: ‘Uishi maisha marefu mfalme!’

Adui za Israeli ni wenye nguvu kama kawaida. Bado wanawafanyia Waisraeli matata mengi. Upesi baada ya Sauli kufanywa mfalme, Waamoni wanakuja kupigana nao. Lakini Sauli anakusanya jeshi kubwa, anashinda Waamoni. Jambo hilo linafurahisha watu kwa vile Sauli ni mfalme.

Wakati kunapita miaka, Sauli anaongoza Waisraeli kwenye ushindi mwingi juu ya adui zao. Sauli pia anapata mwana hodari jina lake Yonathani (Yonatana). Yonathani naye anasaidia Waisraeli kushinda vita vingi. Bado Wafilisti ni adui wabaya zaidi wa Israeli. Siku moja maelfu na maelfu ya Wafilisti wanakuja wapigane na Waisraeli.
Samweli anamwambia Sauli amngojee ndipo amtolee Yehova zawadi. Lakini Samweli anakawia kuja. Sauli anaogopa kwamba

Wafilisti wataanza vita, basi anaanza peke yake kutoa dhabihu. Kisha Samweli anapokuja, anamwambia Sauli kwamba amekosa kutii. ‘Yehova atachagua mtu mwingine awe mfalme juu ya Israeli,’ asema Samweli.
Baadaye Sauli akosa kutii tena. Basi Samweli anamwambia: ‘Ni bora kutii Yehova kuliko kumtolea zawadi ya kondoo bora zaidi. Kwa kuwa hukumtii Yehova, Yehova atakuondoa usiwe mfalme wa Israeli.’
Twaweza kujifunza somo zuri kutokana na hayo. Yanatuonyesha ubora wa kumtii Yehova sikuzote. Pia, yanaonyesha kwamba mtu mzuri kama Sauli, anaweza kuwa mbaya. Sisi hatutaki hata kidogo tuwe wabaya, sivyo?
1 Samweli sura za 9 mpaka 11; 13:5-14; 14:47-52; 15:1-35; 2 Samweli 1:23.


 

Attachments

  • Sauli—Mfalme Wa Kwanza Wa Israeli.jpg
    Sauli—Mfalme Wa Kwanza Wa Israeli.jpg
    17 KB · Views: 207
Hadithi ya 57: Mungu Anamchagua Daudi

attachment.php



UNAWEZA kuona yaliyotokea? Mvulana huyu amemwokoa mwana-kondoo mdogo asiliwe na dubu. Dubu huyo alikuja akamchukua mwana-kondoo amle. Lakini mvulana huyo akafuatia, akamwokoa mwana-kondoo katika kinywa cha dubu. Dubu aliporukia mvulana, alimkamata na kumwua! Wakati mwingine aliokoa kondoo mmoja asiliwe na simba. Je! huyo si mvulana hodari? Unajua ni nani?

Ni kijana Daudi. Anakaa katika mji wa Bethlehemu. Babu yake ni Obedi, mwana wa Ruthu na Boazi. Unawakumbuka? Baba ya Daudi ni Yese. Daudi anachunga kondoo za baba yake. Daudi alizaliwa miaka 10 baada ya Yehova kuchagua Sauli awe mfalme.
Unafika wakati Yehova anapomwambia Samweli hivi: ‘Chukua mafuta ya pekee uende nyumbani kwa Yese huko Bethlehemu. Nimechagua mmoja kati ya wanawe awe mfalme.’ Samweli anapomwona Eliabu mwana mkubwa wa Yese, anasema hivi: ‘Bila shaka huyu ndiye Yehova amechagua.’ Lakini Yehova anamwambia: ‘Usitazame urefu na uzuri wake. Sikumchagua awe mfalme.’
Basi Yese anamwita Abinadabu mwanawe na kumpeleka kwa Samweli. Lakini Samweli anasema: ‘Hapana, Yehova hakumchagua wala huyu.’ Tena, Yese amleta Shama mwanawe. ‘Hapana, Yehova hakuchagua wala huyu,’ asema Samweli. Yese ampelekea Samweli wanawe saba, lakini Yehova hachagui ye yote kati yao. ‘Je! wavulana ni hawa tu?’ Samweli auliza.
‘Bado kuna mdogo wao,’ Yese asema. ‘Lakini yeye anachunga kondoo.’ Daudi anapoingizwa, Samweli anamwona kuwa kivulana mzuri. ‘Huyu ndiye,’ Yehova asema. ‘Mmwagie mafuta.’ Samweli anafanya hivyo. Utafika wakati Daudi atakapokuwa mfalme wa Israeli.
1 Samweli 17:34, 35; 16:1-13.


 

Attachments

  • Mungu Anamchagua Daudi.jpg
    Mungu Anamchagua Daudi.jpg
    20.7 KB · Views: 222
Hadithi ya 58: Daudi Na Goliathi

TENA Wafilisti wanakuja kupigana na Israeli. Wakati huu ndugu zake Daudi wakubwa watatu wamo katika jeshi la Sauli. Basi siku moja Yese amwambia Daudi hivi: ‘Wapelekee ndugu zako nafaka na mikate. Kaone kama ni wazima.’
attachment.php



Daudi anapofika kwenye kambi ya jeshi, anapiga mbio kwenda kwenye mapigano akawatafute ndugu zake. Goliathi (Goliata), jitu la Wafilisti anajitokeza ili awacheke Waisraeli. Kwa muda wa siku 40 amekuwa akifanya hivyo asubuhi na jioni. Anapaza sauti: ‘Haya, chagueni mmoja apigane nami.’
Daudi anauliza askari fulani hivi: ‘Atapata nini mtu anayemwua Mfilisti huyu na kuwaondolea Waisraeli aibu hii?’
‘Sauli atampa mtu huyo mali nyingi,’ askari anasema. ‘Naye atampa binti yake awe mke wake.’
Lakini Waisraeli wote wanamwogopa Goliathi kwa sababu ni mkubwa mno. Urefu wake ni zaidi ya mita tatu, na ana askari mwingine wa kumchukulia ngao.
Askari fulani wanakwenda kumwambia Mfalme Sauli kwamba Daudi anataka kupigana na Goliathi. Lakini Sauli anamwambia Daudi hivi: ‘Wewe huwezi kupigana na Mfilisti huyu. Wewe ni mtoto tu, yeye amekuwa askari maisha yake yote.’ Daudi anajibu hivi: ‘Mimi niliua dubu na simba aliyechukua kondoo wa baba. Na Mfilisti huyu atakuwa kama huyo. Yehova atanisaidia.’ Basi Sauli anasema: ‘Nenda, Yehova awe nawe.’
Daudi anatelemkia njia ya kijito na kuchagua mawe matano laini, na kuyaweka mfukoni mwake. Kisha anachukua kombeo lake na kwenda kukutana na jitu lile. Goliathi anapomwona anamdharau. Anadhani itakuwa rahisi sana kumwua Daudi.
attachment.php



‘Wewe njoo tu kwangu,’ Goliathi asema, ‘nami nitawapa ndege na wanyama wapate kula mwili wako.’ Lakini Daudi anasema: ‘Wewe unakuja kwangu kwa upanga na mkuki, lakini mimi ninakuja kwako kwa jina la Yehova. Leo hii Yehova atakutia wewe mikononi mwangu nami nitakuangusha chini.’
Papo hapo Daudi anamkimbilia Goliathi. Anachukua jiwe katika mfuko wake, analiweka katika kombeo lake, na kulitupa kwa nguvu zake zote. Jiwe hilo linaingia moja kwa moja kichwani mwa Goliathi, anaanguka na kufa! Wafilisti wanapoona bingwa wao ameanguka, wote wanageuka na kukimbia. Waisraeli wanawafuatia mbio na kushinda vita.
1 Samweli 17:1-54.


 

Attachments

  • Daudi Na Goliathi.jpg
    Daudi Na Goliathi.jpg
    25.1 KB · Views: 201
  • Daudi Na Goliathi 1.jpg
    Daudi Na Goliathi 1.jpg
    8.8 KB · Views: 215
Hadithi ya 59: Sababu Yampasa Daudi Akimbie

BAADA ya Daudi kumwua Goliathi, Abneri mkuu wa jeshi anampeleka kwa Sauli. Sauli anapendezwa sana na Daudi. Anamfanya mkuu katika jeshi lake na kumchukua akakae katika nyumba ya mfalme.
Baadaye, jeshi linaporudi kupigana na Wafilisti, wanawake wanaimba hivi: ‘Sauli ameua maelfu, lakini Daudi makumi ya maelfu.’ Hilo lamfanya Sauli aone wivu, kwa sababu Daudi anaheshimiwa kuliko Sauli. Lakini Yonathani mwana wa Sauli haoni wivu. Anampenda Daudi sana, naye Daudi anampenda Yonathani pia. Hao wawili wanapeana ahadi kwamba watakuwa rafiki sikuzote.
attachment.php



Daudi anajua sana kupiga kinubi, naye Sauli anapenda muziki anaopiga Daudi. Lakini siku moja wivu wa Sauli wamfanya atende jambo baya. Wakati Daudi anapopiga kinubi, Sauli anachukua mkuki wake na kuutupa, akisema: ‘Nitampigilia Daudi ukutani!’ Lakini Daudi apiga chenga (aepa), na mkuki wamkosa. Baadaye Sauli akosa tena kumpiga Daudi kwa mkuki wake. Basi Daudi anajua yampasa awe mwangalifu sana.

Unajua ahadi ya Sauli! Alisema angetoa binti yake awe mke wa yule mtu ambaye angeua Goliathi. Mwishowe Sauli anamwambia Daudi achukue Mikali binti yake, lakini kwanza yampasa aue Wafilisti adui 100. Ebu wazia hilo! Sauli anatumaini kwamba Wafilisti watamwua Daudi. Lakini hawamwui, hivyo Sauli anampa Daudi binti yake awe mke wake.
Siku moja Sauli anamwambia Yonathani na watumishi wake wote kwamba anataka kumwua Daudi. Lakini Yonathani anamwambia babaye hivi: ‘Usimwumize Daudi. Hajakukosea. Kila alichofanya kimekuwa msaada mkubwa kwako. Aliweka uhai wake katika hatari alipomwua Goliathi, na ulipoona, ukafurahi.’
attachment.php



Sauli amsikiliza mwanawe, na kuahidi asimwumize Daudi. Daudi anarudishwa, naye anamtumikia Sauli tena nyumbani mwake kama zamani. Lakini, siku moja wakati Daudi anapopiga muziki, Sauli anamtupia Daudi mkuki wake tena. Daudi apiga chenga, mkuki unapiga ukuta. Hii ndiyo mara ya tatu! Sasa Daudi ajua yampasa akimbie!

Usiku huo Daudi aenda nyumbani kwake. Lakini Sauli anatuma watu fulani wakamwue. Mikali anajua mipango ya baba yake. Anamwambia mume wake hivi: ‘Usipoondoka usiku huu, kesho utakuwa umekufa.’ Inampasa Daudi ajifiche hapa na pale muda wa karibu miaka saba, Sauli asimwone.
1 Samweli 18:1-30; 19:1-18.


 

Attachments

  • Sababu Yampasa Daudi Akimbie.jpg
    Sababu Yampasa Daudi Akimbie.jpg
    14.1 KB · Views: 193
  • Sababu Yampasa Daudi Akimbie 1.jpg
    Sababu Yampasa Daudi Akimbie 1.jpg
    14.9 KB · Views: 202
Hadithi ya 60: Abigaili na Daudi

JE! UNAMJUA mwanamke huyu mzuri anayekuja kumlaki Daudi? Jina lake ni Abigaili. Ni mwenye akili nzuri, naye anamzuia Daudi asifanye ubaya. Lakini kabla ya kujifunza hayo, tuone ni mambo gani yamekuwa yakimpata Daudi.
Daudi akiisha kumkimbia Sauli, anajificha katika pango. Ndugu zake na wengine wa jamaa yake wanajiunga naye huko. Karibu jumla ya watu 400 wanamwendea, Daudi anakuwa kiongozi wao. Kisha Daudi anamwendea mfalme wa Moabu na kusema: ‘Tafadhali ruhusu baba na mama yangu wakae nawe mpaka nione yatakayonipata.’ Baadaye Daudi na watu wake wanaanza kujificha vilimani.
Ni baada ya hayo kwamba Daudi akutana na Abigaili. Nabali mume wake ni mtu tajiri mwenye mashamba. Ana kondoo 3,000 na mbuzi 1,000. Nabali ni mchoyo. Lakini Abigaili mkewe ni mwenye sura nzuri sana. Pia, anajua kutenda mema. Wakati mmoja hata aliokoa jamaa yake. Na tuone ilivyokuwa.
Daudi na watu wake wamemtendea mema Nabali. Wamelinda kondoo zake. Basi siku moja Daudi anatuma watu wake wakamwombe Nabali awasaidie. Watu wa Daudi wanamwendea Nabali wakati yeye na wasaidizi wake wanakata manyoya ya kondoo. Ni siku ya karamu, naye Nabali ana chakula kingi kizuri. Basi watu wa Daudi wanamwambia hivi: ‘Sisi tumekutendea mema. Hatukuiba kondoo wako ye yote, ila tumesaidia kuwachunga. Basi, tafadhali, utupe chakula kidogo.’
‘Siwezi kuwapa chakula watu kama ninyi,’ Nabali anasema. Anasema kwa njia mbaya sana, na kumtukana Daudi. Watu hao wanaporudi na kumwambia Daudi, Daudi anakasirika sana. ‘Jivikeni panga zenu!’ awaambia watu wake. Nao wanaanza safari kwenda kuua Nabali na watu wake.
Mmoja wa watu wa Nabali, waliosikia matusi ya Nabali, anamwambia Abigaili yaliyotokea. Mara hiyo Abigaili anatayarisha chakula. Anakiweka juu ya punda wake, anapokutana na Daudi njiani, ainama na kusema: ‘Tafadhali, bwana, usimwangalie mume wangu yule Nabali. Yeye ni mpumbavu, anafanya mapumbavu. Hii ni zawadi. Tafadhali ichukue, utusamehe yaliyotokea.’
attachment.php



‘Wewe ni mwanamke mwenye akili,’ Daudi ajibu. ‘Umenizuia nisimwue Nabali na kumlipa kwa choyo yake. Basi nenda zako kwa amani.’ Baadaye, Nabali anapokufa, Abigaili anakuwa mke wa Daudi.
1 Samweli 22:1-4; 25:1-43.

 

Attachments

  • Abigaili na Daudi.jpg
    Abigaili na Daudi.jpg
    47.9 KB · Views: 214
Haleluyaaaaaaaa!

Hadi Ibilisi anatangaza Injili, shukrani kwako Yesu.

Hii ndio namna tunayofundisha watoto wetu kwa picha na upendo badala ya kuwatandika bakora za makalio tukiwalazimisha kukariri maandishi ya kiarabu ambayo hawaelewi.

Tumsifu Yesu Kristo!
 
Haleluyaaaaaaaa!

Hadi Ibilisi anatangaza Injili, shukrani kwako Yesu.

Hii ndio namna tunayofundisha watoto wetu kwa picha na upendo badala ya kuwatandika bakora za makalio tukiwalazimisha kukariri maandishi ya kiarabu ambayo hawaelewi.

Tumsifu Yesu Kristo!
Mkuu Mwana Mtoka Pabaya Hizi ni Hadithi ndani ya Biblia kuna ukweli ndani yake na uongo ndani yake sio mambo ya Dini ndio maana nikaweka hapa kwenye jukwaa la Mapenzi ingelikuwa ipo kule kwenye jukwaa

la mambo ya dini ninafikiri kungelikuwepo na maswali mengi na majibu yasingeweza kupatikana acha ujinga wako wa

kusema kuwa Iblisi anatangaza injili Iblisi ni wewe mwenyewe ndio unakuwa ni wa kwanza kisha ndio Iblisi anakuingia ndani ya moyo wako hizi ni hadithi tu zinaweza kuwa ni za kweli au za kutunga tu acha ulokole wako huo.
 
Last edited by a moderator:
Hadithi ya 61: Daudi Anafanywa Mfalme



TENA Sauli anajaribu kumkamata Daudi. Anachukua askari wake bora zaidi 3,000 na kwenda kumtafuta. Daudi anapojua hivyo, anatuma wapelelezi ajue mahali ambapo Sauli na watu wake wamepiga kambi walale usiku. Ndipo Daudi anawaambia watu wake hivi: ‘Ni nani atakayekwenda pamoja nami kwenye kambi ya Sauli?’
61.jpg

‘Mimi,’ Abishai anajibu. Abishai ni mwana wa Seruya dada yake Daudi. Wakati Sauli na watu wake wamelala, Daudi na Abishai wanaingia kambini kimya-kimya. Wanachukua mkuki na mtungi wa Sauli, kando ya kichwa cha Sauli. Hakuna mtu anayeona wala kuwasikia kwa sababu wote wamelala sana.
Ebu mwone sasa Daudi na Abishai. Wamekwisha kwenda mbali, nao wako salama juu ya kilima. Daudi anampazia sauti mkuu wa jeshi la Israeli hivi: ‘We-e Abneri, sababu gani humlindi bwanako, mfalme? Tazama! Mkuki na mtungi wake viko wapi?’
Sauli anaamka. Aitambua sauti ya Daudi, kisha auliza: ‘Ni wewe, Daudi?’ Unaweza kumwona Sauli na Abneri chini kule?
‘Ndiyo, bwanangu mfalme,’ Daudi amjibu Sauli. Naye Daudi auliza hivi: ‘Kwa nini wataka kunikamata? Nimefanya ubaya gani? Mkuki wako huu, Ee mfalme. Mtume mmoja wa watu wako aje auchukue.’
61a.jpg

‘Nimekosa,’ Sauli anakubali. ‘Nimetenda kipumbavu.’ Ndipo Daudi anakwenda zake, naye Sauli anarudi kwake. Lakini Daudi anajisemesha hivi: ‘Siku fulani Sauli ataniua mimi. Yanipasa nikimbie niende kwenye nchi ya Wafilisti.’ Anafanya hivyo. Daudi anapumbaza Wafilisti na kuwafanya waamini yuko upande wao.
Wakati fulani baadaye Wafilisti wanakwenda kupigana na Israeli. Huko vitani, Sauli na Yonathani wanauawa. Hilo lamhuzunisha Daudi sana, naye anaandika wimbo mzuri, akiimba hivi: ‘Naona huzuni kwa ajili yako, ndugu yangu Yonathani. Jinsi nilivyokupenda!’
Baada ya hayo Daudi anarudi Israeli kenye mji wa Hebroni. Kwatokea vita kati ya watu wanaochagua Ishiboshethi mwana wa Sauli, awe mfalme, na watu wengine wanaotaka Daudi awe mfalme. Lakini mwishowe watu wa Daudi wanashinda. Sasa Daudi ni mwenye miaka 30 anapofanywa kuwa mfalme. Anatawala katika Hebroni kwa miaka saba na nusu.
Wakati wafika wa Daudi na watu wake kwenda kuteka mji mzuri unaoitwa Yerusalemu. Yoabu, mwana mwingine wa Seruya, dada yake Daudi, anaongoza vita. Basi Daudi anamfanya Yoabu kuwa mkuu wa jeshi lake. Sasa Daudi anaanza kutawala katika mji wa Yerusalemu.
1 Samweli 26:1-25; 27:1-7; 31:1-6; 2 Samweli 1:26; 3:1-21; 5:1-10;1 Nyakati 11:1-9.

 

Attachments

  • Daudi Anafanywa Mfalme.jpg
    Daudi Anafanywa Mfalme.jpg
    14.8 KB · Views: 73
  • Daudi Anafanywa Mfalme 1.jpg
    Daudi Anafanywa Mfalme 1.jpg
    13.8 KB · Views: 70
Mkuu Mwana Mtoka Pabaya Hizi ni Hadithi ndani ya Biblia kuna ukweli ndani yake na uongo ndani yake sio mambo ya Dini ndio maana nikaweka hapa kwenye jukwaa la Mapenzi ingelikuwa ipo kule kwenye jukwaa

la mambo ya dini ninafikiri kungelikuwepo na maswali mengi na majibu yasingeweza kupatikana acha ujinga wako wa

kusema kuwa Iblisi anatangaza injili Iblisi ni wewe mwenyewe ndio unakuwa ni wa kwanza kisha ndio Iblisi anakuingia ndani ya moyo wako hizi ni hadithi tu zinaweza kuwa ni za kweli au za kutunga tu acha ulokole wako huo.

hiri rijamaa cjui ra daresirame! rinachangia kama rimekimbizwa na panya road akiri ikawehuka,eti rinamwita mtu ibirisi
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom