Sehemu 1: Uumbaji Mpaka Gharika

Sehemu 1: Uumbaji Mpaka Gharika

Mkuu mzizi mkavu,ubarikiwe sana kwa hili neno la kiroho,
endelea kutupa chakula ya kiroho,
 
Hadithi ya 14: Mungu Anajaribu Imani ya Ibrahimu

UNAWEZA kuona Ibrahimu anafanya nini hapa? Ana kisu, ni kama anataka kumwua mwanawe. Kwa nini afanye hivyo? Na tuone kwanza namna Ibrahimu na Sara walivyopata mwana wao.
14.jpg


Kumbuka, Mungu aliwaahidi kwamba wangezaa mwana. Lakini lilikuwa jambo gumu, kwa sababu Ibrahimu na Sara walikuwa wazee sana. Lakini Ibrahimu aliamini kwamba Mungu anaweza kufanya jambo gumu. Basi jambo gani lilitokea?
Mungu alipokwisha kutoa ahadi yake, mwaka mzima ukapita. Ndipo, Ibrahimu alipokuwa mwenye miaka 100 na Sara 90, wakazaa mtoto wa kiume jina lake Isaka. Mungu alikuwa ametimiza ahadi yake!

Lakini
Ismael alipokuwa mtu mzima, Yehova alijaribu imani ya Ibrahimu. Akasema: ‘Mchukue mwana wako Ismael uende kwenye mlima ambao nitakuonyesha. Ukamwue huko mwana wako umtoe dhabihu.’ Lakini kumbuka, Mungu alikuwa ameahidi kwamba watoto wa Ibrahimu wangekaa

Kanaani. Ingekuwa namna gani kama
Ismael angekufa? Ibrahimu hakufahamu hilo, lakini alimtii Mungu.
Alipofika kwenye mlima, Ibrahimu alimfunga
Ismael na kumweka juu ya madhabahu aliyojenga. Lakini alipotaka kumwua Ismael, malaika wa Mungu alitoa sauti kubwa: ‘Ibrahimu, usimwumize mtoto wala kumfanya lolote. Sasa najua kwamba unaniamini, kwa sababu hukuninyima mwana wako mmoja tu!’
Lo! Ibrahimu alimwamini Mungu sana! Aliamini kwamba hakuna jambo gumu kwa Yehova, hata angemfufua
Ismael katika wafu. Lakini Mungu hakutaka Ibrahimu amwue Isaka. Basi Mungu aliongoza kondoo akamatwe na miti midogo iliyokuwa karibu. Kisha akamwambia Ibrahimu amtoe kondoo huyo awe dhabihu mahali pa mwana wake.
Mwanzo 21:1-7; 22:1-18.

Mkuu MziziMkavu, Shalom!

Nalazimika kutokukupongeza kwa jambo hili ambalo ulilianza vizuri, lkn kwa roho ya Shetani iliyo ndani yako umeamua kulipotosha. Naam, hii ndio namna SHETANI hufanya kazi, huanza na ukweli ili apate kuaminika na baadaye huingiza uongo ndani yake. Mfano wa hili ni pale alipomwambia Eva

''Hakika hamtakufa, kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya''
Mwanzo 3:4-5

Kwenye kauli hii ya Shetani, ni hapo kwenye RED tu ndio uongo, the rest ni ukweli kwani walipokula tu tunda la mti ule walianza kujua mema na mabaya.

Hata nilipoona mwanzo mzuri wa mada yako, ilibakia kidogo nishawishike namna ile Eva alishawishika kusikiliza maneno ya Nyoka (Shetani). Lakini kwa uweza wake Yesu, nilipata kuibaini nia yako OVU nami nayakataa yote uliyoyaandika kwa sababu za nia hiyo danganyifu.

Mkuu MziziMkavu, Shalom...Shalom!!
Mwanzo 21:1-7 inasema hivi:


Bwana akamjia Sara kama alivyonena, na Bwana akamfanyia kama alivyosema. Sara akapata mimba akamzalia Ibrahim mwana wa kiume katika uzee wake, kwa muhula alioambiwa na Mungu. Ibrahim akamwita jina lake ISAKA, yule mwana aliyezaliwa, ambaye Sara alimzalia. Ibrahim akamtahiri Isaka mwanawe..........

Mtoto aliyezaliwa na Sara, aliitwa Isaka (Isaack)

Mkuu MziziMkavu, Shalom!
Mwanzo 22:1-? inasema hivi:


Ikawa baada ya mambo hayo Mungu alimjaribu Ibrahim, akamwambia, "Ewe Ibrahim!" Naye akasema, "Mimi hapa." Akasema, "Umchukue mwanao, mwana wako wa pekee, umpendaye, Isaka, ukaende zako katika nchi ya Moria, ukamtoe sadaka ya kuteketezwa huko juu ya mlima mmojawapo nitakaokuambia" Ibrahim akaondoka alfajiri, akatandika punda wake, akachukua vijana wawili pamoja naye, na Isaka mwanawe, akachanja kuni kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa, akaondoka, akaenda mpaka mahali alipoambiwa na Mungu. Siku ya tatu Ibrahim akainua macho akaona mahali pakali mbali. Ibrahim akawaambia vijana wake, "Kaeni ninyi hapa na punda, na mimi na kijana tutakwenda kule, tukaabudu, na kuwarudia tena." Basi Ibrahim akazitwaa kuni za hiyo sadaka, akamtwika Isaka mwanawe; akatwaa moto na kisu mkononi mwake, wakaenda wote wawili pamoja. Isaka akasema na Ibrahim baba yake, akinena, "Babaangu!" Naye akasema, "Mimi hapa mwanangu" Akasema, "Tazama! moto upo, na kuni zipo, lakini yupo wapi mwanakondoo kwa sadaka ya kuteketezwa?"...................;Ibrahim akajenga madhabahu huko, akaziweka tayari kuni, kisha akamfunga Isaka mwanawe, akamweka juu ya madhabahu, juu ya zile kuni. Ibrahim akanyoosha mkono wake, akakitwaa kisu ili amchinje mwanawe, ndipo malaika........


Hakuna sehemu yeyote yenye kuonesha jina la Ishmail, ambaye ni mtoto Ibrahim alizaa kwa mjakazi wake. Kwa hiyo dhahiri utaona kuwa umeamua kupotosha jambo fulani.

Mkuu MziziMkavu, Shalom!

Yawezekana wayafanya haya ili watu wasifie weledi wako wa maneno na kujitia u mwenye hekima. Lakini si vyema kuongezea maneno yako juu ya maneno ya Mungu. Mkuu MziziMkavu, kwa ajili yako nitakupa maneno ya busara hata ujisomee kila utakapo kutafuta sifa na umaarufu usijitie matatizo na Mungu:


[SUP]5[/SUP]Kila neno la Mungu limehakikishwa,
yeye ni ngao ya mwaminio.
[SUP]6[/SUP]Usiongeze neno katika maneno yake,
asije akakulaumu, ukaonekana u mwongo.

Mithali 30:5-6

Umeonekana kuchanganya maneno kwa makusudi,
wakazaa mtoto wa kiume jina lake Isaka. Mungu alikuwa ametimiza ahadi yake!

Lakini
Ismael alipokuwa mtu mzima, Yehova alijaribu imani ya Ibrahimu.
Huu ni uhuni usio na manufaa, na ni upumbavu mbele za Mungu. Tumia muda wako ulihubiri lililo jema nawe utaandikiwa yaliyo mema.

Mkuu MziziMkavu, Shalom!
Shalom JF!


Wasalaaaaam, La Biblicana
 
Last edited by a moderator:
neno jema linalofaaa kwa binadamu mwenye pumzi,naamini tunamrudisha lara1 kundini
 
Asante sana La Biblicana nawafurahia sana watu kama nyie msiopenda upotoshaji.
"
Ubarikiwe mkuu!
 
Last edited by a moderator:
Hadithi ya 20: Dina Anaingia Katika Taabu

UNAONA Dina anaenda kutembela nani? Ni wasichana wanaokaa Kanaani. Je! Yakobo baba yake atafurahia? Ili uweze kujibu ulizo hilo, jaribu kukumbuka Ibrahimu na Isaka walivyofikiria wanawake wa Kanaani.


Je! Ibrahimu alitaka Isaka aoe msichana wa Kanaani? Sivyo. Je! Isaka na Rebeka walitaka Yakobo aoe msichana wa Kanaani? Sivyo. Unajua sababu yake?


Ni kwa sababu watu hao wa Kanaani waliabudu miungu ya uongo. Hawakufaa kuwa waume na wake, nao hawakufaa kuwa rafiki wa kushirikiana nao. Basi tunaweza kuwa na hakika kwamba Yakobo hangependezwa na urafiki wa binti yake pamoja na wasichana hao Wakanaani.

Bila shaka, Dina aliingia katika taabu. Je! unamwona mwanamume huyo Mkanaani katika picha anayemtazama Dina? Ni Shekemu. Siku moja Dian alipokuwa akitembelea, Shekemu alimchukua na kumlazimisha alale naye. Hilo lilikuwa kosa, kwa sababu ni wanaume na wanawake waliooana tu ndio
wanaotakiwa kulala pamoja. Ubaya huo ambao Shekemu alimtendea Dina uliongoza kwenye taabu nyingi zaidi.

Ndugu zake Dina waliposikia yaliyotokea, walikasirika sana. Simeoni na Levi, walikasirika sana hata wakachukua panga wakaingia mjini na kuwafikia wanaume hao ghafula. Wao na ndugu zao wakamwua Shekemu na wanaume wengine wote. Yakobo alikasirika kwa sababu wanawe walifanya ubaya huo.

Taabu yote hiyo ilianza namna gani? Ni kwa sababu Dina alifanya urafiki na watu ambao hawakutii sheria za Mungu. Hatutaki tufanye urafiki na watu kama hao, sivyo?
Mwanzo 34:1-31.

Hadithi ya 21: Yusufu Anachukiwa na Ndugu Zake

TAZAMA namna mvulana huyu hana furaha na tumaini. Ni Yusufu. Ndugu zake wamemwuza kwa wanaume hawa wanaokwenda Misri. Huko Yusufu atafanywa mtumwa. Sababu gani ndugu zake walifanya ubaya huo? Walikuwa na wivu.


attachment.php


Yakobo baba yao alimpenda sana Yusufu. Alimpendelea kwa kumshonea vazi refu ambalo ni zuri sana. Ndugu zake wakubwa 10 walipoona namna Yakobo alivyompenda sana Yusufu, walianza kuwa na wivu na kumchukia Yusufu. Lakini kulikuwako sababu nyingine pia ya kumchukia.
Yusufu aliota ndoto mbili. Katika ndoto zote mbili za Yusufu ndugu zake walimpigia magoti. Yusufu alipowasimulia ndugu zake ndoto hizo, chuki yao iliongezeka zaidi
Basi siku moja ndugu wakubwa wa Yusufu walipokuwa wakichunga kondoo za baba yao, Yakobo alimwomba Yusufu aende kuona kama walikuwa salama. Ndugu za Yusufu walipomwona akija, wengine kati yao walisema: ‘Tumwue!' Lakini Reubeni, ndugu mkubwa wao wote, alisema, ‘Tusifanye hivyo!' Badala yake walimkamata Yusufu wakamtupa katika shimo kavu.
Karibu na wakati huo wanaume fulani Waishmaeli wakaja. Yuda akawaambia ndugu zake hivi: ‘Na tumwuze kwa Waishmaeli hawa.' Ndivyo wanavyofanya. Wanamwuza Yusufu kwa vipande 20 vya fedha. Lo! walikuwa bila huruma kama nini!
Ndugu zake watamwambia baba yao nini? Wanamwua mbuzi na kuchovya vazi zuri la Yusufu katika damu ya mbuzi huyo. Kisha wanampelekea Yakobo baba yao vazi hilo na kusema: ‘Tumeona hili. Ebu litazame, kama ni vazi la Yusufu.'
Yakobo anaona hivyo. ‘Mnyama mkali amemwua Yusufu,' analia. Hivyo ndivyo ndugu za Yusufu wanavyotaka baba yao afikiri. Yakobo anahuzunika sana sana. Anaomboleza siku nyingi. Lakini Yusufu hakufa. Tuone yanayompata kule alikopelekwa.
Mwanzo 37:1-35.


 
Hadithi ya 22: Yusufu Anawekwa Katika Gereza

YUSUFU ana miaka 17 tu anapopelekwa Misri. Anauzwa kwa Potifa. Potifa anafanya kazi ya mfalme wa Misri, anayeitwa Farao.

attachment.php



Yusufu anafanya kazi ya bwana wake, Potifa, kwa bidii. Kwa nini Yusufu amewekwa humu ndani ya gereza? Ni kwa sababu ya mke wa Potifa.
Yusufu anakuwa mwanamume mwenye sura nzuri sana, mke wa Potifa anataka alale naye. Lakini Yusufu anajua hilo ni kosa, hawezi kulifanya. Mke wa Potifa anakasirika sana. Basi mume anaporudi nyumbani, anamwambia uongo na kusema: ‘Yusufu huyo mbaya alitaka kulala nami!’ Potifa anamwamini mke wake, naye anamkasirikia sana Yusufu. Basi anamtupa gerezani.
Upesi msimamizi wa gereza aona Yusufu ni mtu mzuri. Basi anamweka kuwa msimamizi wa wafungwa wengine wote. Baadaye Farao akamkasirikia mnyweshaji wake na mwokaji wake, na kuwatia gerezani. Usiku mmoja kila mmoja wao anaota ndoto ya pekee, lakini hawajui maana ya ndoto zao, kesho yake Yusufu anasema: ‘Niambieni ndoto zenu.’ Wanamwambia. Na kwa msaada wa Mungu, Yusufu anawaambia maana ya ndoto zao.
Kwa mnyweshaji, Yusufu anasema: Kwa siku tatu utafunguliwa utoke gerezani , uwe mnyweshaji wa Farao tena.’ Lakini kwa mwokaji, Yusufu anasema: ‘Katika siku tatu Farao atakukata kichwa chako.’
Katika muda wa siku tatu inakuwa kama Yusufu alivyosema. Farao anamkata kichwa mwokaji wake. Lakini mnyweshaji, anafunguliwa gerezani na kuanza kumtumikia mfalme tena. Lakini mnyweshaji huyo anamsahau Yusufu! Hamwambii Farao habari zake, naye Yusufu anaendelea kukaa gerezani.
Mwanzo 39:1-23; 40:1-23.

attachment.php



Hadithi ya 23: Ndoto za Farao


attachment.php



MIAKA miwili inapita, Yusufu angali gerezani. Mnyweshaji hamkumbuki. Ndipo usiku mmoja Farao anaota ndoto mbili za pekee sana, naye hajui maana yazo. Unamwona akilala pale? Kesho yake Farao anawaita wenye akili na kuwaambia mambo ambayo ameota. Lakini hawawezi kumwambia maana ya ndoto zake.
Mwishowe yule mnyweshaji anakumbuka Yusufu. Anamwambia Farao hivi: ‘Nilipokuwa gerezani alikuwako mtu huko aliyeweza kuniambia maana ya ndoto.’ Farao anaagiza Yusufu atolewe gerezani mara moja.
Farao anamsimulia Yusufu ndoto zake hivi: ‘Niliona ng’ombe saba wanono na wazuri. Kisha nikawaona ng’ombe saba waliokonda sana. Na wale waliokonda wakawala ng’ombe wanono.’

‘Katika ndoto yangu ya pili niliona masuke saba yenye kujaa nafaka ziizoiva, yakikua katika bua moja. Kisha nikaona masuke saba membamba, yaliyokauka sana ya nafaka. Na yale masuke membamba ya nafaka yalianza kumeza masuke mazuri saba ya nafaka.
Yusufu anamwambia Farao hivi: ‘Maana ya ndoto zile mbili ni moja. Wale ng’ombe saba wanono na masuke saba ya nafaka yenye kujaa ni miaka saba, na walek ng’ombe saba waliokonda na masuke ya nafaka membamba saba ni miaka mingine saba. Kutakuwako miaka saba ya chakula kingi katika Misri. Kisha itakuwako miaka saba ya chakula kidogo sana.’
Basi Yusufu anamwambia Farao hivi: ‘Mchague mtu mwenye akili awe msimamizi wa kukusanya chakula wakati wa miaka mizuri saba. Hapo watu hawatakufa njaa wakati wa miaka mibaya saba inayofuata ya chakula kidogo.’
Farao anapenda wazo hilo. Anamchagua Yusufu akusanye chakula, na kukiweka akiba. Yusufu anakuwa mkuu katika misri, wa pili kwa Farao.
Miaka minane baadaye, wakati wa njaa kuu hiyo, Yusufu anona watu fulani wkaija. Unawajua? Ala, ni ndugu zake wakubwa 10! Yakobo baba yao amewatuma Misri kwa sababu chakula ni kidogo kule Kanaani. Yusufu anwajua ndugu zake, lakini wao hawamjui. Unajua sababu? Yusufu amekuwa mkuu, amevaa mavazi ya pekee.
Yusufu anakumbuka kwamba alipokuwa mvulana aliota ndoto akiona ndugu zake wakija kumpigia magoti. Unakumbuka ulisoma habari hiyo? Hivyo Yusufu anafahamu kwamba ni Mungu aliyemtuma aende Misri, kwa sababu nzuri. Unadhani Yusufu anafanya nini? Na tuone.
Mwanzo 41:1-57; 42:1-8; 50:20.


 

Attachments

  • yusuph.jpg
    yusuph.jpg
    28 KB · Views: 104
  • Yusuph gerezani.jpg
    Yusuph gerezani.jpg
    20.1 KB · Views: 98
  • farao ndoto zake.jpg
    farao ndoto zake.jpg
    20 KB · Views: 97
Hadithi ya 24: Yusufu Anajaribu Ndugu Zake

YUSUFU anataka kujua kama ndugu zake 10 bado hawana huruma. Basi anasema hivi: ‘Ninyi ni wapelelezi. Mmekuja kuona udhaifu wa nchi yetu.’
‘Sivyo,’ wanasema. ‘Sisi ni watu wanyofu. Sote ni ndugu. Tuko 12. Lakini ndugu mmoja hayupo, na yule mdogo zaidi yuko nyumbani pamoja na baba yetu.’

Yusufu anajifanya kuwa haamini. Anamweka ndugu anayeitwa Simeoni gerezani, na kuwaachilia wengine wakachukue chakula na kwenda kwao. Lakini anawaambia hivi: ‘Mtakaporudi, lazima mmlete ndugu yenu mdogo zaidi.’

Wanaporudi kwao Kanaani, ndugu hao wanamwambia Yakono baba yao yote yaliyowapata. Yakobo anahuzunika sana. ‘Yusufu hayupo,’ analia, ‘na sasa Simeoni hayupo. Sitawaruhusu mmchukue mwanangu mdogo zaidi Benyamini.’ Lakini chakula chao kinapoanza kuwa kidogo, Yakobo anawaruhusu wamchukue Benyamini kwenda Misri ili wakanunue chakula zaidi.

Sasa Yusufu anawaona ndugu zake wakija. Anafurahi sana kumwona Benyamini mdogo wake. Lakini hakuna kati yao nayejua kwamba mkuu huyo ni Yusufu. Sasa Yusufu anawajaribu ndugu zake kumi.
Anawaagiza watumishi wake wajaze mifuko yao yote chakula. Lakini bila kuwajulisha, anawaagiza pia watie kikombe chake cha pekee cha fedha katika mfuko wa Benyamini. Wote wakiisha kuondoka na kutmebea mwendo mfupi njiani, Yusufu anawatuma watumishi wake wawafuate. Wanapowakuta, watumishi hao wanasema hivi: ‘Kwa nini mmeiba kikombe cha fedha cha bwana yetu.’

‘Hatukuiba kikombe chake,’ ndugu wote wanajibu. ‘Ukiona kikombe hicho kwa ye yote kati yetu, mtu huyo na auawe.’
Basi watumishi wanachunguza mifuko yote, wanakiona kikombe katika mfuko wa Benyamini, kama unavyoona hapa. Watumishi

hao wanasema: ‘Ninyi wengine nendeni, lakini Benyamini atakwenda nasi.’ Sasa ndugu hao 10 watafanya nini?
Wote wanarudi pamoja na Benyamini kwenye nyimba ya Yusufu. Yusufu anwaambia ndugu zake hivi: ‘Nyote nendeni kwenu, lakini Benyamini atakaa huku awe mtumwa wangu.’

Yuda anapaza sauti, hivi: ‘Tukirudi kwetu bila kijana huyu, baba yangu atakufa kwa sababu ampenda sana. Tafadhali, unifanye mimi niwe mtumwa wako huku, lakini mruhusu kijana huyu aende nyumbani.’
Yusufu anajua kwamba ndugu zake wamebadilika. Sasa wana huruma. Na tuchunguze tuone anyofanya Yusufu sasa.
Mwanzo 42:9-38; 43:1-34; 44:1-34.




attachment.php




 

Attachments

  • yusuph anawajaribu ndugu zake.jpg
    yusuph anawajaribu ndugu zake.jpg
    50.6 KB · Views: 97
Hadithi ya 25: Jamaa Inahama Kwenda Misri

YUSUFU hawezi kujizuia tena. Anawaambia watumishi wake wote waondoke chumbani. Anapokuwa peke yake pamoja na ndugu zake, Yusufu anaanza kulia. Twaweza kuwazia jinsi ndugu zake wanavyoshangaa, kwa sababu hawajui sababu analia. Mwishowe anawaambia hivi: ‘Mimi ni Yusufu. Je! baba yangu angali hai?

Ndugu zake wanashangaa sana hata hawawezi kusema. Wanaogopa. Lakini Yusufu anawaambia hivi: ‘Tafadhali njoni karibu zaidi.’ Wanapokaribia zaidi, anawaambia hivi: ‘Mimi ni ndugu yenu Yusufu, ambaye mliuza Misri.’

Yusufu anaendelea kusema kwa huruma hivi: ‘Msijilaumu kwa sababu mliniuza huku. Ni Mungu aliyenituma nije Misri niokoe maisha za watu. Farao amenifanya niwe mtawala wa nchi yote. Basi sasa fanyeni haraka mrudi kwa baba yangu mkamwambie hivyo. Mwambieni aje kukaa huku.’
Kisha Yusufu anawakumbatia ndugu zake, na kuwabusu wote. Farao anaposikia kwamba ndugu za Yusufu wamekuja anamwambia Yusufu hivi: ‘

Na wachukue magari waende kumchukua baba na jamaa zao warudi huku. Nitawapa nchi iliyo bora zaidi katika Misri yote.’
Ndivyo walivyofanya. Hata unaweza kumwona Yusufu akimlaki baba yake anapofika Misri akiwa na jamaa yake yote.

Jamaa ya Yakobo imekuwa kubwa sana. Walipohama kwenda Misri wote walikuwa 70, kutia Yakobo na watoto wake na wajukuu wake. Lakini walikuwako pia wake, na labda watumishi wengi. Wote hao wakahama kwenda Misri. Wakaitwa Waisraeli, kwa sababu Mungu alikuwa amebadili jina la Yakobo kuwa Israeli. Waisraeli wakawa watu wa pekee sana kwa Mungu kama tutakavyoona baadaye.
Mwanzo 45:1-28; 46:1-27.

attachment.php
 

Attachments

  • jamaa inahama kwenda misri.jpg
    jamaa inahama kwenda misri.jpg
    21 KB · Views: 83
Hadithi ya 26: Ayubu Ni Mwaminifu Kwa Mungu
attachment.php



UNAMSIKITIKIA mgonjwa huyu? Anaitwa Ayubu (Yobu). Mwanamke huyu ni mke wake. Unajua anamwambia Ayubu nini? ‘Mtukane Mungu ufe.’ Tuone sababu anasema hivyo, na sababu Ayubu aliteswa sana.

Ayubu alimwamini na kumtii Yehova. Alikaa katika nchi ya Usi, karibu na Kanaani. Yehova alipenda Ayubu sana. Lakini mtu mmoja alimchukia. Unamjua?

Ni Shetani Ibilisi. Kumbuka, Shetani ni yule malaika mbaya anayemchukia Yehova. Alishawishi Adamu na Hawa wasitii Yehova. Alifikiri anaweza pia kushawishi kila mtu asitii Yehova. Je! aliweza? Hapana. Wafikirie wanaume na wanawake wengi waaminifu ambao tumejifunza habari zao. Unaweza kutaja majina ya wangapi?

Yakobo na Yusufu wakisha kufa huko Misri, Ayubu akawa ndiye mtu mwaminifu sana kwa Yehova katika dunia yote. Yehova alitaka kujulisha Shetani kwamba hawezi kushawishi kila mtu afanye mabaya. Akasema hivi: ‘Tazama Ayubu. Ni mwaminifu sana kwangu.’
Shetani akapinga hivi: ‘Ni mwaminifu kwa sababu unambariki tena ana vitu vizuri vingi. Lakini ukivichukua, atakutukana.’

Yehova akasema: ‘Haya, vichukue. Mfanyie Ayubu mambo yote mabaya. Tutaona kama atanitukana. Lakini usimwue.’
Kwanza, Shetani akaongoza watu waibe ng’ombe za Aybu na ngamia, na kondoo zake zikauawa. Akaua wana 10 na binti zake katika upepo

mkali. Kisha, Shetani akapiga Ayubu kwa ugonjwa huo mbaya sana. Ayubu aliteswa sana. Ndiyo sababu mke wake alimwambia: ‘Mtukane Mungu ufe.’ Ayubu hakufanya hivyo. Rafiki watatu wa uongo wakaja kumwambia ana maisha mabaya. Lakini Ayubu aliendelea kuwa mwaminifu.
Yehova alifurahi sana na kumbariki Ayubu, kama unavyoona katika picha hii. Alimponya ugonjwa wake. Ayubu akawa na watoto wengine wazuri 10, ng’ombe, kondoo na ngamia wengi mara mbili kuliko zamani.
Je! utakuwa mwaminifu kwa Yehova sikuzote kama Ayubu? Ukiwa hivyo, Mungu atakubariki wewe pia. Utakaa milele wakati dunia yote itafanywa nzuri sana kama bustani ya Edeni.
Ayubu 1:1-22; 2:1-13; 42:10-17.

attachment.php


 

Attachments

  • Ayubu.jpg
    Ayubu.jpg
    14.2 KB · Views: 73
  • Ayubu 2.jpg
    Ayubu 2.jpg
    39.9 KB · Views: 89
Hadithi ya 27: Mfalme Mbaya Anatawala Misri

WANAUME hawa wanalazimisha watu kufanya kazi. Mtazame yule mwanamume anayempiga mfanya kazi mmoja kwa fimbo! Wafanya kazi hao ni wa jamaa ya Yakobo, nao wanaitwa Waisraeli. Na wanaume hao wanaowalazimisha kufanya kazi ni Wamisri. Waisraeli wamekuwa watumwa wa Wamisri. Ilikuwa hivyo namna gani?
attachment.php

Kwa miaka mingi jamaa ya Yakobo ilikaa kwa amani huko Misri. Yusufu, aliyekuwa mkuu katika Misri na wa pili kwa mfalme Farao, aliwaangalia vizuri. Lakini Yusufu akafa. Farao mpya, ambaye hakuwapenda Waisraeli, akawa mfalme wa Misri.
Basi Farao huyo mbaya akawafanya Waisraeli kuwa watumwa. Naye akaweka wasimamizi juu yao, wanaume waliokuwa wakali na bila huruma. Wakawalazimisha Waisraeli kufanya kazi ngumu wakijenga miji ya Farao. Lakini Waisraeli waliendelea kuongezeka. Baada ya muda mfupi Wamisri waliogopa kwamba Waisraeli wangekuwa wengi mno na wenye nguvu mno.
attachment.php



Unajua Farao alifanya nini? Aliwaambia wanawake waliosaidia akina mama Waisraeli wakati wa kuzaa watoto wao, akasema: ‘Ueni kila mtoto wa kiume anayezaliwa.’ Lakini wanawake hao walikuwa wazuri, hawakuwaua watoto wachanga.
Basi Farao akaamuru watu wake hivi: ‘Waueni watoto wachanga Waisraeli. Acheni tu watoto wa kike waishi.’ Ilikuwa amri mbaya sana, sivyo? Na tuone namna mtoto mmoja wa kiume alivyookolewa.
Kutoka 1:6-22.


 

Attachments

  • mfalme mbaya2.jpg
    mfalme mbaya2.jpg
    36.5 KB · Views: 86
  • mfalme.jpg
    mfalme.jpg
    31 KB · Views: 84
Hadithi ya 28: Namna Mtoto Musa Alivyookolewa

TAZAMA mtoto mchanga analia, akakikamata kidole cha mama yule. Huyu ni Musa. Unajua mama huyo mzuri ni nani? Ni binti mfalme wa Misri, binti ya Farao mwenyewe.
attachment.php



Mama ya Musa alimficha mtoto wake mpaka alipokuwa mwenye umri wa miezi mitatu, kwa sababu hakutaka auawe na Wamisri. Lakini alijua kwamba huenda Musa akaonekana, basi akafanya hivyo ili amwokoe.
Alichukua kikapu akakitengeneza ili maji yasiingie ndani. Kisha akamweka Musa ndani yake, akakiweka kikapu hicho katika majani marefu kando ya Mto Nailo. Miriamu, dada yake Musa alambiwa asimame karibu aone itakavyokuwa.
Upesi binti Farao akaja kwenye Mto Nailo aoge. Mara moja akaona kikapu katika majani marefu. Akamwita mtumishi wake mmoja, akamwambia: ‘Kaniletee kikapu kile.’ Binti mfalme alipofungua kikapu hicho, lo! aliona mtoto mzuri kama nini! Mtoto Musa alikuwa akilia, naye binti mfalme akamhurumia. Hakutaka amruhusu auawe.
Miriamu akaja. Unaweza kumwona katika picha hii. Miriamu akamwuliza binti Farao hivi: ‘Niende nikamwite mwanamke Mwisraeli akulelee mtoto huyu?’
‘Nenda tafadhali,’ akasema binti mfalme.
Basi Miriamu akakimbia haraka kwenda kumwambia m ama yake. Mama ya Musa alipokuja kwa binti mfalme, binti mfalme akasema: ‘Mchukue mtoto huyu unilelee, nami nitakulipa.’
Basi mama ya Musa akalea mtoto wake mwenyewe. Baadaye Musa alipokuw amkubwa kidogo, mama yake alimpeleka kwa binti Farao, aliyemlea kama mwanawe mwenyewe. Hivyo ndivyo Musa alivyokua katika nyumba ya Farao.
Kutoka 2:1-10.

 

Attachments

  • mtoto musa.jpg
    mtoto musa.jpg
    25.4 KB · Views: 80
Hadithi ya 29: Sababu Musa Alikimbia

TAZAMA Musa anakimbia Misri. Unaweza kuwaona wanaume hao wanaomfuata? Unajua kwa nini wanataka kumwua Musa? Ebu tuone kama twaweza kujua.
attachment.php


Musa alikua katika nyumba ya Farao, mtawala wa Misri. Akawa mwenye akili na mkuu sana. Musa alijua kwamba yeye si Mmisri, bali wazazi wake ni watumwa Waisraeli.
Siku moja, alipokuwa mwenye miaka 40, Musa alamua kwenda kuona namna watu wake walivyokuwa. Walikuwa wakiteswa sana. Alimwona Mmisri akimpiga mtumwa Mwisraeli. Musa akatazama huku na huku, na alipokosa kumwona mtu yeyote, alimpiga Mmisri mpaka akafa, kisha Musa akaficha mwili wake katika mchanga.
Kesho yake Musa akatoka tena kuwaona watu wake. Alifikiri angeweza kuwasaidia wasiwe watumwa tena. Lakini aliona wanaume Waisraeli wakipigana, basi akamwambia yule aliyekuwa na kosa hivi: ‘Kwa nini unampiga sana ndugu yako?’
Mwanamume huyo akasema: ‘Nani aliyekufanya wewe uwe mtawala na hakimuw etu? Je! utaniua mimi kama ulivyomwua yule Mmisri?’
Musa akaogopa. Alifahamu kwamba watu wamejua alilomtenda yule Mmisri. Hata Farao alisikia habari hizo, naye akawatuma watu wakamwue Musa. Ndiyo sababu Musa alilazimika kukimbia Misri.
Musa alipoondoka Misri, alikwenda mbali kwenye nchi ya Midiani. Niko alikokutana na jamaa ya Yethro, akaoa binti yake mmoja jina lake Sipora. Musa akawa mchugnaji wa kondoo za Yethro. Alikaa katika nchi hiyo ya Midiani kwa miaka 40. Sasa akawa mwenye umri wa miaka 80. Ndipo siku moja, Musa alipokuwa akichunga kondoo za Yethro, kulitokea ajabu moja iliyogeuza maisha yote ya Musa. Tuone ajabu hiyo ni nini.
Kutoka 2:11-25; Matendo 7:22-29.


 

Attachments

  • musa alikimbia misri.jpg
    musa alikimbia misri.jpg
    22 KB · Views: 79
Hadithi ya 30: Mti Mdogo Unaowaka Moto

MUSA alikuwa amekwenda mpaka kwenye Mlima wa Horebu ili atafute majani ya kondoo zake. Akaona mtu mdogo ukiwaka moto, lakini haukuteketea!

attachment.php




‘Hii ni ajabu,’ Musa akawaza. ‘Nitakaribia zaidi nione vizuri.’ Alipokaribia, sauti ikatoka katika mtu huo mdogo ikisema: ‘Usije karibu zaidi. Ondoa viatu vyako, kwa sababu unasimama mahali patakatifu.’ Mungu alikuwa akisema kupitia kwa malaika, hivyo Musa akafunika uso wake.
Kisha Mungu akasema: ‘Nimeyaona mateso ya watu wangu huko Misri. Basi nitawaokoa, nami nanakutuma wewe ukawatoe watu wangu Misri.’ Yehova alikusudia kuwapeleka watu wake kwenye nchi nzuri ya Kanaani.
Lakini Musa akasema: ‘Mimi ni mtu tu. Nifanyeje hivyo? Nikienda nao waisraeli wataniuliza, “Nani aliyekutuma?” Nitasema nini?’
‘Utasema hivi,’ Mungu akajibu. ‘“YEHOVA Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakoo amenituma kwenu.”’ Yehova akaongezea: ‘Hilo ndilo jina langu milele.’
‘Lakini kama hawaniamini nikisema umenituma, hapo itakuwaje,’ Musa akajibu.
‘Nini hicho mkononi mwako?’ Mungu akauliza.
Musa akajibu: ‘Fimbo.’
‘Itupe chini,’ Mungu akasema. Musa alipoitupa chini, fimbao ikawa nyoka. Kisha Yehova akamwonyesha Musa muujiza mwingine. Akasema: ‘Ingiza mkono wako katika vazi lako.’ Musa akaingiza, na alipoutoa mkono wake, ulikuwa mweupe kama theluji! Mkono huo ulikuwa kama umepatwa na ugonjwa mbaya unaoitwa ukoma. Kisha Yehova akampa Musa uwezo wa kufanya mwujiza wa tatu. Halafu akamwambia hivi: ‘Utakapofanya miujiza hii Waisraeli wataamini kwamba nimekutuma.’
Baada ya hayo Musa akaenda nyumbani na kumwambia Yethro hivi: ‘Tafadhali uniruhusu nirudi kwa watu wangu huko Misri nione wa hali gani.’ Basi Yethro akamwambia Musa, kwa heri, naye Musa akaanza safari ya kurudi Misri.
Kutoka 3:1-22; 4:1-20.


 

Attachments

  • mti wa moto.jpg
    mti wa moto.jpg
    21.4 KB · Views: 69

Hadithi ya 31: Musa na Haruni Wanamwona Farao

MUSA aliporudi Misri, akamwambia Haruni ndugu yake habari ya miujiza yote. Musa na Haruni walipowaonyesha Waisraeli miujiza hiyo, watu wote wakaamini kwamba Yehova alikuwa nao.
Kisha Musa na Haruni wakaenda kumwona Farao. Wakamwambia: ‘Yehova Mungu wa Israeli anasema, “Waruhusu watu wangu waende mwendo wa siku tatu, wakaniabudu jangwani.” ’ Lakini Farao akajibu hivi: ‘Mimi simwamini Yehova. Na sitawaruhusu Waisraeli waende.’
Farao alikasirika, kwa sababu watu walitaka wapewe ruhusa ya kwenda kumwabudu Yehova. Basi akawalazimisha wafanye kazi ngumu hata zaidi. Waisraeli wakamlaumu Musa kwa sababu waliteswa vibaya sana, naye Musa akahuzunika. Lakini Yehova akamwambia asisumbuke. ‘Nitamfanya Farao aruhusu watu wangu waende,’ Yehova akasema.
attachment.php



Musa na Haruni wakaenda kumwona Farao tena. Wakati huu walifanya mwujiza. Haruni akaitupa fimbo yake chini, nayo ikawa nyoka mkubwa. Lakini watu wenye akili wa Farao pia wakazitupa fimbo zao chini, nyoka wakatokea. Lakini, ebu tazama! Yoka wa Haruni anakula wale nyoka wa watu wenye akili. Hata hivyo Farao hataki kuwaruhusu Waisraeli waende.
Basi wakati wa Yehova ukafika wa kuonyesha yeye ana uwezo kuliko Farao. Unajua alivyofanya? Ni kwa kuleta mapigo 10 au taabu kubwa, juu ya Misri.
Baada ya mapigo mengi kidogo, Farao akaagiza Musa itwe, na kusema: ‘Lizuie pigo, nami nitawapa ruhusa Waisraeli waende.’ Lakini pigo hilo lilipozuiwa, Farao aligeuza nia yake. Hakuwaruhusu watu waende. Lakini, mwishowe, baada ya pigo la 10, Farao alifukuza Waisraeli.
Je! Unajua mapigo hayo 10 yalikuwa gani? Na tujifunze juu yao.
Kutoka 4:27-31; 5:1-23; 6:1-13, 26-30; 7:1-13.

 

Attachments

  • musa na haruni.jpg
    musa na haruni.jpg
    19 KB · Views: 81
Hadithi ya 32: Mapigo 10

TAZAMA picha hizi. Kila moja inaonyesha pigo ambalo Yehova alileta juu ya Misri. Katika picha ya kwanza unaweza kumwona Harui akiupiga Mto Nailo kwa fimbo yake. Alipoupiga, maji ya mto yakawa damu. Samaki wakafa, nao mto ukaanza kunuka vibaya.
attachment.php


Kisha, Yehova akafanya vyura watoke katika Mto Nailo. Walikuwa mahali pote—katika majiko ya kuokea mikate, vikaangio, katika vitanda vya watu—mahali pote. Vyura hao walipokufa Wamisri waliwakusanya wengi sana, na nchi ikanuka vibaya.

Halafu Haruni akaipiga ardhi kwa fimbo yake, nayo mavumbi yakawa chawa. Hao ni wadudu wadogo wanaouma. Chawa walikuwa pigo la tatu juu ya nchi ya Misri.

Mapigo mengine yaliumiza Wamisri peke yao, si Waisraeli. Pigo la nne lilikuwa mainzi wakubwa waliojaa katika nyumba za Wamisri wote. Pigo la tano lilikuwa juu ya wanyama. Ng’ombe na kondoo na mbuzi wengi wa Wamisri wakafa.

Kisha, Musa na Harui wakachukua majivu na kuyatupa angani. Yakawa vidonda vibaya juu ya watu na wanyama. Hilo lilikuwa pigo la sita.

Baada ya hapo Musa akainua mkono wake kuelekea angani, naye Yehova akapeleka ngurumo na mvua ya mawe. Ilikuwa mvua ya mawe iliyo mbaya zaidi kuipiga Misri.

Pigo la nane lilikuwa kundi la nzige. Nzige hao wengi sana hawakuwa wameonekana kabla ya hapo wala baadaye. Walikula kila kitu ambacho mvua ya mawe haikuharibu.

Pigo la tisa lilikuwa giza. Kwa muda wa siku tatu giza zito liliifunika nchi, lakini Waisraeli wakawa na nuru katika makao yao.

Mwishowe Mungu akawaambia watu wake wapake damu ya mwana-mbuzi au mwana-kondoo juu ya milango yao. Kisha malaika wa Mungu akapita juu ya Misri.

Malaika huyo alipoiona damu, hakuua mtu ye yote katika nyumba hiyo. Lakini katika nyumba zote ambazo damu haikupakwa juu ya milango, malaika wa Mungu aliua wazaliwa wa kwanza wa wanadamu na wa wanyama. Hilo lilikuwa pigo la 10.

Baada ya pigo hilo, Farao akawaambia Waisraeli waondoke. Watu wa Mungu wote walikuwa tayari kwenda, na usiku uo huo wakaanza kutoka Misri.
Kutoka sura ya 7 hadi 12.


 

Attachments

  • mapigo 10.jpg
    mapigo 10.jpg
    29.1 KB · Views: 74
Hadithi ya 33: Kuvuka Bahari Nyekundu (Ya Shamu)

TAZAMA tukio hili! Yule ni Musa akiwa na fimbo imenyoshwa juu ya Bahari Nyekundu. Wale walio pamoja naye salama upande mwingine ni Waisraeli. Lakini Farao na jesho lake lote wanazama katika bahari. Na tuone ilivyokuwa.
attachment.php



Kama tulivyojifunza, Farao aliwaambia Waisraeli waondoke Misri Mungu alipokwisha kuleta pigo la 10 juu ya Wamisri. Wanaume Waisraeli karibu 600,000 wakaondoka, pia wanawake na watoto wengi. Pia, hesabu kubwa ya watu wengine, waliokuwa wamemwamini Yehova, wakaondoka pamoja na Waisraeli. Wote walichukua kondoo na mbuzi na ng\ombe zao wakaenda nazo.
Kabla ya kuondoka, Waisraeli waliwaomba Wamisri wawape mavazi na vitu vya dhahabu na fedha. Wamisri hao waliogopa sana, kwa sababu ya lile pigo la mwisho lililowapata. Basi wakawapa Waisraeli kila kitu walichowaomba.
Baada ya siku chache Waisraeli wakafika kwenye Bahari Nyekundu. Wakapumzika huko. Wakati huo, Farao na watu wake walianza kuhuzunika kwa vile wamewafukuza Waisraeli. ‘Tumeacha watumwa wetu wakaenda!’ wakasema.
Hivyo Farao akabadili tena nia yake. Upesi akatayarisha gari lake la vita na jeshi lake. Kisha akaanza kuwafuatia Waisraeli akiwa na magari ya pekee 600, pia magari mengine yote ya Misri.
Waisraeli walipomwona Farao na jeshi lake wakiwafuata, waliogopa sana. Hakukuwa na njia ya kukimbilia. Ile Bahari Nyekundu ilikuwa upande wao mmoja na Wamisri upande mwingine. Lakini Yehova aliweka wignu kati ya watu wake na Wamisri. Hivyo Wamisri hawakuweza kuwaona Waisraeli wawashambulie.
Kisha Yehova akamwambia Musa anyoshe fimbo yake juu ya Bahari Nyekundu. Alipoinyosha, Yehova akafanya upepo wenye nguvu wa mashariki uvume. Yale maji ya bahari yalitengana, yakasimama pande mbili.
Ndipo Waisraeli wakaanza kutembea katika bahari katika nchi kavu. Ilichukua saa nyingi ili mamilioni ya watu pamoja na wanyama wao wapite salama katika bahari kwenda upande mwingine. Mwishowe Wamisri waliweza kuwaona Waisraeli tena. Watumwa wao walikuwa wakikimbia! Basi wakaingia haraka katika bahari wakiwafuata.
Walipoingia, Mungu alifanya magurudumu ya magari yao yatoke. Wamisri wakaanza kuogopa na kupaza sauti hivi: ‘Yehova anawapigania Waisraeli. Na tuondoke huku!’ Lakini walikuwa wamechelewa.
Wakati huo ndipo Yehova alipomwambia Musa anyoshe fimbo yake juu ya Bahari Nyekundu, kamaulivyoona katika picha. Musa alipofanya hivyo, zile kuta zilianza kurudi na kuwafunika Wamisri na magari yao. Jeshi lote lilikuwa limewafuata Waisraeli katika bahari. Hakuna hata mmoja wa Wamisri hao aliyeokoka!
Lo! watu wote wa Mungu walifurahi kwa vile walivyookoka! Wanaume wakaimba wimbo wa kumshukuru Yehova, wakisema: ‘Yehova amepata ushindi mtukufu. Amewatupa farasi na wanaowapanda baharini.’ Miriamu dada ya Musa akachukua matari yake, nao wanawake wote wakamfuata wakiwa na matari yao. Na walipokuwa wakicheza kwa furaha, waliimba wimbo ule ule walioimba wanaume wakisema: ‘Yehova amepata ushindi mtukufu. Amewatupa farasi na wanaowapanda baharini.’
Kutoka sura ya 12 mpaka 15.


 

Attachments

  • kuvuka bahari.jpg
    kuvuka bahari.jpg
    32.1 KB · Views: 91
Sehemu 3: Kukombolewa Misri Mpaka Mfalme wa Kwanza wa Israeli

Musa aliwaongoza Waisraeli kutoka utumwa wa Misri kwenda kwenye Mlima Sinai, ambako Mungu aliwapa sheria zake. Baadaye, Musa akawatuma wanaume 12 wakapeleleze nchi ya Kanaani. Lakini 10 kati yao wakarudisha ripoti mbaya. Waliwafanya watu watake kurudi Misri. Kwa kukosa imani, Mungu aliwaadhibu Waisraeli kwa kuwafanya watange-tange jangwani muda wa miaka 40.
Mwishowe, Yoshua akachaguliwa aongoze Waisraeli kuingia nchi ya Kanaani. Ili kuwasaidia waichukue nchi hiyo Yehova alifanya miujiza mingi. Alifanya maji ya Mto Yordani yaache kutiririka, kuta za Yeriko zianguke, jua lisimame bila kwenda kwa siku nzima. Baada ya miaka sita, nchi hiyo ikachukuliwa kutoka kwa Wakanaani.
Kuanzia na Yoshua, Waisraeli walitawalwa na mahakimu (waamuzi) muda wa miaka 356. Twajifunza habari za wengi wao, kutia Baraki, Gideoni, Yeftha, Samsoni na Samweli. Pia twasoma habari za wanawake kama Rahabu, Debora, Yaeli, Ruthu, Naomi na Delila. Kwa jumla, Sehemu ya 3 inasimulia historia ya miaka 396.
attachment.php
 

Attachments

  • kukombolewa kwa misri.jpg
    kukombolewa kwa misri.jpg
    38 KB · Views: 90
Back
Top Bottom