Sehemu 1: Uumbaji Mpaka Gharika

Sehemu 1: Uumbaji Mpaka Gharika

Hadithi ya 34: Aina Mpya ya Chakula

UNAJUA watu wanaokota nini chini? Ni cheupe, na chembamba na chenye kupasuka vipande vyembamba. Ni chakula.
attachment.php



Umekuwa karibu mwezi mmoja tu tangu Waisraeli waondoke Misri. Wamo jangwani. Humo chakula kidogo kinamea, watu wanalia, wakisema: ‘Afadhali Yehova angetuua huko Misri. Tulikula huko kila chakula tulichotaka.’
Basi Yehova asema: ‘Nitatelemsha chakula kutoka angani.’ Ndivyo Yehova anafanya. Kesho yake Waisraeli wanapoona chakula hicho cheupe kilichoanguka, wanaulizana hivi: ‘Ni nini hiki?’
Musa anajibu: ‘Ndicho chakula ambacho Yehova amewapa mle.’ Watu wanakiita MANA. Utamu wake ni kama keki (mkate) nyembamba zenye asali.
‘Kila mtu aokote anachoweza kula,’ Musa anawaambia watu. Basi kila asubuhi wanaokota hivyo. Jua linapokuwa kali, ile mana iliyoachwa chini inayeyuka.
Pia Musa anasema: ‘Mtu asiweke mana ikae mpaka kesho.’ Lakini watu wengine hawasikii. Unajua inavyokuwa? Kesho yake ile mana waliyoweka inajaa wadudu, inaanza kunuka vibaya!
Walakini kuna siku moja katika juma ambayo Yehova anawaambia watu wakusanye mana nyingi mara mbili. Siku hiyo ni ya sita. Yehova anawaambia waweke akiba ya kesho, kwa sababu hataangusha mana yo yote siku ya saba. Wanapoweka akiba ya siku ya saba, haijai wadudu wala kunuka! Huo ni mwujiza mwingine.
Miaka yote ambayo Waisraeli walikuwa jangwani Yehova aliwalisha mana.
Kutoka 16:1-36; Hesabu 11:7-9; Yoshua 5:10-12.


 

Attachments

  • aina mpya ya chakula.jpg
    aina mpya ya chakula.jpg
    56.9 KB · Views: 81
Hadithi ya 35: Yehova Anatoa Sheria Zake

KARIBU miezi miwili baada ya Waisraeli kuondoka Misri, wanakuja kwenye Mlima Sinai unaoitwa pia Horebu. Ni pale pale ambapo Yehova alisema na Musa katika mti mdogo uliowaka moto. Watu wanapiga kambi hapa na kukaa kidogo.
Watu wanapongojea chini, Musa apanda mlima. Katika mlima, Yehova anamwambia Musa kwamba Yeye anataka Waisraeli wamtii na kuwa watu Wake wa pekee. Musa anaposhuka, anawaambia Waisraeli maneno ya Yehova. Watu hao wanasema kwamba watamtii Yehova, kwa sababu wanataka kuwa watu wake.
Sasa Yehova anafanya mwujiza. Anafanya kilele cha mlima kitoke moshi, na kufanyiza ngurumo yenye sauti kubwa. Pia anawaambia watu hivi: ‘Mimi ni Yehova Mungu wenu niliyewatoa Misri.’ Kisha anawaamuru hivi: ‘Usiabudu miungu mingine isipokuwa mimi.’
attachment.php


Mungu anawapa Waisraeli amri nyingine tisa, au sheria. Watu wanaogopa sana. Wanamwambia Musa hivi: ‘Wewe sema na sisi, kwa sababu Mungu akisema na sisi huenda tukafa.’
Baadaye Yehova anamwambia Musa hivi: ‘Njoo kwangu mlimani. Nitakupa mabamba mawili ya mawe ambapo nimeandika sheria ninazotaka watu washike.’ Tena Musa anapanda mlimani. Anakaa huko muda wa siku 40 mchana na usiku.
Mungu ana sheria nyingi nyingi za kuwapa watu. Musa anaziandika sheria hizo. Pia Mungu anampa Musa mabamba mawili ya mawe. Juu ya hayo, Mungu mwenyewe ameandika sheria 10 alizowaambia watu wote. Zinaitwa Amri Kumi.
attachment.php



Amri Kumi ni sheria za maana. Hata sheria nyingine nyingi ambazo Mungu anawapa Waisraeli ni za maana. Moja ya hizo sheria ni hii: ‘Inakupasa umpende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa akili zako zote, kwa nafsi yako yote na nguvu zako zote.’ Nyingine ni hii: ‘Inakupasa umpende jirani yako kama unavyojipenda.’ Yesu Kristo, Mwana wa Mungu, alisema kwamba hizo ndizo sheria mbili zilizo kubwa kuliko zote ambazo Yehova aliwapa watu wake Waisraeli. Baadaye tutajifunza mambo mengi juu ya Mwana wa Mungu na mafundisho yake.
Kutoka 19:1-25; 20:1-21; 24:12-18; 31:18; Kumbukumbu la Torati 6:4-6; Mambo ya Walawi 19:18; Mathayo 22:36-40.


 

Attachments

  • sheria.jpg
    sheria.jpg
    4.3 KB · Views: 77
  • musa na sheria.jpg
    musa na sheria.jpg
    12.6 KB · Views: 81
Hadithi ya 2: Bustani Nzuri

TAZAMA dunia hii! Kila kitu ni kizuri sana! Tazama majani na miti, maua na wanyama wote. Unaweza kumjua tembo na simba hapa?
02.jpg

Bustani hii nzuri ilitokea namna gani? Na tuone Mungu alivyotuwekea dunia tayari.
Kwanza, Mungu aliumba majani mabichi yaifunike nchi. Alifanya namna zote za mimea na miti midogo. Mimea hiyo inapamba dunia. Zaidi ya hivyo, mimea mingi inatupa chakula kitamu sana.
Tena Mungu aliumba samaki waogelee katika maji na ndege waruke katika anga. Aliumba mbwa na paka na farasi; wanyama wakubwa na wadogo. Ni wanyama gani wanaokaa karibu na nyumba yenu? Je! si vizuri kufurahi kwa vile Mungu alitufanyia vyote hivyo?
Halafu, Mungu alifanya sehemu moja ya dunia kuwa ya pekee sana. Aliiita bustani ya Edeni. Ilikuwa nzuri sana. Kila kitu ndani kilikuwa kizuri. Mungu alitaka dunia nzima iwe kama bustani nzuri hii.
Lakini tazama tena picha hii ya bustani. Je! unajua kitu ambacho Mungu aliona hakipo? Tuone.
Mwanzo 1:11-25; 2:8, 9.


MziziMkavu natamani duniaingekua hivi lol!
 
Last edited by a moderator:
Hadithi ya 36: Ndama ya Dhahabu

MAMA WEE! Sasa watu wanafanya nini? Wanaabudu ndama! Kwa nini wanafanya hivyo?
Musa anapokawia mlimani, watu wasema hivi: ‘Hatujui yaliyompata Musa. Basi na tufanye mungu atutoe katika nchi hii.’
attachment.php



‘Vema,’ Haruni ndugu yake Musa asema. ‘Vueni pete zenu za dhahabu masikioni mniletee.’ Haruni anaziyeyusha na kufanya ndama ya dhahabu. Kisha watu wasema hivi: ‘Huyu ni Mungu wetu, aliyetutoa katika Misri!’ Halafu Waisraeli wanafanya karamu kubwa, na kuiabudu ndama hiyo ya dhahabu.
Yehova anapoona hayo, anakasirika sana. Anamwambia Musa hivi: ‘Fanya haraka ushuke. Watu wanafanya vibaya sana. Wamesahau sheria zangu nao wanaabudu ndama ya dhahabu.’
attachment.php



Musa anashuka haraka mlimani. Anapokaribia, anaona hivi. Watu wanaimba na kucheza wakizunguka ndama ya dhahabu! Musa anakasirika sana hata anayatupa chini mabamba mawili ya mawe yenye kuandikwa sheria, nayo yanavunjika-vunjika. Kisha anachukua ndama ya dhahabu na kuiyeyusha kabisa. Halafu anaisaga kuwa unga.
Watu wamefanya jambo baya sana. Musa anawaambia wanaume kati yao wachukue panga zao. ‘Wale watu wabaya walioiabudu ndama ya dhahabu lazima wafe,’ Musa anasema. Basi wanaume hao wanawaua watu 3,000! Inatupasa tumwabudu Yehova pekee kuliko miungu ya uongo, sivyo?
Kutoka 32:1-35.


 

Attachments

  • Ndama ya Dhahabu.jpg
    Ndama ya Dhahabu.jpg
    39.9 KB · Views: 82
  • Ndama ya Dhahabu 2.jpg
    Ndama ya Dhahabu 2.jpg
    32.7 KB · Views: 88
Hadithi ya 37: Hema ya Ibada

UNAJUA jengo hili? Ni hema ya pekee ya kuabudia Yehova. Watu walimaliza kuijenga mwaka mmoja baada ya kuondoka Misri. Unajua aliyetoa wazo la kuijenga?
attachment.php



Ni Yehova. Musa alipokuwa katika Mlima Sinai, Yehova alimwambia namna ya kuijenga. Alimwambia ijengwe ili iwe vyepesi kubomolewa. Kwa njia hiyo sehemu zake zingeweza kuchukuliwa mahali pengine, na kuunganishwa tena. Basi Waisraeli walipokuwa wakihama hapa na pale jangwani, walichukua hema hiyo.
Ukitazama ndani ya chumba kidogo mwishoni mwa hema, unaweza kuona sanduku, au kasha. Hilo laitwa sanduku la agano. Kila upande ulikuwa na malaika au kerubi mmoja wa dhahabu. Tena Mungu aliziandika Amri Kumi juu ya mabamba mawili ya mawe, kwa sababu Musa alikuwa ameyavunja yale ya kwanza. Na mawe hayo yalitunzwa ndani ya sanduku la agano. Pia, mtungi wa mana ulitunzwa ndani yake. Unakumbuka mana ni nini?
Yehova anachagua Haruni ndugu yake Musa awe kuhani mkuu. Anawaongoza watu wamwabudu Yehova. Na wanawe ni makuhani pia.
Sasa kitazame chumba kikubwa zaidi cha hema hiyo. Ni kikubwa mara mbili kuliko kile chumba kidogo. Unaliona lile sanduku au kasha dogo, na moshi kidogo ukipanda kutoka ndani yake? Ndiyo madhabahu ambapo makuhani wanachoma uvumba. Halafu kuna kinara cha taa chenye taa saba. Na kitu cha tatu chumbani ni meza. Mikate 12 inatunzwa juu yake.
Uani mwa hema mna bakuli kubwa, au birika, iliyojaa maji. Makuhani wanaitumia kwa kuogea. Pia kuna madhabahu kubwa. Hapo ndipo wanyama wafu wanapochomwa wawe toleo kwa Yehova. Hema iko katikati ya kambi, na Waisraeli wanakaa katika hema zao kuizunguka.
Kutoka 25:8-40; 26:1-37; 27:1-8; 28:1; 30:1-10, 17-21; 34:1, 2;Waebrania 9:1-5.


 
Hadithi ya 38: Wapelelezi 12

attachment.php


TAZAMA matunda ambayo wanaume hawa wanabeba. Tazama kichala kile cha zabibu kilivyo kikubwa. Kinataka wanaume wawili wakibebe kwa mti. Zitazame tini na yale makomamanga. Matunda hayo mazuri yalitoka wapi? Nchi ya Kanaani. Kumbuka, wakati mmoja Ibrahimu, Isaka na Yakobo walikaa Kanaani. Lakini kwa sababu kulikuwako njaa kuu, Yakobo na jamaa yake, walihama wakaenda Misri. Sasa, miaka kama 216 baadaye, Musa anawarudisha Waisraeli Kanaani. Wamefika mahali panapoitwa Kadeshi huko jangwani.
Watu wabaya wanakaa Kanaani. Basi Musa anawatuma wapelelezi 12, akiwaambia: ‘Nendeni mkaone ni watu wangapi wanaokaa huko, na wana nguvu gani. Mjue kama udongo unafaa mimea. Mhakikishe kurudisha matunda fulani.’
Wapelelezi hao wanaporudi Kadeshi, wanamwambia Musa hivi: ‘Ni nchi nzuri kweli kweli.’ Na kama ushuhuda wa hayo, wanamwonyesha Musa matunda fulani. Lakini wapelelezi 10 wanasema hivi: ‘Watu wanaokaa huko ni wakubwa na wenye nguvu sana. Tutauawa tukijaribu kuichukua nchi hiyo.’
Waisraeli wanaogopa kwa kusikia hayo. ‘Afadhali tungefia Misri au hata humu jangwani,’ wanasema. ‘Tutauawa vitani, wake zetu na watoto watatekwa nyara. Na tuchague kiongozi mpya mahali pa Musa, turudi Misri!’
Lakini wapelelezi wawili wanamtumaini Yehova, wanajaribu kuwatuliza watu. Ni Yoshua na Kalebu. Wanasema: ‘Msiogope. Yehova yuko pamoja na sisi. Itakuwa rahisi kuichukua nchi hiyo.’ Lakini watu hawasikii. Hata wanataka kuwaua Yoshua na Kalebu.
Hilo lamkasirisha Yehova sana, anamwambia Musa hivi: ‘Hakuna ye yote kati ya watu hao kuanzia wale wenye miaka 20 na zaidi watakaoingia Kanaani. Wamekwisha kuiona miujiza niliyofanya huko Misri na jangwani, lakini bado hawanitumaini. Basi watatanga-tanga jangwani muda wa miaka 40 mpaka mtu wa mwisho afe. Yoshua (Yosua) na Kalebu peke yao wataingia Kanaani.’
Hesabu 13:1-33; 14:1-38.




 

Attachments

  • Wapelelezi 12.jpg
    Wapelelezi 12.jpg
    66.4 KB · Views: 73
Hadithi ya 39: Fimbo ya Haruni Inamea Maua

YATAZAME maua na lozi hizo zilizoiva zikimea katika fimbo hiyo. Hiyo ni fimbo ya Haruni. Maua na matunda hayo yalimea katika fimbo ya Haruni usiku mmoja tu! Ebu tuone sababu yake.
attachment.php


Waisraeli wamekuwa wakitanga-tanga jangwani kwa muda fulani sasa. Wengine kati ya watu hawataki Musa awe kiongozi, wala Haruni kuwa kuhani mkuu. Kora anafikiri hivyo, pia Dathani, Abiramu na viongozi wa watu 250. Wote hao wanakuja kumwambia Musa hivi: ‘Kwa nini wewe unajiweka juu ya wengine wetu?’
Musa anamwambia Kora na wafuasi wake hivi: ‘Kesho asubuhi mchukue makoleo ya moto mweke uvumba ndani yake. Ndipo mje kwenye hema ya Yehova. Tutaona ni nani ambaye Yehova atachagua.’
Kesho yake Kora na wafuasi wake 250 wanafika kwenye hema. Wengine wengi wanafuata ili wawaunge mkono wanaume hao. Yehova anakasirika sana. ‘Ondokeni kwenye hema za watu hao wabaya,’ Musa anasema. ‘Msishike mali yao.’ Watu wanasikiliza, na kuondoka kwenye hema za Kora, Dathani na Abiramu.
Kisha Musa anasema hivi: ‘Kwa hili mtajua ni nani ambaye Yehova amechagua. Ardhi itafunguka na kuwameza watu hawa wabaya.’
Mara Musa anapomaliza kusema, ardhi inafunguka. Hema ya Kora na mali yake na Dathani na Abiramu na wale walio pamoja nao wanazama, nayo ardhi inawafunika. Watu wanaposikia kilio cha hao wanaotumbukia katika ardhi, wanapiga kelele hivi: ‘Kimbieni! Ardhi isitumeze sisi pia!’
Kora na wafuasi wake 250 bado wako karibu na hema. Basi Yehova anapeleka moto, na wote wanateketezwa. Kisha Yehova anamwambia E·le·a′zari mwana wa Haruni achukue makoleo ya moto ya watu hao waliokufa ayafanye yawe kifuniko chembamba cha madhabahu.
Yehova anataka wafahamu sana kwamba Haruni na wanawe ndio amechagua wawe makuhani. Basi anamwambia Musa hivi: ‘Mwambie kiongozi wa kila kabila la Israeli alete fimbo yake. Kisha weka kila moja ya fimbo hizo katika hema mbele ya sanduku la agano. Ile fimbo ya mtu niliyemchagua awe kuhani itamea maua.’
Musa anapotazama kesho yake, lo! fimbo ya Haruni imemea maua hayo na lozi zilizoiva! Basi unaona sasa kwa nini Yehova alifanya fimbo ya Haruni imee maua?
Hesabu 16:1-49; 17:1-11; 26:10.

 

Attachments

  • Fimbo ya Haruni Inamea Maua.jpg
    Fimbo ya Haruni Inamea Maua.jpg
    31.9 KB · Views: 76
Hadithi ya 40: Musa Anaupiga Mwamba

MWAKA baada ya mwaka unapita—miaka 10, miaka 20, miaka 30, miaka 39! Waisraeli wangali jangwani. Lakini miaka hiyo yote Yehova anawaangalia watu wake. Anawalisha mana. Anawaongoza mchana kwa nguzo ya wingu, na usiku kwa nguzo ya moto. Na wakati wa miaka yote hiyo mavazi yao hayamaliziki na miguu haipati vidonda.
Sasa ndio mwezi wa kwanza wa mwaka wa 40 tangu waondoke Misri. Tena Waisraeli wanapiga kambi katika Kadeshi. Hapo ndipo walipokuwa wakati wapelelezi 12 walipotumwa kwenda kwenye nchi ya Kanaani karibu miaka 40 iliyopita. Miriamu dada yake Musa anakufa katika Kadeshi. Na kama zamani, matata yanatokea hapa.
Watu hawawezi kupata maji. Hivyo wanamlilia Musa hivi: ‘Afadhali tungekufa. Kwa nini ukatutoa Misri kuja mahali hapa pabaya pasipomea kitu? Hakuna nafaka, hakuna tini, hakuna zabibu, hakuna komamanga. Wala hakuna maji ya kunywa.’
attachment.php



Musa na Haruni wanapokwenda kwenye hema wakasali, Yehova anamwambia Musa hivi: ‘Wakusanye watu. Kisha mbele yao wote useme na mwamba ule. Maji mengi yatatoka watu na wanyama wao wote wanywe.’
Basi Musa anakusanya watu, na kusema: ‘Sikilizeni, ninyi msiomtumaini Mungu! Je! Haruni na mimi tuwatolee maji katika mwamba huu?’ Kisha Musa anaupiga mwamba huo mara mbili kwa fimbo, maji mengi yatiririka katika mwamba huo. Kuna maji mengi ya kunywa watu wote na wanyama.
Lakini Yehova anawakasirikia Musa na Haruni. Unajua kwa nini? Kwa sababu Musa na Haruni walisema kwamba wao watatoa maji katika mwamba. Lakini Yehova ndiye aliyetoa. Na kwa vile Musa na Haruni hawakusema kweli hiyo, Yehova anasema kwamba atawaadhibu. ‘Hamtawaingiza watu wangu Kanaani,’ anasema.
Upesi Waisraeli wanaondoka Kadeshi. Baada ya kitambo kidogo wanafika kwenye Mlima Hori. Huko ndiko Haruni alikufa juu ya kilele cha mlima. Anakufa akiwa mwenye miaka 123. Waisraeli wanahuzunika sana, na watu wote wanamlilia Haruni muda wa siku 30. E·le·a′zari mwanawe anakuwa kuhani mkuu wa pili wa taifa la Israeli.
Hesabu 20:1-13, 22-29; Kumbukumbu la Torati 29:5.


 

Attachments

  • Musa Anaupiga Mwamba.jpg
    Musa Anaupiga Mwamba.jpg
    35.7 KB · Views: 77
Hadithi ya 41: Nyoka wa Shaba

attachment.php

JE! HUYO anaonekana kama nyoka wa kweli aliyezungushwa juu ya mti? Hapana. Nyoka huyo amefanyizwa kwa shaba. Yehova alimwambia Musa amweke juu ya mti ili watu wamtazame waishi. Lakini nyoka wengine chini ni wa kweli. Wamewauma watu na kuwafanya wagonjwa. Unajua kwa nini?
Ni kwa sababu Waisraeli wamempinga Mungu na Musa. Wanalaumu hivi: ‘Kwa nini ulitutoa Misri ili tufe huku jangwani? Hakuna chakula wala maji huku. Tumechoka kula mana hii.’
Lakini mana hiyo ni chakula kizuri. Yehova amewapa mana hiyo kwa mwujiza. Na kwa mwujiza amewapa maji pia lakini watu hawamshukuru Mungu kwa vile alivyowaangalia. Basi Yehova anawapeleka nyoka hao wenye sumu ili awaadhibu Waisraeli. Nyoka hao wanawauma, na wengi wao wanakufa.
attachment.php



Mwishowe watu wanamwendea Musa na kusema: ‘Tumefanya dhambi, kwa sababu tumepinga Yehova na wewe. Basi mwombe Yehova awaondoe nyoka hawa.’
Musa anaombea watu. Naye Yehova anamwambia Musa afanyize nyoka huyu wa shaba. Anamwambia amweke juu ya mti, ili mtu anayeumwa amtazame. Musa anafanya kama anavyoambiwa na Mungu. Watu walioumwa wanamtazama nyoka wa shaba wanapona.
Kuna jambo la kujifunza kutokana na hayo. Sote tuko kama Waisraeli hao walioumbwa na nyoka hao. Sote tuko katika hali ya kufa. Ebu tazama uku na huku, utaona kwamba watu wanazeeka, wanakuwa wagonjwa, na kufa. Ni kwa sababu yule mwanamume na mwanamke wa kwanza, Adamu na Hawa walijitenga na Yehova, na sote ni watoto wao. Lakini Yehova amefanya njia ili tuweze kuishi milele.
Yehova alimtuma Mwanawe, Yesu Kristo, duniani. Yesu aliwekwa juu ya mti, kwa sababu watu wengi walidhani alikuwa mbaya. Lakini Yehova alimtoa Yesu atuokoe. Tukimtazama, tukimfuata, ndipo twaweza kuwa na uzima wa milele. Lakini tutajifunza zaidi juu ya hilo baadaye.
Hesabu 21:4-9; Yohana 3:14, 15.

 

Attachments

  • Nyoka wa Shaba 1.jpg
    Nyoka wa Shaba 1.jpg
    8.5 KB · Views: 70
  • Nyoka wa Shaba.jpg
    Nyoka wa Shaba.jpg
    8 KB · Views: 79
Hadithi ya 42: Punda Anasema

JE! UMEPATA kusikia kwamba punda anasema? ‘Hapana,’ labda unasema. ‘Wanyama hawawezi kusema.’ Lakini Biblia inasimulia hivyo. Na tuone ilivyokuwa.
attachment.php


Waisraeli wako karibu sana kuingia nchi ya Kanaani. Balaki, mfalme wa Moabu, anawaogopa Waisraeli. Basi anapeleka habari ili mtu mwerevu jina lake Balaamu awalaani Waisraeli. Balaki anaahidi kumpa Balaamu fedha nyingi sana, basi Balaamu anapanda punda wake kwenda kumwona Balaki.
Yehova hataki Balaamu alaani watu wake. Basi anamtuma malaika mwenye upanga mrefu akasimame njiani amzuie Balaamu. Balaamu hawezi kumwona malaika, lakini punda anamwona. Basi punda huyo anaepa-epa huyo malaika, na mwishowe analala njiani. Balaamu anakasirika sana, na kumpiga punda wake kwa fimbo.
Ndipo Yehova anamfanya Balaamu asikie punda wake akisema naye. ‘Nimekukosea nini hata unipige?’ punda anauliza.
attachment.php


‘Umenifanya mpumbavu,’ Balaamu anasema. ‘Kama ningekuwa na upanga ningekuua!’
‘Je! nimekufanyia hivyo zamani?’ punda anauliza.
‘Hapana,’ Balaamu anajibu.
Ndipo Yehova anamwonyesha Balaamu malaika aliye na upanga anasimama njiani. Malaika anasema hivi: ‘Kwa nini umempiga punda wako? Nimekuja nikuzuie njia usiende kulaani Waisraeli. Kama punda wako hangeniepa, ningekupiga ufe.’
Balaamu anasema: ‘Nimefanya dhambi. Sikujua kama ulikuwa ukisimama njiani.’ Malaika huyo anamruhusu Balaamu aende, naye Balaamu anaendelea na safari ya kumwona Balaki. Bado anajaribu kulaani Waisraeli, lakini, badala yake, Yehova anamwongoza abariki Waisraeli mara tatu.
Hesabu 21:21-35; 22:1-40; 23:1-30; 24:1-25.


 

Attachments

  • Punda Anasema.jpg
    Punda Anasema.jpg
    9.6 KB · Views: 73
  • Punda Anasema 1.jpg
    Punda Anasema 1.jpg
    17.2 KB · Views: 68
Adam na Eva/Hawa waliwazaa Habili na Kaini, Hivi hawa watoto waliwaoa (na kuzaa na) wakina nani? na wakati huo mwanamke alikuwa mama yao tu?
 
ase hiyo biblia ya watoto i had it with them same pictures hata sijui ipo wapi now daah shame on ma face. Safi sana lkn sasa kwann umeweka hii kitu huku MMU
 
MziziMkavu....??!!

Hivi huku ndiko unakochukuaga zile dawa zako kama za dokta ndodi?
 
Hii story ni MAPENZI?MAHUSIANO? AU URAFIKI? ipeleke kwenye jukwaa husika.
 
ase hiyo biblia ya watoto i had it with them same pictures hata sijui ipo wapi now daah shame on ma face. Safi sana lkn sasa kwann umeweka hii kitu huku MMU

Hii ndio namna bora kabisa ya kufundisha watoto. Wakatoliki hufanya hivi na ndio sababu watoto hulilia kwenda Sunday School kila jumapili. Tatizo ni mleta mada kuingiwa na shetani kiasi anathubutu kuongezea maneno yake kwenye Biblia pasina kuwa na tahadhari kuwa Neno la Mungu halihitaji nyongeza ya mwanadamu

Watoto wanaelewa zaidi kwa picha kuliko fimbo
 
Hadithi ya 43: Yoshua Anakuwa Kiongozi

MUSA anataka kuingia Kanaani pamoja na Waisraeli. Hivyo anauliza hivi: ‘Yehova, uniruhusu nivuke Mto Yordani, niione nchi nzuri.’ Lakini Yehova anasema: ‘Basi! usiseme tena hivyo?’ Unajua kwa nini Yehova alisema hivyo?
Ni kwa sababu ya jambo lililotokea wakati Musa alipoupiga mwamba. Kumbuka, yeye na Haruni hawakumheshimu Yehova. Hawakuwaambia watu kwamba ni Yehova aliyekuwa akiwaletea maji katika mwamba ule. Kwa sababu hiyo Yehova alisema hangewaruhusu waingie Kanaani.
Basi miezi michache baada ya Haruni kufa Yehova anamwambia Musa hivi: ‘Mchukue Yoshua umsimamishe mbele ya E·le·a′zari kuhani na watu. Na mbele ya wote mwambie kila mtu kwamba Yoshua ndiye kiongozi ndiye kiongozi mpya.’ Musa anafanya kama Yehova anavyosema, kama unavyoona katika picha.
attachment.php



Kisha Yehova anamwambia Yoshua hivi: ‘Uwe hodari, usiogope. Utawaingiza Waisraeli katika nchi ya Kanaani niliyowaahidi, mimi nitakuwa na wewe.’
Baadaye Yehova anamwambia Musa apande juu ya Mlima Nebo katika nchi ya Moabu. Musa anatazama ng’ambo ya Mto Yordani na kuiona nchi nzuri ya Kanaani. Yehova anasema hivi: ‘Hii ndiyo nchi niliyoahidi kuwapa wana wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo. Nimekuruhusu uione, lakini sitakubali uingie ndani yake.’
Huko juu ya Mlima Nebo Musa anakufa. Alikuwa mwenye miaka 120. Alikuwa bado ana nguvu, macho yake yalikuwa bado yakiona vizuri. Watu wanahuzunika sana na kulia kwa sababu Musa amekufa. Lakini wanafurahi kuwa na Yoshua kiongozi wao mpya.
Hesabu 27:12-23; Kumbukumbu la Torati 3:23-29; 31:1-8, 14-23;32:45-52; 34:1-12.

 

Attachments

  • Yoshua Anakuwa Kiongozi.jpg
    Yoshua Anakuwa Kiongozi.jpg
    15.1 KB · Views: 73
Hadithi ya 44: Rahabu Anaficha Wapelelezi

WANAUME hao wana taabu. Lazima waondoke, ama watauawa. Ni wapelelezi Waisraeli, na anayewasaidia ni Rahabu. Rahabu anakaa katika nyumba hiyo juu ya ukuta wa mji wa Yeriko. Ebu tuone sababu gani wanaume hao wana taabu.
Waisraeli wako tayari kuvuka Mto Yordani waingie Kanaani. Lakini kwanza, Yoshua anatuma wapelelezi wawili. Anawaambia hivi: ‘Nendeni mkaitazame nchi na mji wa Yeriko.’
attachment.php



Wapelelezi hao wanapoingia Yeriko, wanakwenda nyumbani kwa Rahabu. Lakini mtu fulani anamwambia mfalme hivi: ‘Waisraeli wawili waliingia mjini usiku huu ili wapeleleze nchi.’ Anaposikia hivyo, mfalme anatuma watu kwa Rahabu, wakimwambia hivi: ‘Watoe wale wanaume walioingia nyumbani mwako!’ Lakini Rahabu ameficha wapelelezi hao juu ya dari lake. Anasema: ‘Wanaume fulani walikuja kwangu, lakini sijui walikotoka. Waliondoka kulipoanza kuwa usiku, kabla ya kufungwa lango. Mkifanya haraka, mtawakuta!’ Watu hao wanaanza kuwafuata.
Wakiisha kuondoka, Rahabu anapanda haraka juu ya dari. ‘Najua Yehova atawapa ninyi nchi hii,’ anawaambia wapelelezi hao. ‘Tulisikia alivyoikausha Bahari Nyekundu mlipoondoka Misri, na alivyowaua wafalme Sihoni na Ogu. Nimewahurumia ninyi, basi tafadhali mnipe ahadi, ya kwamba mtanihurumia mimi. Mwokoe baba na mama yangu, ndugu na dada zangu.’
Wapelelezi hao wanaahidi kufanya hivyo, lakini inampasa Rahabu atende jambo fulani. ‘Chukua kamba hii nyekundu uifunge katika dirisha,’ wapelelezi wanamwambia, ‘kisha ukusanye watu wako wote wa ukoo ndani ya nyumba yako pamoja nawe. Tutakaporudi sote kuutwaa Yeriko, tutaiona kamba hii katika dirisha lako tusimwue ye yote nyumbani mwako.’ Wapelelezi hao wanaporudi kwa Yoshua, wanamwambia kila jambo lililotokea.
Yoshua 2:1-24; Waebrania 11:31.


 

Attachments

  • Rahabu Anaficha Wapelelezi.jpg
    Rahabu Anaficha Wapelelezi.jpg
    30.8 KB · Views: 69
Hadithi ya 45: Kuvuka Mto Yordani

TAZAMA! Waisraeli wanavuka Mto Yordani! Lakini maji yako wapi? Kwa kuwa mvua nyingi zinaanguka wakati huo wa mwaka, mto huo ulijaa maji sana dakika chache zilizotangulia. Lakini sasa maji yamekauka! Waisraeli wanavuka katika nchi kavu kama walivyovuka Bahari Nyekundu! Maji yote hayo yalikwenda wapi? Ebu tuone.
attachment.php


Ulipofika wakati Waisraeli wavuke Mto Yordani, Yehova alikuwa amemwagiza Yoshua awaambie watu hivi: ‘Makuhani wabebe sanduku la agano watutangulie. Watakapoweka miguu yao katika maji ya Mto Yordani, maji yatasimama.’
Basi makuhani hao wanachukua sanduku la agano, wakilibeba mbele ya watu. Wanapofika Yordani, makuhani wanaingia moja kwa moja ndani ya maji. Maji yanatembea kwa nguvu sana na Mto una kilindi kirefu sana. Lakini mara miguu yao inapokanyaga maji, maji hayo yanaanza kusimama! Ni mwujiza huo! Upande wa juu wa mto, Yehova amekusanya maji kama ziwa. Kwa muda mfupi mto hautakuwa na maji tena!
Wale makuhani wanaobeba sanduku la agano wanaingia moja kwa moja katikati ya mto mkavu. Unaweza kuwaona katika picha? Wanaposimama humo, Waisraeli wote wanavuka moja kwa moja Mto Yordani katika nchi kavu!
Kila mtu akiisha kuvuka, Yehova anamwagiza Yoshua awaambie wanaume hodari 12 hivi: ‘Ingieni mtoni mahali wanaposimama makuhani walio na sanduku la agano. Chagueni mawe 12, myapange pamoja mahali mtakapolala nyote usiku huu. Kisha, wakati ujao, watoto wenu watakapouliza maana ya mawe hayo, mwambie kwamba maji yalisimama wakati sanduku la agano la Yehova lilipovuka Yordani. Mawe hayo yatawakumbusha mwujiza huo!’ Pia Yoshua anasimamisha mawe 12 mahali walipokuwa wamesimama makuhani katika bonde la mto.
attachment.php

Mwishowe Yoshua anawaambia makuhani wanaolichukua sanduku la agano hivi: ‘Pandeni mtoke Yordani.’ Na mara wanapopanda, mto unaanza kutiririka maji tena.
Yoshua 3:1-17; 4:1-18.

 

Attachments

  • Kuvuka Mto Yordani.jpg
    Kuvuka Mto Yordani.jpg
    41.5 KB · Views: 178
  • Yoshua.jpg
    Yoshua.jpg
    3.3 KB · Views: 172
Hadithi ya 46: Kuta za Yeriko

NI NINI kinachoangusha kuta hizo za Yeriko? Ni kama zimepigwa na kombora kubwa. Lakini siku hizo hawakuwa na makombora; wala hawakuwa na bunduki. Ni mwujiza mwingine wa Yehova! Na tujifunze inavyotukia.
attachment.php



Sikiliza Yehova anavyomwambia Yoshua: ‘Wewe pamoja na watu wako wa vita zungukeni mji. Mzunguke mara moja kila siku muda wa siku sita. Mchukue na sanduku la agano. Makuhani saba watangulie na kupiga tarumbeta zao.

‘Siku ya saba mzunguke mji mara saba. Kisha mpige sauti ndefu ya tarumbeta zenu, na kila mtu apige yowe kuu ya vita. Kuta zitaanguka chini kabisa!’
Yoshua na watu wanafanya kama Yehova anavyosema. Wanapozunguka, kila mtu yuko kimya. Hakuna anayesema. Sauti ya tarumbeta na mshindo wa miguu tu ndio unasikika. Bila shaka adui za watu wa Mungu waliogopa huko Yeriko. Unaiona ile kamba nyekundu inayoning’inia katika dirisha? Ni dirisha la nani lile? Ndiyo, Rahabu amefanya alivyoambiwa na wale wapelelezi wawili. Jamaa yake yote imo nyumbani ikitazama pamoja naye.
attachment.php



Mwishowe, siku ya saba, wakiisha kuuzunguka mji mara saba, tarumbeta yalia, watu wa vita wanapiga kelele, na kuta zaanguka. Ndipo Yoshua anasema: ‘Ueni kila mtu mjini. Okoeni tu fedha, dhahabu, shaba na chuma, mvipeleke kwenye hazina ya hema ya Yehova.’

Yoshua anawaambia wale wapelelezi wawili hivi: ‘Ingieni nyumbani kwa Rahabu, mmtoe yeye na jamaa yake yote.’ Rahabu na jamaa yake wanaokolewa, kama wale wapelelezi walivyokuwa wamemwahidi.
Yoshua 6:1-25.


 

Attachments

  • Kuta za Yeriko.jpg
    Kuta za Yeriko.jpg
    45.9 KB · Views: 175
  • Kuta za Yeriko 2.jpg
    Kuta za Yeriko 2.jpg
    12.1 KB · Views: 169
Back
Top Bottom