Scholes Amtaka Ronaldo kuwa Goalkeeper😃

Scholes Amtaka Ronaldo kuwa Goalkeeper😃

Mjomba Malume

JF-Expert Member
Joined
Apr 8, 2025
Posts
903
Reaction score
1,317
Paul Scholes ameibua mjadala mkubwa baada ya kumchana Cristiano Ronaldo kufuatia mwanzo mbovu wa Portugal kwenye World Cup.

Akiongea kwenye podcast ya The Good, The Bad & The Football, gwiji huyo wa Manchester United alisema:

“ Nadhani ni ngumu kwa kocha… nilimuuliza Roberto Martinez off-camera kama Ronaldo ni tatizo kwake, kwa sababu nahisi ni tatizo kidogo. Ukiwa na miaka 41 kuna nafasi moja tu unaweza kuanza uwanjani… goalkeeper ”

Kauli hiyo imezua mjadala mkubwa baada ya Ronaldo kushindwa hata kupiga shot on target dhidi ya DR Congo.

Scholes akaongeza kuwa kinachoweza kumuuma zaidi CR7 ni kuona rivals wake wakianza World Cup kwa moto mkubwa huku yeye akihangaika🤣🤣🤣

Wakati Ronaldo:

  • Alimaliza first half bila shot yoyote
  • Bila duel yoyote ya maana
  • Na Portugal wakionekana hoi😅😅

Kwa upande mwingine:

  • Lionel Messi alianza kwa hat-trick 🔥
  • Kylian Mbappé akaanza kwa brace 🔥

CR7, Mr. Champions League, The Portuguese Machine, Captain wa Portugal na Mnyama wa Madeira ameendelea kuwa mjadala kutokana na performance yake ya hivi karibuni.

Kinachowafariji mashabiki wake ni kuwa jamaa bado anaongoza kwa kuwa na followers wengi Instagram akiongoza kwa 667m followers na pia ndiye mchezaji tajiri kuliko wote.
 
Nadhani kichwa cha mada umepotosha boss, Hajamtaka kuwa goal keeper. Amesema kwa umri wa miaka 41 uhakika wa kuanza kwenye kikosi cha kwanza ni goal keeper ndio mwenye hiyo nafasi akimaanisha Cr7 anapaswa kuanzia bench sababu yeye ni mshambuliaji.
 
Nadhani kichwa cha mada umepotosha boss, Hajamtaka kuwa goal keeper. Amesema kwa umri wa miaka 41 uhakika wa kuanza kwenye kikosi cha kwanza ni goal keeper ndio mwenye hiyo nafasi akimaanisha Cr7 anapaswa kuanzia bench sababu yeye ni mshambuliaji.
Yeah sasa kama Ronaldo anataka kuanza first eleven akubali kuwa goalkeeper🤣🤣
 
Haya ndo madhara ya kumtukuza mchezaji fulani kuliko wengine, kwamba ukimkosoa mchezaji fulani bc dunia nzima watakuona umekosea.

Teammate wa Ronaldo aliongea Ukweli 100% kwamba Ronaldo n mchezaji kama wachezaji wengine, ila kwakuwa binadamu ni wapuuzi bc anaonekana yeye n mbaya
 
Haya ndo madhara ya kumtukuza mchezaji fulani kuliko wengine, kwamba ukimkosoa mchezaji fulani bc dunia nzima watakuona umekosea.

Teammate wa Ronaldo aliongea Ukweli 100% kwamba Ronaldo n mchezaji kama wachezaji wengine, ila kwakuwa binadamu ni wapuuzi bc anaonekana yeye n mbaya
We unadhan kuna fala ataongea ujinga huo pale argentina akabaki salama, mulize dogo gernacho
 
Haya ndo madhara ya kumtukuza mchezaji fulani kuliko wengine, kwamba ukimkosoa mchezaji fulani bc dunia nzima watakuona umekosea.

Teammate wa Ronaldo aliongea Ukweli 100% kwamba Ronaldo n mchezaji kama wachezaji wengine, ila kwakuwa binadamu ni wapuuzi bc anaonekana yeye n mbaya
Mkuu mimi ni team Messi ila napata ukakasi kidogo kusema Ronaldo ni mchezaji wa kawaida labda niseme tu hajafika level ya Messi na ameisha kwa sasa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom