Bilionea Asigwa
JF-Expert Member
- Sep 21, 2011
- 16,578
- 28,701
Mkuu nenda ukaombewe aisee...huyo ni jini............
Wiyelele, Acha 'kugegeda' mke wa mtu (yule anayekimbilia kwako mara kwa mara baada ya kupigwa na mumewe) !!
Hiyo 'sauti' unayoisikia ndio 'malipo' ya kazi yako ya kushika-shika mke wa mtu.
Who knows, labda mwenye mke kaamua 'kukutengeneza' a.k.a 'kukufanyia ukarabati' !!
Na hiyo 'sauti' ni chambo cha kukunasa, na jinsi unavyosema mwenyewe, hauko mbali sana na 'ndoano' !!
Sasa ndio utajua mke wa mtu ni sumu hata kama anajileta mwenyewe kwako !!
Kule kwetu kuna msemo unasema kuwa "..sasa ndio utajua kuwa kachumbari sio mboga, na majani ya mbuyu sio kisamvu.."
Mbona mimi nilishamuacha kitambo? Wala simuwazii tena kabisa. Huamini kwamba mtu anaweza kutubu na kuwa muumini na mfuasi wa kweli? Nimekuwa kiumbe kipya katika Kristu.
Hapo kwenye blue,
Kama ni kweli, basi na iwe hivyo na kufahamika hivyo kwake (mke wa mtu), na kwa mumewe.
Maana, hata kama umemuacha, lakini hujamtamkia yeye mwenyewe (mke wa mtu), basi atazidi kuja kwako.
Pia kama mumewe alikuwa anajua uhusiano wenu, basi na yeye anatakiwa ajue kuwa sasa hamna uhusiano huo.
Vinginevyo, kama mumewe bado anaamini kuwa unaendelea na uhusiano na mkewe, atakutengeneza tu, hata kama umemuacha mkewe !!
Ndio maana Biblia imetuagiza wanaume tuwapende wake zetu (bila kujali wakoje).
Amri ni kuwapenda wake zetu.
Kama mke ana mambo yasiofaa, kaa naye umuonye, pia muombee.
Usipompende mkeo, shetani atakutafutia 'mke' mwingine,
Na usipoangalia utampenda huyo 'mke' toka kwa shetani (iwe ni jini mahaba au mwanamke wa nje).
Mpende mkeo bila masharti yoyote, na hakika hiyo 'sauti' hutaisikia tena.
Soma hapa chini...
Waefeso 05:25-33 inasema...
25 Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake;
26 ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno;
27 apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa.
28 Vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe.
29 Maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake po pote; bali huulisha na kuutunza, kama Kristo naye anavyolitendea Kanisa.
30 Kwa kuwa tu viungo vya mwili wake.
31 Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja.
32 Siri hiyo ni kubwa; ila mimi nanena habari ya Kristo na Kanisa.
33 Lakini kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mumewe.
'
MwaJ, bahati mbaya huwezi kuyaona machozi yangu yakichuluzika hapa JF, na huwezi kuiona sura yangu ikiwa na huzuni hapa JF. Unachoweza kukiona na maandishi yanayoelezea uhalisia wa mambo yanayonipata.
Mkuu, nakushukuru sana kwa ushauri wako ila hili la kwamba nimjuulishe mmewe mbona unanza kunitega? Mi niliyasahau na kama nilitubu Mungu alinisamehe, iweje nianze kuyarudia ya nyuma? Take it from me that i am a new creature.
Mimi nilijua tu, kumtoa kasoro na kumchukia mkeo kiasi kile ni dalili ya kuwa na spiritual husaband; sasa fuatilia business au kazi zako; uwezekano mkubwa zinayumba, hopefully hautasema mkeo ana gundu.
sio anamnyemelea hilo ni jini mahaba kamili
anachotakiwa ni kuchukua hatua na kukutana na watumishi wa Mungu ili aweze kufunguliwa
maana huwa yanakuwa kizuizi hasa pale unapofika wakati wa wewe kutaka kuanzisha mahusiano na mwanamke mwingine
zingatia mapema kweupe kabla haijwa ndivyo sivyo
Hahahaahaha! kama kawaida yako, huwa unanifurahisha sana Wiyelele, hiyo ni hisia tu, kwa sababu unaweza kuta mchana kutwa kulikuwa unawaza kupata mwanamke mzuri na mwenye sauti nyororo. ukifika wakati wam kulala akili inaanza kurudia kile ulichokiwaza wakati wa mchana.Kama ni jini mbona siku nikiitwa nakuwa na furaha sana?
Hahahaahaha! kama kawaida yako, huwa unanifurahisha sana Wiyelele, hiyo ni hisia tu, kwa sababu unaweza kuta mchana kutwa kulikuwa unawaza kupata mwanamke mzuri na mwenye sauti nyororo. ukifika wakati wam kulala akili inaanza kurudia kile ulichokiwaza wakati wa mchana.