Sauti ya "kike" inanisumbua usingizini

Sauti ya "kike" inanisumbua usingizini

Jamani, nimeone niliseme hapa ili muweze kunisaidia kutokana na tatizo ambalo lilianza mwaka jana mwezi wa 11. Nimevumilia lakini niliseme tu hapa.

Nikiwa nimelala usiku, ikifika muda wa saa kumi hivi, inanijia sauti "nyororo na yenye kuvutia sana" inaita "Wiyelele, Wiyelele". Sauti hiyo inaning'ongoneza kwenye sikio langu la kulia nikiwa nimelala. Sauti hii ni nzuri sana na imekuwa ikijirudia mara tatu kwa wiki tena muda na wakati huo huo.

Nionavyo mimi, ni sauti ya mwanamke au msichana mzuri sana ambaye ambae simjui. Picha yake ilinijia usingizini siku moja kwenye ndoto na ni mzuri sana. Ni sauti inayoniita kwa kunibembeleza... natamani niedelee kuisikiliza jamani. Nahisi sauti hii imeona shida ninazozipata.

Kila niskikiapo sauti hii basi siku hiyo nakuwa na raha na amani sana. Sijajua bado maana yake ni nini. Hata hivyo, sio sauti ya mke wangu lahasha! Kwanini istokee siku hizi? Bado nafikiri na sipati majibu. Najitahidi kusali sana ili isije, lakini, kama ni sauti mbaya, mbona ikitokea nakua na furaha sana siku hiyo?

ukisikia sauti hiyo vp huwa unasisimuka?
 
wiyelele,mbwa hujipeleka mwenyeewe mdomoni mwa chatu,nasikia eti chatu hutengeza harufu nzuri ya nyama ambayo mbwa akiisikia huwa anaifuata mpaka anajikuta yu kinywani mwa chatu,hivyo hivyo kwako,hiyo sauti ya kike ni zuga,huyo ni popobawa anataka kukukigamboni!!!!!
 
Weyelele, maisha ni kitendawili na pia ni safari ndefu yenye mambo mengi tunayoyajua na tusoyajua.

*Kitendo cha wewe kuja kutafuta ushauri/suluhu ya tatizo lako hapa JF, inaonyesha ni jinsi gani umeona kuwa sio tukio la kawaida kunong'onezwa na mwanamke (sielewi ni ukiwa usingizini au ukiwa macho na pia sielewi ni maono au ni ndoto.

*Jambo la kutisha ni wewe kuwa curious kutaka ama kujua zaidi ni sauti ya nani na pengine kujenga uhusiano nae/kumfuata (maana unadai ni mzuri).
*Nadhani una mke (unaonekana usingejali kama ukipata mwingine mzuri zaidi.

TATIZO lako umelileta hapa na kila mchangiaji analeta anavyojua yeye ama kwa kudhani au kwa experiences zao. lakini nadhani itakuwa ni vigumu zaidi mwisho wa haya kujua ushauri mzuri ni upi. mimi ningesema hivi:

1. Tatizo lako inawezekana ni psychological au ni Spiritual. Spiritual issues lazima zitafutiwe solution yake iwe spiritually. na pia psychological issues zipelekewe wenye utaalam huo.

2. Matatizo ambayo ni spiritually based yanaombewa. Na labda niseme kuwa mimi ni mtu wa kanisa, na nimeona watu wengi wakiombewa na kupona kabisa (Tatizo ni kujua mwoombeaji ambae amesimama na akakusaidia tatizo hilo. Maana uzoefu unaonyesha kuwa mambo kama haya huwa hayaji na moja (Utaanza kusikia sauti, mara unakuja ona ndoa imevunjika, mara watoto wanaumwa tuuu, mara hupati pesa nk.

3. Suala lingine nikuwa unaweza wewe mwenyewe kujiombea na kusimama na Mungu. Hii inahitaji mtu msoma neno na anaetenda kuzingatia neno la Mungu (Righteous person). Hilo unalikemea dakika chache tu, na hutasikia tena.

4. baya zaidi inaonekana katika maelezo yako kuwa umefikia kujenga uhusiano na hilo(shetani - it doesnt matter its name).

5. The minute you try to have a conversation with demonic agents you will be setting yourself to fail. Break that relationship as soon as you can and start your deliverance battle.
tetere my dear! this is Wiyelele we are talking with!
Kwa tunaomfahamu tunajua tatizo hapa ni nini!
NA YEYE MWENYEWE ANALIJUA!hajaamua tu kutii kiu ya kile anachokiamini!
 
Last edited by a moderator:
kijana kimbia fasta, satan or call it jini mahaba whatever name you give bado ndugu yangu uko pabaya maana umekamatwa na 'shetwani'

sali mkuu, unahitaji maombezi ili ufunguliwe.....
 
chukua hatua ya kubreak hiyo relationship na jini mahaba before it is worse, if you don't, you will soon be subscribed to their family
 
Mkuu Wiyelele mbona unajichanganya? Kwenye kichwa cha habari umeandika kuwa sauti inakusumbua lakini kwenye kiini umeonesha unasikia raha na unapata amani ukiisikia! Sasa sijui unasimamia wapi!

Kama kiini kinge fanana na heading yako mimi ninge kuuliza kama una sali au kuswali kabla ya kulala!
 
Last edited by a moderator:
Mimi nilijua tu, kumtoa kasoro na kumchukia mkeo kiasi kile ni dalili ya kuwa na spiritual husaband; sasa fuatilia business au kazi zako; uwezekano mkubwa zinayumba, hopefully hautasema mkeo ana gundu.
 
tetere my dear! this is Wiyelele we are talking with!
Kwa tunaomfahamu tunajua tatizo hapa ni nini!
NA YEYE MWENYEWE ANALIJUA!hajaamua tu kutii kiu ya kile anachokiamini!

Nimefurahia sana ushauri wa tetere, lakini yawezekana snowhite una yale ya mwaka jana. Ina maana kama mtu unamfaham kwamba ni mlevi akija kukuomba ushauli jinsi ya kuacha huo ulevi huwezi kumshauri?
 
Mkuu Wiyelele mbona unajichanganya? Kwenye kichwa cha habari umeandika kuwa sauti inakusumbua lakini kwenye kiini umeonesha unasikia raha na unapata amani ukiisikia! Sasa sijui unasimamia wapi!

Kama kiini kinge fanana na heading yako mimi ninge kuuliza kama una sali au kuswali kabla ya kulala!

Ni kweli, kama kitu kinajirudia rudia na hukielewi kinaanza kukusumbua japo kinaweza kuwa kinavutia.
 
Mimi nilijua tu, kumtoa kasoro na kumchukia mkeo kiasi kile ni dalili ya kuwa na spiritual husaband; sasa fuatilia business au kazi zako; uwezekano mkubwa zinayumba, hopefully hautasema mkeo ana gundu.

Hapana mambo ya business na kazi yako shwari tu. Simchukii mtu, bali nachukia tabia mbaya.
 
nikwambie!
hakuna cha jini mahaba wala nini! umemchukia sana mkeo kiasi cha kuamini kuna mwanamke mwingine mzuri anayekufaa umemtengeneza kichwani kwako na hiyo ni akili yako tu inarudisha kile unachowaza mchana kutwa!

Mimi nahitaji msaada ili hata kama unayoyasema ni ya kweli niweze kuaachana nayo ni focus kwa mke wangu tu. Jamani msinihukum kwa yale ya mwaka jana, mbona hata vitabu vinasema "tazama, yakele yamepita na sasa nimekuwa kiumbe kipya".
 
Weyelele, maisha ni kitendawili na pia ni safari ndefu yenye mambo mengi tunayoyajua na tusoyajua.

*Kitendo cha wewe kuja kutafuta ushauri/suluhu ya tatizo lako hapa JF, inaonyesha ni jinsi gani umeona kuwa sio tukio la kawaida kunong'onezwa na mwanamke (sielewi ni ukiwa usingizini au ukiwa macho na pia sielewi ni maono au ni ndoto.

*Jambo la kutisha ni wewe kuwa curious kutaka ama kujua zaidi ni sauti ya nani na pengine kujenga uhusiano nae/kumfuata (maana unadai ni mzuri).
*Nadhani una mke (unaonekana usingejali kama ukipata mwingine mzuri zaidi.

TATIZO lako umelileta hapa na kila mchangiaji analeta anavyojua yeye ama kwa kudhani au kwa experiences zao. lakini nadhani itakuwa ni vigumu zaidi mwisho wa haya kujua ushauri mzuri ni upi. mimi ningesema hivi:

1. Tatizo lako inawezekana ni psychological au ni Spiritual. Spiritual issues lazima zitafutiwe solution yake iwe spiritually. na pia psychological issues zipelekewe wenye utaalam huo.

2. Matatizo ambayo ni spiritually based yanaombewa. Na labda niseme kuwa mimi ni mtu wa kanisa, na nimeona watu wengi wakiombewa na kupona kabisa (Tatizo ni kujua mwoombeaji ambae amesimama na akakusaidia tatizo hilo. Maana uzoefu unaonyesha kuwa mambo kama haya huwa hayaji na moja (Utaanza kusikia sauti, mara unakuja ona ndoa imevunjika, mara watoto wanaumwa tuuu, mara hupati pesa nk.

3. Suala lingine nikuwa unaweza wewe mwenyewe kujiombea na kusimama na Mungu. Hii inahitaji mtu msoma neno na anaetenda kuzingatia neno la Mungu (Righteous person). Hilo unalikemea dakika chache tu, na hutasikia tena.

4. baya zaidi inaonekana katika maelezo yako kuwa umefikia kujenga uhusiano na hilo(shetani - it doesnt matter its name).

5. The minute you try to have a conversation with demonic agents you will be setting yourself to fail. Break that relationship as soon as you can and start your deliverance battle.

Tetere, nakushukuru sana kwa ushauri wako na kweli nimefarijika mno. Naamini maombi ni njia pekee ya kuikimbia hiyo sauti. Asante sana
 
wiyelele,mbwa hujipeleka mwenyeewe mdomoni mwa chatu,nasikia eti chatu hutengeza harufu nzuri ya nyama ambayo mbwa akiisikia huwa anaifuata mpaka anajikuta yu kinywani mwa chatu,hivyo hivyo kwako,hiyo sauti ya kike ni zuga,huyo ni popobawa anataka kukukigamboni!!!!!

Lahasha sitajipeleka huko mkubwa!
 
tetere my dear! this is Wiyelele we are talking with!
Kwa tunaomfahamu tunajua tatizo hapa ni nini!
NA YEYE MWENYEWE ANALIJUA!hajaamua tu kutii kiu ya kile anachokiamini!
snowhite mara nyingi Wiyelele akisema ana tatizo huwa siamini kama ni kweli ana tatizo maana issue ambayo wengine wanatetemeka kwa hofu yeye ndio kwanza anafanya mzaha ili hali inamkabili yeye. Anyway, ngoja wataalamu wa majini wamshauri maana naona wapo wengi.
 
Last edited by a moderator:
snowhite mara nyingi Wiyelele akisema ana tatizo huwa siamini kama ni kweli ana tatizo maana issue ambayo wengine wanatetemeka kwa hofu yeye ndio kwanza anafanya mzaha ili hali inamkabili yeye. Anyway, ngoja wataalamu wa majini wamshauri maana naona wapo wengi.
'

MwaJ, bahati mbaya huwezi kuyaona machozi yangu yakichuluzika hapa JF, na huwezi kuiona sura yangu ikiwa na huzuni hapa JF. Unachoweza kukiona na maandishi yanayoelezea uhalisia wa mambo yanayonipata.
 
Back
Top Bottom