Wiyelelee
JF-Expert Member
- Nov 9, 2012
- 1,071
- 348
Jamani, nimeone niliseme hapa ili muweze kunisaidia kutokana na tatizo ambalo lilianza mwaka jana mwezi wa 11. Nimevumilia lakini niliseme tu hapa.
Nikiwa nimelala usiku, ikifika muda wa saa kumi hivi, inanijia sauti "nyororo na yenye kuvutia sana" inaita "Wiyelele, Wiyelele". Sauti hiyo inaning'ongoneza kwenye sikio langu la kulia nikiwa nimelala. Sauti hii ni nzuri sana na imekuwa ikijirudia mara tatu kwa wiki tena muda na wakati huo huo.
Nionavyo mimi, ni sauti ya mwanamke au msichana mzuri sana ambaye ambae simjui. Picha yake ilinijia usingizini siku moja kwenye ndoto na ni mzuri sana. Ni sauti inayoniita kwa kunibembeleza... natamani niedelee kuisikiliza jamani. Nahisi sauti hii imeona shida ninazozipata.
Kila niskikiapo sauti hii basi siku hiyo nakuwa na raha na amani sana. Sijajua bado maana yake ni nini. Hata hivyo, sio sauti ya mke wangu lahasha! Kwanini istokee siku hizi? Bado nafikiri na sipati majibu. Najitahidi kusali sana ili isije, lakini, kama ni sauti mbaya, mbona ikitokea nakua na furaha sana siku hiyo?
Nikiwa nimelala usiku, ikifika muda wa saa kumi hivi, inanijia sauti "nyororo na yenye kuvutia sana" inaita "Wiyelele, Wiyelele". Sauti hiyo inaning'ongoneza kwenye sikio langu la kulia nikiwa nimelala. Sauti hii ni nzuri sana na imekuwa ikijirudia mara tatu kwa wiki tena muda na wakati huo huo.
Nionavyo mimi, ni sauti ya mwanamke au msichana mzuri sana ambaye ambae simjui. Picha yake ilinijia usingizini siku moja kwenye ndoto na ni mzuri sana. Ni sauti inayoniita kwa kunibembeleza... natamani niedelee kuisikiliza jamani. Nahisi sauti hii imeona shida ninazozipata.
Kila niskikiapo sauti hii basi siku hiyo nakuwa na raha na amani sana. Sijajua bado maana yake ni nini. Hata hivyo, sio sauti ya mke wangu lahasha! Kwanini istokee siku hizi? Bado nafikiri na sipati majibu. Najitahidi kusali sana ili isije, lakini, kama ni sauti mbaya, mbona ikitokea nakua na furaha sana siku hiyo?