Ni sawa na ngoma ivumayo sana...! Tangu lini ngozi ya kitimoto ikawamba ngoma?
Shy land wee ni mshkaji wangu sana tu hapa JF lakini kwa hili nina maoni tofauti
Kwanza ni dhambi kabisa tena ni kejeli kubwa kwa Zito kujilinganisha na Nyerere R.I.P, Mwalimu hakujijenga binafsi na alipigania ukombozi wa kweli wa taifa hili, mwalimu hakuwa na tamaa ya Mali na alikuwa na maono
Zito ni mbinafsi, hii ni hulka yake hashauriki na haambiliki, yeye anajiona ni bora zaidi na popote alipo na chochote anachofanya hupenda kuwa juu/ kujikweza
Zito si mnyenyeku na akifanya hivyo hufanya kwa manufaa binafsi
Zito si mtu wa kutaka changamoto, kitu ambacho kitamgharimu hata huko ACT, akitokea mwanachama atakayepingana na misimamo yake ndipo hapo rangi zake halisi Zitakapoonekana
Kwasasa yupo HONEYMOON!kila kitu ni shangwe tu. Fungate hili likiisha akatulia ofisini ajenge chama ndipo hapo tutakaposhuhudia maajabu! Ni suala la muda tuu..!!!