Baada ya kutafakari kwa kina na kuangalia kila pande za Tanzania huku nikichunguza kwa undani vyama vya siasa hapa nchini kuanzia CCM, CDM, CUF, NCCR-MAGEUZI, n.k.
Nimeelewa yafuatayo:
1. CCM ni chama cha mafisadi ambacho kwa hakika hakiwezi kuleta unafuu wa maisha kwa mtanzania masikini asiye na mbele wala nyuma. Hivyo, hakuna ukombozi ndani ya CCM.
2. CDM ni chama kilichojaa unafiki, fitina, uzandiki na uhafidhina. Kuweka matumaini ndani ya chama hicho ni sawa na kupaka rangi upepo. Hakuna ukombozi kwa mtanzania wa hali ya chini utakaopatikana kupitia chama hicho.
CDM ina mwonekano wa kifamilia, vilevile ina kila dalidali ya mwelekeo wa Ki-CCM. Huku viongozi wake wakiwa wanasukumwa sana na nguvu za kusaka tonge.
3.Vyama vingine vyote vya kisiasa vilivyosalia ndani ya Tanzania havina demokrasia ya wazi na harisi yenye mwelekeo wa kumkomboa mtu masikini ndani ya nchi hii.
Hivyo, nguvu zangu zote na akili yangu yote sasa navielekeza kwenye chama kipya cha ACT.
Nashawishika kufanya hivyo kutokana na sera za chama hicho zilizo wazi pamoja na demokrasia ya wazi inayokiendesha chama hicho.
Lakini kikubwa zaidi ni namna safu ya uongozi wa chama hicho ulivyo na weledi wa kisiasa wa kutosha kutokana na kufahamu kwa kina siasa za nchi hii zilivyo.
Zitto Zuberi Kabwe, Prof. Kitila Nkumbo, Samson Mwigamba, Nyakarungu, na vichwa vingine vya uhakika naamua kuungana navyo katika harakati za kukomboa watanzania kutoka katika kucha za mkoloni mweusi CCM.