Salute Comrades..
Nitaelezea kwa ufupi kwa mujibu navyofahamu mimi..
Mkuu Kashi sanduku la agano ni sanduku lililotengezwa kwa
mbao likiwa limenakshiwa kwa
dhahabu safi lilitumiwa na wana wa Israel, ndani ya sanduku la agano kulikua na
mawe mawili yaliyoandikwa
Amri kumi za Mungu alizopewa babu yetu Musa pale mlima Sinai (kama sijakosea),kulikua na
Fimbo ya Aaron (Haruni) ambayo ni fimbo ya kichungaji pia kulikua na chungu kilichokua kimewekwa
Manna chakula ambacho Mungu aliwalisha Wana Wa Israel jangwani (soma Waebrania 9:4)
Mkuu
Kashi
sanduku la agano halipo tena kati ya Waisraeli. Tangu nyakati za kuanguka kwa jiji la Yerusalemu na kuangamizwa kwa hekalu, na hatimaye kuchukuliwa kwa Waisraeli na kupelekwa utumwani Babeli mwaka 587 K.K.; kulikuwa ni chanzo cha kupotea kwa sanduku la agano. Na wakati hekalu la pili linajengwa baada ya utumwa wa Babeli mnamo mwaka 537-515 K.K.; sanduku la agano lilikuwa lilishapotea miaka mingi iliyopita. Na hakuna sanduku jipya lililotengenezwa.
Hivyo manabii waliwaasa watu kuwa wasijitaabishe kwa kulihangaikia sanduku la kihistoria lililoaminika kuwa ni kiti cha enzi cha Mungu. Na wasijisumbue kutengeneza sanduku jingine kwani Yerusalemu mpya itakuwa ndiyo kiti cha enzi cha Mungu. Yer.3:16-17 “kisha itakuwa mtakapoongezeka na kuwa wengi katika nchi hiyo asema Bwana, siku zile hawatasema tena, ‘sanduku la Bwana’ wala halitaingia moyoni wala hawatalikumbuka, wala hawatalizuru, wala hayatafanyika hayo tena. Wakati ule watauita Yerusalemu kiti cha enzi cha Bwana.”
Kwa vile hakuna anayejua sanduku la agano liliko, yanayosikika sasa ni masimulizi yasiyo na uhakika. Maana baadhi ya watu wanasema kuwa sanduku la agano lilifichwa na nabii Eliya ambaye alilifukia ardhini mlimani Karmeli. Na wengine wanasema sanduku la agano lipo nchini Ethiopia.
BTW tusubiri michango ya wenzetu.
Astelia