mshana jr ahsante kwa kunipunguzia maumivu, maana mwezi wa kwanza mwanzoni nilifiwa na Bibi yangu mzaa Mama nilikuwa nampenda kupita kiasi yaani yeye ndo alikuwa kama Baba na Mama, hii ilitokana na wazazi wangu kufariki nikiwa kwenye umri mdogo
huyu Bibi yangu alikuwa akitunzwa na Dada mpaka mauti yalipomfika, kwa kweli tulihuzunika sana ilifikia kipindi mi nilikuwa sipendi kumtembelea sister, maana nilishazoea nikienda huwa naanza kupiga stori na bibi kwanza pia alikuwa akinipa ushauri mkubwa sana na akiona kuna jambo nachelewa kulitekeleza hakuchoka kunisihi maana mimi ndo mjukuu wake wa kiume
niliye karibu nae,
pia nilikuwa na utaratibu wa kumpelekea Zawadi kila mwezi, sasa baada ya yeye kufariki ikifika zile siku ambazo huwa namtembelea( maana nilikuwa napenda kwenda siku ya jumapili ) najisikia vibaya kiasi kwamba pindi nikifika tu nikiingia ndani namwambia Dada,
"huku ntakuwa siji,maana nilitegemea kumkuta Bibi kakaa hapa",
Dada ananijibu, "mwenyewe nataka kuhama hapa maana kuna kipindi huwa namkumbuka sana"
Pia kuna mtoto wake wa kiume sasa akisikia mama yake anaenda Hospital tu anamwambia," ukirudi njoo na Bibi". Maana huyu nae alikuwa ni rafiki mkubwa wa bibi kiasi kwamba mpaka anaumwa alikuwa akimlalia bibi
ULIPONISAIDIA SASA;
1. Nikimkumbuka bibi yangu/kusikia taarifa ya msiba/nikiona maiti/nikiona majeneza sishituki yaani naona kitu cha kawaida sana kiasi kwamba najikuta nataka kutabasamu, yaani siogopi/sihuzuniki wala nini
2. Tabia ya kwenda kwa Dada imekuwa ya kawaida sa hv zawadi niliyokuwa nampelekea Bibi nampa yeye na watoto
3. Hili ni kubwa zaidi nalifanyia utafiti linahusu Recaination(sijui kama nmepatia hzo tarakimu), ntalithibitisha baada ya muda mrefu kidogo.
USHAURI;
Naomba usichoke kutupa hii elimu maana umenisaidia sana kiasi kwamba nashindwa kueleza, yaani sa hv sina tabia ya kubabaika babaika nikiona au kusikia msiba najisemea kimoyo moyo,"kafaulu mtihani huyo" kisha maisha yanaendelea