Kumbe kuna wasomi wanaomshangilia huyu mnafiki?..
Mkuu Sitta ndiye aliyezima ule mjadala kwasababu zake,kama aliweza kusimamia mpaka eddo akajiuzulu kwanini akaizima hoja bila sababu tena kwa ukali kabisa.kama wabunge akina Dr slaa wangepewa nafasi ya kuendelea kuibana tume na ukweli kuwa wazi sheria ingechukua mkondo.mjadala aliuzima kihuni mwenyewe alafu leo analalama nini? Tena mbaya zaidi akijitamba kuwa atasema mengi wakati hata kumtaja mmiliki wa Richmond anaogopa anaishia kusema tunawajua!Tatizo hapa ni kuwa watu wamelishwa maneno na hawajui hata maana yake halisi. Samuel Sitta angekuwa mnafiki basi angepinga posho ili kupata umaarufu wa bure kumbe kwa undani anaunga mkono. Kwa kuwa Sitta si mnafiki hata kidogo, akasema kweli Bungeni kuwa yeye anaunga mkono posho. Sitta akiwa Spika alisimama kidete na kuruhusu mjadala na uchunguzi huru wa Richmond mpaka waziri mkuu mpenda mali na mawaziri wake wakalazimika kujiuzulu. Utekelezaji wa maazimio ya ripoti ya Richmond umeharibiwa na serikali, Sitta hahusiki hapo. Ndio maana kasimama kidetete bila kutetereka na kusema hadharani kuwa DOWANS WASILIPWE!!
Wewe usiseme kuhusu cda, hapo ndiyo aliharibu kabisa na aliemuokoa ni mwalimu nyerere! Aliwaajiri ndugu zake akina ismael rage wakafanya ufisadi wa ajabu! Jamani kama mmezaliwa majuzi tafuteni historia ya nchi hii kwanza ndiyo mposti habari zenu! Leo ukitaja cda enzi ya sitta kuna watu watakutafuna!
Aaaah wapi!Hata ukitumia maandishi makubwa na bold ukweli utabaki palepale, Edward Lowassa hafai kuwa kiongozi Tanzania. Ni mpenda mali, ana utajiri mkubwa wa mashaka, amehusika na kashfa ya ufisadi ya Richmond ndio maana akalazimika kujiuzulu na ni kibaraka wa Rostam Aziz.
Samuel Sitta na Harrison Mwakyembe ni viongozi makini wanaopinga ufisadi na ni mtaji mkubwa kwenye uchaguzi wa 2015. Watanzania tunatambua hilo.
ok kumbe utajiri wa lowassa ndiyo chuki yako? Sasa ukae ukijua utajiri wake ni wa halali, yeye ndiyo rais mtarajiwa, hakuna wa kumzuia na hao unaowataja hawana watu kwani wanachotegemea ni ukabila. Hakuna wa kumzuia lowassa kuwa rais wa nchi hii kwa njia yoyote ile, fedha, umma au kisiasa, hakuna! ni swala la muda tu sasa.
ni kweli mkuu kama asingeuzima haya niliyoyaeleza kuhsu unafiki wake yeye na karamagi na msabaha yangekuwa wazi mapema ile, chuki yake ni kukosa kazi iliyochukuliwa na dowans, mbona imechukuliwa na simbion kwa njia ile ile ya dowans watu hawasemi? Tuache unafiki watanzania.
Aje ajiunge kama mwanachama wa kawaida si kutaka kugombea uongozi, huku watu wamejipanga!!!!!!!!!!Jina la Samwel Sitta lilipotajwa ili apokee recognition pale udsm kama Spika aliyesoma kitivo cha sheria alishangiliwa sana. Ukumbi ulilipuka kwa shangwe. Kushangiliwa kwake tena na wasomi inaonyesha watanzania wana imani kubwa nae. CCM wakifanya mizengwe namshauri ajiunge Chadema, atapata nafasi nzuri, watanzania wanamhitaji sana.
Jina la Samwel Sitta lilipotajwa ili apokee recognition pale udsm kama Spika aliyesoma kitivo cha sheria alishangiliwa sana. Ukumbi ulilipuka kwa shangwe. Kushangiliwa kwake tena na wasomi inaonyesha watanzania wana imani kubwa nae. CCM wakifanya mizengwe namshauri ajiunge Chadema, atapata nafasi nzuri, watanzania wanamhitaji sana.
Waberoya umeibuka kumbe bado upo, hee umeona watu wako wanavyopambana?????????? Chomoka huko uje CDM tupiganie kukomboa nchi mikononi mwa maghamba's wacha kuishabikia uozo unaouona!!!!!!du naona kama wanafanana kwa kila kitu mkuu! unafiki wao ni wa kihistoria na mbaya zaidi ni marafiki
unafiki wa sitta ni huu.
richmond ilipofutwa, sitta aliamua kuanzisha kampuni yao yeye, karamagi na msabaha lakini wakachelewa kwenda brela wakazidiwa ujanja na dowans, kuona wamezidiwa ujanja na dowans sitta akamshawishi waziri wa nishati afute mkataba na dowans. Pamoja na kwamba dk. Rashid alielezea athari zake na ambazo ni hizi za sasa kuilipa dowans mabilioni ya shilingi hawakusikia. Kisha akamteua dk. Mwakyembe kuongoza tume kwa kushirikiana na wabunge wa chadema wakati anajua mwakyembe, (waziri mkuu wa sitaa ikiwa atapata urais), ana interests zake za umeme wa upepo singida! Huo ndiyo unafiki mkubwa wa samuel sitta. Mgombea urais kwa tiketi ya chadema 2015! Sasa watanzania ukweli wameujua, icc imeeleza ukweli wote, lowasa hajaonekana mahali ametajwa, walioshirikishwa kwenye unafiki wa sitta na wenzake wakiwemo chadema kumdhalilisha mpiganaji lowassa sasa wanahaha wengine wameanza kujikomba kwa lowassa! Jamani watanzania tutafuteni ukweli kwanza kabla ya kujigongagonga. Huu ndiyo ukweli na wananchi wameanza kuujua na ndiyo maana pale udsm juzi alipoingia akiwa na rais, wasomi wa kweli walimshangilia.
Samuel Sitta ni kiongozi shupavu pekee kwenye serikali ya Jakaya Kikwete, kwani amekuwa na guts za kusimama hadharani na kusema ukweli kupingana na ufisadi wa Dowans, mgao wa umeme, kukosekana kwa maadili ya uongozo na mwingineo. Wanafiki ni wale viongozi waliopo serikalini halafu wanalalamika chini kwa chini.
Long live Samuel Sitta, una maadui wengi sana mafisadi, but God and the people of Tanzania are with you all the way!!!
kwa hiyo unaniambia sitta anatumia mawazo ya kisasa kulikabili suala la dowans?basi badala ya kumuita manafiki tutamuita mchochezi na muhuni!Kweli wewe mstaafu mawazo ya kizamani sana, your ideas are not workable in the closed and corrupt system like Tanzania.
Katika kamusi, neno Mnafiki maana yake ni mtu mwenye kigeugeu au mwenye kuwa na sura mbali mbali: Leo hivi kesho vile. Nyie mnaosema eti Sitta ni mnafiki, je ni kwa lipi? Huyu kiongozi Watanzania wengi wanamkubali kwa kuwa amekuwa na msimamo usiotetereka. Mfano ni kupinga malipo ya kifisadi kwa Dowans, Sitta amesimama kidete na hata kusema hadharani kila mara kuwa anapinga malipo haya ya kifisadi na yuko tayari kwa lolote.
If anything, Sitta is the complete opposite of unafiki, kwani amekuwa daima akisimamia anachoamini bila kutetereka. Hata walipomtishia kumfukuza kazi serikalini au kwenye CCM kwa kupingana na msimamo wa serikali juu ya Dowans na ufisadi mwingine alisimama kidete na kukataa kuwa kigeugeu kwenye msimamo wake. Huyu ndiye aina ya kiongozi ambaye Tanzania inamhitaji.
Mafisadi ndiyo wamejaribu kumchafua Sitta kuwa eti ni "mnafiki" kwa kuwa amekuwa ni mwiba mkali sana asiyetetereka ndani na CCM na serikali kupinga ufisadi. Ni aibu kubwa na jambo la kusikitisha kuona baadhi ya The so-called Great Thinkers wa JF nao wameingia kwenye mkumbo wa mafisadi...