sammata tumsaidiaje ili awike Ulkaya?

sammata tumsaidiaje ili awike Ulkaya?

Tango73

JF-Expert Member
Joined
Dec 14, 2008
Posts
2,227
Reaction score
1,362
nikiangalia ligi kuu za ulaya na latin america, sijaona mtu mweusi mwenye kiwango cha kumpita sammata. hata huyo demba Ba hajafikia kiwango cha samata. sasa tufanye nini watanznaia wenzangu ili tumtangaze huyu son of our pride?
 
Mi nadhani akiendelea kujituma tu atatoka. Sidhani kama kuna kingine cha kufanya, anacheza kwenye klabu kubwa hvyo ni rahisi kwake kuonekana. Lakini pia Taifa Stars ijitahidi ili angalau tupate nafasi za kushiriki makombe makubwa barani Afrika ka AFCON na wachezaji kama Samata wanaweza kuonekana hata nje na kupata nafasi za kucheza huko.
 
Hana afya ya kutosha kukipiga ulaya...
 
Hana afya ya kutosha kukipiga ulaya...

Hili ni kweli mkuu, ukiangalia kwa undani wachezaji wetu hawana miili yenye nguvu sana. Hii inatokana na kutokukuwa vizuri, na lishe duni walipokuwa wadogo, najuwa wengi watapinga kwa kujilinganisha na wakorea na wajapani, lakini ukiangalia, vizuri utaliona hili.
 
Huyu si alikataa kwenda ulaya? Alipata timu ya ligi kuu hapa Ureno akadai hakuna tofauti kubwa ya kimaslahi kati hii timu na timu yake ya sana..! Tatitzo ni uelewa mdogo, hakuona kuwa ulaya ni ulaya tu angeweza kupata more exposure..!
 
Hana afya ya kutosha kukipiga ulaya...

wachezaji wengi hufika ulaya wakiwa hawana nguvu za kutosha kwa hiyo kule hupatiwa wataalamu wa mazoezi na vyakula na hatimae hukaa sawa.unakumbuka CR alivyokuja united alikuwaje?
 
Hana afya ya kutosha kukipiga ulaya...

Afya unayoizungumzia wewe ni ipi, messi ana afya?? mata ana afya?? au wewe unataka maumbo makubwa kama Drogba ndio unasema afya, mpira si afya according to you, mpira ni mbinu na akili...tambua hilo
 
Ngasa alienda kwenye interviw westham. Akafanya majaribia ya uwanjani kwa kiasi kikubwa alikidhi kiwango.
Akapewa interview ya kula hapo ndipo alipo chemsha. Unajua makuku ya uengereza makubwa sana. Akapikiwa moja ammalize, mama yangu kala robo tu anatokwa na majasho kama anachimba shimo la choo. Alivyo maliza tu, kapewa tiketi yake ya kurudi bongo. Embu siku moja mwangalie drogba akipata menu, mtakimbia
 
Messi? Mata? bora labda umzunguzie Oscar na Neymar
 
huyu haendi ulaya mpaka mkataba na simba uishe halafu anauzwa bila simba kuchukua chochote chezea wazee wa mipango..
 
Kwamba ulaya hakuna mchezaji anayemzidi! Ama kweli mashabiki wa tz kama w uk.
 
Ngasa alienda kwenye interviw westham. Akafanya majaribia ya uwanjani kwa kiasi kikubwa alikidhi kiwango.
Akapewa interview ya kula hapo ndipo alipo chemsha. Unajua makuku ya uengereza makubwa sana. Akapikiwa moja ammalize, mama yangu kala robo tu anatokwa na majasho kama anachimba shimo la choo. Alivyo maliza tu, kapewa tiketi yake ya kurudi bongo. Embu siku moja mwangalie drogba akipata menu, mtakimbia

Hizi Story mkuu ni za kuchangamsha baraza mkuu..., Hivi unajua diet wanayopewa wachezaji, na kula makuku ndio afya ?

Labda useme ufupi unaweza ukawa disadvantage kwa mchezaji na kama hana nguvu au stamina wanampeleka Gym kama walivyomshauri Joe Cole kipindi fulani aongeze bidii Gym
 
Hili ni kweli mkuu, ukiangalia kwa undani wachezaji wetu hawana miili yenye nguvu sana. Hii inatokana na kutokukuwa vizuri, na lishe duni walipokuwa wadogo, najuwa wengi watapinga kwa kujilinganisha na wakorea na wajapani, lakini ukiangalia, vizuri utaliona hili.
Hii ni kweli, na ndio maana hata waKorea/Japan hawatumiki kwa kila mechi. Lakini anaweza kujituma zaidi, na hivyo sababu ya umbo ikawa ndogo hata kumkwaza. Lakini pia wenzetu wanaangalia achievement zake...na ndo maana mwanzoni haikua afya kwao kuizarau T-stars.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom