Samadu Hassan Maduhu

Samadu Hassan Maduhu

Mr Anold

JF-Expert Member
Joined
Jan 19, 2012
Posts
218
Reaction score
47
Wadau nimekuwa mtazamaji wa Habari za Kimataifa wa TV za Tanzania kwa kipindi kifupi tu ila huyu jamaa/mzee nampigia saluti.
Anaandaa vizuri mpaka 99% anapozisoma sasa 100%

Star Tv mna kichwa japo ndo kinazeeka hivyo
 
Anaitwa Samadu Hassan na siyo Samadu Hassan Maduhu. Maduhu alikuwa kama si mwandaaji basi mhariri wa vipindi RFA.
Umenena, hata mimi Samadu Hassan namkubali sana, nadhani kwa habari za kimataifa anashikilia usukani kwa tz kwa mujibu wa maoni yangu.
 
Mzee Samadu yupo sawa sana, siyo akina Mukhsin Mambo, Benard James, Hemed Kivuyo, Salum Mkambala etc.

Samadu Hassan ni level nyingine.
 
Samadu Hassan huyu ni mkongwe kwenye
fani ya Utangazaji pia ameanza mbali sana
tangu RTD,Redio One,DW Swahili,RFA.

Ni hazina hii japo utashangaa sana vichwa
hivi havithaminiwi hapa nyumbani kama
ulivyoona kwa Dastan Tido Mhando.
 
Nadhani Samadu level yake ilibidi awe hata BBC, ananiachaga hoi na matangazo yake, kiswahili chake pamoja misemo yake.
 
Alitangaza KBC ya Kenya pia miaka ya nyuma wakati inaitwa SAUTI YA KENYA. Mwanzo nilifikiri Mkenya.
 
Huwa najiuliza sauti zao za kimataifa wanazitengeneza(wanafanyia mazoezi) au wanazaliwa nazo?
 
^^
Chanda chema hukikwa pete!
Namsifu sana, ni hazina yenye manufaa. Uishi maisha marefu Samadu
^^
 
Samadu level nyingine wakuu Anga za makitaifa,anaanza hivi sasa ni washington dc jiji hilo lenye ukimya lisilo na pilikapilika nyingi',,,,,,,!!!!!....
 
jamaa yuko poa sana,ni mtangazaji wa kimataifa yule mzee,kati ya vichwa vinavyotangaza habari hapa bongo,yule ni nambari oneakifuatiwa na djaro warungu,oooh,no nimekosea sio djaro warungu,anafuatiwa na hemedi kivuyo.
 
ile sauti yake kama inatisha huku muda huohuo inavutia then anayapanga matukio na misemo.yuko creative sana huyu mzee naipongeza kazi yake
 
no comment............namweshimu mzeee wangu, hakuna mtangazaji TZ wa kulinganishwa naye
 
Alifanya kazi Kenya kisha akaenda London,baba yake alikuwa katibu wa tawi wa TANU (nasikia baba yake alikosana na mwalimu,so akakamatwa na kuwekwa ndani wakati huo Samadu ni mwanaharakati za kweli,ndo Samadu akakimbilia nje)
 
Back
Top Bottom