Salamu za CHADEMA Iramba Magharibi

Salamu za CHADEMA Iramba Magharibi

Makamanda,

Hii shughuli ya kutoa elimu ya uraia na ukombozi uwa ni kujitolea au ina malipo?

Kwa maana kama ni kujitolea, ina maana ni wito, hivyo dhana nzima ya ukombozi inakua na maana na mantiki.

Ila kama ni shughuli yenye malipo, ina maana hiyo ni ajira (kazi) ya kwenda kupiga domo na kupotezea muda wananchi, kwa maana kwamba hao makamanda hawana jipya.

Hamida mbona wewe na magamba wenzako baada yakusikia ujio wa makamanda mnaweweseka sana..hahaha .dada hamida tulieni mpate dose
 
attachment.php
 
Mwigulu ni mwanaume suruali...dume zima linakyja hapa jamvini huku likilia lia na kutoa keheli na vitisho kwa msichana kamanda ambaye kiumri ni mdogo jesca....hii ni aibu kubwa sana kwa mwigulu.
 
Duh ndugu zetu hebu tumieni busara, babu na helicopter yake na Budgeting isiyo na kipimo, kashindwa, itakuwa nyinyi Askari wa miguu Huku mnaomba lift hapa na pale. Ndio mtamweza huyu kijana aliyekuwa na kipawa cha kupendwa hapo Iramba. Hebu jiondekeeni kabla hamjafukuzwa kwa mawe.
 
Kila lililo la kheri,nimeipenda idea ya kuwaalika makamanda wengine walio na nafasi ya kuja huko,wazo hili la kupiga kambi kwa Mwigulu naliunga mkono lakini kwangu mimi nimekuwa nikiwaza kwa mapana zaidi,kwamba tuunde timu maalum ya kuwatembezea operation maalum wabunge na mawaziri ambao kazi yao ni kupindisha ukweli hasa pale ambapo wanapambana na CDM,ni vema tukawashughulikia kisiasa kwa kupeleka timu maalumu itakayokuwa inakwenda majimboni mwao ili kwenda kutoa elimu ya uraia hadi wananchi wapate ukombozi wa kweli.tukifanya hivyo nadhani tutakuwa tumewaadhibu ipasavyo wabunge magaidi kama alivyo Nchemba.
Djemba na wenzio leo nitajaribu kuzungumza na makamanda hapa tuone namna ya kuja kuwaunga mkono huko jimbo la Iramba Magharibi.tupeni namba zenu ili tuwasiliane.
 
Piga kazi kamanda Djumbe wala usiogope mikwara mbuzi ya Lameck Madelu kwa kamanda mwenzako Jesca Kishoa. Kwa namna mwigulu anavyotapaatapa hadi kuanza kumtishia Jesca ni dhahiri kuwa maji yamemfika shingoni na hana namna ya kujinasua ni lazima azame mtoni hata kama anajiita mamba basi uwezo wake wa kukata maji mtoni umekwisha.

Imani yangu ni kwamba kazi unayoifanya kanda ya kati hasa mkoani Singida ni kubwa sana na Mungu ataendelea kuwasimamia na kuwalinda kwakuwa tunawaombea kila siku ili Mungu awaepushe na kuwalinda na hila za muovu mwigulu asije akafanikiwa kuwadhuru ili hatimaye wana wa Iramba wapate kutambua hila za mbunge wao aliyeshindwa kutimiza majukumu yake na kujikita katika kufanya siasa za majitaka dhidi ya watanganyika wenzake.

Kamanda Nyahende Thomas tupo pamoja sana, muziki huu ameutaka yeye mwenyewe kwa kujitangaza adui wa harakati za mabadiliko nchini, wakati sisi tunamuona panya tu, mkoa wa Singida hatukubali kuwa na viongozi wanaotutia aibu kama hawa, tumejiandaa kulinda heshima yetu kwa lolote lile>>> asante sana
 
Njooni Iramba na mutaona Kama mtapata kitu maana wanyiramba sio wachaga ambao mnawaburuza kila kitu. Ila tu musikimbie mambo yakiwa yameharibika maana yake mjuwe nasi tumejiandaa kuwasikiliza. Tutashindana kwa nguvu ya hoja na sio kwa hoja ya nguvu. Lakini Chonde Chonde djembe wake zetu maana unasifa mbaya sana ikifika kwa wanawake
 
Njooni Iramba na mutaona Kama mtapata kitu maana wanyiramba sio wachaga ambao mnawaburuza kila kitu. Ila tu musikimbie mambo yakiwa yameharibika maana yake mjuwe nasi tumejiandaa kuwasikiliza. Tutashindana kwa nguvu ya hoja na sio kwa hoja ya nguvu. Lakini Chonde Chonde djembe wake zetu maana unasifa mbaya sana ikifika kwa wanawake

cjawahi kuona diwani bogus ka wewe.ni busara ukafanya siasa za kistaarabu,na hayo majini unayofuga yatakugarimu,yuko wapi Zingula na ubabe wake.take care Baba Bashiri
 
Back
Top Bottom