Salaam kwa Mh. Edward Lowassa na wenzake

Mzee kasori, heshima mbele mkuu! Huyu Lowassa aliangushwa vibaya sana mwaka 1995, na hakuna alietarajia kuwa angerudi katika ulingo wa kisiasa! FISADI alirudi kwa kishindo na akapanda ngazi alizozipanda hadi kuwa Waziri mkuu! achilia mbali mali alizojilimbikizia mara tu baada ya CCM kuwa na uelekeo wa ki-fisadi! Maneno uliyoyatamka hapa umeyatoa wakati muafaka sana maana tayari alikwisha andaliwa madaraka mapya!! Mzee wetu kasori NAKUSHUKURU SANA KWA KUINUSURU NCHI YETU!... Ewe Fisadi LOWASSA this time HAKUNA KURUDI... TOKAAA EWE PEPO MCHAFU UNYONYAE WANYONGE WA NCHI HII!!!!!!GO GO NEVER EVER COME BACK!!!

Poor Lowasa, atanunua kila mwandishi wa habari lakini hakuna cha kumsafisha hata akitumia nyukilia bomb bado atabaki yule yule mchafu kama pal wake ROstam Azizi!
 
Namalizia kwa kusema “Tuheshimu na kudumisha kitu UKWELI”. Kwa viongozi, zingatieni na kwa unyenyekevu heshimuni viapo vyenumnapokabidhiwa madaraka. Baba wa Taifa daima katika mkoba wake alibeba Bibilia na Azimio La Arusha. Nyinyi kwa kipindi hiki kigumu cha ufisadi na kukithiri kwa rushwa na mikataba mibovu; bebeni daima photo-copy za viapo vyenu pamoja na Bibilia au Koran pamoja na katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mnazo dini zenu. Sikusikia yeyote akiapa kwa dini za asili kwa Rais au kwa Spika wa Bunge...

Halmashauri kuu ya CCM inayokutana Butiama naitakia mafanikio makubwa katika maazimio watakayofikia . baada ya hapo muonekane mmedhamiria kutenda kwa kuleta maendeleo yenye kuzingatia uadilifu na uwajibikaji . viongozi wabovu wawajibishwe tu. Watanzania wengi leo bado wanamlilia Mwalimu J.K. Nyerere hasa kwa matatizo kama haya ya mikataba mibovu ya Madini, RICHMOND n.k. Wanasema sorry Mwalimu lived ahead of his time. Alituangazia kwa mengi, hakuna wa kutu tetea leo kwa matatizo yote haya.

Mungu Ibariki Tanzania. Mungu Ibariki Africa.


Yetu macho yaso-kuwa na machozi na masikio yalioharibiwa na mabomu ya ufisadi! Mzee kasori umesema yote, Mungu akupe maisha marefu!
 
Poor Lowasa, atanunua kila mwandishi wa habari lakini hakuna cha kumsafisha hata akitumia nyukilia bomb bado atabaki yule yule mchafu kama pal wake ROstam Azizi!

Mwafrika wa kike, Nakushukuru kwa michango yako isiyokuwa na chembe ya uoga wala upendeleo... Hawa mafisadi hawajui kabisa maana ya time n space! huu si wakati wa kuwahadaa watanzania tena! Ubashiri wa CASTILO uko wazi sana if one can read between the lines...
Ona alivyosema CASTILLO wa Guatemala kuhusu wabakaji/wakwepuaji wa raslimali za nchi:-“One day the apolitical intellectuals of my country will be interrogated by the simplest of our people. They will be asked what they did when their nation died out slowly like a sweet fire small and alone. No one will ask them about their dress their long siestas after lunch. No one will want to know about their sterile combats with the ideas of nothing. No one will care about their higher financial Learning. They won’t be questioned on Greek mythology or regarding their self disgust when someone within them begins to die the coward’s death. They will be asked nothing about their absurd justifications born in the shadow of total lie. On that day the simple men will come.Those who have no place in the books and poems of the apolitical intellectuals but daily delivered their bread and milk, their tortillas and eggs those who mended their clothes, those who drove their cars, those who cared for their dogs and gardens and worked for them and they will ask: WHAT DID YOU DO WHEN THE POOR SUFFERED WHEN TENDERNESS AND LIFE BURNED OUT IN THEM?
 
Nimeipata kama forwarded mail, ningependa kushare the expressed views.

SALAAM KWA MH. EDWARD LOWASA NA WENZAKE KUHUSU


I Removed the topic ... ... you can see it merged.
 
Mama Karibu JF

Hii kitu ya Kasori SH, iliishakuwepo hapa long long ago...alipost mwenyewe....
 
na mie pia nakukaribisha Mumy (mama) sio mbaya umeanza vizuri inaonyesha utakua mchangiaji mzuri ambae utakua unakuja na evidence kama ulivyojaribu hapo....keep it up JF ndio kwetu na wewe tunakuhitaji nakukaribisha kwa mikono miwili japo sio kazi yangu kukaribisha wageni
 
Asanteni sana Ushirombo na Nyerererist kwa kunikaribisha katika jukwaa hili adhimu. Tuko pamoja.

Mama.
 
..jamani hivi Mawaziri,Waziri Mkuu,VP,na Raisi, wanapata mshahara na marupurupu kiasi gani? naomba mwenye kufahamu atupe walau estimate kwa mwaka.

..halafu naona Nyerere alikuwa very abusive kwa rafiki yake Rashidi Kawawa.

..kwanini Kawawa alimruhusu Nyerere kum-treat kama mwanawe wa kumzaa?
 
..jamani hivi Mawaziri,Waziri Mkuu,VP,na Raisi, wanapata mshahara na marupurupu kiasi gani? naomba mwenye kufahamu atupe walau estimate kwa mwaka.

..halafu naona Nyerere alikuwa very abusive kwa rafiki yake Rashidi Kawawa.

..kwanini Kawawa alimruhusu Nyerere kum-treat kama mwanawe wa kumzaa?


nini kimekupelekea kuona kuwa Nyerere alikuwa very abusive kwa Kawawa?
 
Mama said:
nini kimekupelekea kuona kuwa Nyerere alikuwa very abusive kwa Kawawa?


Mwalimu Nyerere said:
"Nenda umwambie Mzee Rashidi Mfaume Kawawa asiwe mjinga kama Lowasa"!

MAMA,

..hilo neno MJINGA ndiyo nimeona kama ni kumvunjia heshima[abusive] Mzee Rashidi Kawawa.

..kwa mtizamo wangu hiyo ilikuwa ni kauli ya matusi, na ndiyo maana Samuel Kasori hakupeleka ujumbe huo kwa Rashidi Kawawa.

..tena naamini Kasori amefanya makosa makubwa kuiweka kauli hiyo hadharani.
 
Joka Kuu, angalia kilichofuatia baada ya hapo utaona kuwa Mwalimu alikuwa ni bingwa wa hoja, na neno "ujinga" alilichagua vizuri kwamba Kawawa ana akili asiwe "mjinga"...
 
Mwanakijiji,

..sasa ina maana Kawawa alishakuwa mjinga kama Lowassa kwa hiyo arejee kwenye werevu aliokuwa nao mwanzo? i just dont understand!!

..lakini kwa mila za wazee wangu, kumuita Mzee mwenye mji wake, anayejitegemea, mliyetoka naye mbali, mjinga ni kosa kubwa sana. labda ni suala la mila na utamaduni tu linalotufanya tusielewane ktk hili.

..nadhani ndiyo maana hata Samuel Kasori alishindwa kuwasilisha ujumbe wa Baba wa Taifa kwa Mzee Rashidi Kawawa.

..nasisitiza kama Kasori alishindwa kumpa ujumbe huo Mzee Kawawa basi hakupaswa kuuweka mbele ya kadamnasi. kwa maoni yangu, Kasori amefanya makosa makubwa sana.

NB:

..naomba turudi kwenye mada.

..sijui ni vigezo gani walivitumia Mkapa na Kikwete kumrudisha Lowassa serikalini.

..halafu hawaisha kujibaraguza kwa familia ya Mwalimu. mara wakazuru kaburi. mara wapokee Biblia toka kwa Mama Maria.

..watakoma lini hawa??!!
 
mzee mjinga ni tusi kwa mtu ambaye si mjinga; na mjinga huwa mjinga katika mambo fulani lakini katika mambo mengine huwa mwerevu. Mimi ni mjinga yanapokuja mambo ya kemia na biolojia, sijui; ukiniita mimi mjinga unaelezea hali halisi na siyo tusi.

Ujinga huondoka pale mtu anapopata ujuzi wa jambo fulani husika. Mwalimu angesema "Mwambie kawawa asiwe Mpumbavu" basi atakuwa amemtukana. Neno hili la "upumbavu" Mwalimu alilitumia aliposema kuwa uamuzi wa serikali ya Mwinyi kuamua kuondoa haki ya raia kuchaguliwa bila kulazimika kuwa na chama kuwa nii "wa kipumbavu".
 
..kauli ya kumtaja Mzee Kawawa kwa majina yake matatu/kamili na kutamka asiwe mjinga hakikuwa kitendo kizuri.

..kauli yenyewe inaelekea ilitolewa katika hali ya kukaripia na kwa hasira.

..ingetolewa ktk mazingira ya mzaha na utani kidogo ningeelewa na kuivumilia. kwa kweli imenisikitisha.

..hata mwandishi naye anapaswa kumuomba radhi Mzee Rashidi Mfaume Kawawa.
 
Hiyo lugha ilikuwa abusive, watu wanaoheshimiana hawaitani wajinga hata kama mmoja atakapofanya kitu cha kijinga.Tena afadhali Nyerere angekuwa anaongea na Kawawa na kumwambia "usiwe mjinga" kuliko kumtumia ujumbe kwa secretary junior kama Kasori.

Nnamdi Azikiwe aliposikia Nyerere amemuachia nchi Kawawa briefly ili aimarishe chama, na baadaye akarudi kuichukua nchi kutoka kwa Kawawa alishangaa sana.Alisema nipeni huyo Kawawa nimfanye mtoto wangu.Nigeria kitu kama kile kilikuwa hakiwezekani kwani Nyerere angerudi angeambiwa baki huko huko kwenye chama mzee, tena ukileta ujuaji tunakufunga.

Kawawa mwenyewe ndiye wa kulaumiwa kwa kuwa "yes man" wa Nyerere kiasi cha kumpa Nyerere confidence ya abuse kama hiyo.Ndiyo maana Nyerere hakuweza kukaa na watu kama kina Kambona.
 
Kawawa, hakufanya kosa lolote kushika uongozi wa taifa na kumpisha Mwalimu, alipoamua kurudi, Kawawa was just being himself na who he is as a human being, bila ya kujali power, na ni uzalendo pia,

Sasa hapa ninaona juhudi zile zile za kujaribu kusafisha kitendo cha Mwalimu, kumshusha hadhi kiongozi mwenziwe, ambayo ukweli ni kwamba ilikuwa moja ya mapungufu makubwa ya Mwalimu, ilikuwa siku zote kutowapa nafasi wasaidizi wake kufanya maamuzi ya kuwapa fursa ya kujiamini kiuongozi, matokeo yake ni taifa letu kuwa mahali lilipo sasa kiuongozi,

Ni mpaka siku tutakapokubali kuwa Mwalimu, naye alikuwa na mapungufu na ndiyo hasa tatizo kubwa la taifa letu sasa hivi, na tukayachambua wazi kwa undani, tutaendelea tu kulaumiana bila sababu. Mwalimu alimuita Kawawa mjinga, lakini akasema Mkapa ana akili na ni Mr. Clean, lakini bado tu watu wanamtetea Mwalimu ku3wa hakuwa na makosa.

Only in Tanzania!
 
Sasa hapa ninaona juhudi zile zile za kujaribu kusafisha kitendo cha Mwalimu, kumshusha hadhi kiongozi mwenziwe, ambayo ukweli ni kwamba ilikuwa moja ya mapungufu makubwa ya Mwalimu, ilikuwa siku zote kutowapa nafasi wasaidizi wake kufanya maamuzi ya kuwapa fursa ya kujiamini kiuongozi, matokeo yake ni taifa letu kuwa mahali lilipo sasa kiuongozi,

Mkuu Field Marshall ES, Kuna wakati huwa sikuelewi elewi vile! one time unakuja na hoja za nguvu nzuri endelevu na za kusisimua na kuna wakati unakuja na hoja zinazoelea elea... Hivi? katika nchi hii ambapo ktk kila idara kuna mapungufu makubwa na ukondoo uliokithiri unategemea Kiongozi mwenye upeo kama mwalimu awachekee chekee watendaji wake kama anavyofanya JK? Ngoja nikupe mifano michache jinsi ambavyo nchi hii inavyojikongoja kinyumenyume; siku ina masaa 24, katika masaa hayo, masaa 2-3 yanaishia ktk kulipia bili ya umeme TANESCO, Masaa 2-3 kupata huduma za ki-benk! Masaa 3-4 Yanaishia ktk foleni za barabarani! masaa 2 kulipia maji! sokoni masaa 4, hospitalini masaa 5-8! na masaa 3-6 ktk ofisi nyeti za serikali kama TRA n.k, kana kwamba haitoshi kuna mpumbavu kama sio mjinga/wajinga kama ambavyo mwalimu alivyokuwa anawaita, akaweka sheria eti MA_BASI yasi safiri usiku! wengine wakabinafsisha bandari, huduma za anga na reli!! ... Rushwa na UFISADI wa viongozi wetu ndo wala hakuna haja tena ya kuyazungumzia...Sasa mkuu, ulitaka mwalimu achekelee uozo na mapungufu ya watendaji wake? ...KILA NIKIANGALIA BADO SIMUONI HATA WA KUMKARIBIA MWALIMU!! Thanks mzee kasori, endelea kutufunulia yale mwalimu aliyoya-kemea kwa nguvu zote!!
Just the matter of time n space ...kama ambavyo nukuu ya mzee kasori kutoka kwa CASTILLO ktk makala yake UADILIFU NA UWAJIBIKAJI;One day the apolitical intellectuals of my country will be interrogated by the simplest of our people. They will be asked what they did when their nation died out slowly like a sweet fire small and alone. No one will ask them about their dress their long siestas after lunch. No one will want to know about their sterile combats with the ideas of nothing. No one will care about their higher financial Learning. They won't be questioned on Greek mythology or regarding their self disgust when someone within them begins to die the coward's death. They will be asked nothing about their absurd justifications born in the shadow of total lie. On that day the simple men will come.Those who have no place in the books and poems of the apolitical intellectuals but daily delivered their bread and milk, their tortillas and eggs those who mended their clothes, those who drove their cars, those who cared for their dogs and gardens and worked for them and they will ask: WHAT DID YOU DO WHEN THE POOR SUFFERED WHEN TENDERNESS AND LIFE BURNED OUT IN THEM?
... Ipo siku si nyingi tutawahoji enyi MAHARAMIA-MAFISADI...
 
Chief,

Mbona unapotea namna hiyo Mkuu?

.......eti wanasema kakosea maadili.......oopps.........sijui kama yalikuwepo tangia awali!!
 
Ndugu Kasori,



iii) Katika makala yako umejitahidi kumtenga Lowasa na Kikwete, huku ukijua wazi kuwa Lowasa asingefika alipofika na pengine asingefanya aliyoyafanya bila kubebwa na Kikwete. Sasa nakuuliza, huoni kwamba na wewe unaingia kwenye kundi hilohilo la wakwepa ukweli? Hebu nitoe wasiwasi. Hivi karibuni familia na watu waliokuwa karibu na mwalimu Nyerere wanafanya bidii kuwa karibu na Kikwete kwa kumuonyesha kwamba yeye ni tofauti sana na wengine. Kwa kufanya hivi wamekuwa wakiwashambulia viongozi waliostaafu au ambao wameng'oka madarakani. Sasa hebu nitoe wasiwasi, je nitakuwa nimekosea nikisema kuwa kuna kajitahada mnakokafanya kakujipendekeza kwa Kikwete ili mrudi kundini? Je, na nyie mnajaribu kukwepa ukweli?

iv) Hili ni la kwetu sote watanzania. Kuna tabia ambayo tumeijenga ambayo pia imethibitika kwenye makala ya ndugu Kasori. Nayo ni kuogopa kuwasema viongozi wetu wakiwa madarakani lakini mara wanapoondoka ndipo tunapata nguvu za kuwabebea mabango. Tulifanya hivi kwa Mkapa; tulimsifia sana Mkapa akiwa madarakani na wana CCM kama Kasori waliandaa kila aina ya makongamano na maandamano ya kumpongeza kuanzia lile la kumpongeza kwa kufanikisha nchi yetu kufutiwa madeni pale Ubungo Terminal hadi lile la kumpongeza kukuza uchumi pale Mnazi Mmoja. Na tena Butiku na Mwalimu Nyerere Foundation walimsifu sana Mkapa wakati ule angali akiwapa pesa za kuendesha foundation. Lakini mara alipotoka, tulimrushia mawe mpaka huwezi kuamini kwamba ni yuleyule. Sasa tunafanya yaleyale kwa Lowasa. Wana CCM hawa hawa wanaomchamba Lowasa leo baada ya kutoka madarakani ndio hawahawa ambao walikuwa hawachoki kutukumbusha ujemadari wa Lowasa alipokuwa waziri mkuu.

Na sasa tunamkwepa Kikwete, tunasubiri tuje tumvurumshie matope akitoka madarakani.Tafsiri ya yote haya ni maneno mawili kwa kiswahili: Woga na Unafiki. Wenzetu hawafanyi hivi. Wenzetu wanashughulika na viongozi wao wakiwa madarakani, hawahangaiki na wastaafu. Ndivyo walivyofanya kwa Blair kuhusu vita ya Iraq na sasa wameachana naye baada ya kuondoka na wana-deal na Gordon Brown. Ndivyo walivyofanya na wanavyoendelea kumshughulisha George Bush kuhusu Iraq lakini wataachana naye mara baada ya Rais mwingine kuapishwa hapa January 2009.

Ukweli ni kwamba tunaelekeza nguvu zetu pasipo. Lowasa tulishindwa kumshughulisha alipokuwa kwenye madaraka. Tutamchukia na kumsuta sana sasa hivi lakini ukweli ni kwamba hili halitabadili kitu madamu yeye sasa hana alichoshikilia ambacho kinatusaidia au kutuathiri sisi kama taifa. Ushauri wangu ni kwamba tushughulike na waliopo madarakani. Na wito wangu mkubwa zaidi ni kwamba tushughulike na Rais Kikwete na serikali yake. Ninachosema ni kwamba tufike mahala watanzania tuache woga na unafiki.

Hongera Ndugu Kasori kwa makala yako.

Hapa ndipo unapokosea kaka, suala sio unafiki wala uoga...ni busara za kimikakati. Tatizo ndugu zangu ninyi ni kuwa mnashindwa kutambua kuwa katika hali kama hii ambapo watenda maovu (si unajua tamko la butiama limekwepa kutumia ajenda yenu ya UFISADI") wametanda kila kona na mbadala bora wa uozo wa CCM haupo machoni (alternative power)ni vizuri kuinvest katika asasi ya URAIS kwa kutomjumuisha na maadui watenda maovu ili aweze kufanya angalao kidogo cha kupunguza mwendokasi ya maovu wakati tukijua hana ubavu wa kuondoa......Unataka LOWASA na wenziwe wakae pembeni na kumnong'oneza JK kuwa "kaka si unaona hawa wakorofi wanavyokufanyia hata na wewe,tuwe pamoja kaka"

Bora kidogo kuliko kukosa kabisa.....labda nanyi muweze kutuhakikishi watanzania kuwa mtakuwa Mbadala bora na sio Bora mbadala kama hali ilivyo sasa.....

Tanzaniannjema
 
Back
Top Bottom