Yaliyosemwa waziwazi kumhusu Lowasa ni mazito; lakini pia tusisahau mengi mazito yaliyosemwa kiustaarabu bila ya kutaja majina moja kwa moja.
Tofauti tu ya yaliyosemwa kwenye makala hii na yale ambayo siku zote tumekuwa tukiyazungumzia hapa JF, ni moja tu, kwamba mzee katoa mfano dhahiri ya jambo lililomhusu Lowasa. Mengine yote, hasa kuhusu CCM na udhaifu wa viongozi wetu kulinda maslahi ya wananchi wetu tumeyasema kwa njia mbalimbali.
Kwenda kufanyia kikao Butiama hakutakuwa na maana yoyote kama hakuna dhamira ya dhati ya kutaka kukisafisha chama kiondokane na viongozi walafi, wasema uongo, wachoyo, wanafiki, n.k.
Inabidi sasa Kikwete akubali kuukata muungano wake na watu hawa bila ya kusita tena. Asipoonyesha ujasiri huo, nafasi yake katika historia ya uongozi wa taifa la Tanzania itakuwa ni hafifu, na pengine atatupeleka katika machafuko kabla ya mwisho wa uongozi wake. Nafasi hii ni yake, inafaa aitumie ipasavyo.
Tofauti tu ya yaliyosemwa kwenye makala hii na yale ambayo siku zote tumekuwa tukiyazungumzia hapa JF, ni moja tu, kwamba mzee katoa mfano dhahiri ya jambo lililomhusu Lowasa. Mengine yote, hasa kuhusu CCM na udhaifu wa viongozi wetu kulinda maslahi ya wananchi wetu tumeyasema kwa njia mbalimbali.
Kwenda kufanyia kikao Butiama hakutakuwa na maana yoyote kama hakuna dhamira ya dhati ya kutaka kukisafisha chama kiondokane na viongozi walafi, wasema uongo, wachoyo, wanafiki, n.k.
Inabidi sasa Kikwete akubali kuukata muungano wake na watu hawa bila ya kusita tena. Asipoonyesha ujasiri huo, nafasi yake katika historia ya uongozi wa taifa la Tanzania itakuwa ni hafifu, na pengine atatupeleka katika machafuko kabla ya mwisho wa uongozi wake. Nafasi hii ni yake, inafaa aitumie ipasavyo.