Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini ni Lowassa (fisadi), Mwenyekiti wa kamati ya maadili ya CC ni Bwana Chenge nae pia ni fisadi. Kaimu Kamanda wa UVCCM ni Mzee Kingunge nae ni fisadi mzuri tu. Katibu Mkuu wa CCM ni mpambe wa mafisadi na mwana mtandao mzuri sana. Ukipanda juu kwa JK ndio huyo ambaye anawakwepa kuwashughulikia maswahiba zake. Hivi kweli hapo tutegemee mabadiliko kwenye uongozi wa Jumuiya za CCM? Maana akitokea mwanachama wa kuleta mabadiliko atafungiwa jiwe na kutupwa baharini ili azame na kuwaacha mafisadi wakitesa.
Hao niliowa bold hapo juu ni mafisadi pia kwani ni siri?
 
Nadhani tatizo moja kubwa la CCM ..ingawa mara nyingi wanasema matatizo ya chama inabidi wayaongelee kwenye vikao, ukweli ni kuwa kwenye vikao hakuna jipya ..utatoa hoja au malalamiko hata kama ni genuine yatazimwa kwa kutumia nguvu za mizengwe au hoja za nguvu.....kwa ujumla hawataki na hawakubali mabadiliko au kujitakasa.

Sababu hiyo ndio inawafanya watu wenye hayo madonge moyoni wayazungumze mambo yao nje ya vikao ili umma wote ujue na kuamua nani yuko sawa, ilikuwa hivyo kwa kina Mrema, Kolimba na sasa Nape .....
 
.......wait a minute, hicho kikao cha kumvua wamefanya lini na saa ngapi?


Wapo Dodoma usiku huu mkuu...kumbuka ni NEC ya UVCCM sio Taifa. Pamoja na mambo mengine wanajadili majina ya wagombea ungozi wa UVCCM kuanzia ngazi za mikoa mpaka Taifa.
 
Duh! Hii CCM ndiyo mufilisi kabisa 🙁 Badala ya kumkumbatia Shujaa Nape wameamua kuwakumbatia mafisadi akina Lowassa na mafisadi wa kihindi. Mafisadi wote wa EPA, Richmond, Rada, Ndege ya Rais, Helicopters na magari ya jeshi bado wamekumbatiwa ndani ya chama hicho!! lakini mpambanaji wa mafisadi ndiyo wa kumfukuza!!! Sasa tumepata uthibitisho rasmi kwamba kweli CCM ni Chama Cha Mafisadi na hawastahili kabisa kuwepo madarakani kwa kuwa matatizo yetu mengi Tanzania yanasababishwa na CCM. CCM ni kikwazo kikubwa cha maendeleo ya Tanzania.

CCM sio wote mafisadi bali wameelemewa na mafisadi.

Kila wakati mimi nasema kwamba kama wapinzani wakichukua ikulu basi yale matunda yaliyooza kwenye CCM yote yataondolewa ili yasiambukize wenzao
Na hapo ndio CCM itabakia na watu wazuri.

Mpaka sasa sina msimamo wowote wa chama lakini bila CCM kuondolewa hatutafika popote.
 
Kwa kweli imenisikitisha sana hili suala. mpaka natafakari uanachama wangu CCM. hii indumaza na kudhoofisha nguvu za kichama.

ILA YOTE YANAKUJA KWA KUWA MAKAMBA HANA SHULE NA MSEKWA KAPACHIKWA!!!!

Ingekuwa Malecela hali ingekuwa tofauti! yule bwana ni TREKTA kweli kweli!
Pole sana ndugu yangu. Kwani umri wako ni miaka mingapi? maana mimi miaka kama 25 sasa nilitupa ****** kadi yangu ya ccm kwa sababu ya haya haya. Nashangaa nyinyi mnayaona leo.

Ukitaka kuula ccm wewe uwe wa kujipendekeza kama Masatu na au uwe Yes man Kama Pundamilia.

Lakini ukiwa mchukia mafisadi utapatwa na yanayompata Nape.

Masikini Nape. Pole.
 
Wapo Dodoma usiku huu mkuu...kumbuka ni NEC ya UVCCM sio Taifa. Pamoja na mambo mengine wanajadili majina ya wagombea ungozi wa UVCCM kuanzia ngazi za mikoa mpaka Taifa.

..hivi, uamuzi wa hiyo "nec" hauwezi kuwa vetoed na vikao vya juu?
 
..hivi, uamuzi wa hiyo "nec" hauwezi kuwa vetoed na vikao vya juu?

Unaweza kuwa vetoed na mwenyekiti peke yake, sasa kama Lowassa, Mkamba, Kingunge na Nchimbi wako upande mmoja, the political wisdom inakataa kuwa hawezi,

The history ni only Mkapa could do that! Hata Mwalimu mwenyewe kwenye hili asingeweza.
 
...CCM should and must die la sivyo future imedoda!
 
Unaweza kuwa vetoed na mwenyekiti peke yake, sasa kama Lowassa, Mkamba, Kingunge na Nchimbi wako upande mmoja, the political wisdom inakataa kuwa hawezi,

The history ni only Mkapa could do that! Hata Mwalimu mwenyewe kwenye hili asingeweza.

..kama mkapa aliweza, kwanini nyerere alishindwa?

..my bet is, utakuwa vetoed!
 
Unaweza kuwa vetoed na mwenyekiti peke yake, sasa kama Lowassa, Mkamba, Kingunge na Nchimbi wako upande mmoja, the political wisdom inakataa kuwa hawezi,

The history ni only Mkapa could do that! Hata Mwalimu mwenyewe kwenye hili asingeweza.


Hata huyo unayemuita MWENYEKITI hana tena nguvu ndani ya Chama anachokiongoza.Upole,Uzembe na Uoga wake unamfanya pia nae anakuwa mtu wa kuburuzwa ndani ya Chama....Huyu Bwana mdogo wanamfukuza kabisa Chamani kwa sababu wanayoiita "Utovu wa Nidhamu"..Ama kweli Lowassa ana nguvu za ajabu....
 
CCM sio wote mafisadi bali wameelemewa na mafisadi.

Kila wakati mimi nasema kwamba kama wapinzani wakichukua ikulu basi yale matunda yaliyooza kwenye CCM yote yataondolewa ili yasiambukize wenzao
Na hapo ndio CCM itabakia na watu wazuri.

Mpaka sasa sina msimamo wowote wa chama lakini bila CCM kuondolewa hatutafika popote.

Utaelemewaje na mafisadi kama wewe kama kiongozi wa nchi vyombo vya dola vyote viko chini ya himaya yako. Hata muasisi wa CCM aliwahi kutamka hadharani kwamba CCM kimejaa wahuni na kinawakumbatia matajiri (mafisadi) na leo kama angekuwa hai asingeshindwa kutamka kwamba CCM imejaa mafisadi.

Jeshi, polisi na mahakama vyote viko chini ya himaya yako na wananchi pia wako nyuma yako ili upambane na ufisadi na bado unaelemewa na mafisadi!!! Eti mafisadi ni matajiri wakubwa mno!!! wakikamatwa nchi itawaka moto!!! Wacha nchi iwake moto ili tujue nani zaidi serikali au mafisadi. Come on!!! we know better that that!

Serikali yoyote ile duniani iliyoelemewa na kikundi cha watu wachache wanaojitajirisha kwa njia za haramu haistahili kuwepo madarakani. Kama JK kaelemewa na mafisadi basi ajiuzulu na serikali yake yote na kumpisha kiongozi atakayekuwa na ujasiri wa kupambana na mafisadi uso kwa uso na bila woga.
 
Haya ya nape ni blessing in disguise kwa wapenda mageuzi! Nape unasubiri nini kuihama hiyo CCM! Kajiunge na akina Zitto na wengine. Hao wazee chochote watakachokuambia, watakuwa wanafiki tu! Wewe jina huko limechafuka na haliwezi kusafishika! Maadam wewe ni mwanasiasa, hamia upinzani
 
..kama mkapa aliweza, kwanini nyerere alishindwa?

..my bet is, utakuwa vetoed!

Ikiwa Vetoed wakati Lowassa, Mkamba, Kingunge na Nchimbi wanaiunga mkono eti kwa sababu ya Nape basi tujue CCM ndio imegawanyika na sasa kila mtu na lwake. It will never happen (at least not this decade)..!!
 
Hata huyo unayemuita MWENYEKITI hana tena nguvu ndani ya Chama anachokiongoza.Upole,Uzembe na Uoga wake unamfanya pia nae anakuwa mtu wa kuburuzwa ndani ya Chama....Huyu Bwana mdogo wanamfukuza kabisa Chamani kwa sababu wanayoiita "Utovu wa Nidhamu"..Ama kweli Lowassa ana nguvu za ajabu....


Ni sababu ya Damu ya Kimasai au Damu ya Kifisadi..???!!!
 
Hata huyo unayemuita MWENYEKITI hana tena nguvu ndani ya Chama anachokiongoza.Upole,Uzembe na Uoga wake unamfanya pia nae anakuwa mtu wa kuburuzwa ndani ya Chama....Huyu Bwana mdogo wanamfukuza kabisa Chamani kwa sababu wanayoiita "Utovu wa Nidhamu"..Ama kweli Lowassa ana nguvu za ajabu....

Mkuu Mwawado huyo Mwenyekiti naye pia ni fisadi anajua fika kwamba Urais kaupata kwa kutoa rushwa ya hali ya juu, na hichi ndiyo kinamfanya aogope kuchukua hatua zozote dhidi ya mafisadi. Ndiyo matatizo ya kuingia madarakani kwa njia za haramu. Kama anaona hawezi kutetea maslahi ya Tanzania kwa kuogopa naye kulipuliwa na mafisadi wenzake ni bora aachie ngazi mapema ili kuiepusha Tanzania kuangamia.
 
Utaelemewaje na mafisadi kama wewe kama kiongozi wa nchi vyombo vya dola vyote viko chini ya himaya yako. Hata muasisi wa CCM aliwahi kutamka hadharani kwamba CCM kimejaa wahuni na kinawakumbatia matajiri (mafisadi) na leo kama angekuwa hai asingeshindwa kutamka kwamba CCM imejaa mafisadi.

Jeshi, polisi na mahakama vyote viko chini ya himaya yako na wananchi pia wako nyuma yako ili upambane na ufisadi na bado unaelemewa na mafisadi!!! Eti mafisadi ni matajiri wakubwa mno!!! wakikamatwa nchi itawaka moto!!! Wacha nchi iwake moto ili tujue nani zaidi serikali au mafisadi. Come on!!! we know better that that!

Serikali yoyote ile duniani iliyoelemewa na kikundi cha watu wachache wanaojitajirisha kwa njia za haramu haistahili kuwepo madarakani. Kama JK kaelemewa na mafisadi basi ajiuzulu na serikali yake yote na kumpisha kiongozi atakayekuwa na ujasiri wa kupambana na mafisadi uso kwa uso na bila woga.

CCm sio fisadi ila bahati mbaya wananchi walichagua viongozi wa juu kabisa wachache ambao ni mafisadi.
 
Sasa inakuwaje hata Mwenyekiti wa CCM JK naye akubaliane na Nape kuwa mkataba haukuwa na maslahi kwa UVCCM lakini bado NEC ya UVCCM wampe adhabu hiyo...ina maana Lowassa, Makamba, Kingunge, Nchimbi na Kawawa hawakubaliani na Mwenyekiti JK??
 
Utaelemewaje na mafisadi kama wewe kama kiongozi wa nchi vyombo vya dola vyote viko chini ya himaya yako. Hata muasisi wa CCM aliwahi kutamka hadharani kwamba CCM kimejaa wahuni na kinawakumbatia matajiri (mafisadi) na leo kama angekuwa hai asingeshindwa kutamka kwamba CCM imejaa mafisadi.

Jeshi, polisi na mahakama vyote viko chini ya himaya yako na wananchi pia wako nyuma yako ili upambane na ufisadi na bado unaelemewa na mafisadi!!! Eti mafisadi ni matajiri wakubwa mno!!! wakikamatwa nchi itawaka moto!!! Wacha nchi iwake moto ili tujue nani zaidi serikali au mafisadi. Come on!!! we know better that that!

Serikali yoyote ile duniani iliyoelemewa na kikundi cha watu wachache wanaojitajirisha kwa njia za haramu haistahili kuwepo madarakani. Kama JK kaelemewa na mafisadi basi ajiuzulu na serikali yake yote na kumpisha kiongozi atakayekuwa na ujasiri wa kupambana na mafisadi uso kwa uso na bila woga.

Ukishasema kiongozi umerudi pale pale kwenye sentensi yangu kwamba CCM Imeelemewa na mafisadi na sio wote mafisadi.

Angalia sentensi yako:

Duh! Hii CCM ndiyo mufilisi kabisa 🙁 Badala ya kumkumbatia Shujaa Nape wameamua kuwakumbatia mafisadi akina Lowassa na mafisadi wa kihindi.
 
Mkuu Mwawado huyo Mwenyekiti naye pia ni fisadi anajua fika kwamba Urais kaupata kwa kutoa rushwa ya hali ya juu, na hichi ndiyo kinamfanya aogope kuchukua hatua zozote dhidi ya mafisadi. Ndiyo matatizo ya kuingia madarakani kwa njia za haramu. Kama anaona hawezi kutetea maslahi ya Tanzania kwa kuogopa naye kulipuliwa na mafisadi wenzake ni bora aachie ngazi mapema ili kuiepusha Tanzania kuangamia.


kwani ni akina nani NYERERE aliwakataa 1995 mwenye kumbu kumbu atupe.
 
Back
Top Bottom