Kama vikao vinaendeshwa kwa ubabe namna hiyo, hapo ndio unaweza kusema kwamba utatumia vikao halali vya Chama ama Jumuiya kukosoa uongozi wa Chama ama Jumuiya?
Hivi mwanachama wa UVCCM anaweza kuvuliwa uanachama kwa pendekezo la mtu mmoja na Mwenyekiti akafanya maamuzi kwamba imepitishwa? Hiyo ni demokrasia?
Kama kanuni za UVCCM zina kigezo cha umri, kwanini mtu ahangaike kupoteza muda wa kumjadili mtu ambaye hana sifa inayotakiwa? Kwa mfano kama kigezo cha mtu kugombea urais ni miaka 40, halafu atokee mtu mwenye umri wa miaka 38 akagombea, kweli watu wanaweza kupoteza muda wao kukaa wanamjadili mtu ambaye hana sifa?
Kwanini Nape anawanyima usingizi wakati wanadai kwamba kigezo cha umri kinamtupa nje ya kinyang'anyiro? Kwanini waendelee kum-discuss mtu ambaye kanuni za Jumuiya yao zinamtupa nje?
Kama habari hiyo hapo juu ina ukweli kwa yale yaliyoandikwa, basi UVCCM na uongozi mzima una matatizo na hilo ni tatizo la ugonjwa unaoitwa ufisadi.
Kansa ya Ufisadi haitakuja kuondoka ndani ya CCM mpaka watokee wapiganaji wenye balls za kuwakemea wakubwa/viongozi kwa kuwaambia waache ufisadi na hilo ndiyo alilolifanya Nape na sasa naona vigogo wenye chama chao wameanza kumkoromea kwamba anawavua nguo. Sasa akaongelee kwenye kikao kipi wakati viongozi wa vikao vyote ni mafisadi.
Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini ni Lowassa (fisadi), Mwenyekiti wa kamati ya maadili ya CC ni Bwana Chenge nae pia ni fisadi. Kaimu Kamanda wa UVCCM ni Mzee Kingunge nae ni fisadi mzuri tu. Katibu Mkuu wa CCM ni mpambe wa mafisadi na mwana mtandao mzuri sana. Ukipanda juu kwa JK ndio huyo ambaye anawakwepa kuwashughulikia maswahiba zake. Hivi kweli hapo tutegemee mabadiliko kwenye uongozi wa Jumuiya za CCM? Maana akitokea mwanachama wa kuleta mabadiliko atafungiwa jiwe na kutupwa baharini ili azame na kuwaacha mafisadi wakitesa.
Hivi mwanachama wa UVCCM anaweza kuvuliwa uanachama kwa pendekezo la mtu mmoja na Mwenyekiti akafanya maamuzi kwamba imepitishwa? Hiyo ni demokrasia?
Kama kanuni za UVCCM zina kigezo cha umri, kwanini mtu ahangaike kupoteza muda wa kumjadili mtu ambaye hana sifa inayotakiwa? Kwa mfano kama kigezo cha mtu kugombea urais ni miaka 40, halafu atokee mtu mwenye umri wa miaka 38 akagombea, kweli watu wanaweza kupoteza muda wao kukaa wanamjadili mtu ambaye hana sifa?
Kwanini Nape anawanyima usingizi wakati wanadai kwamba kigezo cha umri kinamtupa nje ya kinyang'anyiro? Kwanini waendelee kum-discuss mtu ambaye kanuni za Jumuiya yao zinamtupa nje?
Kama habari hiyo hapo juu ina ukweli kwa yale yaliyoandikwa, basi UVCCM na uongozi mzima una matatizo na hilo ni tatizo la ugonjwa unaoitwa ufisadi.
Kansa ya Ufisadi haitakuja kuondoka ndani ya CCM mpaka watokee wapiganaji wenye balls za kuwakemea wakubwa/viongozi kwa kuwaambia waache ufisadi na hilo ndiyo alilolifanya Nape na sasa naona vigogo wenye chama chao wameanza kumkoromea kwamba anawavua nguo. Sasa akaongelee kwenye kikao kipi wakati viongozi wa vikao vyote ni mafisadi.
Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini ni Lowassa (fisadi), Mwenyekiti wa kamati ya maadili ya CC ni Bwana Chenge nae pia ni fisadi. Kaimu Kamanda wa UVCCM ni Mzee Kingunge nae ni fisadi mzuri tu. Katibu Mkuu wa CCM ni mpambe wa mafisadi na mwana mtandao mzuri sana. Ukipanda juu kwa JK ndio huyo ambaye anawakwepa kuwashughulikia maswahiba zake. Hivi kweli hapo tutegemee mabadiliko kwenye uongozi wa Jumuiya za CCM? Maana akitokea mwanachama wa kuleta mabadiliko atafungiwa jiwe na kutupwa baharini ili azame na kuwaacha mafisadi wakitesa.