Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Hapana tunachotafuta hapa ni haki na ukweli, kwangu ukweli ni kwamba Nape atakuwa mwenda wazimu kwenda kuchukua fomu ya uongozi wa chama cha taifa, ambacho anajua kabisa kuwa hatimizi masharti yake, au akiamini kuwa eti ana nguvu ya kumsukuma kuweza kubadili sheria hai za UV-CCM, ili aweze kugombea that is insane na ninaamini kuwa that is not the ishu here,

The ishu haiko clear, kwa sababu ingekuwa clear wala hakutakiwi kuwa na even mjadala, the fact kwamba hata kuna mjadala tena wa pembeni lakini sio official ndani ya UV-CCM as it should, maana yake ni kwamba kuna mtu huko UV-CCM, anataka kufanya uhuni,

We have had Enough of it, sheria ni msumeno Nape amepitisha umri wa kugombea then why even discuss him mpaka kumpa E? Wewe Mtanzania ni mwenyekiti wa UV-CCM, leo unaletewa fomu ya mtu aliepitisha umri wa sheria za chama chako, eti unamjadili mpaka kumpa E ya uongozi? Is that so?

Mimi nilifikiri kuwa fomu yake inatupwa kwenye garbage bin, ndio iliyokuwa tabia ya Mwalimu, kuna wapuuuzi waliokuwa wakijaribu kugombea uongozi, alikuwa akichukua fomu zao na kutupa kwenye uchafu, bila kelele wala kuwajadili kwenye vikao, sasa hapa UV-CCM kilichoshindikana ni nini hasa kama sio kuna uhuni na not even worthy kuujadili hapa JF!

Tunazungumza haki na sio kwamba tunajali jina la mtu au kiongozi kuliko sheria, tunasema haki itendeke, that is all!
Unajua kama kweli unataka kumsaidia nape unaweza kwa kumwambia ukweli aseme nini anchojua kuhusu kanuni ya umri,kanuni hii ilipitishwa na ccm kupitia kamati kuu na nec mwaka 2003. Baraza kuu la kwanza likasemakuhutubiwa na jk la uvccm akafafanua kwamba sababu ya kufanya hivyo ni kuhakikisha kuwa mgombea anamaliza muda wa uongozi akiwa bado ni kijana.mfano ni kweli mtu wa miaka34 ni kijana,lakini akigombea leo atamaliza na miaka 39.

Haitokuwa sawa wala haki kwa vijana. Sasa nape hajapewa E kwa sababu ni kiongozi hasiefaa bali alama E anapewa mtu yeyote ambae ameomba na hajatimiza sifa za msingi za nafasi husika,alama E inapotolewa ndani ya vikao vya ccm unapaswa na kuandika sababu.sasa watu wote humu hamwadiki sababu iliowekwa ya E...unasema walipaswa kutupa fomu yake...huo sio utaratibu wa ccm,utaratibu ni watu wote kujadiliwa mpaka kikao cha mwisho cha maamuzi,wanachoweka ni alama tu....

Nape anayajua yote hayo ndio maana aliamua kutoka na issue ya jengo ili akikatwa ionekane ni sababu hio..watu kama Nape ambao vichwa vyao havijatulia kimipango ndio wanampaga nchimbi ulahisi wa kuwamaliza...Sasa atamshinda kama mtoto mdogo kwa kuwa toka katika uchaguzi wa kata watu wote wa umri wa Nape wamekatwa majina,sasa unakujaje kubadili kanuni kwenye ngazi ya taifa???

Wafundisheni watu mnaowapenda kuzingatia sheria na kanuni,afrika tunapenda sheria zitungwe kwa kufata matakwa yetu.
 
Lakini hiyo variance ya umri atakapo kuwa anamaliza muda wake ni ndogo saana kuleta malumbano, tena issue yenyewe ni kwamba kipindi chake kikiwa kinaisha in 5 years time , so nealy 905 ya tenure yake atakuwa kijana, kama atachaguliwa. So hapa sioni kama ni issue.
 
1.
Unajua kama kweli unataka kumsaidia nape unaweza kwa kumwambia ukweli aseme nini anchojua kuhusu kanuni ya umri,kanuni hii ilipitishwa na ccm kupitia kamati kuu na nec mwaka 2003.baraza kuu la kwanza likasemakuhutubiwa na jk la uvccm akafafanua kwamba sababu ya kufanya hivyo ni kuhakikisha kuwa mgombea anamaliza muda wa uongozi akiwa bado ni kijana.mfano ni kweli mtu wa miaka34 ni kijana,lakini akigombea leo atamaliza na miaka 39.haitokuwa sawa wala haki kwa vijana.

1. Mkuu mimi sipo hapa kumsaidia mwananchi yoyote kutafuta uongozi kwa njia isiyo halali, ila nipo hapa kutafuta ukweli unaolihusu taifa langu, Nape na Nchimbi ni small picture kwangu, the big picture ni taifa langu.

2. Umri wa kiongozi wa UV-CCM, sio the ishu hapa kwenye UV-CCM, the ishu ni kama mtandao bado una nguvu au hauna tena, that to me is the bottm line, sheria za chama chochote duniani hazihallalishwi au kupitishwa na hotuba ya rais, kama ni kweli CC ingekua imewahi kupitisha hiyo sheria kusingekua na ishu hapa, ninajua mara nyingi sana ambapo CC knowing kuwa the ishu mbele yao ni ujinga kama hii unavyosema, hukataa kabisa kuzigusa ishu namna hii sasa iweje waikubali hii ya umri wa Nape, huku wakijua kuwa ni wao waliopitisha sheria hiyo mwaka 2003 kama ulivyosema na Kikwete alihalalisha? wewe huoni kuwa kuna utata hapo na kauli zako mwenyewe

- Kuna ishu kwa sababu kuna mtu anataka kupindisha ukweli, anaweza kuwa Nape au Nchimbi, mimi kwangu mwenye problem hapa ni Nchimbi mwenyekiti wa sasa wa UV-CCM, kwa sababu sheria ya US inasema ni lazima uwe a US citizen ili kugombea urais, Gavana wa Carlifornia mkuu Arnold amekwama hapo, amejaribu kila njia lakini jibu ni no, sio kuchukua fomu na kupewa E, nonesense!,

-Kama hutimizi masharti ya chama huwezi kugombea na wala hakuna mwanachama wa kile chama atakayepoteza muda wake kukujadili na kukupa E, na wala huwezi kuruhusiwa kuchukua fomu ya kugombea, hata ukijaza hakuna atakayekujibu, wewe unajua kuwa that is not the case hapa! WHY?


2.
Sasa nape hajapewa E kwa sababu ni kiongozi hasiefaa bali alama E anapewa mtu yeyote ambae ameomba na hajatimiza sifa za msingi za nafasi husika,alama E inapotolewa ndani ya vikao vya ccm unapaswa na kuandika sababu.sasa watu wote humu hamwadiki sababu iliowekwa ya E...unasema walipaswa kutupa fomu yake...huo sio utaratibu wa ccm,utaratibu ni watu wote kujadiliwa mpaka kikao cha mwisho cha maamuzi,wanachoweka ni alama tu....

1. Hii ni mara yangu ya kwanza toka nimeijua CCM na matawi yake kwa mwanachama kupewa eti alama ya E, what is it? Halafu yeye Nchimbi anapewa alama gani?

2. Mkuu naomba history kidogo ni kiongozi gani mwingine wa CCM, aliyewahi kupewa E, na lini hiyo? Mimi ninajua CCM enzi za Mwalimu, alikuwa anatupa tu fomu yako kama hutimizi masharti, au akikuheshimu sana basi anasema wazi kuwa amekutoa au kamati imekutoa kwa sababu one, two, and three!

- Mifano ipo chungu nzima, mtu kama Shibuda aliwahi kuchukua fomu mara nyingi sana enzi za Mwalimu, lakini uliwahi kusikia hata akitajwa? Kina Jumbe, Seif, Seif Bakari, si waliitwa CC na kufukuzwa, eti walipewa alama ya
E?

3. Ni wapi hapo ambapo sababu zimetolewa za Nape kupewa E, kilichomshinda Nchimbi na kamati yake kumwambia ukweli Nape kama wanao kuwa umepita umri kwa hiyo forget it, I mean sheria ni sheria kwa nini wameota kigugumizi kwenye hilo, badala yake Nchimbi anakwenda kwenye vijiwe na kuanzisha haya majungu kuwa eti Nape tutamtoa tu amepitisha umri, what a joker?

- Halafu bila aibu unajaribu ku-spin uongo hapa kuwa eti alama ya E ndani ya CCM hupewa mwananchi asiyetimiza masharti ya umri toka lini hiyo mkuu? CCM haijadili wananchi wote hata siku moja hujadili wale tu wenye kukingiwa ubavu na makundi yao, ndani ya uongozi wa juu wa CCM, majina chungu mzima hutumwa na huwa hayarudi wala hayaguswi,

kwa mfano Rita mlaki na Mama Ntimizi, walishindwa uchaguzi wa unbunge uliopita, lakini wakapitishwa anyways, bila ya alama ya E wala C, au A kwa walioonewa kwa hiyo hoja eti CCM hujadili kila mwaanchi huenda ni kweli, lakini huwa sio lazima ijibu alama ya E, Mbunge Nyimbo alipofukuzwa CCM haikuwa kwa sababu amepewa alama ya E kwanza!


3
. Nape anayajua yote hayo ndio maana aliamua kutoka na issue ya jengo ili akikatwa ionekane ni sababu hio..watu kama Nape ambao vichwa vyao havijatulia kimipango ndio wanampaga nchimbi ulahisi wa kuwamaliza...Sasa atamshinda kama mtoto mdogo kwa kuwa toka katika uchaguzi wa kata watu wote wa umri wa Nape wamekatwa majina,sasa unakujaje kubadili kanuni kwenye ngazi ya taifa???wafundisheni watu mnaowapenda kuzingatia sheria na kanuni,afrika tunapenda sheria zitungwe kwa kufata matakwa yetu.

1. Hayo ya kumpenda Nape, naona ni yako kwa sababu unampenda Nchimbi, unafikiri sisi wote hapa tuna hiyo tabia, hapana mkuu tunajali ukweli na haki, hoja. Halafu unajua wazi kuwa huwa ninajiepusha sana na ishu zako na Nape na Nchimbi, ni mpaka this time ndio nilipoamua kuku-challenge kwa sababu naona umefikia mahali unaamini kuwa unaweza kututisha na matusi yako ya nguoni na kubadili majina tukaogopa kusema ukweli kuhusu rafiki yako Nchimbi, now you know better kuwa hapa hatuogopi mtu wala sura ila tunaheshimu na kukata hoja!

2. Ishu ya jengo haihusiki na anything to do na umri wa Nape, mkataba wa jengo tuliouleta hapa haukusema anything kwamba umri wa Nape ndio uliowafanya Nchimbi na Lowassa na wengine kuifisadi Uv-CCM, Masilingi alipolalamika kuwa hahusiki na mkataba mbuzi kama huo, hakusema kuwa chanzo chake ni Nape na umri wake.

3. Nape ni mjumbe wa NEC tena wa kuchaguliwa na wanachama wa CCM, the ishu sio Nape kumshinda Nchimbi kama unavyolizmisha maana unajua kuwa huwezi kusimama kwenye debate ya hoja, kwa hiyo ni lazima ujaribu kulazimisha u-yanga na simba type of debate, that is not the ishu here,

- Hapa ni incompetence ya uongozi wa Nchimbi at the display, ubinafsi na uchoyo unajua kuna umasikini wa aina nyingi sana kwenye maisha, wote sisi ni masikini lakini huwa tunajaribu kuu-control umasikini wetu, kwa sababu ukiuuruhusu ukaingia mpaka kichwani matokeo yake ndio haya, hutaki mwingine achukue nafasi kwa ajili ya maendeleo ya wananchi na taifa maana sasa unaamini kuwa ile nafasi ni mali yako, halafu the sad thing ni unapata wengine wenye akili kama yako wanaoweza kukushangilia,

Waziri mzima unaenda mpaka kwenye public kulila kuwa huwezi kukubali nafasi hiyo achukue usiyemtaka, what a shame? Toka shule ya msingi jamaa alifeli, mpaka leo bado anafeli tu, pamoja na kutumia nguvu kupata vyeo lakini bado record hakuna ila ufisadi tu, unatuambia kua Nchimbi ni best thing kwa taifa letu, kiongozi mwenye uwezo mkubwa kama unavyodai anaweza kutolewa kamasi namna hii na bwana mdogo kama Nape, mpaka kufikishana CC?

Mkuu sisi tunasimamia mabadiliko ya taifa, hatujali nani anayapigia kelele mabadiliko haya, hata Nchimbi akibadilika leo akasimamia mabadiliko tutampa support, it does not matter kama Nape, atashidna au hatashinda, lakini tunachothamini ni kwamba amefikisha ujumbe na bado Nape kijana mdogo ana nafasi kubw ana zipo nyingi sana kwenye taifa letu, na wewe unajua kua ana ofisi pale Lumumba, HQ ya CCM huyu Nape kama Obama ni agent of change, kwa hiyo tunasimama na his message, regardless ya his or her personality au jina! Ni taifa mbele kwanza!

Ahsante Mkuu!
 
Karibu Kamati kuu CC wataka mzizi wa fitna, tutajua pumba na mchele. Stay tuned!
 
Karibu Kamati kuu CC wataka mzizi wa fitna, tutajua pumba na mchele. Stay tuned!


1. Kikao kilishanza tayari, according to the dataz kulikuwa na agenda 19, muungwana akachagua agenda mbili kwanza ambazo hazihusiani kabisa na UV-CCM.

2. Suala la umri wa Nape, halitaguswa na hiki kikao kwa sababu kuna vikao vingi sana vya UV-CCM vinatakiwa kukutana kabla ya kulipeleka kwenye CC, kwa hiyo the dataz ni kwamba hiki kikao hakiligusa hilo kwa sababu bado halijaenda huko!

3. CC italigusa sana tena sana la Jengo, Mwenyekiti wa CCM, aliagiza watafutwe mawakili wa binafsi, wa serikali, na wa CCM yenyewe na kuuangalia tena huo mkataba, wote wametoa kauli moja nayo ni kwamba mktaba ni bomu la kutupwa!

4. Wadhamini wote wa UV-CCM, kuanzia Masilingi, Lukuvi, na Mary Nagu wamewakana Nchimbi na Lowassa, kwamba hawakuhusika na kuupitisha huu mkataba, meaning kwamba Nape was telling the truth!

5. In desparation mood, Lowassa na wenziwe leo wamenunua magazeti flani katika kujaribu kupotosha kinachoendelea huko ndani ya CC, lakini ukweli unafahamika kuwa wako ukutani!

Tutaendelea kuhabarishana, tunachotaka ni ukweli tu na haki, huku taifa letu likiwa mbele na sio jina la mtu wala kiongozi!

Ahsante Wakuu!
 
Mkuu FMES,

Naona umeamua kumtolea uvivu huyo huyo mkuu.Kwa kweli sijaona cha kuongeza.Heshima Mbele nawe!
 
wadau hebu tuhabarishane,hivi ni kweli kuwa CC imemchinjia Nape baharini na kubariki mkataba wa jengo la UVCCM?
 
Naona umeamua kumtolea uvivu huyo huyo mkuu.Kwa kweli sijaona cha kuongeza.Heshima Mbele nawe!

Mkuu heshima ikurudie, tunatafuta ukweli na haki hatupendi kupotoshwa, nothing personal ila taifa letu tu ndio mbele!
 
Lowassa, Nape wawekwa kiporo

na Mwandishi Wetu
Tanzania Daima~Sauti ya Watu


KIKAO cha Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CC), kimeweka kiporo baadhi ya ajenda zake nyeti, ikiwamo ile inayogusia suala lenye utata la mradi wa ujenzi wa jengo la Makao Makuu ya Umoja wake wa Vijana (UVCCM), ambalo linatishia umoja na mshikamano miongoni mwa viongozi wa CCM.

Hoja ya mradi huo, iliyoibuliwa na mwanasiasa chipukizi ndani ya UVCCM, Nape Nnauye, anayewatuhumu Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini la UVCCM, Edward Lowassa, Mwenyekiti wa umoja huo anayemaliza muda wake, Dk. Emmanuel Nchimbi na Katibu Mkuu wa jumuiya hiyo, Francis Isaac, kwa kuiingiza jumuiya yao katika mradi usio na tija wala masilahi kwao.

Habari ambazo Tanzania Daima imezipata kutoka ndani ya kikao hicho cha CC kilichokutana juzi zinaeleza kwamba, suala hilo sasa linatarajiwa kujadiliwa Jumanne ijayo na uamuzi kuhusu mradi huo mzima utafikiwa kabla ya mapendekezo ya Kamati Kuu kupelekwa katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho tawala (NEC), kwa maamuzi siku hiyo hiyo.

Suala hilo la ujenzi litajadiliwa kwa kupitia mapendekezo yaliyotolewa na timu ya wanasheria wa chama hicho ambao walipewa kazi ya kuvipitia upya vipengele vyote vilivyo katika mkataba huo ambavyo vimekuwa vikilalamikia na wana UVCCM kadhaa, akiwamo Nape.

Taarifa kutoka ndani ya CC hiyo zinaeleza kuwa, ajenda nyingine muhimu ambayo iliwekwa kiporo juzi ni ya kupitia majina ya wanaowania uongozi ndani ya jumuiya za chama hicho, ambapo sasa ajenda hiyo itajadaliwa Jumanne ijayo mjini Dodoma, kabla ya maamuzi kufikiwa ndani ya NEC.

Hata hivyo, kabla ya vikao vya CC na NEC, havijakabidhiwa majina ya wanaowania nafasi za uongozi, Baraza Kuu la UVCCM, linatarajia kupitia majina hayo katika kikao chao kitakachofanyika Jumapili wiki hii kutokana na kile ambacho kimeelezwa na baadhi ya wajumbe hao kuwa ni uamuzi wa kushinikizwa.

Uamuzi wa kufanyika kwa kikao hicho cha Baraza Kuu la UVCCM unakuja baada ya kuwapo kwa taarifa za awali zilizokuwa zikidai kwamba, kilikwama kufanyika mapema kwa madai kwamba umoja huo ulikuwa umekwama kifedha.

Mbali ya Nape, waombaji wengine katika uchaguzi huo wa UVCCM unaoendelea kuvuta hisia za watu kila kukicha ni Benno Malisa, Zainab Kawawa, Mohammed Bashe, Said Mtanda na Suleiman Muhsein, Jerry Slaa, Hamad Masauni, Issa Haji Ussi, Anthony Mtaka, Said Mtanda, Haule Pangisa, Samuel Marero, Stephen Deya, Geofrey Mwankenja, David Manoti, Mussa Mnyeti, Edson Lubua, Mwamini Lusingu, Asmah Kalokola, Marco Zablon Allute, Harold Adamson, Adila Hilal Vuai, Ashura Ismail, Rashid Masalaka na Raha Ahamada.

Wanaowania uteuzi wa nafasi ya makamu mwenyekiti ni Happy Mahava, Raha Ahamada Ally, Riziki Pembe Juma, Michael Bundala, Rabia Hamid Shaka, Nuru Mohammed Ahamed na Twaha Ally Muhaji.

Vyanzo vyetu vya habari kutoka ndani ya kikao cha Kamati Kuu, kilichokuwa chini ya Uenyekiti wa Rais Jakaya Kikwete, zilisema kuwa CC ilishindwa kumaliza ajenda zake kutokana na sababu mbili, mosi ni muda mwingi uliotumika kujadili suala la hadhi ya Zanzibar na kasoro za Muungano.

Vyanzo vyetu vya habari ndani ya kikao hicho, zilisema hoja hiyo ilitumia muda mwingi kutokana na mgawanyiko wa kimitazamo kutoka kwa wajumbe.

Sababu nyingine ya kutomalizika kwa ajenda 19 za kikao hicho, inaelezwa kwamba ilitokana na ugeni wa Rais wa Chama tawala cha ANC cha Afrika Kusini, Jacob Zuma, ambaye alikuwa na mazungumzo na Rais Kikwete.

"Kwa hiyo ajenda zingine hazijaguswa kabisa na kikao kimeahirishwa na sasa kitafanyika mjini Dodoma Septemba 9, kabla ya kikao cha Halmashauri Kuu (NEC), kinachotarajiwa kufanyika Septemba 9 hadi 10 mwaka huu," alisema mmoja wa wajumbe wa kikao hicho.

Kwa mujibu wa habari hizo zilizothibitishwa na wajumbe wengine tofauti, ajenda ya mradi wa jengo haikupata nafasi kabisa ya kujadiliwa licha ya shauku ya baadhi ya wajumbe kutaka ijadiliwe ili kubaini ukweli wa tuhuma dhidi ya Lowassa, Dk. Nchimbi pamoja na viongozi wengine ndani ya jumuiya hiyo.

Akizungumza na Tanzania Daima jana kwa njia ya simu, Katibu Mkuu wa CCM, Yussuf Makamba, alithibitisha kuwa kikao hicho hakikumaliza ajenda zake na kwamba kitaendelea tena mjini Dodoma.

"Siwezi kutoa maazimio ya CC jana, kwa sababu kikao bado kinaendelea, ila hatujajadili jina la Nape, kwa sababu kikao hicho ni kikubwa na cha kitaifa, hivyo hakiwezi kujadili jina la mtu," alisema Makamba bila kuingia kwa undani wa ajenda zilizojadiliwa.

Kwa hatua hiyo basi, suala la mkataba wa mradi huo ambao katika siku za hivi karibuni umezua maneno mengi ndani ya chama hicho tawala, litajadiliwa mjini Dodoma kabla ya suala hilo kupelekwa kwenye kikao hicho kupata baraka za NEC.

Nape ambaye ni mtoto wa aliyekuwa mwanasaiasa wa siku nyingi, Moses Nnauye, kwa mara ya kwanza alitoa hoja ya utata wa mradi huo, saa chache tu baada ya kuchukua fomu za kugombea nafasi hiyo inayompa fursa mshindi kuwa mjumbe wa vikao vya kimaaamuzi vyenye nguvu kubwa ndani ya chama hicho tawala, Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC).

Katika madai yake, Nape alimshutumu moja kwa moja Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa umoja huo, Edward Lowassa na viongozi wengine wa juu wa UVCCM kwa kuingia katika mkataba huo ambao alisema hauna masilahi yoyote ya maana kwa umoja huo.

Tangu Nape atoe tuhuma hizo, hali ya mambo ndani ya CCM na hususan katika UVCCM imekuwa ni ya vuta nikuvute, ikiwagawa viongozi waandamizi ndani ya chama hicho tawala katika makundi mawili.

Kundi la kwanza ni lile linalomuunga mkono Nape likijumuisha wakongwe kadhaa wa siasa za CCM (majina tunayo) ambao wanakiona kitendo cha mwanasiasa huyo kijana kuwa ni cha kijasiri na ambacho kinapaswa kuungwa mkono na kila mwanachama wa chama hicho.

Miongoni mwa watu wanaomuunga mkono Nape katika siku za hivi karibuni wanadaiwa kuwa wamekuwa wakifanya kila linalowezekana ili kuhakikisha kwamba; ‘kijana wao' huyo anashinda uteuzi wa uenyekiti wa UVCCM kwa gharama zozote.

Kundi la pili katika msigano huo ni lile linalomuunga mkono Lowassa, likiwajumuisha wanasiasa kama Makamba, ambao wamekuwa wakimtaja Nape kuwa kijana anayejaribu kujenga hoja ili kujihalalishia ushindi kwa gharama zozote zile.

Habari kutokana ndani ya CCM zinaeleza kuwa, wanasiasa wanaounda kundi hili ambalo linamuungamo mkono Lowassa na Nchimbi wameshaanza kupanga mikakati ya kuhakikisha wanamuengua Nape katika mchuano huo, wakitumia hoja mbalimbali, zikiwamo zile wa umri wake kuzidi miaka inayotakiwa kwa mtu kugombea nafasi hiyo.

Wana CCM walio katika kundi hilo ambao baadhi yao wamepata kufanya mahojiano na Tanzania Daima kwa nyakati tofauti, wamekuwa wakimuelezea Nape kuwa mwanasiasa mzushi na mtu anayetumiwa na kundi la wazee kadhaa wa ndani ya chama hicho wenye lengo la kuhakikisha wanawaengua watu wote walio karibu kisiasa na Rais Jakaya Kikwete ambaye ndiye atakayekuwa mwenyekiti katika mchakato huu wa leo.

Katika hoja zake, Nape amenukuliwa akisema kwamba, mkataba huo ulipitishwa kinyemela hata kabla haujafikishwa kwenye vikao vya juu vya CCM kwa maana ya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu (NEC) ya chama hicho ili kupata baraka za mwisho.

Vipengele vingine ambavyo Nape analalamikia ni kuhusu uhai wake kwani kinasema mwekezaji ataendesha mradi huo milele huku jumuiya hiyo ikipata asilimia 25 na mwekezaji asilimia 75.

Kasoro nyingine anazozitaja Nape katika tuhuma hizo ni pamoja na ile ya kukiukwa Sheria ya Ardhi (kiwanja), kuhamishwa kwa wabia kabla ya shughuli yoyote ya ujenzi kuanza.

Utaratibu ni kwamba, kabla hatua hiyo haijachukuliwa, sharti Kabidhi Wasihi Mkuu wa Serikali, atoe kibali kwa ajili ya uhamisho wa aina hiyo.

Mkataba wa mradi huo unaosomeka kwa kichwa kisemacho ‘Development Agreement', ulisainiwa Januari 2 mwaka 2007 kati ya UVCCM na makampuni mawili ya M.M. Integrated Steel Mills (MMISML) na Estim Construction Company Limited (ECCL).

Mkataba huo pia hauelezi kiasi cha uwekezaji kutoka kwa wabia ambacho kinaweza kutumika kuelezea mgawo wa asilimia 25 ambayo inadaiwa UVCCM, watachukua.

Aidha, mkataba huo hauna ufafanuzi wa matumizi na mapato hatua kwa hatua, jambo ambalo linaonyesha kutokuwa makini au kuashiria ghiliba katika mahusiano ya wabia.

Vilevile mkataba hauelezi iwapo ubia ni wa miliki ya pamoja au itaundwa kampuni tofauti ya kuendesha kitega uchumi.
 
Ni chama cha mafisadi tu ambacho kinahitaji wanasheria kuupitia mkataba ambao UVCCM inapata 25% tu ya mapato, title deed ya Kiwanja cha jengo la UVCCM kubadilishwa na kuwa kwenye jina la mhindi ili akaombee mkopo bank na mhindi huyo kuwa mwenye final say bila kuingiliwa na yeyote kuhusu biashara zitakazofanyika katika jengo hilo. Mimi si mwanasheria lakini nilipoona baadhi ya vipengele katika mkataba huo nilijua hauna maslahi kwa UVCCM. Kweli CCM ni mafisadi na wasanii wa hali ya juu!
 
Wakuu yamekuwa yakizungumzwa mengi hapa naomba kutoa yafuatayo:

1. Hoja ya jengo hata Nape mwenyewe ameshakana mara nyingi sana kwamba sio agenda ya uchaguzi na akatoa mifano mizuri sana kuonyesha sio ajenda...namnukuu...'Hivi unawezaje kumwambia kijana wa KAaragwe hoja ya jengo la DSM eti ikawa ndo hoja ya kuombea kura badala ya kuzungumza mambo yanayomuhusu yeye katika mazingira yake!!!!!!!!!!!!!'

2.Swala la umri, mnaomtetea Nchimbi nadhani hamuelewi mlitendalo...hapa hoja ni kwamba kanuni inataka anapomaliza uongozi awe si zaidi ya miaka 35..sasa Nape tarehe 07.11.2013 ndo anamaliza miaka yake 35 anaanza mwaka wa 36, mwaka 2013 ni mwaka wa uchaguzi hivyo ndio mwaka wa ukomo wa uongozi utakaoingia hivi sasa, sasa mgogoro wa Nape ki umri unatoka wapi?

3.Mwanawasa kafa kabla ya siku 23 kufikisha miaka 60 dunia nzima inasema kafa na miaka59, haya makadirio ya Nchimbi na vibaraka wake wanayafanya kwa utaratibu upi? Hivi ni kweli hamjui kuwa tunahesabu miaka na sio miezi katika umri?

4.Uchaguzi ni mchakato,hivi kweli mchakato ni siku moja tu ya kupiga kura?Mchakato unaanza lini? si pale mtu anapochukua fomu ya kuomba uteuzi?
 
Angalia sasa nchimbi kapika stori ya nipashe jana kampa kibaraka wake msaki, masikini kachapa gazeti kamati kuu haikufikia ajenda wameambuklia aibu kubwa mungu kawaumbua waliyotaka kumfanyia kijana nape, shame on you nchimbi na wapambe wako woteeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee
 
Angalia sasa nchimbi kapika stori ya nipashe jana kampa kibaraka wake msaki, masikini kachapa gazeti kamati kuu haikufikia ajenda wameambuklia aibu kubwa mungu kawaumbua waliyotaka kumfanyia kijana nape, shame on you nchimbi na wapambe wako woteeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee

Really? Duh very interesting!
 
Ni chama cha mafisadi tu ambacho kinahitaji wanasheria kuupitia mkataba ambao UVCCM inapata 25% tu ya mapato, title deed ya Kiwanja cha jengo la UVCCM kubadilishwa na kuwa kwenye jina la mhindi ili akaombee mkopo bank na mhindi huyo kuwa mwenye final say bila kuingiliwa na yeyote kuhusu biashara zitakazofanyika katika jengo hilo. Mimi si mwanasheria lakini nilipoona baadhi ya vipengele katika mkataba huo nilijua hauna maslahi kwa UVCCM. Kweli CCM ni mafisadi na wasanii wa hali ya juu!

BUBU, tunafahamu mengi sana na tunasema negi sana kuhusu nchi yetu inavyohujumiwa, cha kusikitisha ni kuwa kila kitu bado kiko vilevile wezi wanaendelea kutanua na wanyonge wanaendelea kuwa wanyonge, mikataba ya wizi bado inaendelea kuwepo na waliosaini bado wanatesa. Which one is the way forward.
 
Tizama habari iliyopikwa na Nchimbi, ambayo imewafanya Nipashe leo waombe radhi na kusema wazi kuwa chanzo cha haabri zao siku zote amekuwa waziri mmoja ambaye walikuwa wakimuamini sana kwamba hawakuwa na sababu ya kutafuta ukweli zaidi, aibuuu sana hii:-

Kamati Kuu CCM yamkaanga Nape

2008-09-05
Na Mwandishi Wetu


Safari ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Mnauye, ya kusaka uenyekiti wa Taifa wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa chama hicho (UVCCM) imezidi kuwa ngumu baada ya Kamati Kuu ya chama chao kutaka ajadiliwe na kamati ya nidhamu.

Vyanzo vyetu vya habari vimetupasha kwamba uamuzi wa kumjadili Nape kwenye kamati hiyo ulifikiwa jana wakati wa kikao cha Kamati Kuu kilichokaa jana kutokana na madai kwamba amekuwa akiwajadili viongozi wake nje ya vikao rasmi vya chama.

Hatua hii inakuwa ni pigo la pili kwa Nape katika safari yake ya kuwania uenyekiti huo. Tayari kiongozi huyo machachari wa UVCCM amekwisha kuwekewa kizingiti cha umri, akidaiwa kwamba kulingana na kanuni za uchaguzi wa umoja huo, umri wake haumpi fursa ya kuwania nafasi hiyo kwani tayari amevuka miaka 30.

Kanuni ya umri katika uchaguzi wa viongozi wa UVCCM inataka kiongozi anayewania nafasi hiyo asiwe amevuka miaka 30 ili atakaopochaguliwa atumikie kipindi chake cha miaka mitano akiwa bado ni kijana.

Katiba ya UVCCM inatambua kijana kama ni wale tu wasiozidi miaka 35.

Kutokana na kigezo cha umri, Kamati ya Utekelezaji ya UVCCM iliyokaa kupitia majina ya wanachama waliojitokeza kuwania nafasi za uongozi wa taifa wa jumuiya hiyo, Nape alipewa alama E, ikimaanisha kwamba hana sifa za kuwania nafasi hiyo.

Kigezo kilichotumika katika kikao hicho kilichoongozwa na Mwenyekiti wa UVCCM, Emmanuel Nchimbi, kumpa Nape alama hiyo ni umri, kikimaanisha hana sifa za kuwania nafasi hiyo.

Hatua ya jana ya Kamati Kuu kutaka Nape na wale wote ambao wamekuwa wakitoa kauli za kuwajadili viongozi nje ya vikao rasmi vya chama wajadiliwe, inaongeza ugumu wa Nape kujinasua katika vikwazo vinavyomzuia kuwania nafasi hiyo ya uongozi akiwa amejaribu mara moja na kubwagwa na mpinzani wake, Nchimbi katika uchaguzi uliofanyika mwaka 2003.

Kamati ya maadili inaongozwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete.

Wajumbe wengine ni pamoja na Andrew Chenge na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ambao sasa wanaelekea kushikilia hatima ya kisiasa ya Nape.

Nape amefikishwa hapo kutokana na msimamo wake usioyumba wa kuhoji mkataba wa ujenzi wa jengo jipya la UVCCM lililoko barabara ya Morogoro jijini Dar es Salaam.

Nape alipochukua fomu za kuwania uenyekiti wa UVCCM Julai mwaka huu, alimtaka Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini wa UVCCM, Edward Lowassa, kuwajibika kutokana na kuiingiza jumuiya hiyo katika mkataba ambao hauna maslahi nayo.

Mwanasiasa huyo kijana na machachari pia alisema kwamba UVCCM haikushiriki kwa hali yoyote kupitisha mkataba huo ambao unampa mwekezaji hati miliki ya milele kwenye kiwanja kilichoko nyuma ya jengo kuu la sasa la umoja huo.

Katika jengo hilo jipya ambalo ujenzi wake umekwisha kuanza, uongozi wa UVCCM na CCM kwa ujumla umeshikilia kwamba mkataba haujafikiwa wakati mjenzi tayari ameanza kazi ya ujenzi.

Katika hatua nyingine, Kamati Kuu jana iliafiki mradi huo wa kuuza kiwanja cha UVCCM ambacho mwekezaji anamiliki asilimia 75 ya jengo hilo wakati UVCCM itakuwa na asilimia 25 tu.

Mkataba huo ni wa milele na mgawanyo wa miliki hautabadilika hata kama mradi mpya ukiendelezwa kwenye kiwanja hicho.

Vyanzo vyetu kutoka ndani ya kikao hicho vilisema kwamba Kamati Kuu imeubariki mradi wa jengo hilo jipya na kuupongeza umoja huo kwa kuwa `wabunifu` ili kuukwamua na ukata ambao umekuwa ukiwaandama kwa miaka mingi sasa, hasa baada ya kurejea mfumo wa vyama vingi nchini.

Katika mradi huo, UVCCM itakuwa ikipata kodi ya Sh. milioni 107 kwa mwezi, mapato ambayo yatasaidia umoja huo kujiendesha kwa ufanisi zaidi.

Jengo jipya linalojengwa litakuwa ni pacha, lenye ghorofa 23.

Kumekuwa na taarifa kwenye vyombo vya habari kwamba mkataba wa mradi huo haukujadiliwa na kupata baraka za Baraza Kuu la UVCCM ambalo ni chombo cha juu kabisa cha maamuzi.

Kadhalika imedaiwa kwenye vyombo vya habari kwamba Lowassa akiwa ni Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini wa UVCCM, ndiye alisaini mkataba huo bila hata kuwashirikisha wajumbe wengine wa Baraza hilo, wakiwamo Waziri wa Viwanda na Biashara, Mary Nagu na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, William Lukuvi.
 
JAMANI CCM watafanya nini kama si kumuita Nchimbi na kumjadili katika kamati ya "Chenge?". Pamoja na kuwa Nipashe wamekiuka maadili ya uandishi wa habari kwa kuonyesha chanzo, kwa mtu kama Nchimbi ambaye ni HATARI anastahili na tena alistahili hata kutajwa jina ili asizoeee. LAKINI JAMANI HILI DUDE LI- SISIEMU huwa halina AIBU TUSUBIRI MAAJABU DODOMA LEO


CCM: Mkataba tata Jengo la UVCCM kitaeleweka wiki ijayo

2008-09-06
Na Mwandishi Wetu


Utata uliougubika mkataba wa mradi wa ujenzi wa jengo jipya la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), umefikishwa kwenye Kamati Kuu ya chama hicho, ambayo inajipanga kuujadili wiki ijayo.

Naibu Katibu Mkuu wa CCM Tanzania Bara, George Mkuchika, alisema mradi wa ujenzi wa jengo hilo lililoko Barabara ya Morogoro, jijini Dar es Salaam, sasa utajadiliwa Septemba 9, mwaka huu, baada ya kushindikana kujadiliwa juzi.


Alisema ajenda ya mradi huo haikuweza kujadiliwa juzi kutokana na chama hicho kutingwa na mambo mengi, ikiwamo ziara ya Mwenyekiti wa Chama cha African National Congress (ANC), Jacob Zuma, aliyekuwa nchini kwa ziara ya kuimarisha uhusiano kati ya chama chake na CCM.


Mkuchika alisema suala la wagombea wa UVCCM, pia linasubiri kikao cha Baraza Kuu la Umoja huo linalotarajia kukutana kesho mjini Dodoma.


Alisema baada ya kikao hicho, Sekretarieti italipokea suala hilo keshokutwa kisha kuwasilisha ajenda hiyo kwenye Kamati Kuu na baadaye kupelekwa kwenye Halmashauri Kuu (NEC) ya Taifa.


Gazeti hili jana kimakosa lilikariri vyanzo vya habari kutoka Kamati Kuu ya CCM, vikisema kwamba mkataba wa jengo huo, ulijadiliwa na pongezi zikatolewa kwamba unafaa kwani unalenga kuikwamua UVCCM na ukata.

Pia Vyanzo hivyo viliiambia Nipashe kuwa Nape aliagizwa ajadiliwe na kamati ya maadili.

Lakini Kamati Kuu haikujadili suala lolote kuhusu Nape. Nipashe haikuona sababu ya kutomuamini mtoa habari huyo ambaye yuko katika hadhi ya uwaziri.

Pia, mtoa habari huyo amekuwa akitoa habari za ukweli mara kwa mara.


Baada ya kauli ya Mkuchika, ukweli sasa umebainika kwamba suala la jengo jipya la Umoja huo, halikujadiliwa na bado ni la moto hadi hapo Kamati Kuu itakapoamua.


Suala la mradi wa jengo jipya la UVCCM limekuwa tata kwa muda mrefu kutokana na mvutano baina ya viongozi wa CCM, hasa wa UVCCM wanaoeleza wazi kupingana na mradi huo kutokana na kile wanachosema hauna maslahi na chama na kwamba, ulipitishwa kinyemela bila kuhusisha vyombo stahili vya umoja huo.


Miongoni mwa viongozi wa UVCCM ambao wamekuwa mstari wa mbele kupambana kwa lengo la kutetea haki za chama katika mradi huo, ambao Umoja huo utamiliki asilimia 25 na mwekezaji asilimia 75 milele, ni mjumbe wa NEC, Nape Nnauye.


Hivi karibuni, Nape alimbebesha lawama Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini wa UVCCM, Edward Lowassa, kutokana na kusaini mkataba huo bila kupitishwa kwanza na Baraza Kuu la Umoja huo.


Nape alimtaka Lowassa awajibike kwa sababu mkataba huo kama ulivyo, hauna maslahi yoyote kwa UVCCM na chama na ulikuwa na dalili za ufisadi kutokana na kupitishwa kinyemela.


Jengo hilo, ambalo tayari ujenzi wake umekwishaanza, litakuwa pacha la ghorofa 23. Mbali ya UVCCM kumiliki asilimia 25, mwekezaji atamiliki asilimia 75 na pia atawajibika kuligharimia wakati wote.


UVCCM inaelezwa kwamba itakuwa inapata kodi ya sh. milioni 107 kwa mwezi hivyo kuiwezesha kujikwamua na ukata.


Ingawa uongozi wa UVCCM kupitia kwa Katibu Mkuu wake, Isaac Francis, umesisitiza kwamba mkataba wa mradi huo haujafikiwa, baadhi ya vyombo vya habari vimeweka hadharani mkataba unaodaiwa kwamba ni wa ujenzi wa jengo hilo.


Mkataba huo, ambao Isaac alidai ni makubaliano ya awali na si mkataba halisi ulionyeshwa kwenye vyombo vya habari, ulisainiwa na Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini na aliyekuwa Katibu Mkuu wa UVCCM, Amos Makalla ambaye sasa ni Mweka Hazina wa CCM.


Lowassa mwenyewe amekanusha kusaini mkataba huo na kutishia kufikisha mahakamani gazeti moja kutokana na kuandika habari hizo.


Hata hivyo, hadi jana, Lowassa ambaye baada ya kujiuzulu uwaziri mkuu alibakia na ubunge wa Monduli, hajafungua kesi hiyo.


Kilio cha Nape na baadhi ya viongozi wengine wa Baraza Kuu la UVCCM ambao walinukuliwa na vyombo vya habari Julai mwaka huu, walikana kuhusika kupitisha mradi huo.


Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, mwezi Julai alimwita Nape ofisini kwake, baada ya kutoa kauli kali dhidi ya Lowassa akimtaka ajiuzulu kwa kuingiza UVCCM katika mkataba `feki` na kumkaripia kwamba hakupasa kumsema Lowassa hadharani kwa kuwa (Nape) ana nafasi ndani ya vikao vya chama kumkosoa kiongozi mwenzake.


Mbali na viongozi wa UVCCM kuruka kuhusika kupitisha mkataba huo, hata wajumbe wengine wa Baraza la Wadhamini, wakiwamo Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Mary Nagu na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, William Lukuvi, nao walinukuliwa na gazeti moja la kila wiki wakisema kwa nyakati tofauti kwamba hawaujui mkataba wa ujenzi wa jengo hilo.


SOURCE: Nipashehttp://www.ippmedia.com/ipp/nipashe/2008/09/06/122034.html
 
Mkuu Halisi, sasa ngoja tumsikie Nchimbi leo na kikao chake cha baraza la UV-CCM kule Dodoma, maana he is not done yet!
 
Wazee CCM wamkaanga Nape Nnauye, wajumbe wataka afutwe uanachama

Na Habel Chidawali, Dodoma

WAZEE wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wametoa kauli ambazo zinaonyesha wazi kumshughulikia kijana machachari ndani ya chama hicho Nape Nnauye, katika mbio zake za kuwani Uenyekiti wa Umoja wa Vijana wa chama hicho (UV-CCM).

Sambamba na hilo Baraza la Umoja wa Vijana limemfuta Nnauye uanachama wa jumuia hiyo kwa kumnyang'anya kadi na kumzuia kuhudhuria vikao vyote ya UVCCM kuanzia sasa.


Wakizungumza katika mkutano wa Baraza hilo lililofanyika mjini Dodoma jana, wazee hao Katibu wa CCM, Yusufu Makamba, Kaimu Kamanda wa Vijana, Kingunge Ngombale Mwiru na Mshauri wa Vijana Mzee Rashid Kawawa waliwaonya wagombea wote na wapambe wao kuacha kukikosoa chama hicho badala yake wawe wapole.


Baadhi ya wazee hao walizungumza kwa lugha ya mafumbo zilizoonyeshga wazi kwamba zilikuwa zinaekezwa kwa kijana machachari Nape Nnauye anayewania uenyekiti wa umoja huo.


Akizungumza kwenye baraza hilo, Makamba alisema kuwa kijana yeyote anayependa kukisoa chama hafai kuwa kiongozi kwani kila anayetaka kuwa kiongozi ni lazima awe mpole na akubali siku zote kuwatii wakubwa.


Makamba alisema kuwa kuna vijana wanaodai heshima kwa nguvu na matokeo yake hununua dharau, kauli ambayo ilionekana kuwakasirisha baadhi ya wajumbe walinaodhaniwa kuwa upande wa Nape na kundi lake.


Alisema wao kama viongozi hawezi kukaa kimya kuona watu wanakivuruga chama kwa kukiuka maadili na kukikosoa chama nje ya vikao.


Naye Mwanasiasa Mkongwe na kada wa CCM wa siku nyingi, ambaye pia Kaimu Kamanda wa Vijana Tanzania Bara, Kingunge Ngombale Mwiru alisema anashangazwa sana na tabia ya baadhi ya wanachama wa CCM kupita mabarabarani na kusema ovyo.


Alisema tabia hiyo haivumiliki kwani inakivuruga chama na inatakiwa kushughulikiwa ipasavyo kadri inavyowezekana.


Kingunge alitoa historia ya umoja huo akisema umeanzishwa miaka mingi iliyopita ikiwa chini ya mmoja wa waasisi Mzee Kawawa ambaye ndiye Kamanda wa umoja huo hadi sasa.


Naye Kamanda wa Taifa wa Vijana, Rashidi Kawawa alisisitiza kuwa vijana wanatakiwa kufanya kazi kwa bidii na kuondokana na utegemezi.


Alisema ili kufanya ndoto hizo ziwe kweli wiki ijayo atakwenda Liwale katika utaratibu wa kuwakopesha vijana matrekta ili waweze kujitegemea.


Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi CCM, (UVCCM), anayemaliza muda wake, Dk Emmanuel Nchimbi wakati akifungua mkutano wa Baraza kuu alirusha vijembe kuwa katika uteuzi wa nafasi hizo hawatamuangalia nyani usoni.


Dk Nchimbi aliliambia baraza hilo kuwa katika uteuzi wa nafasi hizo hawatatumia busara za kwamba fulani ana rekodi katika jumuiya hiyo, bali watazingatia kanuni walizojiwekea kufikia maamuzi sahihi.


Hata hivyo hotuba hiyo ambayo moja kwa moja ilionekana kumlenga Nnauye ilikosolewa na baadhi ya wajumbe wa kikao hicho na kusema kuwa inatokana na mahusiano mabaya baina ya wanasiasa hao.


Dk Nchimbi ambaye alikuwa Mwenyekiti wa mkutano alinza kuhutubua kwa kuelekeza suala la umri huku akitoa mifano kadhaa.


"Leo tunapitia majina ya wagombea wa nafasi mbalimbali katika jumuiya yetu, jambo moja ninaloweza kuwakumbusha ni kuwa hapa hatuna cha ajabu zaidi ya kurudisha heshima ya umoja wetu kwa kufuata kanuni, hakuna kumuonea haya mtu na atakayetaka kufanya hivyo naomba atushinde kwa vifungu vya kanuni na si vinginevyo," alisema Nchimbi na kuongeza kuwa, "Miaka mitano iliyopita mimi nilimkata rafiki yangu kutokana na kigezo cha umri lakini sikuona aibu na leo hii nasisitiza wajumbe kuwa umri ni lazima uangaliwe kwa kufuata kanuni asisimame mtu na kuniambia kuwa fulani anafaa licha ya kuwa ana umri mkubwa hapana lazima anionyeshe kanuni," alisisitiza Dk Nchimbi.


Mwenyekiti huyo alisema taasisi ya vijana ni kubwa hivyo kwa wanaoshangaa na kusema kuwa kuna migogoro hawajui kuwa taasisi kama hiyo haikosi kuwa na wendawazimu wengi ambao ndio wanaoleta migogoro na mivutano ndani ya jumuiya hiyo.


"Hatuwezi kuwa na taasisi kubwa kama hii halafu tukakosa wendawazimu, hilo haliwezekani na ninasema leo hadharani kuwa wendawazimu wote ni lazima tutawashughulikia ili iwe ni fundisho kwa wengine, hilo linawezekana na liko ndani ya uwezo wetu," alisema Dk Nchimbi huku akishangiliwa na kikundi cha wachache na baadhi ya wajumbe wakiguna.


Habari kutoka ndani ya mkutano huo zinasema kuwa, wakati Dk Nchimbi akiendelea kuhutubia, mjumbe mmoja alisimama na kusema kwa nini mtu huyo asinyang'anywe kadi ya umoja wa vijana na kuadhibiwa? Mwenyekiti akajibu, ''imepitishwa".


Mbali na hiyo hilo, baraza liliazimia kuwa kuanzisa sasa asihudhurie vikao vyote vya umoja huo pamoja na kupeleka mapendekezo kwa Halmashauri Kuu ili aweze kushughulikiwa zaidi ikiwa ni pamoja na kunyang'anywa ujumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM.


Katika hatua nyingine Nchimbi alisema kuwa kuna mtu miongoni mwa wajumbe ambaye amekuwa akisambaza makala mbalimbali kwa vyombo vya habari kwa nia ya kukichafua Chama Cha Mapinduzi na jumuiya ya vijana jambo alilosema kuwa ni hatari sana kwa chama hasa katika kipindi hiki nchi inapoelekea katika uchaguzi.


Bila kumtaja jina, Dk Nchimbi alisema kijana huyo ni hatari sana kwa umoja wao na kuongeza kuwa hata ikiletwa mbele ya wajumbe kompyuta yake ndogo inaweza kukutwa na makala zisizopungua 40 kwa wakati mmoja ambazo anasuburi kuzisambaza kwa vyombo mbalimbali vya habari.


Kikao hicho ambacho ni cha tatu tangu kuanza kwa zoezi la mchujo wa vikao kwa wagombea, kama ilivyo kwa vikao vingine vilivyopita kinatarajiwa kutoa mapendekezo kwa Kamati Kuu ya CCM, itakayofanya uteuzi wa mwisho kwa majina yanayoomba nafasi za uwakilishi kwa jumuiya.


Hotuba hiyo ya mwenyekiti wa umoja huo ilielezewa kama ni njia ya kuwatisha wajumbe ili wasiweze kutenda haki kama walivyokusudia.


Baadhi ya wajumbe toka Kanda ya Ziwa walisikika wakisema hatua hiyo ni sawa na kuwaburuza bila ya ridhaa yao kwa kuwa Nnauye ndiyo lilikuwa ndio chaguo lao.


Wakati wakijiandaa kufunga mkutano huo, ilitolewa taarifa kuwa Katibu wa Uchumi na Fedha wa CCM, Amos Makala amewandalia chakula cha jioni lakini baadhi ya vijana wanaodhaniwa kuwa wa kambi ya Nnauye walikataa wakidai kuwa hakuna wanachokwenda kujipongeza.


Source: Mwananchi
 
Akizungumza kwenye baraza hilo, Makamba alisema kuwa kijana yeyote anayependa kukisoa chama hafai kuwa kiongozi kwani kila anayetaka kuwa kiongozi ni lazima awe mpole na akubali siku zote kuwatii wakubwa.

Kama ilivyotegemewa, wote hawana jipya yale yale!
 
Back
Top Bottom