William J. Malecela
R I P
- Apr 27, 2006
- 26,584
- 10,464
Hoja hujibiwa kwa hoja:-
1.
Quote: Sober
Wakuu,
1. Kuhusu suala la umri kwenye uchaguzi wa UVCCM, utakuta kanuni zenyewe za UVCCM zinajichanganya. Na, hii ni kwa sababu kipengele cha umri kiliingizwa kimizengwe.
2.[*]Kanuni zinaainisha umri ambao mwanachama wa UVCCM atakua ni kijana wa miaka 15 mpaka 35.
3.[*]Kanuni hizohizo zinasema wakati wa uchaguzi, kila mwanachama atakua na haki ya kuchagua au kugombea nafasi ya uongozi wa UVCCM kama atakua na sifa.
4.[*]Halafu kanuni hizohizo tena zinakuja kusema, ili kugombea nafasi ya uongozi mwanachama unatakiwa usiwe umezidi umri wa miaka 30. Tayari haki mojawapo iliyoyajwa na kanuni za hapo juu imekiukwa.
5. Sasa hapa unaona kuna kundi kubwa sana(30-35yrs) ambao lina sifa za kupiga kura lakini haliwezi kugombea uongozi.
6. Kwa akili ya kawaida tu utaona hizi kanuni zina walakini. Hii ndio mifano ya kanuni zinazochomekwa kwa maslahi ya mtu mmojammoja badala ya kutizama maslahi ya chama kwa ujumla.
Kiko wapi chama cha Mwalimu???....
1.
Quote: Mtanzania
Ben,
Nakubaliana na baadhi uliyoandika hapo juu ila ni muhimu mno kufuata sheria/taratibu na pia hakuna sababu ya kubadili sheria kwa ajili ya mtu mmoja. Nape alikuwa na miaka zaidi ya mitano ya kuipinga hiyo kanuni mbovu na hakufanya hivyo. Kama ni kweli ana umri zaidi ya unaotakiwa ningelikuwa mimi Mwenyekiti wa CCM ningelimpiga stop!
Sheria ni sheria wakuu hata kama inakukaba mwenyewe bado ni sheria na inabidi ifuatwe. Ila kwa jinsi CCM walivyo wanaweza kubadili na kumwacha Nape agombee. Nape mwenyewe kama anang'ang'ania kuwa Mwenyekiti pamoja na kujua hana sifa, inaonyesha tuna aina gani za wanasiasa Tanzania. Ma opportunists ambao wako tayari kusema lolote ili wachaguliwe. Binafsi siwataki wanasiasa wa namna hiyo.
Maneno ya kale ka mama ka McCain yamenigusa sana hata kama siwapendi Republicans. Aliongea kitu karibu na haya maneno "some use change to further their careers while others use their careers to bring change"
Siasa za slogans zimepitwa na wakati, vijana mnaotaka kuingia kwenye siasa lazima muamini na kutenda mnayohubiri. Yale ya slogan nzito kama JK huku matendo sifuri hayatufai kabisa. Nape kama umri umepita basi asubiri 2010 na awe cheche kwenye ubunge.
Quote: Sober
Wakuu,
1. Kuhusu suala la umri kwenye uchaguzi wa UVCCM, utakuta kanuni zenyewe za UVCCM zinajichanganya. Na, hii ni kwa sababu kipengele cha umri kiliingizwa kimizengwe.
2.[*]Kanuni zinaainisha umri ambao mwanachama wa UVCCM atakua ni kijana wa miaka 15 mpaka 35.
3.[*]Kanuni hizohizo zinasema wakati wa uchaguzi, kila mwanachama atakua na haki ya kuchagua au kugombea nafasi ya uongozi wa UVCCM kama atakua na sifa.
4.[*]Halafu kanuni hizohizo tena zinakuja kusema, ili kugombea nafasi ya uongozi mwanachama unatakiwa usiwe umezidi umri wa miaka 30. Tayari haki mojawapo iliyoyajwa na kanuni za hapo juu imekiukwa.
5. Sasa hapa unaona kuna kundi kubwa sana(30-35yrs) ambao lina sifa za kupiga kura lakini haliwezi kugombea uongozi.
6. Kwa akili ya kawaida tu utaona hizi kanuni zina walakini. Hii ndio mifano ya kanuni zinazochomekwa kwa maslahi ya mtu mmojammoja badala ya kutizama maslahi ya chama kwa ujumla.
Kiko wapi chama cha Mwalimu???....